BEKI chipukizi Mtanzania, Alphonce Mabula Msanga amesajiliwa na Klabu ya Spartak Seubotica ya Serbia kwa Mkataba wa miaka minne na nusu.
Mabula mwenye umri wa miaka 18 sasa, aliibukia timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys na akacheza Fainali za Vijana chini ya umri wa miaka 17 (AFCON U17) mwaka 2019 zilizofanyika hapa nchini kabla ya kupandishwa timu ya vijana U20.