UNAMFUNGIA CHAMA NA AZIZI KI MECHI 3 KISA?

JohBwax

Mgeni
Nov 4, 2022
84
72
5
"Unamfungia Chama, Aziz Ki mechi 3. Kisa? Walikwepa kuwapa mikono wapinzani. Na nasikia kanuni ipo kabisa. Tangu lini fair play ikawa lazima?. Upuuzi kwa waliotunga na kuzipokea. Kuna mambo ya umuhimu hatutekelezi tumeona wachezaji kupeana mikono ni muhimu,” Edokumwembe

"Napelekeshwa zaidi na mtumizi ya common sense kuliko kanuni au sheria. kwa mfano ile sheria ya PF3 kwamba unakaribia kua lakini manesi na madokta wanasema hawakutibu hauna PF3 kutoka polisi, Na tukirudi katika common sense kanuni inayomlazimisha mchezaji kumpa mwezake mkono.

Aishi manula anamuona Prince Dube Anapaka mafuta ya Nguruwe kabla ya mechi, atampa mkono? Na mgeni wa heshima ambaye jana kanitukana Baa kwanini nimpe mkono? Ndiomana wazungu wakaamua fair play isiwe lazima. Zaha hapigi magoti wakati issue hizi zakupiga magoti kabla ya match hazijaanza. Hakuna adhabu.

Ferdinanes waliogoma kumpa mkono John Terry. , hakuna adhabu Suarez aligoma kumpa mkono Evra Hakuna adhabu, Adhabu aliyopewa ilihusiana na masuala ya ubaguzi.

Inachekesha watu wanapodeal na kanuni ambazo zilitungwa huku nusu ya wajumbe wakivuta sigara nje. Na walizoikubali walikua busy na wakisubiri posho zao. katika soka la wanawake zipo? kuna dada zetu wa kiislamu wamefundishwa kutompa mkono mwanaume. Ni kama yule mama aliyekwepa kumpa mkono Uhuru
Kenyata.
Napenda kutumia common sense kuliko kanuni kwa sababu kanuni nyingi zinatungwa na watu wasiotumia common sense, hata huku dunia ya watu" "Edokumwembe" Anaandika Instagram.

1667917661589.png