NAMUNGO FC YALAZIMISHWA SARE 1-1 NA BIASHARA.

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
1640937880629.png
WENYEJI, Namungo FC wamelazimishwa sare ya 1-1 na Biashara United katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Ilulu mjini Lindi.
Namungo FC walitangulia kwa bao la mshambuliaji wake tegemeo, Relliant Lusajo dakika ya 10, kabla ya Dennis Nkane kuisawazishia Biashara United dakika 37.
Kwa sare hiyo kwenye mchezo wa 11 kwa wote, Namungo FC wanafikisha pointi 13 katika nafasi ya nane, wakati Biashara wanafikisha pointi tisa katika nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16, ambayo mwisho wa msimu mbili zitashuka na mbili zitakwenda kumenyana na timu za Championship kuwania kubaki Ligi Kuu.