Tetesi Zote Za USAJILI Hizi Hapa

Kijiweni

Administrator
Staff member
Nov 7, 2022
281
396
25
⛳Wazir Jr bado hajasaini mkataba na Singida Black Stars. Ofa yao ya mkataba wa miaka miwili na masuala binafsi yalikubaliwa.Kinachosubiriwa ni pesa iingie kwenye akaunti yake.

⛳Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga, Ali Kamwe amethibitisha kuwa wataanza maboresho ya Kikosi chao cha msimu unaokuja ikifika mwezi July mwaka huu. Kamwe amefunguka kuwa Nani atabaki au kuondoka mitaa ya Jangwani itafahamika kuanzia tarehe 01/07/2024.

⛳Simba SC imeachana na kiungo wake mshambuliaji Luis Miquessone raia wa Msumbiji kwa kumpa THANK YOU.Simba SC imeachana na nyota huyo aliyeshindwa kufanya vyema tangu ajiunge na kikosi hicho msimu uliopita akitokea Al Ahly.

⛳Mabosi wa Azam FC wamekamilisha dili la kumbakiza nyanda, Mohammed Mustafa, Inaelezwa kuwa tayari amesaini kandarasi ya miaka miwili (2) kilichobaki ni biashara baina ya Klabu-Klabu.

⛳Klabu ya Tanzania Prisons imemuongezea mkataba wa miaka miwili golikipa wake Yona Amos

⛳Simba SC wameendelea kuisuka upya timu yao kwa kuachana na mshambuliaji Shaban Chilunda kwa kumpa THANK YOU. Nyota huyo aliyetolewa mkopo na Simba SC kwenda KMC hatokuwa sehemu ya kikosi cha Simba SC kwa msimu ujao.

⛳Ismail Mgunda amejiunga na Mashujaa Kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea Singida Black Stars. Mgunda alijiunga na Singida Black Stars zamani Ihefu fc akitokea Tanzania Prisons mwaka Jana mwezi July.

⛳Mlinzi tegemeo wa klabu ya Simba SC Tanzania Che Fondoh Malone aanzisha mtifuano akifosi aondoke kuwa hana furaha Utata umeongezeka baada ya Future ya Misri kuonyesha nia ya kumtaka beki huyo aliyejiunga na Simba msimu uliyopita. Viongozi hawatak kumuuza kwani inshu ya Henock nayo imekaa vibaya.

⛳Klabu ya pambajijifootballclub yenye masikani yake jijini Mwanza imetangaza kumalizika kwa mikataba ya waliokuwa viongozi wa Benchi la ufundi na wachezaji wake waliofanikisha kuipandisha timu hiyo ligi kuu ya NBC.

⛳Coastal Union yaachana na mchezaji wake Roland Beakou

⛳Klabu ya Simba ipo kwenye mazungumzo na beki wa kushoto wa timu ya taifa ya Burkina Faso na FC Saint Eloi Lupopo ya DR Congo, Valentin Nouma kwa ajili ya kuipata huduma yake.

⛳Coastal Union iko kwenye mazungumzo na beki wa zamani wa Yanga, Djuma Shaaban. Mkongomani huyo amekuwa nje ya uwanja kwa msimu mzima bila ya kuwa na timu baada ya kuachana na Yanga aliyoitumikia kwa misimu miwili 2021-2022 na 2022-2023.

⛳Klabu ya Ken Gold FC iko katika mazungumzo ya kumsajili kiungo wa zamani wa Lipuli, Mbeya Kwanza, Polisi Tanzania na Dodoma Jiji FC, Jimmy Shoji Mwaisondola.

⛳Klabu ya Coastal Union iko katika mazungumzo na beki mzoefu Kelvin Yondani ili akajiunge na wagosi hao ili kuziba nafasi ya Lameck Lawi anayetajwa kutua Simba msimu ujao

⛳Vilabu ya Dodoma Jiji FC, Mashujaa FC na JKT Tanzania vinapigana vikumbo kuinasa saini ya kiungo Nassoro Kapama aliyemaliza mkataba wake na Mtibwa Sugar iliyoshuka daraja.

⛳Klabu ya Ken Gold FC iko katika mazungumzo na makocha wawili raia wa Uganda, Abdallah Mubiru na Matthias Lule ili kupata saini ya mmoja kuja kufundisha katika msimu ujao wa ligi kuu NBC Tanzania.

⛳Dodoma Jiji FC imemtambulisha rasmi kocha Mecky Maxime kama ilivyoripotiwa katika ukurasa huu

⛳Kocha wa Namungo FC, Mwinyi Zahera anaangalia uwezekano wa kumsajili kiungo mshambuliaji Ibrahim Ajibu aliyemaliza mkataba wake na Coastal Union ya Tanga

⛳Kocha wa Kagera Sugar Fred Felix Minziro amewaagiza viongozi wake kumrudisha mshambuliaji wao wa zamani Yusuph Mhilu baada ya klabu yake ya Geita Gold FC kushuka daraja

Mtaa Unaongea
 

Esther

Mgeni
Jun 20, 2024
1
1
5
Huenda wachezaji wa simba hawana Raha kwa sababu ya management iliyopo wanashindwa kufanya vizuri kwa sababu hawazingatiwi kabisa. Simba ya sasa hivi sio kama simba ya zamani
 
  • Like
Reactions: Godfrey ngoda

Isdory

Mgeni
Jun 20, 2024
1
1
5
Dah kuhsu pamaba jiji inauma Sana huwezi pandisha timu then una achana na watu waloipandisha kwa sahabu waloipandisha ndo Wana uchungu na timu brooo
 
  • Like
Reactions: JeffBunKauga

Nasma mrisho

Mpiga Chabo
Jun 20, 2024
2
0
0
⛳Wazir Jr bado hajasaini mkataba na Singida Black Stars. Ofa yao ya mkataba wa miaka miwili na masuala binafsi yalikubaliwa.Kinachosubiriwa ni pesa iingie kwenye akaunti yake.

⛳Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga, Ali Kamwe amethibitisha kuwa wataanza maboresho ya Kikosi chao cha msimu unaokuja ikifika mwezi July mwaka huu. Kamwe amefunguka kuwa Nani atabaki au kuondoka mitaa ya Jangwani itafahamika kuanzia tarehe 01/07/2024.

⛳Simba SC imeachana na kiungo wake mshambuliaji Luis Miquessone raia wa Msumbiji kwa kumpa THANK YOU.Simba SC imeachana na nyota huyo aliyeshindwa kufanya vyema tangu ajiunge na kikosi hicho msimu uliopita akitokea Al Ahly.

⛳Mabosi wa Azam FC wamekamilisha dili la kumbakiza nyanda, Mohammed Mustafa, Inaelezwa kuwa tayari amesaini kandarasi ya miaka miwili (2) kilichobaki ni biashara baina ya Klabu-Klabu.

⛳Klabu ya Tanzania Prisons imemuongezea mkataba wa miaka miwili golikipa wake Yona Amos

⛳Simba SC wameendelea kuisuka upya timu yao kwa kuachana na mshambuliaji Shaban Chilunda kwa kumpa THANK YOU. Nyota huyo aliyetolewa mkopo na Simba SC kwenda KMC hatokuwa sehemu ya kikosi cha Simba SC kwa msimu ujao.

⛳Ismail Mgunda amejiunga na Mashujaa Kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea Singida Black Stars. Mgunda alijiunga na Singida Black Stars zamani Ihefu fc akitokea Tanzania Prisons mwaka Jana mwezi July.

⛳Mlinzi tegemeo wa klabu ya Simba SC Tanzania Che Fondoh Malone aanzisha mtifuano akifosi aondoke kuwa hana furaha Utata umeongezeka baada ya Future ya Misri kuonyesha nia ya kumtaka beki huyo aliyejiunga na Simba msimu uliyopita. Viongozi hawatak kumuuza kwani inshu ya Henock nayo imekaa vibaya.

⛳Klabu ya pambajijifootballclub yenye masikani yake jijini Mwanza imetangaza kumalizika kwa mikataba ya waliokuwa viongozi wa Benchi la ufundi na wachezaji wake waliofanikisha kuipandisha timu hiyo ligi kuu ya NBC.

⛳Coastal Union yaachana na mchezaji wake Roland Beakou

⛳Klabu ya Simba ipo kwenye mazungumzo na beki wa kushoto wa timu ya taifa ya Burkina Faso na FC Saint Eloi Lupopo ya DR Congo, Valentin Nouma kwa ajili ya kuipata huduma yake.

⛳Coastal Union iko kwenye mazungumzo na beki wa zamani wa Yanga, Djuma Shaaban. Mkongomani huyo amekuwa nje ya uwanja kwa msimu mzima bila ya kuwa na timu baada ya kuachana na Yanga aliyoitumikia kwa misimu miwili 2021-2022 na 2022-2023.

⛳Klabu ya Ken Gold FC iko katika mazungumzo ya kumsajili kiungo wa zamani wa Lipuli, Mbeya Kwanza, Polisi Tanzania na Dodoma Jiji FC, Jimmy Shoji Mwaisondola.

⛳Klabu ya Coastal Union iko katika mazungumzo na beki mzoefu Kelvin Yondani ili akajiunge na wagosi hao ili kuziba nafasi ya Lameck Lawi anayetajwa kutua Simba msimu ujao

⛳Vilabu ya Dodoma Jiji FC, Mashujaa FC na JKT Tanzania vinapigana vikumbo kuinasa saini ya kiungo Nassoro Kapama aliyemaliza mkataba wake na Mtibwa Sugar iliyoshuka daraja.

⛳Klabu ya Ken Gold FC iko katika mazungumzo na makocha wawili raia wa Uganda, Abdallah Mubiru na Matthias Lule ili kupata saini ya mmoja kuja kufundisha katika msimu ujao wa ligi kuu NBC Tanzania.

⛳Dodoma Jiji FC imemtambulisha rasmi kocha Mecky Maxime kama ilivyoripotiwa katika ukurasa huu

⛳Kocha wa Namungo FC, Mwinyi Zahera anaangalia uwezekano wa kumsajili kiungo mshambuliaji Ibrahim Ajibu aliyemaliza mkataba wake na Coastal Union ya Tanga

⛳Kocha wa Kagera Sugar Fred Felix Minziro amewaagiza viongozi wake kumrudisha mshambuliaji wao wa zamani Yusuph Mhilu baada ya klabu yake ya Geita Gold FC kushuka daraja

Mtaa Unaongea
Magungu ndio tatizo simba
 

Kiama

Mpiga Chabo
Jun 20, 2024
1
0
0
Kiama Daa! Inauma sana unapambania timu ipande daraja alafu unatimuliwa so vizur
Wakiwa vibay ndo watawakumbuka​
 

Lucky___

Mpiga Chabo
Jun 14, 2024
7
0
0
Simba hizo thankyou fanyenii kama pamba jiji fc waachee kusumbuka kila siku thankyou fyeka wote kwa siku mojaa