Kwani Nini Kinawafanya Azam FC Kukosa Kuwa Na Timu Ya Wanawake?

May 27, 2024
7
2
5
Azam Fc Ni Timu Kubwa Nchini Tanzania Ambayo Ina Miliki Timu Za Vijana Kuanzia Umri Wa Miaka 13,15,17,20 Na Senior.

Timu Yake Ya Kiume (Senior Team) Ina Wachezaji Toka Mataifa Mbalimbali Wenye Thamani Kubwa Kuanzia Milioni 300 Hadi Bilioni 1, Sioni Kama Azam Watashindwa Kumiliki Timu Yao Moja Tu Ya Wanawake Ambayo Kwa Mwaka Itahitaji Bajeti Ya Shilingi Milioni 200,150 Au Hata 100 Tu.

Kuweka Ushiriki Kila Mwaka Na Timu Zingine Pasi Na Kuanzisha Timu Yao Ya Kike Inaweza Kufikiriwa Kama Azam Wanawanyima Au Hawapo Tayari Kutoa Sapoti/Nafasi Ya Moja Kwa Moja Kwa Wachezaji Wa Kike Kutimiza Ndoto Zao Kupitia Logo Ya Timu Yao Kama Ilivyo Kwa Wenzao Wa Kiume ...

⛔️ USHAURI KWA TIMU ZOTE ZA WANAWAKE ...

Ifike Hatua Timu Zinazoingia Makubaliano Haya Na Timu Za Kiume (Mfano Azam Fc) Kuweka Ngumu Ili Kuwa Upande Wa Kulikuza Soka La Wanawake Endapo Tu Timu Hizo Za Kiume Zitakuwa Mmiliki Wa Moja Kwa Moja Wa Timu Ya Wanawake ...

NB;

Kitendo Cha Timu Ya Kike Kuweka Ushiriki Na Timu Ya Kiume Ambayo Inashiriki Mashindano Ya CAF Kwasababu Ya Kukidhi Tu Matakwa Ya CAF Basi Ni Kujinyima Haki Zako Za Msingi Toka CAF Kwani Atakae Julikana CAF Ni Brand Ya Timu Ya Kiume Na Sio Ya Kike ...

Ni Wakati Sasa Azam Fc Kuwa Na Timu Yenu Rasmi Ya Wanawake, Ni Wakati Sasa Azam Muingie Kusapoti Wachezaji Wa Kike Moja Kwa Moja Kwa Kuwa Na Timu Ya Wanawake Itakayomilikiwa Na Azam kama Ambavyo Mnafanya Kwa Wanaume ...