KIMEWAKA KAGAME CUP, LAWI BADO YUPO COASTAL.

Jul 10, 2024
1
1
5
Dar-es-salaam.

Klabu ya Coastal union imeanza kwa kishindo michuano ya Darport Kagame Cup kwa kushinda goli 1-0 dhidi ya Dekadaha FC ya nchini Somalia. Michuano hii imeanza rasmi siku ya jana tarehe 9 Julai na inategemewa kufikia tamati tarehe 28 Julai huku viwanja vinavyotumika ni uwanja mpya wa KMC uliopo mwenge jijini Dar es salaam na Azam Complex uliopo Chamazi.

Coastal.jpg
(Kikosi cha Coastal Union. Picha: Cecafa Online)

Jambo lililokua linasubiriwa na wapenzi wa soka ni kumuona Lameck Lawi ambae Sakata lake la usajili limekua na mvutano kwakuwa klabu ya simba ilitangaza kumsajili huku klabu yake ya Coastal Union ikikanusha usajili huo na kuthibitisha kwamba biashara yao na Simba ilishavurugika baada ya Simba kukiuka makubaliano yao.

Lameck Lawi bado yupo Coastal na jana alionekana katika dimba la KMC ila hakucheza alikaa jukwaani na viongozi wa klabu hio huku akivaa uzi rasmi wa klabu yake. Jambo hilo linashindilia msimamo wa Coastal Union huku kwa upande mwingine tayari wachezaji wa Simba tayari wameshaanza mazoezi katika kambi yao nchini Misri.

Matokeo ya mechi zingine ni Ali Wadi Nyala FC 1-0 JKU, klabu ya SC Villa ilitoka suluhu ya bila kufungana dhidi ya El-Merreikh huku APR kutoka Rwanda ikiichapa goli 1-0 Singida Black stars. Michuano inaendelea leo pale dimba la Azam Complex Chamazi na mechi ya kwanza itakua Al Hilal dhidi ya Djibout Telecom saa kumi na mbili jioni na saa tatu usiku mabingwa kutoka kenya Gor Mahia itachuana na Red Arrows kutoka Zambia.

Juvenalius Rugambwa.

WhatsApp Image 2024-07-10 at 11.16.16.jpeg
(Victor Mboma mchezaji wa APR. Picha: Cecafa Online)
 
  • Like
Reactions: Kijiweni