Ni leo: Argentina vs Ufaransa
Mechi ya finali ya kombe la Dunia kati ya Ufaransa na Agentina inachezwa leo saa 12 jioni nchini Qatar, huku wachezaji wawili wa zama tofauti wakipanda kuweka historia.
Lionel Messi anaangazia kutwaa
kombe la Dunia kwa mara ya kwanza katika maisha yake ya soka .
Lakini pia huenda michuano hiii ikawa ndiyo ya mwisho kwa staa huyo ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 35. Atakuwa na miaka 39 katika michuano ijayo ya kombe la Dunia.
Swali pekee , je Messi atathibitisha kuwa mchezaji bora wa muda wote?
Swali ambalo mashabiki wa soka wanajiuliza, je Messi ni bora kuliko Diego Maradona?
Lakini mshindi wa kombe la Dunia la 2006 Francesco Totti anasema Maradona ' is the best'.
Kabla ya mechi ya leo usiku, Messi tayari ameweka rekodi ya kuwa mfungaji bora zaidi ya Maradona katika timu ya Argentina , akifunga mara tano katika mechi 6.
Kwa upande mwingine, Kylian Mbappé anataka kuweka rekodi ya kuwa mchezaji kinda zaidi kutwaa kombe la Dunia mara mbili, kufikia rekodi ya Pele aliyoiweka mwaka 1962.
Mbappe, licha ya kuwa na miaka 23, tayari amefanya makubwa katika historia yake.
Alishinda kombe la Dunia akiwa na miaka 19 na atakuwa mchezaji wa pili kufanya hivyo katika umri mdogo.
Je nani atacheka kati yao?
Mechi ya finali ya kombe la Dunia kati ya Ufaransa na Agentina inachezwa leo saa 12 jioni nchini Qatar, huku wachezaji wawili wa zama tofauti wakipanda kuweka historia.
Lionel Messi anaangazia kutwaa
kombe la Dunia kwa mara ya kwanza katika maisha yake ya soka .
Lakini pia huenda michuano hiii ikawa ndiyo ya mwisho kwa staa huyo ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 35. Atakuwa na miaka 39 katika michuano ijayo ya kombe la Dunia.
Swali pekee , je Messi atathibitisha kuwa mchezaji bora wa muda wote?
Swali ambalo mashabiki wa soka wanajiuliza, je Messi ni bora kuliko Diego Maradona?
Lakini mshindi wa kombe la Dunia la 2006 Francesco Totti anasema Maradona ' is the best'.
Kabla ya mechi ya leo usiku, Messi tayari ameweka rekodi ya kuwa mfungaji bora zaidi ya Maradona katika timu ya Argentina , akifunga mara tano katika mechi 6.
Kwa upande mwingine, Kylian Mbappé anataka kuweka rekodi ya kuwa mchezaji kinda zaidi kutwaa kombe la Dunia mara mbili, kufikia rekodi ya Pele aliyoiweka mwaka 1962.
Mbappe, licha ya kuwa na miaka 23, tayari amefanya makubwa katika historia yake.
Alishinda kombe la Dunia akiwa na miaka 19 na atakuwa mchezaji wa pili kufanya hivyo katika umri mdogo.
Je nani atacheka kati yao?