Simba katika njia ngumu ya kusaka taji Afrika

Mkwavinyika

Administrator
Staff member
Dec 2, 2021
49
9
26
Dar es Salaam
Wawakilishi wa Tanzania katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika Simba, wamefanikiwa kutinga hatua ya makundi baada ya ushindi wa jumla wa mabao 4-2 dhidi ya Red Arrows ya Zambia katika hatua ya mwisho ya mchujo ambapo mechi zake za mwanzo zilichezwa Novemba 28 na mechi za marudiano ilikuwa Desemba 5.

Bado tarehe ya droo ya hatua ya makundi haijapangwa lakini kwa mujibu wa utaratibu, Simba ina nafasi kubwa ya kuwekwa katika chungu cha pili hivyo haiwezi kukutana na timu ambazo itapangwa nazo pamoja katika chungu kimoja ingawa inaweza kujikuta ikiangukia kundi moja na miongoni mwa timu 12 anbazo zitakuwa katika vyungu vingine.

Katika chungu cha pili, Simba itakuwa na Coton Sport na Orlando Pirates.

Chungu cha kwanza kina TP Mazembe na RS Berkane, Pyramids wakati cha tatu kuna Zanaco, JS Saoura, Asec Mimosas na Al Ahli Tripoli na cha nne kina AS Otoho, US Gendarmarie.

Bado mechi kati ya Enyimba na Al Ittihad haijaamriwa kama ilivyo kwa mechi kati ya Royal Leopards na JS Kabylie.

Makala hii inakuletea dondoo fupi za mafanikio katika mashindano ya Afrika kwa timu 10 zilizojihakikishia kutinga hatua ya 16 ambazo miongoni mwazo Simba inaweza kupangwa na tatu kwenye hatua ya makundi.

simba-pic.jpg