Kikosi cha Yanga dhidi ya KMC Nabi kafanya mabadiliko makubwa

Brenda

Mgeni
Oct 31, 2022
489
403
5
Dar es salaam
Nabi amefanya mabadiliko makubwa kwenye kikosi kinachoenda kukutana na KMC baada ya kutoka kukipiga na TP Mazembe match za kimataifa

Professor Nabi hatabiriki kabisa kamuanzisha Bayson, Bacca, Mwanyeto, Clement, Ambundo hawa wote kwenye kikosi chake kawaida wanatokeaga bench.

Huku wakitokea bench Djuma, Bangala, Lomalisa wamekua wakianza kwenye mechi nyingi, Moloko amekua akianza kila mechi hata kimataifa, Mudathiri ambae amekua akinza kwenye kikosi tangu ajiunge na Yanga, na Hata Mayele mshambuliaji pekee ambae kikawaida ni mchezaji muhimu na tegemeo kubwa kwenye kikosi cha Yanga.

Nabi anataka kutupa somo gani ukiacha suprise ya Juzi dhidi ya TP Mazembe leo tena anaenda kutupa somo tofauti je itakua mserereko kwa KMC, bahati au chance dakika 90 zitatupa jibu nini Nabi anataka kuonesha.

Labda ni kikosi kipana cha Yanga wanacho na sio rahisi sana kuweza kufanya rotation kama ya Nabi 🙌 jinsi unavyopanga kikosi hakuna anayeweka kutabiri aisee. Afu utakuta hana hata Pressure na kikosi chake.

All the best Wananchii ✅

Nini maoni yako kwenye mabadiliko haya?

1AE34E3F-5962-4092-8ED0-ED3E4ABD0EE8.jpeg