Kuhusu Lameck Lawi Tuwaamini SIMBA au COASTAL UNION?

DeviMitupio

Mgeni
May 27, 2024
9
4
5
Baada ya utambulisho wa Lameck Lawi kama mchezaji mpya wa klabu ya Simba, Uongozi wa Coastal Union kupitia kwa Afisa Habari wake Abbas El Sabri umefunguka kwamba hautambui utambulisho huo na kubainisha kwamba hizo ni taarifa za kufurahisha na kuchekesha za mitandaoni.

“Siku hizi mitandaoni kuna mambo mengi sana wakati mwingine kuna mambo ya kufurahisha kuchekesha kwa hiyo ndio Dunia ya sasa ilivyo.”

“Hizo taarifa hata sisi ndio tunaziona mitandaoni lakini ukweli ni kwamba Lameck Lawi bado ni mali ya Coastal Union na ni mchezaji halali wa Coastal Union.”

“Mimi kama Afisa Habari wa Coastal Union nasema Lameck Lawi hajauzwa timu yoyote, ni Mali ya Coastal Union na bado tuna mipango naye.” — Abbas El Sabri

“Ilipokuja ofa tuliwapa taratibu za kufuatia na namna ya kufanya kama wanamuhitaji sasa sijui ni nini kimewafanya wasifanye vile sisi tunataka kwa hiyo na sisi baada ya kuona pengine hawana nia tena tukakaa na kuamua mengine.” — Abbas El Sabri
 

Simon Paul

Mgeni
May 7, 2024
14
12
5
Yani simba sijui tatizo lipo wapi ,,wanasajili wachezaji wa ndani wenye UWEZO wanakuja kukaa benchi na kuwaamini sana wachezaji wa kigeni wasio na UWEZO🙄🙄 kama kina JOBE 😂
 

Ibrahim kaila

Mpiga Chabo
May 27, 2024
1
0
0
Hii nchi ADMN ikifika wakat wa usajili hata ww utasikia umesajikiwa kumbe ni tetesi anyway SIMBA na lameck Lawi kwisha Lawi ni mshikaji aangu kanihakikishia sema alikuwa kapata dili nje ndio coastal wanataka badilisha utaratibu
IT'S OVER
 

Sir tenge

Mgeni
Jun 5, 2024
11
4
5
Inawezekana pia Simba wamemsajiri mchezaji kupitia wakala wake badala ya kufata taratibu,so wamemalizana na wakala wanajua wakala atamalizana na mchezaji pamoja na club.
 

Rhino

Mgeni
May 8, 2024
10
1
5
Yani simba sijui tatizo lipo wapi ,,wanasajili wachezaji wa ndani wenye UWEZO wanakuja kukaa benchi na kuwaamini sana wachezaji wa kigeni wasio na UWEZO🙄🙄 kama kina

Yani simba sijui tatizo lipo wapi ,,wanasajili wachezaji wa ndani wenye UWEZO wanakuja kukaa benchi na kuwaamini sana wachezaji wa kigeni wasio na UWEZO🙄🙄 kama kina JOBE 😂
Yah kama hawawatumii wawaache huko Wapakoneta namba kuliko kupoteza vipaji