USHUHUDA WA MDAU KUHUSU BIASHARA YA NFTS.

mhindi

Mgeni
Nov 29, 2021
17
6
5
Tanzania
Kwanza kabisa nianze na shukrani kubwa kwa walio ni follow mapokeo yamezidi matazamio followers 58 Hadi 1000+ in one night duu. ANGALIZO online business sijaanza mwaka huu hata wakati naanza kufanya biashara ya nft nilikuwa na experience ya biashara nyingine hapo nyuma na imenisaidia katika kazi zangu japo sio muhimu, kama affiliate marketing ambayo niliifanya 2016 kwa kuuza Viagra kama online pharmacy na wateja tulikuwa tuna watafuta katika yahoo answers na facebook groups, nilitumia laptop ya brother alivyokuwa akitoka likizo ya chuo kwa hiyo kulikuwa hakuna consistent.

Baada ya hapo nilianza biashara ya forex nikiwa chuo mnamo 2017 nilipenda sana hii biashara nimenunua signal Sana nimejaribu different bunch of strategy mpaka mwaka 2019 mwishoni ilinifanya nimshawishi mama angu akope 5,000,000/= kwenye kikundi vikoba ili tufanikiwe ila niliipoteza yote na kubakiwa na kama 1,200,000 na nikakata tamaa kabisa maana nilidaiwa marejesho na hela ikawa sina ikanifanya niondoke nyumbani na kwenda kutafuta maisha mbali sababu ya masimango, mnamo mwaka 2020 nilitafuta kazi kuanzia mwezi wa 3 na kuja kupata kazi mwezi wa kumi mwishoni so nikaanza kulipa na marejesho polepole lakini kila nikiangalia laptop yangu nilijua ipo siku nitapiga pesa za online.

So mwaka 2021 mwezi wa 2 nilikutana na trend za crypto gains nikawa nafatilia lakini sio kwa Sana ila nikakutana na post za celebrity wananunua picha za kijinga tu kwa mamilioni ya pesa hii project inaiitwa crypto Punk ndipo nilianza kufatilia kwa umakini nikafungua na Twitter account mnamo may 2021 na kuanza kuwa serious kujifunza na nikagundua hata wengi wanaofanya wengi wao ni beginners na they make a lot of money so nikanunua crypto Toka remitano ili kujaribu nikaanza na Dola 600 nikazituma kwenye wallet yangu ya metamask nimaarufu Sana ila huwezi amini kesho yake nilikuwa nafanya minting kwenye website ya scammers nikajikuta nimeibiwa hela zangu zote na wakaniachia Dolla 2 tu nilichanganyikiwa Sana kiasi cha kukata tamaa ila kila niikiingia TikTok naona mbona watu wnapiga hela ndo mwezi wa tisa mwishoni nikatoa hela zangu zote bank 3.86m nikanunua zote crypto kwenye remitano nikasema kama nikufeli basi bora nife maskini nikajifunza trick zote za kujilinda na mahackers pamoja na scammers maana hakuna maana kama Hauwezi kujaribu wakati unaona watu wanafanikiwa mbele ya macho yako ndipo safari yangu ilipoanzia.

Uzi huu uliandikwa na Dollar Musk kwenye ukurasa wake wa twitter hapa > https://twitter.com/nftsknowledge