Premier League: Uzi maalumu wa matokeo, msimamo wa ligi, wafungaji n.k

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
FULL TIME
Liverpool 3 - 1 Norwich
Arsenal 2 - 1 Brentford
Crystal Palace 0 - 1 Chelsea
Aston Villa 0 - 1 Watford
Brighton 0 - 3 Burnley
Southampton 2 - 0 Everton
274346054_5119457628114146_3219734873329422616_n.jpg
274246073_5119457624780813_5297458238845695795_n.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Wachezaji wa Everton na Boreham Wood hapo jana walivaa fulana maalumu zenye ujumbe uliosomeka "We Stand With Ukraine (Tunasimama na Ukraine)" wakati timu hizo zilipokutana kwenye mchezo wa Kombe la FA kama ishara ya kupinga shambulio linaloendelea huko Ukraine
🇺🇦

Mchezo huo ulimalizika kwa Everton kuondoka na ushindi wa mabao 2-0
275193553_5155913524468556_7553559839808011170_n.jpg
275240546_5155913521135223_3003302460567612776_n.jpg
275144890_5155913517801890_602238161916439739_n.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
FULL TIME
Aston Villa 4-0 Southampton
Burnley 0-4 Chelsea
Newcastle 2-1 Brighton
Norwich 1-3 Brentford
Wolves 0-2 Crystal Palace
Mikeka inasemaje?
😅

275265535_5160025540724021_8576448324424698296_n.jpg
275265523_5160025544057354_6476964885652480699_n.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Keane abadili mkeka, asema Arsenal Top 4​

Keane PIC

LONDON ENGLAND. ROY Keane ameamua kubadilisha utabiri wake wa Top Four na kusema sasa Arsenal itaibwaga Manchester United kwenye mbio za kukamatia tiketi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Manchester City, Liverpool na Chelsea zikiwa zimejiweka pazuri kwenye nafasi tatu za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu England, nafasi moja iliyobaki kwenye kutoa tiketi hiyo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya inashindanisha timu za Arsenal, Man United na Tottenham.

Man United ilionekana ipo pazuri wakati iliposhinda 4-2 dhidi ya Leeds United, lakini matokeo ya hovyo yalifuatia ikiwamo sare na Watford kisha kichapo cha Manchester City kimevuruga kabisa mipango na kuporomoka hadi kwenye nafasi ya tano, huku Arsenal wakishinda mechi yao ya Watford mabao 3-2 juzi Jumapili. Arsenal yenyewe imeshinda mechi tatu mfululizo.

Keane aliamini kwamba Man United itafuzu kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao baada ya ushindi ule wa Elland Road, lakini sasa amebadili utabiri wake, akisema: “Nadhani Man United kushika namna nne itakuwa nzuri kwao. Kumekuwa na kelele nyingi za wachezaji kutaka kuondoka, mikataba yao ikiwa dhida kama Pogba na Jesse Lingard. Mtazamo wa Man United kwa miezi michache ijayo ni kujaribu kuikamatia nafasi nne.

“Wana mechi ngumu ya Ulaya inafuata, wanapaswa kujikusanya na kuwekeza akili kwenye hilo jambo, watakuwa sawa.”

Hata hivyo, kiungo huyo wa zamani wa Man United amebadili mawazo, akisema Arsenal wana nafasi kubwa ya kumaliza Top Four. Keane alikoshwa na ushindi wa Arsenal dhidi ya Wolves uwanjani Emirates na kusema Arsenal ya sasa si timu laini tena.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Fulham Yafanikiwa Kupanda Daraja, Sasa Kucheza Ligi Kuu ya Uingereza Msimu Ujao​


batch_skysports-aleksandar-mitrovic_5744654.jpg

Mshambuliaji wa klabu ya Fulham Aleksandar Mitrovic amefunga jumla ya mabao 40
KLABU ya Fulham yenye makao yake jijini London katika Uwanja wa Craven Cottage imefanikiwa kupanda daraja na kushiriki Ligi Kuu ya Uingereza EPL msimu ujao wa 2022/2023.
Klabu hiyo imefanikiwa kupanda daraja mara baada ya jana kuifunga klabu ya Preston kwa jumla ya mabao 3-0 ambapo mabao mawili yalifungwa na mshambuliaji raia wa Serbia Aleksandar Mitrovic aliyefunga mabao mawili huku bao jingine likifungwa na Fabio Carvalho raia wa Ureno ambaye msimu ujao atajiunga na Liverpool.
Katika harakati za kupanda daraja Fulham imefanikiwa kushinda michezo 26 kutoka sare michezo 8 na kupoteza michezo 8 huku klabu hiyo ikifikisha jumla ya pointi 98.

skysports-fulham-fc_5744644.jpg

Mashabiki wa Fulham wakifurahi klabu yao kurejea Ligi Kuu nchini Uingereza
Kwa upande mwingine mshambuliaji hatari na tegemezi wa klabu hiyo Aleksandar Mitrovic amefikisha jumla ya mabao 40 ikiwa ni mabao mawili nyuma ya rekodi iliyowekwa na Guy Whittingham akiwa na Portsmouth kwenye msimu wa 1992-1993 alipofunga jumla ya mabao 42.
Naye kocha wa Fulham Marco Silva amesema klabu hiyo ilistahili kupanda daraja na kwamba ilikuwa na kila sababu ya kujivunia mafanikio iliyopata.