Ndo hivyo Chama kufuata nyayo za Okwi.

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
1640672672391.png

HABARI za kurejea nchini kwa kiungo fundi raia wa Zambia, Clatous Chama ‘Mwamba wa Lusaka’ zimepamba moto kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo ambapo timu mbalimbali inakitumia kuimarisha vikosi vyao.
Klabu za Simba na Yanga ndio ambazo zimekuwa zikihusishwa na kiungo huyo ambaye anaichezea RS Berkane ya Morocco inayonolewa na Florent Ibenge.
Simba inaonekana kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kupata huduma ya Chama kutokana na kipengele cha kimkataba (wa Chama) ambacho kinaeleza ikiwa fundi huyo atataka kurejea tena Tanzania basi chaguo la kwanza ni timu hiyo.
Kipengele hicho kinaelezwa kuwa kiliwekwa wakati ikifanyika biashara ya uhamisho wa Chama kutoka Simba na kwenda Morocco kuungana na kocha wa zamani wa AS Vita na timu ya taifa ya DR Congo, Ibenge ambaye alivutiwa naye.
Chama anatajwa kutokuwa na furaha huko Morocco na yote hiyo inatokana na kutokuwa chaguo la kwanza la Ibenge kwenye kikosi chake.
Mbali na Chama ambaye muda wowote anaweza kurejea Simba hawa hapa nyota wengine wa kigeni ambao walirejea kwenye klabu zao za awali ambazo walizichezea nchini, akiwemo Heritier Makambo.