Picha ya Messi yaongoza Dunia kwa Like

kidudumtujr

Mgeni
Dec 14, 2022
50
70
5
Tanzania
Picha ya Lionel Messi akiwa amebeba kombe la Dunia imeongoza kwa kupata ' likes' nyingi.

Picha hiyo aliiposti katika page yake ya Instagram baada ya kuiongoza Argentina kutwaa taji la kombe le Dunia nchini Qatar.

Kwa mujibu wa Dail Mail, picha hiyo imepata zaidi ya likes milioni 67.5, ikivunja rekodi ya video ya Bella Poarch iliyokuwa na likes milioni 60 katika mtandao wa Tik Tok.

Bella Poarch ni msanii mwenye asili ya Ufilipino na Marekani mwenye ushawishi katika mitandao ya kijamii.

Messi ametwaa taji hilo kwa mara ya kwanza , lakini ikiwa ni mara ya tatu kwa Argentina.
 

Attachments

  • E5D18654-2C13-4152-B07B-1E5709D34515.jpeg
    E5D18654-2C13-4152-B07B-1E5709D34515.jpeg
    28.3 KB · Somwa: 0