Arsenal Thread

Mkwavinyika

Administrator
Staff member
Dec 2, 2021
49
9
26
Dar es Salaam
Mechi zinazofuata



Matokeo ya Arsenal

 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Kufuatia ukiukaji wake wa kinidhamu wiki iliyopita, Pierre-Emerick Aubameyang hatakuwa tena nahodha wa klabu ya Arsenal, na hatachaguliwa kwa mechi ya Jumatano dhidi ya West Ham United.
 

Mkwavinyika

Administrator
Staff member
Dec 2, 2021
49
9
26
Dar es Salaam
Baada ya kuzuka kwa taarifa kuwa wachezaji wa Arsenal Tomiyasu (23) na Ben White (24) hawapeani pasi mara kwa mara licha ya kucheza katika nafasi jirani, Tomiyasu amelitolea ufafanuzi suala hilo

"Ni kwa sababu Ben White ni mchezaji mzuri. Mara nyingi, pasi kutoka kwa beki wa kati kwenda kwa mabeki wa pembeni huwa 'pasi za shinikizo'. Mimi huwa nacheza beki wa kati pia, mara nyingi pasi rahisi kwa mabeki wa pembeni huwa ni chaguo la mwisho"
"Ikiwa beki wa pembeni hajakabwa kwa nguvu na wapinzani kwa presha kubwa basi nitacheza pasi, lakini kama winga pinzani yupo mbele, lazima utapiga pasi sehemu nyingine. Hivyo Ben White ni mchezaji mzuri ambaye hachezi pasi zinazokupa presha."
Maneno ya Mjapan Takehiro Tomiyasu

266408087_4872218906171354_5792018286818065686_n.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
FULL TIME:
Arsenal 2-0 West Ham
⚽
48': Martinelli
⚽
87': Smith Rowe
✅
ALAMA TATU
✅
CLEAN SHEET
✅
TOP 4
 

Attachments

  • arsenal.PNG
    arsenal.PNG
    537.9 KB · Somwa: 0

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

NKETIAH APIGA HAT-TRICK ARSENAL YAICHAPA SUNDERLAND 5-1

Wenyeji, Arsenal wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Ligi England, maarufu kama Carabao Cup baada ya ushindi wa 5-1 dhidi ya Sunderland usiku wa jana Uwanja wa Emirates Jijini London.
Shujaa wa Arsenal jana alikuwa ni mshambuliaji Eddie Nketiah aliyefunga mabao matatu peke yake dakika za 17, 49 na 58, wakati mabao mengine yamefungwa na Nicolas Pepe dakika ya 27 na kinda wa umri wa miaka 18 aliyekuwa anacheza kwa mara ya kwanza kikosi cha kwanza, Charlie Patino dakika ya 90 na ushei.
 

Attachments

  • arsenal 1.PNG
    arsenal 1.PNG
    515.3 KB · Somwa: 0

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

ARSENAL YAWAPA ZAWADI YA 5-0 MASHABIKI WAKE​

1640609965333.png

TIMU ya Arsenal imewapa zawadi nzuri mashabiki wake jioni ya leo baada ya ushindi wa 5-0 dhidi ya wenyeji, Norwich City FC Uwanja wa Carrow Road mjini Norwich, Norfolk.
Mabao ya Arsenal leo yamefungwa na Bukayo Saka mawili, dakika ya sita na 67, Kieran Tierney dakika ya 44, Alexandre Lacazette kwa penalti dakika ya 84 na Emile Smith Rowe dakika ya 90 na ushei.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 32, ingawa inabaki nafasi ya nne ikizidiwa pointi sita na Chelsea, baada ya timu zote kucheza mechi 18, wakati Norwich inaendelea kushika mkia ikibaki na pointi zake 10 za mechi 17 sasa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Kwa mara ya kwanza Hector Bellerin ameizungumzia timu yake ya Arsenal tangu ajiunge na Real Betis kwa mkopo
"Arsenal wanafanya vizuri na hilo linanifurahisha sana. Mchezaji waliyempata katika nafasi yangu (Tomiyasu) anafanya vyema"
"Nafurahishwa na namna wanavyopambana, mimi huwa natazama kila mchezo na natamani wazidi kufanya vizuri zaidi. Ndivyo soka linavyokwenda"
"Mara zote nilikuwa nawaambia viongozi kuwa nikiondoka hapa sitaki kuwaacha bila mtu yeyote bora katika nafasi yangu au katika nafasi ambayo hamuwezi kuwa katika hali ya bora"
"Kwasasa kazi inafanyika na nafurahi kuona Arsenal inazidi kuimarika"
'Nataka mema kwa sisi sote. Nimekuwa Arsenal kwa miaka 10 na napenda mahali hapa. Ilifanya kazi kwa kila mtu na hiyo ndiyo inanionyesha kuwa ilikuwa jambo sahihi kufanya.
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Tangu Thomas Partey aondoke Arsenal kwenda kujiunga na timu yake ya Taifa ya Ghana
🇬🇭
kwenye michuano ya AFCON 2021 nchini Cameroon
🇨🇲
, klabu hiyo haijacheza mchezo wowote wa EPL
Mpaka sasa akiwa njiani kurejea muda wowote huko London atakuwa hajakosa mchezo wowote wa EPL uliosababishwa na majukumu ya timu ya Taifa.
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1 na maandishi yanayosema 'Emirates FLY BETTER 5 adina'
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
KUHUSU ARTHUR MELO
🇧🇷
KWENDA ARSENAL:
Wawakilishi wa Klabu ya Arsenal hii leo wamekutana na wakala wa kiungo wa Juventus Arthur Melo ili kuona uwezekano wa kupata huduma yake kwa mkopo wa muda mfupi
Imeelezwa kuwa Juventus wapo tayari kumtoa kwa mkopo kiungo huyo kwa kipindi kisichopungua miezi 18 itakayokuwa na chaguo kwa Arsenal kumsajili moja kwa moja kitu ambacho Arsenal hawajakubali huku wakisisitiza kuwa wanamtaka kwa Mkopo utakaomalizika mwishoni mwa msimu huu pasipokuwa na chaguo la kumsajili
Hadi sasa hakuna makubaliano yaliyofikiwa juu ya uhamisho huo.
Chanzo: Fabrizio Romano
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1, amesimama na maandishi yanayosema 'adidas AL *** J Jeep 4XC JJ adidas'
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
FULL TIME
Arsenal 0-2 Liverpool
⚽
Diogo Jota
⚽
Diogo Jota
✅
Liverpool wametinga hatua ya fainali ya Carabao Cup, watavaana dhidi ya Chelsea.
❌
Thomas Partey amekula umeme katika mchezo huo.
272212379_5013642638695646_4636274614927209291_n.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

ARSENAL YAWASHINDWA VIBONDE BURNLEY, 0-0 EMIRATES.​

AVvXsEgHkagDvkqAD6_SNj3GN8Yqj5Gv0nWhba-H6KD97jPpGN9jZTUmJZ0hyxCQTy4amvIcJpPTY18vlbzIfHpGEpbSTE31pAv3pAanSHYkkfaQGiT7X_JQEHnUFzKNylRYrWlxNkZRr0iSt49ZFsa3iaPcJ9VoFyJqXzOU5Ocy8PL7jKv7J59158Nk5iWa=w640-h408

WENYEJI, Arsenal wamelazimishwa sare ya 0-0 na Burnley katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Emirates Jijini London.
Arsenal inafikisha pointi 36 katika mchezo wa 21, ingawa inabaki nafasi ya sita, wakati Burnley inatimiza pointi 12 katika mchezo wa 18 na inaendelea kushika mkia.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

ARSENAL YAICHAPA WOLVES 1-0 MOLINEUX.​

AVvXsEj5VnkuIQlrpo7ChPvqCLx6-XTBrNpUnb2u-k55sGrzI-l5Aa2NnSYol16HsgRIdeNK594ZIYQs4E9rjAQJ4c4hB5IYCZ0dkBSYbqukidbZt4v8NAuAj61pRtu8cDsC82kx-p4hjtrGCvsggvihTW7UGKduKUWuWSrly_Cm31UGJr874GbFRYg6Rtj2=w640-h430

BAO pekee la Gabriel Martinelli dakika ya 25, limeipa Arsenal ushindi wa 1-0 dhidi ya Wolverhampton Wanderers usiku wa Alhamisi Uwanja wa Molineux, Wolverhampton, West Midlands.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 39 katika mchezo wa 22 na kupanda nafasi ya tano ikiizidi wastani wa mabao Manchester United, ambayo pia imecheza mechi moja zaidi.
Wolves inabaki na pointi zake 34 za mechi 22 katika nafasi ya nane.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Emile Smith Rowe amekuwa mchezaji wa kwanza kutoka kwenye Academy ya timu hiyo kufunga mabao 10 ndani ya msimu mmoja tangu alipofanya hivyo Cesc Fabregas msimu wa 2009/10
Inaweza kuwa picha ya Watu 2 na watu wanacheza spoti
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

ARSENAL YAICHAPA WOLVES 2-1 EMIRATES​

AVvXsEhiSg6-QL1g7TKqQuO2xMTS7g56_yV0mlVkvsmg26jkhNL_jYAmxrd0PGqRh-CgKOiUUoNmPgSrXbWVo0uDtsGFvrgVS1OZYrDaJGzci19VoUi05f-WTxFmoaFwUhWHjFHsw23fsMEVVqGFAziaWGgTinrpq4Q_rqr7cxbmk5WZvEzTPsf4A3o5oks1=w640-h428

WENYEJI, Arsenal wameibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Wolverhampton Wanderers katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa jana Uwanja wa Emirates Jijini London.
Hwang Hee-chan aliifungia Wolves bao la kuongoza dakika ya 10, kabla ya Arsenal kutoka nyuma kwa mabao ya Nicolas Pepe dakika ya 82 na Alexandre Lacazette aliyemlazimisha Jose Sa kujifunga dakika ya 90 na ushei.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 45 katika mchezo wa 24 na kusogea nafasi ya tano ikizidiwa pointi moja na Manchester United ambayo hata hivyo imecheza mechi moja zaidi, wakati Wolves inabaki na pointi zake 40 za mechi 25 nafasi ya saba.
 
Last edited:

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Arsenal yatangaza mapema, watasajili​

arteta pic


LONDON ENGLAND. ARSENAL hawataki kupoteza muda katika kufuta machungu ya kushindwa kufanya usajili kwenye dirisha la Januari kwa kuanza kwa kasi kubwa kwenye usajili wa dirisha lijalo la uhamisho wa majira ya kiangazi.
Kinachoelezwa ni kwamba Arsenal wanasubiri tu mambo yaanze. Kwenye dirisha la Januari, Arsenal ilikuwa na dili za kibabe sizizopungua nne mezani, ikiwamo ya straika Dusan Vlahovic, waliyemtaka aje kuchukua buti za Pierre-Emerick Aubameyang - lakini staa huyo aliitosa Arsenal na kutimkia zake Juventus.
Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta kikosi chake kipo kwenye nafasi nzuri ya kukamatia tiketi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao, hivyo kwenye jambo hilo ni lazima kuwa na huduma ya watu wa kazi uwanjani.
Mhispaniola huyo alikiri kwamba timu italeta wachezaji wapya ili kukifanya kikosi kuwa kwenye viwango vingine vya ubora.
“Tuzo tulichopanga, lakini sokoni palikuwa pagumu,î alisema Arteta akizungumzia tukio la kushindwa kusajili mtu kwenye dirisha la Januari.
“Tunafahamu kila kitu. Tunafanya uamuzi wa wachezaji ambao tunaamini watakuja kutusaidia. Wachezaji watakuja kwa ajili ya kutufanya tuwe kwenye anga nyingine kabisa kiubora. Kwa sasa tupo kwenye viwango tunavyotaka kuwa, tunahitaji wengine waje kutotoa hapa tulipo. Ndio maana tutasajili.”
Kwenye dirisha lijalo, Arteta atahitaji kipa mwingine wa kuja kumpa upinzani Aaron Ramsdale, kiungo wa kati wa kucheza kucheza pacha na Thomas Partey
na straika wa kuja kuziba pengo la Pierre-Emerick Aubameyang.
Mkurugenzi wa ufundi wa Arsenal, Edu anafahamu majukumu yake mazito kwenye dirisha lijalo la uhamisho wa majira ya kiangazi katika kuleta wakali watakaofanya Emirates pale mahali pa kutisha kwa wapinzani.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

ARSENAL YAICHAPA WATFORD 3-2 VICARAGE​

AVvXsEjicbM4ZaoD0Y7kzNTfIvvPArVGMScx41rbOOWD196VD--UTMjZykPArrMUsmRxu2nN0Rv1OIXXilVFRtUtAemp9ZpLaL9onKtAh-lhzkwKJsKE-X-LRQm_CqNecl0AOnq2l20TqbhcShq9w3U-AdK-AiDL3SXPItTdH3iTo0CEn9Yc1wG0HEHIHGI6=w640-h454

TIMU ya Arsenal imeibuka na ushindi wa 3-2 dhidi ya wenyeji, Watford katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Vicarage Road mjini Watford.
Mabao ya Arsenal yamefungwa na Martin Odegaard dakika ya tano, Bukayo Saka dakika ya 30 na Gabriel Martinelli dakika ya 52, wakati ya Watford yamefungwa na Cucho Hernandez dakika ya 11 na Moussa Sissoko dakika ya 87.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 48 katika mchezo wa 25 na kupanda nafasi ya nne, wakati Watford inabaki na pointi zake 19 za mechi 27, nafasi ya 19.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mavitu ya Saka, Odegaard yampagawisha Fabregas​

Mavitu PIC


LONDON ENGLAND. NAHODHA wa zamani wa Arsenal, kiungo fundi wa mpira wa Kihispaniola, Cesc Fabregas amesema Bukayo Saka na Martin Odegaard ndiyo silaha ya sasa na ya baadaye ya wababe hao wa Emirates baada ya kile walichowafanya Watford kwenye mchezo wa Ligi Kuu England juzi Jumapili.
Odegaard alifunga bao la kuongoza la Arsenal uwanjani Vicarage Road, kisha Saka na Gabriel Martinelli nao kila mmoja walitikisa nyavu kwenye ushindi wa 3-2 na kuwaporomosha Manchester United kwenye Top Four kabla hata hawajachapwa na mahasimu wao Manchester City.
Saka alifunga bao lake la tisa kwenye klabu hiyo msimu huu, wakati Odegaard amefunga bao lake la tano tangu alipojiunga akitokea Real Madrid.
Kwa Saka, bao hilo la Vicarage Road linampeleka kwenye nafasi nzuri ya kufikia rekodi ya Fabregas kwenye klabu hiyo.
Kwa ujumla wake, Saka amefunga mabao 20 akiwa na uzo wa Arsenal, huku akiwa na umri wa miaka 20, hivyo staa huyo Mwingereza anakuwa mchezaji mwenye umri mdogo kufikisha idadi hiyo ya mabao kwa mara ya kwanza baada ya miaka 15 kupita. Saka amefikisha akiwa na umri wa miaka 20 na siku 182.
Fabregas alisema: “Saka na Odegaard ni silaha ya sasa na baadaye Arsenal. Vipaji viwili vikubwa kabisa,” alisema kiungo huyo wa Monaco, ambaye alifunga mabao 57 kwenye kikosi hicho.
Kabla ya mechi hiyo ya Watford, kocha wa Arsenal, Mikel Arteta alimsifu Odegaard akisema kiungo huyo atafunga mabao mengi sana.
“Martin kwetu sisi ni mchezaji muhimu sana amekuwa akionyesha hilo kila wiki,” alisema Arteta.
“Anapiga kazi kwenykweli, amekuza kiwango cha mpira wake kama tulivyojadili na kukubaliana. Amejiandaa vyema kiakili kwa namna anavyocheza.”
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

ARSENAL YAICHAPA LEICESTER 2-0 EMIRATES​


MABAO ya Thomas Partey dakika ya na Alexandre Lacazette kwa penalti dakika ya baada ya Çaglar Soyuncu kuunawa mpira yameipa Arsenal ushindi wa 2-0 dhidi ya Leicester City Uwanja wa Emirates Jijini London leo.
Arsenal inafikisha pointi 51 na kurejea nafasi ya nne, wakati Leicester inabaki na pointi zake 33 za katika nafasi ya 12 baada ya wote kucheza mechi 26.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0
Klabu ya Arsenal imewataarifu wasimamizi wa kiungo wao mshambuliaji Bukayo Saka (20) kuwa wapo kwenye mpango wa kumuongezea mkataba mpya wa muda mrefu nyota huyo raia wa England
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿

Mkataba wa sasa ambao unamfanya Saka alipwe kiasi cha £30,000 (Tsh 91.5m) kwa wiki unamalizika miaka miwili ijayo
Ofa mpya ya Arsenal itamfanya alipwe kiasi cha £ 125,000 (Tsh 381.5) kwa wiki.
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1 na maandishi yanayosema 'APC FLYBETTER Emirates adidas e 1'

 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

ARSENAL YACHAKAZWA 3-0 NA CRYSTAL PALACE LONDON​

4A0D371E-3484-4E34-B861-FB567B469FF3.jpeg

WENYEJI, Crystal Palace wameibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa jana Uwanja wa Selhurst Park Jijini London.
Mabao ya Crystal Palace yamefungwa na Jean-Philippe Mateta dakika ya 16, Jordan Ayew dakika ya 24 na Wilfried Zaha dakika ya 74 kwa penalti.
Kwa ushindi huo, Crystal Palace ya kocha Patrick Vieira, Nahodha na kiungo wa zamani wa Arsenal, inafikisha pointi 37 katika mchezo wa 30 nafasi ya tisa, wakati Arsenal inabaki na pointi zake 54 za mechi 29 sasa nafasi ya tano.