Liverpool Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

LIVERPOOL YAITANDIKA MAN UNITED 4-0 ANFIELD​


WENYEJI, Liverpool wamewatandika mahasimu, Manchester United mabao 4-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Jumanne Uwanja wa Anfield.
Mabao ya Liverpool yamefungwa na Luis Diaz dakika ya tano, Mohamed Salah mawili, dakika ya 22 na 85 na Sadio Mane dakika ya 68.
Liverpool inafikisha pointi 76 katika mchezo wa 32 na kupanda kileleni, ikiizidi pointi mbili Manchester City ambayo ina mechi moja mkononi na leo inacheza na Brighton & Hove Albion, wakati Man United inabaki na pointi zake 54 za mechi 33 sasa nafasi ya sita.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

LIVERPOOL YAICHAPA EVERTON 2-0 ANFIELD​


WENYEJI, Liverpool wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya mahasimu, Everton katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Anfield, Liverpool.
Mabao ya Liverpool yamefungwa na Andrew ‘Andy’ Robertson dakika ya 62 na Divock Origi dakika ya 85 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 79, ingawa wanabaki nafasi ya pili wakizidiwa pointi moja na Manchester City baada ya wote kucheza mechi 33.
Everton baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 29 za mechi 32 sasa nafasi ya 18 kwenye ligi ya timu 20, ambayo mwisho wa msimu tatu zitashuka.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

LIVERPOOL YAICHAPA VILLARREAL 2-0 ANFIELD​


WENYEJI, Liverpool wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Villarreal ya Hispania katika mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa Jumatano Uwanja wa Anfield, Liverpool.
Bao kwanza la Liverpool beki wa Kimataifa wa Ecuador, Pervis Josué Estupiñán Tenorio alijifunga dakika ya 53 akijaribu kuokoa krosi ya Jordan Henderson.
Na la pili lilifungwa na mshambuliaji wa Senegal, Sadio Mané dakika mbili tu baadaye akimalizia pasi ya nyota wa Misri, Mohamed Salah na sasa timu hizo zitarudiana Mei 3 Uwanja wa De la Cerámica mjini Villarreal.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

LIVERPOOL YAICHAPA SOUTHAMPTON 2-1 ST MARY’S​



TIMU ya Liverpool imetoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya wenyeji, Southampton katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa St Mary's .
Southampton walitangulia na bao la Nathan Redmond dakika ya the 13, kabla ya Liverpool kuzinduka kwa mabao ya Takumi Minamino dakika ya 27 na Joel Matip dakika ya 67.
Kwa ushindi huo, Liverpool inafikisha pointi 89, ingawa inaendelea kushika nafasi ya pili nyuma ya Manchester City wenye pointi moja zaidi baada ya wote kucheza mechi 37.
Southampton yenyewe inabaki na pointi zake 40 za mechi 37 nafasi ya 15.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Liverpool ni timu pekee ambayo haijapoteza mechi yoyote ya EPL
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿
ndani ya mwaka huu 2022.
🏟
Mechi: 18
✅
Kushinda: 15
👏
Sare: 3
280853313_5356332144426692_5087505750490972826_n.jpg
 

Brenda

Mgeni
Oct 31, 2022
489
403
5
Dar es salaam
1667373574861.png
Liverpool waliibuka na ushinda wa mabao 2 kwa 0 dhidi ya wapinzani wao Napoli \

Liverpool wameonekana kuwa bora sana kwenye michuno ya UCL zaidi ya Ligi za ndani, sikuizi imekuwa ni ngumu sana kuwaelewa Liverpool ni kama wamepotea lakini wamo.