Hili la Vunjabei Mdhamini wa Simba kuwamwagia manoti Prisons limekaaje?

Mkwavinyika

Administrator
Staff member
Dec 2, 2021
49
9
26
Dar es Salaam
prison-pic.jpg


Wana Kijiwe

Klabu ya soka ya Tanzania Prisons imeingia mkataba wa kuzalisha vifaa vya michezo na Kampuni ya Vunjabei wenye thamani ya Sh60 milioni.

Mkataba huo uliosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Fredy Ngajiro (Vunjabei) na Kaimu Kamishna wa utawala na usimamizi wa rasilimali watu Jeshi la Magereza Jeremiah Katungu kwenye makao makuu Mkoani hapa.

Aidha licha ya uzinduzi wa jezi pia Vunjabei ameahidi kutoa vifaa vingine katika muda wa mkataba unaendelea ambao ni mwaka mmoja.

Akizungumza kilichomsukuma kufanya ufadhili huo Fredy amesema timu hiyo inajiandaa kuingia kwenye mchezo wake mkubwa wa Disemba 19 dhidi ya Yanga hivyo ni vema wakacheza na Jezi mpya kama ilivyo kwa timu nyingine ikiwa pia ni njia ya kukabiliana na ufinyu wa bajeti unaozikabili timu nyingi nchini.

“Proposal (pendekezo) lilichelewa kuja wakati msimu wa Ligi unaanza lakini kwa uzinduzi wa leo tunatarajia kwenye mchezo wa kesho mtaenda kucheza na Jezi mpya kabla ya mchezo wa Disemba 19” amesema Vunjabei

Vipi unaonaje hii ishu kwako?