MPIRA WETU NI KAMA MSIBA
Ukifiwa watu wanakuja wengi kwako kukusapoti kipindi kigumu unachopitia, unapata nguvu unajikakamua kwakuwa kuna wenzio wamekuja wanakupa maneno mazuri unasahau uhalisia wako unajikuta unacheka unapiga na stori. Baada ya mazishi watu wote wanarudi majumbani kwao unabaki wewe mkeo na watoto, mnajikuta hata mnashindwa kuongea kwa huzuni iliyowatawala kwa msiba, hapo mnakuwa kwenye uhalisia wa majonzi ya kufiwa.
Ligi namba 5 kwa ubora Afrika inakuwepo tunapokuwa na utitiri wa wachezaji kutoka nje ya nchi, uwepo wao unatusahaulisha ukweli wa uwezo wetu kama nchi inapokuja timu ya taifa. Sasa wanapoondoka aidha kwenda kwenye nchi zao au kupisha ratiba ya FIFA tu wakiwa hapahapa nchini wanafanya mazoezi kwenye fukwe zetu za Bahari ya Hindi.
Kile tulichokiona jana pale uwanja wa Benjamin Mkapa ni majonzi ya msiba baada ya akina Pacome, Fuentes, Karabou, Chama, Aziz Ki, Matampi, Camara, Diara, Boka, Ateba, Fernandez, Akaminko, Blanco, etc etc etc ambao wapo kutufariji kwenye msiba kuondoka na kutuachia nchi yetu na hapo ndipo tunapogundua kwamba kumbe tuna msiba na majonzi hutawala.
Kuna mambo meengi jana yameongewa baada ya kutopata ushindi wapo wanaosema makocha, wapo wanaosema upangaji wa timu, wapo wanaosema maandalizi, wapo wanaosema kutokuwepo kwa baadhi ya wachezaji, etc etc. Wachache sana wamesema kuhusiana na ubora wa wapinzani tuliocheza nao, wengi wamewaona wa kawaida sana. Nimejiuliza lini mara ya mwisho timu ya Taifa ya Tanzania imeifunga Misri tena kwenye mashindano? Ethiopia wao mara ya mwisho kuifunga Misri ni 9 Juni 2022 mabao 2-0, bila kujali matokeo mengine hapo katikati. Nimetoa tu huo mfano wa mechi za group stage ambapo mchezo wa marejeo Ethiopia walipoteza 1-0. Kwahiyo wapinzani sio wanyela kama wengi wanavyodhani.
Bado nasisitiza mpira wetu ni kama msiba, lundo la wachezaji wa kigeni linatusahulisha majonzi ya kufiwa ambayo tunayo. Tuanzishe mjadala wa kitaifa kuhusiana na hili jambo, hatuwezi kukwepa uwepo wa wachezaji wa nje, lakini tutafute namna nzuri ya kuwa nao. Sio kama sasa wachache wanaitwa timu zao za Taifa tena wengine wameanza kuitwa kupitia ligi yetu.
BIN KAZUMARI MTIPA (The voice of the voiceless)
Ukifiwa watu wanakuja wengi kwako kukusapoti kipindi kigumu unachopitia, unapata nguvu unajikakamua kwakuwa kuna wenzio wamekuja wanakupa maneno mazuri unasahau uhalisia wako unajikuta unacheka unapiga na stori. Baada ya mazishi watu wote wanarudi majumbani kwao unabaki wewe mkeo na watoto, mnajikuta hata mnashindwa kuongea kwa huzuni iliyowatawala kwa msiba, hapo mnakuwa kwenye uhalisia wa majonzi ya kufiwa.
Ligi namba 5 kwa ubora Afrika inakuwepo tunapokuwa na utitiri wa wachezaji kutoka nje ya nchi, uwepo wao unatusahaulisha ukweli wa uwezo wetu kama nchi inapokuja timu ya taifa. Sasa wanapoondoka aidha kwenda kwenye nchi zao au kupisha ratiba ya FIFA tu wakiwa hapahapa nchini wanafanya mazoezi kwenye fukwe zetu za Bahari ya Hindi.
Kile tulichokiona jana pale uwanja wa Benjamin Mkapa ni majonzi ya msiba baada ya akina Pacome, Fuentes, Karabou, Chama, Aziz Ki, Matampi, Camara, Diara, Boka, Ateba, Fernandez, Akaminko, Blanco, etc etc etc ambao wapo kutufariji kwenye msiba kuondoka na kutuachia nchi yetu na hapo ndipo tunapogundua kwamba kumbe tuna msiba na majonzi hutawala.
Kuna mambo meengi jana yameongewa baada ya kutopata ushindi wapo wanaosema makocha, wapo wanaosema upangaji wa timu, wapo wanaosema maandalizi, wapo wanaosema kutokuwepo kwa baadhi ya wachezaji, etc etc. Wachache sana wamesema kuhusiana na ubora wa wapinzani tuliocheza nao, wengi wamewaona wa kawaida sana. Nimejiuliza lini mara ya mwisho timu ya Taifa ya Tanzania imeifunga Misri tena kwenye mashindano? Ethiopia wao mara ya mwisho kuifunga Misri ni 9 Juni 2022 mabao 2-0, bila kujali matokeo mengine hapo katikati. Nimetoa tu huo mfano wa mechi za group stage ambapo mchezo wa marejeo Ethiopia walipoteza 1-0. Kwahiyo wapinzani sio wanyela kama wengi wanavyodhani.
Bado nasisitiza mpira wetu ni kama msiba, lundo la wachezaji wa kigeni linatusahulisha majonzi ya kufiwa ambayo tunayo. Tuanzishe mjadala wa kitaifa kuhusiana na hili jambo, hatuwezi kukwepa uwepo wa wachezaji wa nje, lakini tutafute namna nzuri ya kuwa nao. Sio kama sasa wachache wanaitwa timu zao za Taifa tena wengine wameanza kuitwa kupitia ligi yetu.
BIN KAZUMARI MTIPA (The voice of the voiceless)