Shaffih Dauda vs Zaka Zakazi Nani Yuko Sahihi?

Kijiweni

Administrator
Staff member
Nov 7, 2022
278
395
25
Wakati ligi kuu ikiwa inakaribia kumalizika kuna mengi ambayo yanazungumzwa haswa kugombea nafasi ya pili kati ya Azam vs Simba tutazame hiki walichokiandika Shaffih Dauda na kile ambacho amekisema Zaka Zakazi kisha tujadiliane hapa

SHAFFIH DAUDA KAANDIKA:

"Niliposema watu/kampuni nyingi zinatamani Simba imalize nafasi ya pili juu ya Azam FC ili ishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika, sikuwa najizungumzia mimi kwamba ndio mnufaika pekee kibiashara bali kuna watu/kampuni/taasisi nyingi zitanufaika na Simba kwa sababu ya fan base yake kuliko Azam FC.

Ukifanya utafiti mdogo kwenye hizi kampuni za TV [Azam TV, DStv, StarTimes] ambazo zinanunua haki za matangazo kuonesha mashindano ya Afrika, ukiuliza kati ya Simba na Azam wangetamani timu gani imalize Ligi katika nafasi ya pili hakuna hata kampuni moja ya TV itakwambia Azam FC!

Kwa nini? Kwa sababu Azam ikimaliza nafasi ya pili na kufuzu kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika ni watu wangapi watalipia ving’amuzi vyao kutazama mechi ya Azam FC vs Petro de Luanda? Lakini vipi kwa Simba?

Kwa sababu hizohizo za kibiashara, hata Azam TV wanatamani sana Simba imalize Ligi ikiwa nafasi ya pili juu ya Azam FC kwa sababu wanajua itawalipa kwenye biashara yao na watapiga mpunga zaidi kupitia subscriptions ya ving’amuzi kuliko timu yao ikifuzu kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika.

Bila shaka hata Simba ilipoifunga Azam FC [Azam 0-3 Simba], watu wa Azam TV walifurahi sana wakijua mbio za kuwania nafasi ya pili zimekwisha! Wakiamini biashara yao itachangamka ikifika msimu mpya wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Ni kitu kizuri na kikubwa kwa Azam FC kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika kwa sababu ya kujitambulisha na kuweka alama kwenye soka la Afrika kama klabu lakini kibiashara hawauzi sokoni ukilinganisha na Simba."

ZAKA ZAKAZI ANASEMA:
"

SABABU 99 ZA KUKWAMA KWA AZAM FC

Huyu ni Shaffih Dauda, mchanbuzi nguli kabisa wa michezo, hasa mpira, hapa nchini.

Na hapa anaelezea matamanio yake kuelekea kumalizika kwa msimu.

Anasema angefurahi Simba kushika nafasi ya pili kwa sababu za kibiashara.

Naam, ukiacha uchambuzi, Shaffih ni mfanyabiashara mzuri sana wa mpira kupitia wachezaji. Na kama kuna watu ambao Tanzania inatakiwa kuwapa heshima kubwa, basi ni Shaffih.

Ana “connection” kubwa sana na mpira wa dunia…yeye ndiye aliyempeleka Ulaya Novatus Dismass, kutoka Azam FC.

Yeye ndiye aliyempeleka Marekani Cyprian Kachwele kutoka Azam FC.

Hapa Shaffih alifanya biashara kubwa sana. Na biashara hii aliifanya na Azam FC, siyo Simba…na hajawahi kufanya biashara kubwa kama hii na Simba.

Mtu mwingine angetegemea kumsikia Shaffih akisema kwamba kwa maendeleo ya mpira, Azam FC ingepaswa kushika nafasi ya pili, ili ipate nguvu zaidi ya kuzalisha akina Kachwele na yeye afanye biashara zaidi…lakini siyo hivyo.

Shaffih anaombea Simba iliyozuia biashara yake ya Ladaki Chasambi, ndiyo iwe ya pili, ili biashara ifanyike!

Na hii ni nafasi ya pili, hapo bado ubingwa. Unadhani hizo mbio za nafasi ya pili ndiyo zingekuwa za ubingwa…ingekuwaje?

Mimi nimpongeze sana kwa kuwa muwazi kwa sababu kuna wengine wengi sana wanawaza kama yeye lakini hawajatoka hadharani na kusema.

Miongoni mwao kuna wachambuzi kama yeye, kuna wafanyabiashara kama yeye, kuna wanasiasa, kuna wafanya maamuzi, wachungaji na mashehe na kadhalika.

Na kila mmoja katika hao ana sababu zake kwanini Azam FC haistahili kuwa ya pili…achilia mbali ubingwa.

Sababu hizi jumla zinakuwa 99 na kuyafanya maisha ya Azam FC kuwa magumu sana…halafu mwisho wa siku hawa hawa wanakuja kuuliza, Azam FC inakwama wap?

1. Sababu za kibiashara kama Shaffih
2. Sababu za kisiasa
3. Sababu za kidiplomasia
4. Sababu za kiuchumi
5. Sababu za kimazingira
6. Sababu za kijiografia
7. Sababu za kihistoria
8. Sababu za kiintelijensia
9. Sababu za kiusalama
10. Sababu za kiimani
11. Sababu za kimahusiano
12. Sababu za kiitikadi
13. Sababu za kimazoea
14. Sababu za kimataifa
15. Sababu za kiroho
16. Sababu kimiundombinu
17. Sababu zilizo nje ya uwezo
18. Sababu za kimbunga Hid

Wewe Maoni Yako Ni Yapi? Tujadiliane Hapa
 
May 22, 2024
2
1
5
Kiushindani Azam bado maana amepata nafasi mara kadhaa ila ametuangusha watanzania maana wanacheza as if hawana cha kupoteza yaaani lonyo lonyo sana kama mlandege vile au kvz...
 
  • Like
Reactions: Kijiweni

Abdulrahim

Mgeni
May 11, 2024
4
4
5
Anachokisema Shafii dauda ni Sahihi..linapokuja suala la Mashindano ya kimataifa Azam wamekuwa wanyonge sana na ndio maana wafanyabiashara wa mpira wanaomba simba aende klabu bingwa ..lakini Sasa Azam inabidi ajipambanue msimu amalize nafasi ya pili, Kisha akatoe ushindani klabu bingwa na kufanya vizur hapo anaweza akawaaminisha watanzania kwamba Azam fc sio wanyonge kwenye Mashindano ya kimataifa
 
  • Like
Reactions: Kijiweni

Mkuda konki

Mgeni
May 2, 2024
3
2
5
Shaffih kaongea ukweli na zakazakazi katetea brand ya klabu yake lakini Azam kumaliza ikiwa nafasi ya pili no ngumu sana labda waweke undugu pembeni dhidi ya Simba SC kitu ambacho shaffih ameshindwa kukiweka wazi
 
  • Like
Reactions: Kijiweni

Tyseem

Mgeni
May 22, 2024
5
3
5
Azam sio kam hawezi kushika nafasi ya pili n kucheza ligi y mabigwa tatiz kubwa la azam ni kwny fan base ambapo hawana watu w kuwalaumu kw chochote,hii kitu inapelekea wachezaj n viongoz kuona saw kweny kla wanachokipata sababu hawapat presha yyte ktka kw mashabiki.for me it's time azam aanze kuchez klabu bigwa kutengeneza fan base kam ya simba na yanga na anastahili nafas ya pili.
 
  • Like
Reactions: Kijiweni

KBE

Mgeni
May 2, 2024
2
2
5
Mimi naamin mabadiliko ya mpira yanakuja pale tu vilabu vyengine vinapopata nafasi ya kushiriki mashindano makubwa tofauti na yale mazoea ya kuwa kila siku kuna timu fulani ndio zinashiriki, hata Azam FC inaweza kupata ñafasi ya kuwa na mashabiki wengi kibiashara kama vile simba na yanga ikiwa utaekeza vizur kwenye wachezaji wazur na motishani.
 
  • Like
Reactions: Kijiweni
May 22, 2024
3
2
5
Wanakijiweni kwangu mimi wote wawili shaffii dauda na zakazakazi wote nawaunga mkono kwamaana Kila mmoja maoni yake yanamaana na umuhimu lakini tukumbuke hata simba na Yanga ni kwakipindi gani wamekua wakishiriki michuano ya kimataifa na walikua hawafiki mahali mpaka pale ambapo simba alipojikwamua kwakuwekeza ndio akaanza kufika robo fainali mwaka jana Yanga akacheza fainali ya kombe la shirikisho na mwaka kafika robo fainali champions league jambo ambalo watu kama akina Dauda na wachambuzi wengine wangetumia nafasi yakushauri kwamba kama Azam mmefanikiwa kwenda champions league basi wawekeze kwenye aicha ya wachezaji ambao wanaweza kutoa ushindani nasio kuongea kwakujali maslahi sitashangaa kuona Azam anapoteza mechi maksudi kwaajili yakuipa simba nafasi kwakigezo Cha kibiashara
 
  • Like
Reactions: Kijiweni
May 22, 2024
10
6
5
Kama walijua mambo kama haya yatatokea wana simba kwanini hawakukaza ili wamalize hata nafasi ya kwanza, unajua simba ni kama Arsenal mtu ana nafasi alf akiipoteza kwa makosa ya mechi mbili anaanza kuombea njaa wenzie kitu ambacho kwa mabingwa ni aibuu. Alaf sasa hiv mpira umekua sana kwa Tanzania hvyo kila anaediserve kwenda kimataifa aendee sababu ni nguvu zakee mwenyewee sababu sio kitototo mapaka kufika hapo. Ukiweka biashara mbele kulko mafanikio ya mpira basi robo fainal kwa team za Tanzania itakua ni our fina destination. Mm kwa upande wangu bora Azam Fc aende ili simba wajue kuwa kama wakiboronga tena msimu ujao hawaendi na hvyo ndo soccer linakua
 
  • Like
Reactions: Kijiweni

Mr Clarpchar

Mgeni
May 22, 2024
1
1
5
Wakati ligi kuu ikiwa inakaribia kumalizika kuna mengi ambayo yanazungumzwa haswa kugombea nafasi ya pili kati ya Azam vs Simba tutazame hiki walichokiandika Shaffih Dauda na kile ambacho amekisema Zaka Zakazi kisha tujadiliane hapa

SHAFFIH DAUDA KAANDIKA:
"Niliposema watu/kampuni nyingi zinatamani Simba imalize nafasi ya pili juu ya Azam FC ili ishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika, sikuwa najizungumzia mimi kwamba ndio mnufaika pekee kibiashara bali kuna watu/kampuni/taasisi nyingi zitanufaika na Simba kwa sababu ya fan base yake kuliko Azam FC.

Ukifanya utafiti mdogo kwenye hizi kampuni za TV [Azam TV, DStv, StarTimes] ambazo zinanunua haki za matangazo kuonesha mashindano ya Afrika, ukiuliza kati ya Simba na Azam wangetamani timu gani imalize Ligi katika nafasi ya pili hakuna hata kampuni moja ya TV itakwambia Azam FC!

Kwa nini? Kwa sababu Azam ikimaliza nafasi ya pili na kufuzu kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika ni watu wangapi watalipia ving’amuzi vyao kutazama mechi ya Azam FC vs Petro de Luanda? Lakini vipi kwa Simba?

Kwa sababu hizohizo za kibiashara, hata Azam TV wanatamani sana Simba imalize Ligi ikiwa nafasi ya pili juu ya Azam FC kwa sababu wanajua itawalipa kwenye biashara yao na watapiga mpunga zaidi kupitia subscriptions ya ving’amuzi kuliko timu yao ikifuzu kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika.

Bila shaka hata Simba ilipoifunga Azam FC [Azam 0-3 Simba], watu wa Azam TV walifurahi sana wakijua mbio za kuwania nafasi ya pili zimekwisha! Wakiamini biashara yao itachangamka ikifika msimu mpya wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Ni kitu kizuri na kikubwa kwa Azam FC kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika kwa sababu ya kujitambulisha na kuweka alama kwenye soka la Afrika kama klabu lakini kibiashara hawauzi sokoni ukilinganisha na Simba."

ZAKA ZAKAZI ANASEMA:
"
SABABU 99 ZA KUKWAMA KWA AZAM FC

Huyu ni Shaffih Dauda, mchanbuzi nguli kabisa wa michezo, hasa mpira, hapa nchini.

Na hapa anaelezea matamanio yake kuelekea kumalizika kwa msimu.

Anasema angefurahi Simba kushika nafasi ya pili kwa sababu za kibiashara.

Naam, ukiacha uchambuzi, Shaffih ni mfanyabiashara mzuri sana wa mpira kupitia wachezaji. Na kama kuna watu ambao Tanzania inatakiwa kuwapa heshima kubwa, basi ni Shaffih.

Ana “connection” kubwa sana na mpira wa dunia…yeye ndiye aliyempeleka Ulaya Novatus Dismass, kutoka Azam FC.

Yeye ndiye aliyempeleka Marekani Cyprian Kachwele kutoka Azam FC.

Hapa Shaffih alifanya biashara kubwa sana. Na biashara hii aliifanya na Azam FC, siyo Simba…na hajawahi kufanya biashara kubwa kama hii na Simba.

Mtu mwingine angetegemea kumsikia Shaffih akisema kwamba kwa maendeleo ya mpira, Azam FC ingepaswa kushika nafasi ya pili, ili ipate nguvu zaidi ya kuzalisha akina Kachwele na yeye afanye biashara zaidi…lakini siyo hivyo.

Shaffih anaombea Simba iliyozuia biashara yake ya Ladaki Chasambi, ndiyo iwe ya pili, ili biashara ifanyike!

Na hii ni nafasi ya pili, hapo bado ubingwa. Unadhani hizo mbio za nafasi ya pili ndiyo zingekuwa za ubingwa…ingekuwaje?

Mimi nimpongeze sana kwa kuwa muwazi kwa sababu kuna wengine wengi sana wanawaza kama yeye lakini hawajatoka hadharani na kusema.

Miongoni mwao kuna wachambuzi kama yeye, kuna wafanyabiashara kama yeye, kuna wanasiasa, kuna wafanya maamuzi, wachungaji na mashehe na kadhalika.

Na kila mmoja katika hao ana sababu zake kwanini Azam FC haistahili kuwa ya pili…achilia mbali ubingwa.

Sababu hizi jumla zinakuwa 99 na kuyafanya maisha ya Azam FC kuwa magumu sana…halafu mwisho wa siku hawa hawa wanakuja kuuliza, Azam FC inakwama wap?

1. Sababu za kibiashara kama Shaffih
2. Sababu za kisiasa
3. Sababu za kidiplomasia
4. Sababu za kiuchumi
5. Sababu za kimazingira
6. Sababu za kijiografia
7. Sababu za kihistoria
8. Sababu za kiintelijensia
9. Sababu za kiusalama
10. Sababu za kiimani
11. Sababu za kimahusiano
12. Sababu za kiitikadi
13. Sababu za kimazoea
14. Sababu za kimataifa
15. Sababu za kiroho
16. Sababu kimiundombinu
17. Sababu zilizo nje ya uwezo
18. Sababu za kimbunga Hid

Wewe Maoni Yako Ni Yapi? Tujadiliane Hapa
Mimi ni Simba Damu Damu ila Huwa Natamani Azam fc nayo iwe kubwa Na kucheza klabu bingwa but kuna Vitu Huwa Sivielewi Sana kwa Azam,, maana Kwa Wachezaji wanaowazuri sana ila Sijajua shida uongozi au Tajiri ndio shida au Kocha au Ushabiki wa Uyanga na Usimba 🤔🤔,, Azam inauwezo wa kumsajili Mchezaji yoyote yule ila Ukubwa ndio unakwamisha Mtu kukubali Moja Moja kwa Moja Moja
 
  • Like
Reactions: Kijiweni