Je, Victor Osimhen ana hatima ya kufanya mambo makubwa zaidi katika ulimwengu wa soka? Wengi wanaamini hivyo.

jamal

Mgeni
Nov 4, 2022
148
90
5
Je, Victor Osimhen ana hatima ya kufanya mambo makubwa zaidi katika ulimwengu wa soka? Wengi wanaamini hivyo.

Mshambulizi huyo wa Napoli, 24, alifunga bao lake la 24 na 25 msimu huu Jumapili na kuwasaidia wababe hao wa Italia kujiimarisha zaidi kwenye kilele cha Serie A kwa ushindi wa 4-0 dhidi ya Torino. Napoli sasa wanaongoza kwa tofauti ya pointi 19 kileleni mwa jedwali zikiwa zimesalia mechi 11 tu kuchezwa, kumaanisha kwamba wako mbioni kutwaa taji lao la kwanza la ligi tangu 1990.

Victor Osimhen anaendelea kuwashawishi mashabiki wa Man United kabla ya dirisha la uhamisho la majira ya joto. Kwa sasa anathibitishwa kuwa ni mshambuliaji anayetafutwa sana barani Ulaya na vilabu kadhaa vikiwa na nia ya kumsajili.

Inasemekana kuwa Manchester United wanavutiwa na kumsaini mshambuliaji huyo wa Napoli wanapojipanga kuongeza mshambuliaji mpya kwenye safu yao ya mbele.

1679400688293.png