Arsenal Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

ARSENAL YAPIGWA 2-1 PALE PALE EMIRATES​


WENYEJI, Arsenal wamechapwa 2-1 na Brighton & Hove Albion kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Emirates Jijini London.
Mabao ya Brighton leo yamefungwa na Leandro Trossard dakika ya 28 na kiungo Mzambia, Enock Mwepu dakika ya 66, wakati la Arsenal limefungwa na Martin Odegaard dakika ya 89.
Kwa ushindi huo, 37 katika mchezo wa 31 ikisogea nafasi ya 11, wakati Arsenal inabaki na pointi zake 54 za mechi 30 nafasi ya tano.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SOUTHAMPTON YAICHAPA ARSENAL 1-0 ST MARY’S​


BAO pekee la beki Jan Bednarek dakika ya 44, limewapa wenyeji, Southampton ushindi wa 1-0 dhidi ya Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa St. Mary's Stadium mjini Southampton, Hampshire.
Kwa ushindi huo, Southampton wanafikisha pointi 39 katika mchezo wa 32 na kusogea nafasi ya 12, wakati Arsenal inabaki na pointi zake 54 za mechi 31 sasa ikishukia nafasi ya sita na kuipisha Manchester United nafasi ya tano.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

ARSENAL YAIPIGA CHELSEA 4-2 PALE PALE DARAJAN​


TIMU ya Arsenal imeibuka na ushindi wa 4-2 dhidi ya wenyeji, Chelsea katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Jumatano Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Mabao ya Arsenal yamefungwa na Eddie Nketiah dakika ya 13 na 57, Emile Smith Rowe dakika ya 27 na Bukayo Saka dakika ya 90 na ushei kwa penalti, wakati ya Chelsea yamefungwa na Timo Werner dakika ya 17 na Nahodha wake, Cesar Azpilicueta dakika ya 32.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 57 katika mchezo wa 32 na kurejea nafasi ya tano, wakati Chelsea inabaki na pointi zake 62 za mechi 31 nafasi ya tatu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

ARSENAL YAICHAPA LEEDS UNITED 2-1 EMIRATES​



WENYEJI, Arsenal wameibuka na wa 2-1 dhidi ya Leeds United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Emirates Jijini London.
Mabao yote ya Arsenal yamefungwa na Eddie Nketiah dakika ya tano na ya 10, wakati la Leeds limefungwa na Diego Llorente dakika ya 66.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 66, ingawa inabaki nafasi ya nne, ikizidiwa pointi moja na Chelsea baada ya wote kucheza mechi 35, wakati Leeds inabaki na pointi zake 34 za mechi 35 pia nafasi ya 18.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SPURS YAICHAPA ARSENAL 3-0 LONDON​



WENYEJI, Tottenham Hotspur wameibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Alhamisi Uwanja wa Tottenham Hotspur Jijini London.
Mabao ya Spurs yamefungwa na Harry Kane mawili, dakika ya 22 kwa penalti na 37 akimalizia pasi ya Rodrigo Bentancur na lingine Son Heung-Min dakika ya 47.
Kwa ushindi huo, Spurs inafikisha pointi 65, ingawa inabaki nafasi ya tano, ikizidiwa pointi moja moja na Arsenal baada wa wote kucheza mechi 36.
Arsenal ilimaliza pungufu baada ya Rob Holding kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 33 kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano kwa kucheza rafu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

ARSENAL YACHAPWA 2-0 NA NEWCASTLE ST JAMES’ PARK​



WENYEJI, Newcastle United wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Jumatatu Uwanja wa Champions League bid in a buoyant 2-0 St James' Park, Newcastle upon Tyne.
Mabao ya Newcastle United yamefungwa na Ben White aliyejifunga dakika ya 55 na Bruno Guimarães dakika ya 85 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 46 katika mchezo wa 37 na kusogea nafasi ya 12.
Arsenal baada ya kipigo hicho wanabaki na pointi zao 66 za mechi 37 sasa nafasi ya tano, wakizidi kupoteza matumaini ya kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao.