Morisson na Dunia yake Tanzania

Feb 7, 2023
61
36
5
Moja ya mchezaji ambaye aliteka vichwa vya habari vingi hapa Tanzania ni mtukutu Benard Morisson, hili likuja baada ya kiwango chake bora ndani ya uwanja tangu kwenye miamba ya Simba na Yanga.
Lakini tatizo kubwa kwake linakuja nje ya uwanja ambapo amekuwa akifanya vituko vingi vya utovu wa nidhamu kupelekea kufungiwa kwa baadhi ya michezo.
Morisson amekuwa mchezaji ambaye anacheza na akili za viongozi na mashabiki wa timu hizi mbili, lakini licha ya yote hayo kufahamika bado anaonekana lulu kwa Yanga.
Kitu ninachojiuliza ni kitu gani kinachowafanya yanga waendelee kuwa na mtukutu huyu ambaye amekuwa hana msaada mkubwa ndani ya timu.
Juzi imetoka taarifa kuwa amepata majeraha ya nyonga,kipindi hiko ametoka kwao Ghana unajiuliza nini Morisson anakihitaji zaidi ya kucheza mpira uwanjani maana atacheza mechi mbili au tatu baada ya hapo utasikia ameumia au umeomba ruhusa akashughulikie masuala ya kifamilia kwao.
Hapa ndo naikumbuka ile kauli ya kama hauna nidhamu kwenye jambo lolote basi ni ngumu kwako kufanikiwa,alishindwa kuonyesha nidhamu akiwa Afrika kusini na Orlando pirates, akiwa na Simba pia hata sasa akiwa na Yanga.
Acha tuone mwisho wa hii sinema ya Morisson na vilabu vyetu vya Bongo itaisha lini,Morisson anajua udhaifu wa timu zetu ndomaana anatumia nafasi hiyo vizuri.20230209_104328.jpg
 
  • Like
Reactions: sharon