Uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera umezidi kuwa mchungu kwa mnyama Simba baada ya kuambulia sare ya 1-1 dhidi ya wenyeji wao Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC.
Simba ilifungwa 1-0 mara ya mwisho walipocheza na wakataka miwa hao bao pekee la Kagera likifungwa na Hamis Kiiza ( Diego).
Katika mchezo wa leo,
Deus Bukenya ndiye aliyeanza kuitanguliza Kagera Sugar katika dakika ya 15.
Lakini baadae beki Henock Inonga akafanikiwa kuisawazishia Simba katika dakika ya 39.
Matokeo hayo yanaifanya Simba SC iwe imetoka sare mara 5 msimu huu na inafikisha alama 38 ikiwa nafasi ya pili.
Inazidiwa pointi 6 na Yanga ambao wanaongoza ligi.
Kagera Sugar imekwea mpaka nafasi ya 6 alama 23 baada ya mechi 17.
Katika mechi nyingine , Tz Prisons imeshinda 2-0 dhidi ya Dodoma Jiji.
Geita Gold pia imetoka sare ya 1-1 na Azam FC.
Kwa matokeo hayo, Azam imesalia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 37 katika mechi 17.
Simba ilifungwa 1-0 mara ya mwisho walipocheza na wakataka miwa hao bao pekee la Kagera likifungwa na Hamis Kiiza ( Diego).
Katika mchezo wa leo,
Deus Bukenya ndiye aliyeanza kuitanguliza Kagera Sugar katika dakika ya 15.
Lakini baadae beki Henock Inonga akafanikiwa kuisawazishia Simba katika dakika ya 39.
Matokeo hayo yanaifanya Simba SC iwe imetoka sare mara 5 msimu huu na inafikisha alama 38 ikiwa nafasi ya pili.
Inazidiwa pointi 6 na Yanga ambao wanaongoza ligi.
Kagera Sugar imekwea mpaka nafasi ya 6 alama 23 baada ya mechi 17.
Katika mechi nyingine , Tz Prisons imeshinda 2-0 dhidi ya Dodoma Jiji.
Geita Gold pia imetoka sare ya 1-1 na Azam FC.
Kwa matokeo hayo, Azam imesalia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 37 katika mechi 17.