Siku za hivi karibuni iliripoti kuwa Simba imekuwa ikimfuatilia kwa ukaribu zaidi kiungo ( Serge N´guessan Archange Pokou), ambaye ni panga pangua wa Asec Mimosas, na wamekubaliana sehemu kubwa ya dili hilo, ili mwamba huyo aje kukipiga kwenye kikosi hicho msimu ujao.
Ni kijana mdogo aliyezaliwa mwaka 2000, na sasa ana umri wa miaka 23, makuzi yake kwa kiasi kikubwa ni kucheza mpira akianzia safari yake kwenye klabu ya Moossou Football Club, ya nchini kwao Ivory Coast, lakini alijiunga na Asec Mimosas na kudumu kwa misimu minne yenye mafanikio makubwa.
Serge Pokou ni sehemu ya kikosi cha Asec kilichocheza na Mnyama Simba kwenye Ligi ya Mabingwa msimu uliomalizika, na hadi sasa kiungo huyo amecheeza mechi 12, amefunga mabao 3 na kutoa pasi 1 ya goli.
Ikumbukwee pia nyota huyu amekuwa akifuatiliwa kwa ukaribu zaidi na Yanga na vilabu vingine vya Afrika, lakini Simba ndiyo wapo kwenye nafasi kubwa zaidi ya kuinasa saini ya Serge Pokou tena kwa dau dogo kabisa la Tsh Milioni 200/=
Ni kijana mdogo aliyezaliwa mwaka 2000, na sasa ana umri wa miaka 23, makuzi yake kwa kiasi kikubwa ni kucheza mpira akianzia safari yake kwenye klabu ya Moossou Football Club, ya nchini kwao Ivory Coast, lakini alijiunga na Asec Mimosas na kudumu kwa misimu minne yenye mafanikio makubwa.
Serge Pokou ni sehemu ya kikosi cha Asec kilichocheza na Mnyama Simba kwenye Ligi ya Mabingwa msimu uliomalizika, na hadi sasa kiungo huyo amecheeza mechi 12, amefunga mabao 3 na kutoa pasi 1 ya goli.
Ikumbukwee pia nyota huyu amekuwa akifuatiliwa kwa ukaribu zaidi na Yanga na vilabu vingine vya Afrika, lakini Simba ndiyo wapo kwenye nafasi kubwa zaidi ya kuinasa saini ya Serge Pokou tena kwa dau dogo kabisa la Tsh Milioni 200/=