Kombe la Shirikisho barani Afrika

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SIMBA NA GENDAMARIE KUCHEZWA SAA 4:00 USIKU​

B336935B-E95C-4214-8669-D2E426DEB728.jpeg

MCHEZO baina ya wenyeji, Simba SC na US Gendamarie ya Niger utachezwa muda mmoja na mchezo mwingine wa mwisho wa Kundi D Kombe la Shirikisho Afrika kati ya wenyeji, RSB Berkane na ASEC Mimosas Jumapili.
Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limeamua mechi zote zianze Saa 4:00 usiku ili kuondoa uwezekano wa upangwaji matokeo iwapo michezo hiyo itachezwa muda tofauti.
Wakati Simba watakuwa wenyeji wa US Gendamarie Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, ASEC watakuwa wageni wa Berkane Uwanja wa Manispaa ya Berkane nchini Morocco, Saa 4:00 usiku.
ASEC ndio inaongoza Kundi D kwa pointi zake tisa, ikifuatiwa na Berkane na Simba zenye pointi saba kila moja, wakati Gendamarie ina pointi tano, maana yake timu zote zinaweza kumaliza nafasi mbili za juu na kwenda Robo Fainali.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Beki Tegemeo wa Orlando Pirates Apata Ajali Mbaya, Akimbizwa Hospitalini​

batch_paseka.jpg

Beki wa Kushoto wa Klabu ya Orlando Pirates Paseka Mako amepelekwa hospitali baada ya kuumia uwanjani

BEKI wa Orlando Pirates, Paseka Mako alikimbizwa Hospitali kupewa huduma jana Aprili 12 baada ya kupata majeraha walipogongana na kipa Richard Ofori kwenye mchezo wa DStv Premiership dhidi ya Baroka FC uliochezwa Uwanja wa Peter Mokaba.
Ilikuwa ni kwenye muda wa nyongeza ambapo beki huyo aliweza kugongana na mchezaji mwenzake ambaye ni kipa Ofori aliyekuwa akitimiza majukumu yake kuweza kuhakikisha kwamba mpira haujazama kwenye nyavu zake.
59C21371-7967-407C-9AFB-F7A853AD41E0.jpeg

Wachezaji wa timu zote mbili wakiweka uzio ili kupisha kupatiwa matibabu kwa Paseka Mako
Imethibitishwa kwamba kwa sasa beki huyo anapambania afya yake baada ya kupata maumivu ya kichwa na haraka sana mwamuzi wa kati Masixole Bambiso ambaye alikuwa karibu kwenye mchezo huo aliwaita watu wa huduma ya kwanza.
Ofori naye aliweza kutazamwa na kupewa huduma ya kwanza na yote yalifanywa kwa haraka ili kuweza kuokoa maisha ya wachezaji hao waliokuwa wakitimiza majukumu yao.
Kutokana na jambo hilo wachezaji wa timu zote mbili Pirates na Baroka waliunda duara ili kuweza kumlinda mchezaji huyo wakati akipewa huduma ya kwanza kwenye mchezo huo uliokamilika kwa sare ya bila kufugana.
Orlando Pirates wanatarajiwa kucheza mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali dhidi ya Simba, Aprili 17, Uwanja wa Mkapa
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SIMBA SC YATANGULIZA KIFUA NUSU FAINALI SHIRIKISHO​



WENYEJI, Simba SC wametanguliza kifua Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Bao pekee la Simba inayofundishwa na kocha Mspaniola, Pablo Franco Martin limefungwa na beki mkongwe wa kulia, Shimari Salum Kapombe kwa penalti dakika ya 68.
Penalti hiyo ilitolewa na refa Mtunisia, Haythem Guirat aada ya winga Mghana, Bernard Morrison kwenye boksi.
Timu hizo zitarudiana Jumapili ijayo Uwanja wa Orlando Jijini Johannesburg.