Manchester United

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Neville adai anawajua wanaotibua Man United.​

ronaldo pic


MANCHESTER, ENGLAND. KIMENUKA. Gary Neville amesema anawajua mastaa wa Manchester United wanaotibua mambo kwenye vyumba vya kubadilishia vya klabu hiyo na kufanya timu kupata matokeo ya hovyo uwanjani.
Upo ushahidi wa kutosha kwamba kuna utovu wa nidhamu mkubwa ndani ya kikosi hicho cha kocha Ralf Rangnick, ambapo mastaa wa Man United wamefikia hatua ya kumpachika jina la hovyo kocha msaidizi, Chris Armas wakifanya dhihaka.
Rangnick yupo kibaruani Man United kama kocha wa mpito kwa zaidi ya miezi miwili sasa, huku timu yake ikipata matokeo yasiyoeleweka na kuelezwa hali si nzuri kwenye vyumba vya kubadilishia.
Ripoti za mapema Januari zilizotolewa na Mirror Football, zilifichua kwamba wachezaji wa Man United wanabeza mbinu za ufundishaji za Rangnick kwamba zimepitwa na wakati na haziwezi kusaidia kitu kwenye Ligi Kuu England. Tatizo jingine kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ni ripoti ya wachezaji wanamtaka kocha wa Paris Saint-Germain, Mauricio Pochettino apewe mikoba ya kuinoa timu hiyo mwishoni mwa msimu huu na sio kumpa ajira ya moja kwa moja Rangnick.
Nahodha na beki wa zamani wa Man United, Neville amewachurukia wachezaji ambao wanapiga kampeni ya kuchafua hali ya hewa kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.
Beki wa kulia huyo wa zamani huko Old Trafford alisema: “Ile Ijumaa kulifanyika utovu mkubwa wa nidhamu, sikupenda. Walikuwa wakimwita msaidizi namba mbili wa Ralf Rangnick jina la Ted Lasso, haukuwa utani, huo ni utovu wa nidhamu, sikupenda kabisa.
“Ile nadhani imefichua kila kitu kuhusu wao, hawana heshima. Nadhami kama ningekuwa Ralf Rangnick na msaidizi wake ningekuwa tofauti na nisingetaka kuendelea kuwa sehemu ya timu hii yenye maneno maneno ya kijinga. Hilo haliwapo kipindi chetu.
“Nakumbuka mwanzoni wakati najiunga na Sky na kulikuwa na mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, hivyo nilikwenda Napoli kwenye mechi dhidi ya Chelsea. Ilikuwa mechi ambayo Andre Villas-Boas aliwaweka benchi Frank Lampard, Michael Essien, Ashley Cole mastaa wanne au watano muhimu kwenye kikosi. Baada ya hapo kila kitu kilitibuka.
“Mambo yalikwenda haraka sana kwenye vyombo vya habari, taarifa zilivuja. Tukasikia kocha anafukuzwa. Nikajiuliza hivi vitu vinatokea kweli? Mawakala wa wachezaji ndio walikuwa wakiviambia vyombo vya habari kilichokuwa kinaendelea ndani ya Chelsea.
“Hicho ndicho kinachoendelea Manchester United kwa sasa.
Hali ya mambo kwenye kikosi cha Man United sio nzuri. Supastaa Cristiano Ronaldo ameambiwa aende kujiunga na Bournemouth kwa sababu yeye ni sehemu ya tatizo la kinachoendelea kwenye kikosi hicho cha Old Trafford. Baada ya sare dhidi ya Southampton Jumamosi iliyopita, Man United inakabiliwa na vita kali kwenye harakati zao za kumaliza ndani ya Top Four msimu huu.
Ronaldo alirudi Man United kwenye dirisha lililopita la uhamisho wa majira ya kiangazi na ndiye kinara wa mabao, akiwa amefunga mara 14.
Lakini, sasa amecheza mechi sita bila ya kufunga na hilo limeibua maswali kama bado ana uwezo wa kuchezea timu kubwa.
Tetesi zinasema amemwambia wakala wake Jorge Mendes amtafutie timu ili aachane na Man United mwisho wa msimu.
Na sasa mtangazaji wa zamani wa Sky Sports, Richard Keys ameiambia beIN Sports, Ronaldo anapaswa kuuzwa haraka.
Alisema: “Jorge Mendes amezungumza na mabosi wa Man United kuhusu kuondoka mwisho wa msimu. Kwa maoni yangu, anapaswa aondolewe haraka. Nimekuwa nikisema karibu msimu wote, nadhani yeye ni sehemu ya matatizo, sio tatizo la timu nzima, hakuna mwingine.”
Mtangazaji mwingine, Andy Gray alisema: “Umri wake ni miaka 37. Kama anataka kucheza kila mechi, aende akasajiliwe Bournemouth huko atacheza kila wiki.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MAN UNITED YAICHAPA LEEDS 4-2 ELLAND ROAD​

AVvXsEirmdMJDGnIzVpNfR0sgkgTJn4aGzfs50MpipvOL2FjI2LJ1T-j3Awjhanhh7FAOdPYaAg3rTGAf6rqk_XKRiRNu052nIjE3iiR3AnyP8-FZmnBLHRhPQ7SraXPUcEEUyUNXd6AChFuNZSlQL5DO1GETnYvoUioW7HPcajHgM7ZfkIh-1RfszrILkmM=w640-h402

TIMU ya Manchester United imepata ushindi wa ugenini wa 4-2 dhidi ya Leeds United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Elland Road.
Mabao ya Man United yamefungwa na Harry Maguire dakika ya 34, Bruno Fernandes dakika ya 45, Fred dakika ya 70 na Anthony Elanga dakika ya 88 wakati ya Leeds yamefungwa na Rodrigo dakika ya 53 na Raphinha dakika ya 54.
Kwa ushindi huo, Man United inafikisha pointi 46 katika mchezo wa 26 na kurejea nafasi ya nne, wakati Leeds inabaki na pointi zake 23 za mechi 24 katika nafasi ya 15.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mtoko wa Pochettino utakuwa balaa kubwa United​

Poche PIC


MANCHESTER, ENGLAND. MANCHESTER United inajiandaa kufanya mabadiliko makubwa kwenye dirisha lijalo la uhamisho wa majira ya kiangazi kwa ajili ya kuunda kikosi cha kazi cha msimu ujao.
Kocha wa kipindi cha mpito, Ralf Rangnick anajiandaa kubadilishwa na kocha wa Paris Saint-Germain, Mauricio Pochettino kwenye benchi la ufundi la miamba hiyo ya Old Trafford.
Pochettino, 49, amewekwa kwenye mipango ya Man United ambayo kwa sasa haionekani inacheza staili gani ya soka lake na kinachoelezwa ni kwamba Muargentina huyo akitua tu Old Trafford, usajili wake wa kwanza atakaofanya ni kumnasa Harry Kane.
Ujio wa Kane bila ya shaka utamweka pembeni Cristiano Ronaldo kwenye kikosi kama atakubali kuendelea kubaki mahali hapo. Jadon Sancho kwa sasa tayari ameshajitengenezea nafasi kwenye wingi ya kushoto na bila ya shaka Pochettino ataendelea kumtumia atakapotua klabuni hapo.
Mpango wa Man United ni kumnasa staa wa Kibrazili, Antony, anayekipiga huko Ajax kuja kucheza wingi ya kulia. Winga huyo Mbrazili amefunga mabao 11 na kuasisti mara nane msimu huu na kuwavutia Man United.
Bruno Fernandes, atabaki kwenye majukumu ya kucheza kiungo ya kushambulia chini ya Pochettino, ikiwa ni wazi alihitaji saini yake wakati alipokuwa Spurs mwaka 2019, bila shaka atakuwa Namba 10 kwenye fomesheni pendwa na Muargentina huyo ya 4-2-3-1.
Nyuma ya fowadi hiyo iliyosheheni mastaa watupu, Pochettino atahitaji kuwa na safu ya kiungo itakayokuwa na wakali wapya.
Man United ipo kwenye mchakato wa kunasa saini ya staa wa West Ham, Declan Rice kwenye dirisha lijalo na huenda saini yake ikagharimu Pauni 100 milioni.
Kwenye dili hilo, Man United inaweza kuamua kuwa na pacha ya Rice na Kalvin Phillips, huku pia ikiwa kwenye mchakato wa kumnasa Amadou Haidara kutoka RB Leipzig kama watamkosa Phillips.
Man United ya msimu ujao kama itamchukua Pochettino bila ya shaka hatakuwa na shaka kwenye safu ya mabeki, ambapo Harry Maguire na Raphael Varane wataendelea kuwa pacha katikati, huku pembeni ni Aaron Wan-Bissaka na Luke Shaw na David de Gea atasimama golini kama kawaida.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MAN U YAPATA SARE MADRID NA ATLÉTICO​

AVvXsEgR7mw_t9LNFgezsWZ4NixUYLvycMTnRGWsFz_KWJl9H4a1E5lS_u5e-cJD-jOFIRe0iOAG5dnZ0J0Owye8bJWn0r8ShA3btknzniel8AbDePw_gJyD9nQgm1wlBy1M0mDujEze0XacS4rsCP0sfInPAFeISDX-rGxKik9TkGXWGYWSjYjGIy9Odu0b=w640-h434

WENYEJI, Atletico Madrid wamelazimishwa sare ya 1-1 na Manchester United katika mchezo wa kwanza Hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa Jumatano Uwanja we Wanda Metropolitano Jijini Madrid.
Joao Felix alianza kuwafungia wenyeji, Atlético dakika ya saba, kabla ya Anthony Elanga kuisawazishia Manchester United dakika ya 80.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Rangnick Kumuanzisha Ronaldo Licha Ya Ukame​

2353-1568-2.62342589.jpg.gallery.jpg

KOCHA Ralf Rangnick anatarajiwa kusimama na Cristiano Ronaldo na atamuanzisha fowadi huyo katika mchezo wa Manchester Dabi, Jumapili dhidi ya Manchester City, kwa mujibu wa taarifa.
Awali, Ronaldo alianza maisha yake vyema Old Trafford akifunga mabao nane katika mechi zake 15 za kwanza za ligi, huku pia akifanya kazi kubwa kuisaidia United kutinga hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Hata hivyo, tangu kuanza kwa mwaka huu, mabao yake yamekauka akiwa amefunga bao moja tu katika mechi 10 zilizopita za michuano yote.
Katika mchezo wake wa hivi karibuni dhidi ya Watford, Ronaldo alikosa nafasi kibao United ilipobanwa kwa suluhu Old Trafford.
Ubutu wake langoni umeanza kuwafanya baadhi wahoji kama atapata nafasi dhidi ya Manchester City, lakini taarifa ya The Sun inaeleza kuwa Rangnick atamuanzisha kwenye first eleven.
Inaelezwa kuwa Rangnick anaamini Ronaldo, 37, aliyewekwa benchi dhidi ya Burnley mwezi uliopita, atakuwa amenufaika na mapumziko ya siku nane kabla ya kuivaa City.
Kwa sasa United wapo nafasi ya nne kwenye msimamo lakini wamejikuta wapo pointi mbili tu mbele ya Arsenal walio na viporo vitatu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Rashford aipigia mkwara Man United​

rashford pic

MANCHESTER, ENGLAND. STRAIKA wa Manchester United, Marcus Rashford anataka uhakika wa namba wa kudumu kikosini kabla ya kufanya maamuzi kuhusu hatima yake kwa mujibu wa ripoti.
Taarifa hiyo imeripotiwa na ripota maarufu wa masuala ya usajili Fabrizio Romano baada ya kupenyezewa na watu wa karibu wa nyota huyo.
Rashford mkataba wake utamalizika itakapofika mwaka 2023 yenye kipengele cha kuongoza mwingine lakini hatasaini hadi atakapopewa uhakika wa namba.
Nguli huyo wa masuala ya usajili ameandika kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa Rashford ameonyesha nidhamu ya hali juu kwani ni mchezaji ambaye amekulia katika kituo cha kukuzia vipaji Man United, hata hivyo kiwango chake bado hakijaridhisha tangu aliporejea baada ya kupona licha ya kufunga mabao manne Ligi Kuu England.
Ikumbukwe Rashford alikuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu baada ya kufanyiwa upasuaji wa bega.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

RONALDO AVUNJA REKODI YA MABAO YA FIFA​

AVvXsEhKhB4S8BHvoPDuepPpByIXLdOTX6-OwmDMiD6V5fggX8bMP1jhZ28r5cYidEpl32DVuXuWA2pamt8mX3rVQpN6twMQfB5mqvp5TrRFOaIjeT3Rbl9ZgOcS6jyAiZwTBMEd7-_ioKtaLOD04P875vrPW0AWz1leTykxqivAEM7TN-IgjxQhNT1rEwBR=w640-h434

MSHAMBULIAJI Mreno, Cristiano Ronaldo jana amevunja rekodi ya mabao ya FIFA baada ya kufunga hat-trick akiiwezesha Manchester United kushinda 3-1 dhidi ya Tottenham Hotspur kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Old Trafford.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 sasa amefikisha mabao 807, akimpiku Josef Bican, aliyekuwa anashikilia rekodi hiyo.
Ronaldo alifunga mabao yake dakika za 12, 38 na 81, wakati mabao ya Spurs yalifungwa na Harry Kane kwa penalti dakika ya 35 na Harry Maguire aliyejifunga dakika ya 72.
Ushindi huo unaifanya Man United ifikishe pointi 50 katika mchezo wa 29 na kurejea nafasi ya nne, ikiizidi pointi mbili Arsenal, ambayo hata hivyo ina mechi nne mkononi, wakati Spurs inabaki na pointi zake 45 za mechi 27 sasa nafasi ya saba.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MAN UNITED YATUPWA NJE LIGI YA MABINGWA​

AVvXsEgI3y2RXl4_e4AMxv78VFbL3VZq4oBLgqqyVv5TH1Bc46VEuhn0-wlJpvDH_LoKcTYNg5hFOFutmwhj5ZLsJ7grjPHbsq1K3RtROklOMp-k2tcRGRQNn_K7ePHB-a5ufI-I_kmMZX9xkzI5i9KFrnbIgIhqBLdxyaW4j56nvYIRQxbcoFZIqh2IFLF7=s320

WENYEJI, Manchester United wamechapwa 1-0 na Atlético Madrid, bao pekee la Renan Lodi katika mchezo wa marudiano Hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester, England.
Kwa matokeo hayo, Atlético Madrid inakwenda Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa 2-1 baada ya sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Hispania.
Nayo Benfica imewachapa wenyeji wengine, Ajax 1-0 bao pekee la Darwin Núñez Ribeiro Uwanja wa Johan Cruijff Arena Jijini Amsterdam, Uholanzi hivyo kwenda Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa 3-2 baada ya sare ya 2-2 kwenye mchezo wa kwanza Ureno.
Timu nyingine zilizokwenda Robo Fainali ni Manchester City ya England iliyoitoa Sporting Lisbon ya Ureno, Real Madrid ya Hispania iliyoitoa PSG ya Ufaransa, Bayern Munich ya Ujerumani iliyoitoa Salzburg ya Austria, Liverpool ya England iliyoitoa Inter Milan ya Italia.
Mechi za mwisho zinachezwa leo, Chelsea walioshinda 2-0 mechi ya kwanza nyumbani England watakuwa wageni wa Lille Uwanja wa Stade Pierre-Mauroy Jijini Villeneuve d'Ascq na Juventus baada ya sare ya 1-1 ugenini Hispania leo watakuwa wenyeji wa Juventus Uwanja wa Allianz Jijini Torino, Italia.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Kwa mujibu wa Fabrizio Romano Man Utd tayari wamemfanyia Interview kocha wa Ajax Erik Ten Hag, Mabosi wa timu hiyo wameridhishwa nae hasa suala la lugha lakini maamuzi ya mwisho yatafanywa kulingana na mahitaji yao
Klabu hiyo pia itaendelea kufanya Interview na makocha wengine.
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Mshambuliaji wa klabu ya Man United U18 Alejandro Garnacho (17) akiwa kambini na timu ya Taifa ya Argentina
🇦🇷

Kinda huyo hajapandishwa kwenye kikosi cha wakubwa cha Man Utd lakini tayari ameitwa kwenye timu ya Taifa
Alejandro mwenye asili ya Argentina
🇦🇷
amezaliwa jijini Madrid, Hispania na kuanzia soka lake Atlético
🇪🇸
kabla ya kujiunga na Man United mwaka 2020
Argentina
🇦🇷
wameamua kumshawishi mapema bwana Mdogo
😋

Inaweza kuwa picha ya Watu 2, watu wanasimama na nje

 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

MAN UNITED YALAZIMISHWA SARE NA LEICESTER 1-1​


WENYEJI, Manchester United wamelazimishwa sare ya 1-1 na Leicester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa Old Trafford, Manchester.
The Foxes walitangulia kwa bao la mshambuliaji wa Kimataifa wa Nigeria, Kelechi Iheanacho dakika ya 63, kabla ya kiungo Mbrazil, kuisawazishia Man Unitef dakika ya 66.
Leicester ingeweza kuondoka na pointi zote tatu kama si bao Lao lingine baadaye lililofungwa na James Maddison kukataliwa kwa msaada wa VAR.
Kwa sare hiyo, United inafikisha pointi 51 katika mchezo wa 30, ingawa inabaki nafasi ya sita, wakati Leicester inafikisha pointi 37 katika mchezo wa 28 nafasi ya tisa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Ronaldo Amjibu Rooney Amuambia Aache Wivu ni Baada ya Sakata la Kumuita Mzee​


RONALDO-2.jpg

Cristiano Ronaldo akishangilia moja ya magoli yake akiwa na Manchester United
MSHAMBULIAJI wa Manchester United Cristiano Ronaldo amemjia juu Gwiji wa Manchester United na mchezaji mwenzake wa zamani Wayne Rooney akimuambia aache kumuonea wivu.

Hivi karibuni Wayne Rooney alinukuliwa akisema Manchester United haikustahili kumsajili Cristiano Ronaldo na Ronaldo pia hakusatahili kurudi Manchester United kutokana na kwamba Klabu hiyo sasa inatakiwa iwekeze kwa vijana kama kina Jadon Sancho na Marcus Rashford.

ROONEY.jpg

Gwiji wa Manchester United Wayne Rooney
Rooney aliendelea kusema kuwa Ronaldo wa sasa si wa zamani japo amejitahidi kufunga mabao muhimu kwa Manchester United mwanzoni mwa msimu lakini kwa maana ya uwekezaji wa miaka miwili au mitatu mbele Ronaldo hawezi kutegemewa.

Kwa upande wake Ronaldo amemjibu kwa kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram akisema “Una wivu sana.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

EVERTON YAICHAPA MAN UNITED 1-0 GOODISON PARK​


BAO pekee la Anthony Gordon dakika ya 27, limeipa Everton ushindi wa 1-0 dhidi ya Manchester United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Goodison Park Jijini Liverpool.
Pamoja na ushindi huo, Everton inabaki nafasi ya 17, ikifikisha pointi 28 katika mchezo wa 30, inazidiwa pointi mbili na Leeds United ambayo pia imecheza mechi moja zaidi.
Baada ya kichapo cha leo, Manchester United inabaki na pointi zake 51 za mechi 31 sasa nafasi ya saba.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0
Kocha Erik ten Hag anataka kuhakikishiwa kama atakuwa na nguvu ya kusajili, nguvu ya maamuzi ya wachezaji watakaoongeza mikataba au kuuzwa pamoja na kupewa muda wa kutosha kuandaa timu yenye ushindani kabla ya kufanya maamuzi ya kujiunga na Manchester United
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿

Chanzo: Fabrizio Romano
278395275_5258266637566577_5327708872957351520_n.jpg
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0
SAKATA LA RONALDO KUBAMIZA SIMU YA SHABIKI
Licha ya nyota wa Man Utd Cristiano Ronaldo kuomba msahama kwa kitendo cha kuibamiza chini simu ya bwana Mdogo Jake (14) wakati wa mchezo wa EPL dhidi ya Everton, mama wa mtoto huyo Sarah Kelly aukosoa msamaha huo
"Msamaha ndio ulinikasirisha zaidi, unamwambia kila mtu kwamba umeomba msamaha wakati hujaomba? Sawa, umeweka kwenye mitandao ya kijamii lakini hukupaswa kufanya vile, unapaswa kumuomba msamaha mwanangu"
"Yeye [Ronaldo] alikuwa na masaa kadhaa ya kutafakari juu yake, alitakiwa apate mawasiliano yetu ili azungumze na sisi na kutoa chochote ningefurahishwa na hilo"
"Kiufupi Kulikuwa na watu wengine wengi wakipunga simu zao pande zote, mwanangu alikuwa katika ulimwengu wa kipekee, alikuwa anafurahia ushindi wetu, wakati Ronaldo anatoka uwanjani, mwanangu akasema "Mama, Ronaldo anaumia, ngoja nimrekodi video.' Nikamwambia, 'Sawa'.
" Sikufikiria chochote juu yake, nakumbuka wakati huo alikuwa hamuangalii Ronaldo tena, badala yake alikuwa akiangalia anachokifanya kwenye simu, Ghafla nikashtuka simu ipo chini, mwanangu akaendelea kushangaa"
"Ilikuwa Ni ngumu sana kwangu kuliamini hilo kwasababu, Ronaldo alijua kuwa sehemu ile kuna watoto wengi na ndio maana kabla ya mechi alikuwa akipeana mikono na hao watoto, mechi ilivyoisha ikawa hadithi tofauti kabisa kwa sababu walikuwa wamepoteza, anachotakiwa kujua mpira hauko hivyo, Huwezi kushinda kila siku"
"Najua Kama mtu akikufanyia hivyo mtaani anakamatwa na kuhojiwa, nina uhakika hata kama angekuwa mtu mwingine ambaye amempeleka mtoto wake kwenye mechi hiyo na kukutana na hali hiyo angefadhaika sana na kushtuka pia"
KUHUSU MWALIKO WA RONALDO OLD TRAFFORD
"Nilimuuliza Mwanangu Je, ungependa kwenda kwasababu Ronaldo ametualika, Akasema, 'Hapana, mama, sitataka kumuona tena" Alizungumza Sarah kupitia Telegraph Sports
Ikumbukwe kuwa Polisi wa Merseyside wanatarajia kupitia picha za CCTV ili kubaini kama Cristiano Ronaldo alitenda kosa la kunyang'anya na kubamiza chini simu ya shabiki huyo kabla hawajachukua hatua zaidi.
278299076_5258318084228099_9106203072259255023_n.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

RONALDO APIGA HAT TRICK MAN UNITED YASHINDA 3-2​


WENYEJI, Manchester United wameibuka na ushindi wa 3-2 dhidi ya Norwich City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester.
Mabao yote ya Man United leo yamefungwa na mshambuliaji Mreno, Cristiano Ronaldo dakika ya saba, 32 na 76, hiyo ikiwa hat trick yake ya 50 kihistoria, wakati ya Norwich yamefungwa na Kieran Dowell dakika ya 45 na ushei na Teemu Pukki dakika ya 52.
Kwa ushindi huo, Man United inafikisha pointi 54 katika mchezo wa 32 na kupanda nafasi ya tano, wakati Norwich inabaki na pointi zake 21 baada ya kucheza mechi 31 pia na kuendelea kushika mkia.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

ERIK TEN HAG KOCHA MPYA MAN UNITED​


KLABU ya Manchester United imemuajiri Erik ten Hag kama kocha wake Mkuu mpya wa tano ndani ya miaka tisa, Mholanzi atajiunga na Mashetani Wekundu baada ya kumaliza majukumu yake Ajax mwishoni mwa msimu.
Ten Hag amesaini mkataba wa hadi 2025 jukumu lake kubwa likiwa ni kurejesha mafanikio yaliyopotea United tangu kustaafu kwa Alex Ferguson mwaka 2013 wakati ambao klabu ilishinda mataji yake ya mwisho ya rekodi England, 20.
United imeongozwa na makocha wawili wa muda- Michael Carrick na Mjerumani wa sasa, Ralf Rangnick – tangu kuondoka kwa Ole Gunnar Solskjaer aliyefukuzwa Novemba.
Ten Hag anakabiliwa na kibaruwa kigumu cha kuiumba upya United iwe tishio, baada ya kuachwa mbali na wapinzani, Manchester City na Liverpool licha ya klabu hiyo kuendelea kutumia fedha nyingi kusajili wachezaji.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

CHELSEA YAICHAPA WEST HAM 1-0 STAMFORD BRIDGE​


BAO pekee la Christian Pulisic dakika ya 90 limewapa wenyeji, Chelsea ushindi wa 1-0 dhidi ya West Ham United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Kwa ushindi huo, Chelsea inafikisha pointi 65 katika mchezo wa 32, ingawa inasalia nafasi ya tatu, ikizidiwa pointi 14 na Liverpool na 15 na Manchester City ambao kwa pamoja wamecheza mechi 33 kila timu.
West Ham baada ya kupoteza mechi hiyo wanabaki na pointi zao 52 za mechi 34 sasa nafasi ya saba.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MAN UNITED SARE 1-1 NA CHELSEA OLD TRAFFORD​



WENYEJI, Manchester United wamelazimishwa sare ya 1-1 na Chelsea katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Alhamisi Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester.
Chelsea ilitangulia kwa bao la Marcos Alonso dakika ya 60 akimalizia pasi ya Kai Havertz kabla ya Cristiano Ronaldo kuisawazishia Man United dakika ya 62 akimalizia pasi ya Nemanja Matić.
Chelsea inafikisha pointi 66 katika mchezo wa 33, ingawa inabaki nafasi ya tatu na Manchester United inatimiza pointi 57 katika mchezo wa 35, japokuwa inasalia nafasi ya sita.