Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa amekutana na wachezaji wa timu ya taifa ya wasichana chini ya umri wa miaka 20, Tanzanite kwa kufuzu Raundi ya Tatu ya kufuzu Kombe la Dunia mwakani.
Tanzanite imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 4-3 baada ya kushinda 3-2 katika mchezo wa kwanza Dar es Salaam kabla ya sare ya 1-1 Bujumbura Jumapili na sasa itamenyana na Ethiopia katika Raundi ya Tatu.
Tanzanite imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 4-3 baada ya kushinda 3-2 katika mchezo wa kwanza Dar es Salaam kabla ya sare ya 1-1 Bujumbura Jumapili na sasa itamenyana na Ethiopia katika Raundi ya Tatu.