Simba kujibu Maswali yote waliyoulizwa na Raja leo dhidi ya Azam?

Feb 7, 2023
61
36
5
Simba baada ya kupokea kipigo kizito cha mabao 3-0 kutoka kwa Raja Casablanca Wikiendi iliyoisha,Leo watashuka dimbani kujiuliza tena dhidi ya Azam

Simba hawakuwa na kiwango bora dhidi ya Raja,hawakuwa bora kwenye eneo la kiungo eneo ambalo ni ubongo wa timu matokeo yake safu ya ulinzi ikawa inavuja, safu ya ushambuliaji ikakosa utulivu pia.

Baada ya hayo naamini mwalimu Robertinho ameyaona hayo na kuyafanyia kazi ndani ya muda mfupi,na leo dhidi ya Azam ana nafasi ya kuona kile alichokifanyia mazoezi.

Je,tutarajie Simba kulipa kisasi kwa Azam na kumalizia hasira zake za Raja,au Azam wataenda kutonesha kidonda?20230221_112834.jpg