Ligi Kuu Thread

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

KAMATI YAIPA USHINDI WA MEZANI NAMUNGO DHIDI YA MBEYA KWANZA​



KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeipa ushindi Namungo FC baada ya wapinzani, Mbeya Kwanza kugomea mechi ya Ligi Kuu Ijumaa Uwanja wa Ilulu mjini Lindi.
Pamoja na hilo, Kamati imechukua hatua mbalimbali juu ya masuala tofauti ya ukiukwaji kanuni katika mechi za hivi karibuni.




 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MPOLE AFUNGA BAO LA 13 GEITA YAIDIDIMIZA MBEYA KWANZA SONGEA​


MSHAMBULIAJI George Mpole amefunga bao la 13 la msimu, timu yake Geita Gold ikiibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Mbeya Kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Maji Maji Jijini Songea mkoani Ruvuma.
Mpole alifunga bao hilo pekee dakika ya 12 na kwa ushindi huo, Geita Gold inafikisha pointi 34 na kupanda nafasi ya nne, ikizidiwa pointi mbili na Namungo FC baada ya wote kucheza mechi 24.
Mbeya Kwanza hali inazidi kuwa tete baada ya kichapo cha leo, ikibaki na pointi zake 21 za mechi 24 na sasa inashika mkia kwenye ligi ya timu 16.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

IHEFU WAKABIDHIWA KOMBE LAO LA CHAMPIONSHIP​



TIMU ya Ihefu SC ya Mbeya baada ya kukabidhiwa ubingwa wa Ligi ya Championship kufuatia mechi ya kirafiki na DTB leo Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

SIMBA NA YANGA ZATOZWA FAINI KWA MAKOSA TOFAUTI KIRUMBA​




KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini kwa makosa tofauti kwenye mechi zao kadhaa zilizopita za Ligi Kuu ya Tanzania Bara zikiewemo za Jumapili na Jumatatu Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.



 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

PRISONS NA GEITA GOLD ZAGAWANA POINTI SOKOINE​



WENYEJI, Tanzania Prisons wamegawana pointi na Geita Gold katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya Leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Jeremiah Juma alianza kuifungia Tanzania Prisons dakika ya 38, kabla ya Danby Lyanga kuisawazishia Geita Gold dakika ya 50.
Kwa matokeo hayo, Prisons inafikisha pointi 25 na kusogea nafasi ya 14, wakati Geita Gold pamoja na kufikisha pointi 36 inabaki nafasi ya tano baada ya wore kucheza mechi 26.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

POLISI TANZANIA YAICHAPA BIASHARA 2-0 MOSHI​


WENYEJI, Polisi Tanzania wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Biashara United katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Mabao ya Polisi Tanzania yamefungwa na Deusdedith Okoyo dakika ya na 31 na Tariq Seif dakika ya 41 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 33 na kusogea nafasi ya saba, wakati Biashara United inabaki na pointi zake 24 katika nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi 26.
Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitateremka daraja moja kwa moja na nyingine mbili zitakwenda kumenyana na timu za Championship kuwania kubaki Ligi Kuu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

DTB YA LIGI KUU NI SINGIDA BIG STARS FC​



BAADA ya kupanda Ligi Kuu ya Tanzania Bara, timu ya DTB imebadilishwa jina na kuwa Singida Big Stars FC na kituo chake kitakuwa ni Uwanja wa Liti uliopo Singida.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SHINDANO LA KUZICHANGIA SIMBA NA YANGA LAZINDULIWA LEO DAR​


SHINDANO maalum la mashabiki wa Simba na Yanga kupigia kura klabu zao, Ipi Zaidi likezinduliwa leo Jijini Dar es Salaam.
AzamTv ndiyo itakayoendesha shindano hilo na kila kura moja itapigwa kwa gharama yake Sh. 1,000 na fedha hizo zitaingia kwenye mfuko wa maendeleo ya klabu itakayopigiwa kura.
AzamTv wamesema kila siku katika kipindi Mshike Mshike Viwanjami watakuwa wanatoa taarifa za maendeleo ya zoezi la kura ili kujua klabu ipi inaongoza.