Samatta Awatosa Ronaldo, Messi Tuzo za FIFA.

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
270758584_218361287042936_691031712871833402_n.jpg

KURA aliyopiga Mtanzania Mbwana Samatta kwa straika Robert Lewandowski wa Bayern Munich, imemfanya nyota
huyo aibuke mshindi waTuzo za Mchezaji Bora wa FIFA, huku akiwatosa kabisa mastaa Cristiano Ronaldo na Lionel Messi.
Samatta anayekipiga Klabu ya Royal Antwerp ya Ubelgiji na nahodha wa Taifa Stars, alikuwa mmoja kati ya wadau waliopiga kura hiyo ambapo tuzo hizo zilifanyika juzi usiku katika Jiji la Zurich, Uswisi yalipo Makao Makuu ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).
Katika kura zake tatu alizopiga kama nahodha wa Tanzania, ya kwanza Samatta ilikuwa kwa Mpolandi, Lewandowski, ya pili alimpigia mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah pia ni nahodha wa Misri na
ya tatu ilienda kwa kiungo Muitaliano anayekipiga Chelsea, Jorginho.