Umeuonaje Mchezo? Azam 0️⃣ Simba Sc 3️⃣

May 9, 2024
2
1
5
Azam ni timu mzuri lakin kiuhalisia inapaswa kushika nafasi ya tatu Kwa sababu Kwa aina ya mchezo walionao azam hawana uwezo kabisa wa kucheza na timu kama AL AHLY hivo binafsi naona hata wakishika nafasi ya pili bado watakuwa wanaend kuaibisha soka la bongo
ADMIN NOTE THIS📌📌📌📌📌
It's @official ommykhan917
 
  • Like
Reactions: Kijiweni
May 9, 2024
1
1
5
Kuna mambo makuu mawili.
1. Wachezaji wanajiamini sana chini ya kocha Mgunda, na wana imani naye na hili utaona jinsi wanavyojituma kuhakikisha hawamuangushi kocha aliyewapa imani. Ni wakati sahihi wakuamini wazawa na kumuachia timu Mgunda, aongezewe tuu technical benchi nzuri ikiwemo ya analysis coach wakuzijua vizuri mechi za Simba ndani na nje ya nchi.

2. Inaonekana pamoja na kumuamini Mgunda wachezaji wamepata psychology advise nzuri. Ni vyema sana viongozi ku invest kwenye psychology ya wachezaji na kumtafuta mtu sahihi kwenye hii sehemu, leo utaona kila mchezaji alikuwa mchezoni achilia makosa madogo madogo tuliyoyaona kwa forward wings lakini wengine wote walikuwa mchezoni kwa dakika zote tisini na za mwamuzi. Ni vizuri kuendelea kuweka hii temper kwa timu yetu kuhakikisha wachezaji mentally wanakuwa uwanjani na sii kwa mashabiki au viongozi etc.

Asante!
 
  • Like
Reactions: Kijiweni
May 2, 2024
7
2
5
Nd

MATAJIRI wa Dar, Azam FC wamepoteza pointi tatu mbele ya Simba inayonolewa na Kocha Mkuu Juma Mgunda katika mchezo wa mzunguko wa pili uliokuwa na ushindani mkubwa.

Baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa umesoma Azam FC 0-3 Simba.

Ni Sadio Kanoute alipachika bao la ufunguzi dakika ya 63 kamba ya pili ni Fabrice Ngoma dakika ya 77 na ile ya tatu ni Duchu dakika ya 89.

Azam FC walikuwa na nafasi yakufunga kipindi cha kwanza walikosa penalti kupitia kwa Feisal Salum aliyegongesha mwamba kipindi cha kwanza.

Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza ubao ulisoma Simba 1-1 Azam FC.

Ndege akikunyea haimaanishi ana shabaha
 
  • Like
Reactions: Kijiweni

Mr.Ri

Mgeni
May 8, 2024
3
4
5
Tokea Jana Nlizungumza Utofaut Was Azam Na Simba Ni Ukubwa Azam No Bora Saana Kuliko Simba But Simba Nikubwa So Hata Mech Wanajua Kuzichez Azam Bado Niwatoto Saana Kwny Soka LA Tanzania Awajajua Jinsi Yakuziendea Hizi Mechi
 
  • Like
Reactions: Kijiweni