Usajili

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

MKONGWE WA KONGO DEO KANDA ATUA MTIBWA SUGAR​

1640522856789.png

KLABU ya Mtibwa Sugar imemtambulisha winga mkongwe wa kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Deo Kanda A Mukok kuwa mchezaji wake mpya wa kwanza katika dirisha hili dogo la Usajili.
Kanda pamoja na kuwika AS Vita ya Kinshasa na TP Mazembe, DC Motema Pembe za Lubumbashi, kwao DRC na Raja Casablanca ya Morocco, pia amewahi kucheza Simba SC ya Dar es Salaam.
1640523193827.png
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

RASMI, SURE BOY NI MCHEZAJI MPYA WA YANGA SC​

KIUNGO Salum Abubakar 'Sure Boy' ametambulishwa rasmi kuwa mchezaji mpya wa kwanza wa Yanga SC katika dirisha dogo la usajili.
Sure Boy anajiunga na Yanga, timu ambayo baba yake aliichezea kati ya mwaka 1986 na 1993 baada ya kuachana na Azam FC aliyojiunga nayo mwaka 2007.
 

Attachments

  • 1640523476697.png
    1640523476697.png
    409.6 KB · Somwa: 0

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
OFFICIAL: Mshambuliaji wa kati Wazir Jr amejiunga na walima zabibu Dodoma Jiji Fc
Wazir amejiunga na Dodoma Jiji Fc baada ya kumalizana na Yanga Sc
1640615025270.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

YANGA YAMSAJILI KIPA WA MTIBWA SUGAR, MSHERY​

1640847892126.png
KLABU ya Yanga imemtambulisha kipa Abdultwalib Hamidu Mshery kutoka Mtibwa Sugar kuwa mchezaji wake mpya wa pili katika dirisha dogo baada ya kiungo mkongwe, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ kutoka Azam FC.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

AJIBU AONDOKA SIMBA SC, AJIUNGA NA AZAM FC.​

1640935888106.png

KIUNGO mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Ibrahim Ajibu Migomba amesaini mkataba wa mwaka mmoja baada ya kuvunja mkataba wake na SimbaSC.
Taarifa ya Simba SC leo imesema; “Kwa maslahi ya pande zote mbili, uongozi wa klabu umefikia makubaliano na mchezaji Ibrahim Ajibu kusitisha mkataba wake kuanzia leo Alhamisi Desemba 30, 2021,”.
“Kipekee tunamshukuru Ajibu kwa namna alivyojitoa kupambana kwa ajili ya Simba, na tunamtakia kila la kheri katika maisha yake,”.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

DENNIS NKANE ATAMBULISHWA RASMI YANGA SC.​

1641100773613.png
KLABU ya Yanga imemtambulisha kinda Denis Nkane kutoka Biashara United ya Musoma mkoani Mara kuwa mchezaji wake mpya wa tatu – akiwafuatia kipa Abdultwalib Mshery kutoka Mtibwa Sugar na kiungo Salum Abubakari ‘Sure Boy’ kutoka Azam FC.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Kiungo wa zamani wa Simba Sc na Kaizer Chiefs James Kotei amejiunga na DTB FC
🇹🇿
inayoshiriki Championship.
1641190230690.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Klabu ya DTB Fc inayoshiriki Championship
🇹🇿
imekamilisha usajili wa aliyekuwa mlinzi wa zamani wa Singida United Shafiq Batambuze
Timu hiyo inaendelea kufanya maboresho ya kikosi hicho katika usajili wa dirisha dogo mwezi huu.
1641190308176.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

𝗡𝗚𝗨𝗦𝗛𝗜 MCHEZAJI MPYA WA NNE YANGA DIRISHA DOGO.​

1641363921142.png

KLABU ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji Crispín Ngushi kutoka Mbeya Kwanza kuwa mchezaji wake mpya wa nne katika dirisha hili dogo linalotarajiwa kufungwa wiki ijayo.
Ngushi anaungana na wachezaji wengine watatu, kipa Abdultwalib Mshery kutoka Mtibwa Sugar na viungo Dennis Nkane kutoka Biashara United na Salum Abubakar kutoka Azam FC kufanya idadi ya wachezaji wanne wapya hadi sasa.
1641364036429.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
OFFICIAL: Salum Mayanga ametangazwa kuwa kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar ya Morogoro
🇹🇿

Mayanga amejiunga na Mtibwa Sugar akitokea Tz Prisons.
1641549210044.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
KOCHA Mkenya, Patrick Omuka Odhiambo amejiunga na Tanzania Prisons kwa mwaka mmoja kutoka Biashara United ya Mara.
Huo ni miongoni mwa mikakati ya Prisons chini ya Kamishina Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Meja Jenerali Suleiman Mzee kuhakikisha msimu ujao timu hiyo inapata tiketi ya kucheza michuano ya Afrika.

1641547496446.png


Pichani Odhiambo akiwa na Mkurugenzi wa Ufundi wa Jeshi la Magereza nchini, Kelvin Frednand wakati wa kusaini mkataba huo.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
OFFICIAL: Mlinzi wa kati Kelvin Yondani amejiunga na Geita Gold Fc
🇹🇿
akiwa kama mchezaji huru mara baada ya kumaliza mkataba wake na Polisi Tanzania
🇹🇿

1641633112328.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

PRISONS YASAJILI WASHAMBULIAJI WAWILI WAPYA.​

KLABU ya Tanzania Prisons imeimarisha safu yake ya ushambuliaji kusajili wachezaji wawili wapya, Mudathir Said kutoka Coastal Union ya Tanga na Abubakar Malika aliyekuwa Mwadui FC ya Shinyanga.


Mudathir Said aliyewahi pia kuchezea Taifa Jang’ombe ya Zanzibar akisaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na Tanzania Prisons.



Abubakar Malika akisaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na Tanzania Prisons.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Golikipa wa Simba, Jeremiah Kisubi ametua kikosi cha Mtibwa Sugar kwa mkopo. Kisubi ataziba pengo la Mshery ambaye amesainiwa Yanga.
1641819717042.png
1641819785119.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
YANGA YAMPA DILI KIPA TAIFA JANG'OMBE.
Aliyekuwa mchezaji bora wa mechi kati ya Yanga dhidi ya Taifa Jang'ombe, golikipa Hussein Thomas amesajiliwa na timu ya Tanzania Prisons. Kipa huyo alicheza kwa ubora licha ya kufungwa mabao 2-0 na Yanga amesaini kuwatumikia 'wajelajela' ambao wamesema wamefanya kazi kubwa kumshawishi asaini.
1641820149725.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kotei ashushwa Dar usiku mnene.​

1641821108357.png
HII inaweza kuwashtua mashabiki wa Simba, ila ndio ukweli ulivyo klabu ya DTB, vinara wa Ligi ya Championship ni balaa baada ya kumshusha usiku mnene kiungo wa zamani wa Msimbazi, James Kotei kisha kumpa mkataba wa miaka miwili fasta ili kuichezea timu yao.
Nyota huyo aliyeitumikia Simba kwa misimu kama mitatu tangu 2016 hadi 2019 kisha kutimkia Sohar SC ya Oman ambako baada ya kuvunja mkataba wake sasa amerejeshwa nchini lakini sio kukipiga tena Msimbazi ila kwa DTB inayozidi kutisha kwenye Championship.
Mmoja wa viongozi wa juu wa DTB ambaye hakutaka jina lake kutajwa aliliambia Mwanaspoti kuwa kiungo huyo atatambulishwa rasmi Januari 15, ambayo ni siku ya mwisho ya dirisha dogo la usajili kufungwa.
“Ni kweli Kotei tupo naye hapa nchini kwa mapendekezo ya kocha Ramadhan Nswanzurimo na tulitarajia kumtangaza kama sapraizi kwenye mchezo wetu na Kitayosce Januari 15,” alisema mtoa taarifa huyo.
Mbali na usajili wa Kotei ila DTB imenasa saini ya beki wa kushoto raia wa Uganda, Shafik Batambuze kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Kabwe Warriors ya Zambia kufuatia kuvunja mkataba wake wa mwaka mmoja.
Licha ya kutoweka wazi taarifa hizo, mratibu wa timu hiyo Muhibu Kanu alisema kuwa wachezaji bora watasajiliwa kwa mapendekezo ya Kocha Mkuu kwani malengo yao ni kucheza Ligi Kuu Bara.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0
Golikipa wa Simba, Jeremiah Kisubi ametua kikosi cha Mtibwa Sugar kwa mkopo. Kisubi ataziba pengo la Mshery ambaye amesainiwa Yanga.
View attachment 244
View attachment 245
BAADA ya tetesi nyingi hatimaye Mtibwa Sugar wamethibitisha kukamilisha mazungumzo na Simba kwaajili ya kunasa saini ya Jeremiah Kisubi ambaye ametolewa kwa mkopo na timu hiyo.
Kisubi alijiunga na Simba kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Tanzania Prisons ameitumikia Simba nusu msimu na sasa amejiunga na Mtibwa Sugar kwa mkopo.
Hata hivyo kama ambavyo Mwanaspoti iliwahi kuripoti kipa huyo kujiunga na walima miwa hao wa mkoani Morogoro, habari ilizopata leo zimethibitishwa rasmi baada ya mchezaji huyo kutambulishwa.
Mtendaji Mkuu wa timu hiyo, Swabri Aboubakari amesema tayari wamemalizana na kipa huyo tayari kuanza kuitumikia timu yao baada ya kumtambulisha leo.
Amesema wanaamini kujiunga kwa kipa huyo kutaziba bengo la aliyekuwa kipa wao namba moja Aboutwalib Mshery (21) aliyetimkia Yanga.
"Tumeshamaliza kila kitu na Kisubi wakati huohuo tunaendelea na kukamilisha utaratibu wa wachezaji wengine ili kuungana na wenzao kikosini" amesema Aboubakari.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Kiungo mshambuliaji Eliuter Mpepo
🇹🇿
amejiunga na Mbeya Kwanza Fc akitokea Interclub ya Angola
🇦🇴

Mpepo ambaye amewahi kuvitumikia vilabu vya Tz Prisons na Singida Utd atawatumikia walima mchele hadi utakapomalizika msimu huu.
1641877810989.png