Ousmane Dembele ameshindwana na klabu yake ya Fc Barcelona juu ya makubaliano ya kuongeza mkataba mpya
Nyota huyo amelalamika kuhusu namna ambavyo Barça hawataki aendelee kuitumikia timu hiyo hadi atakapouzwa kwenda timu nyingine.
Zipo taarifa zilizosambaa kuwa kocha wa timu hiyo Xavi Hernandez amekasirishwa na kitendo hicho na kuamua kumuondoa kabisa Dembele kwenye mipango yake licha ya uongozi wa Barça kusema kuwa Dembele anaumwa tumbo ndio maana hakufanya mazoezi ya mwisho kwaajili ya mchezo uliopita dhidi ya Alaves
Rais wa La Liga
Javier Tebas amezungumzia suala hilo
"Hapana, hapana, sidhani kama Barcelona wamefanya chochote kinyume cha sheria,"
"Ninavyomjua Mateu Alemany (Mkurugenzi wa Barça) naamini kuwa hivyo ndivyo ilivyo, wamesema hakufanya mazoezi kutokana na ugonjwa wa tumbo. Natamani kungekuwa na watu kama Mateu Alemany katika soka.