Rekodi Za Leonel Ateba Mshambuliaji Mpya Wa Klabu Ya Simba

Hammy36

Administrator
Jan 17, 2023
56
54
5
Dar Es Salaam
KLABU ya Simba imetangaza kukamilisha usajili wa mshambuliaji raia wa Cameroon, Lionel Ateba kwa kumsainisha mkataba wa miaka mitatu.

Nyota huyo kutoka klabu ya USM Alger ya Algeria anajiunga na Simba kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji huku viongozi wa timu hiyo wakitakiwa kukata jina moja kwenye orodha ya wachezaji wa kigeni.

Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ahmed Ally, alisema mchezaji huyo amekuja kuongeza makali kwenye kikosi chao kuelekea kwenye Ligi Kuu na mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Hata hivyo rekodi za hivi karibuni za nyota huyo bado hazijahakisi kile ambacho Simba inakihitaji ndani ya klabu hiyo.

Nyota huyo alijiunga na USM Alger, Januari mwaka huu ambapo amecheza michezo 12 ya Ligi Kuu akitumia dakika 754 na kufunga bao moja huku akisaidia kupatikana mabao mawili.

Inaelezwa ujio wa nyota huyo ni mapendekezo na kocha wa klabu hiyo, Fadlu davids ambaye alitaka viongozi kuongeza mshambuliaji mwingine haraka iwezekanavyo.

Kutua kwa nyota huyo kunamaanisha sasa mshambuliaji Fred Michael na golikipa Ayoub Lakred ambaye yupo nje akiuguza majeraha mmoja wapo atampisha Mcameroon huyo kwenye orodha ya wachezaji wa kimataifa watakaoutumiwa msimu huu.

Fred haonekani kupewa kipaumbele sana na kocha Fadlu, lakini takwimu zake kwenye mechi chache za Ligi Kuu alizocheza msimu uliopita zinampa nafasi ya kubaki mbele ya Lakred.


Msimu uliopita Fred aliingia kwenye timu wakati wa dirisha dogo na kufanikiwa kufunga mabao saba licha ya mara kwa mara kutokea benchi.
 

Bplm1664

Mpiga Chabo
May 30, 2024
13
0
0
No mapema Sanaa kusema Ayoub si
Tusuburie muda utasema lakin Bora ayoub aondoke. Abaki Freddy na maana camara kawa Bora kuliko ayubu
N mapema Sanaa kusema Ayoub si Bora kwa Camara ivooo nazani upande wangu Freddy aende n mda was wazee kuipisha timu yetuuu pendwaaa na upande ATE A ngoja inyesheee tujue wapi panapovujaaa
 

Saidy

Mgeni
Jun 5, 2024
64
16
5
Kwenye swala la nani atoke ili kumpisha huyo lipo wazi.. anaeondoka ni kipa Ayoub lakini ukweli usemwe simba ata wafanye usajili gani, kwa msimu huu hawatakaa sawa mpaka timu izoeane.. mfano wake ni Chelsea walifanya usajili mkubwa ila wakawa wanasuasua kutokana na kocha kushindwa kuwaonganisha.. na ninavyoina Simba na kocha aliopo kwa msimu huu wawe wavumilivu tu.. maana hata kocha bado ni Mapepe..🚶🚶🚶

Nakwenda zangu kucheza game la DLS 😃😃😃
 
  • Like
Reactions: Bplm1664
Aug 1, 2024
3
2
5
Lionel Ateba anakuja kuwa mwiba mjungu kweny safu za ulinzi timu nyng Sana nda na nje ya mipaka ya tanzania sabab ya uwezo wake mkubwa wakukimbia kweny nafas na kutumia nafas ztakazotengenezwa Ateba pia unauwezo mkubwa wa kutengenezaaa nafas Kwa kutumia pass za usaidzii au kukimbiaa kweny nafas nakusababsha safu ya ulnzi ya mpinzan kuacha mianya ambavyo inaweza kutumiwa na wachezaj wenzakee kupata mabao
 

Kabazi

Mgeni
May 17, 2024
4
1
5
Camala anaonekana kma hajatulia ana mbwembwe nyingi ambazo zinaweza kuwa hatari kwa timu anaoverconfidence nakaribia sana kumfananisha na onana wa man utd
 

Honest'G

Mgeni
Jun 13, 2024
10
1
5
Fred. Anakwenda misri kwa mkopo wamuda mrefu wenye kipengele cha kumsajili moja kwa moja ikiwa atakidha vigezo.

Ayoub bado yupoyupo sana SSC🅾
 

syang'annko

Mpiga Chabo
Aug 16, 2024
3
0
0
Acha inyeshe tuone wapi panavuja sina mengi nasema tu yanga bingwa kwa mara nyingne tena, ana bao moja mechi 12 🙆🙆🙆
 

syang'annko

Mpiga Chabo
Aug 16, 2024
3
0
0
Acha inyeshe tuone wapi panavuja sina mengi nasema tu yanga bingwa kwa mara nyingne tena, ana bao moja mechi 12 🙆🙆🙆