Yanga Thread

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

MOLOKO YUKO FITI KUIVAA AZAM KESHO CHAMAZI​





WINGA Mkongo wa Yanga , Jesus Moloko akiwa mazoezini viwanja vya Avic Town, Kigamboni kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Azam FC kesho Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.




 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA YAIZIMA AZAM CHAMAZI, YAIPIGA 2-1​

A0CC2771-573B-4BE1-B232-9B2A31AFE174.jpeg

VIGOGO, Yanga SC wamepiga hatua kubwa katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Azam FC usiku huu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Haukuwa ushindi mwepesi, kwani ilibidi Yanga watoke nyuma baada ya kutanguliwa kwa bao la mapema na Azam FC lililofungwa na mshambuliaji Mzambia, Rodgers Kola dakika ya 11.
Iliwachukua dakika sita tu Yanga kusawazisha bao hilo, mfungaji beki Mkongo Djuma Shabani kwa penalti kufuatia kipa Ahmed Ali Suleiman Salula kumdaka miguu kiungo Mrundi, Saido Ntibanzokiza akiwa anakwenda kufunga.
Na kinara wa mabao wa Yanga, Mkongo mwingine, Fiston Kalala Mayele akaifungia timu hiyo bao la ushindi dakika ya 78 akimalizia krosi ya Djuma Shabani, mchezaji mwenzake wa zamani wa AS Vita ya kwao, Kinshasa.
Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 51 katika mchezo wa 19 na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi 14 zaidi ya mabingwa wa zamani, Simba SC ambao hata hivyo wana mechi mbili mkononi.
Azam FC inabaki na pointi zake 28 za mechi 19 sasa katika nafasi ya tatu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Klabu ya Yanga Yatinga Nusu Fainali Ya Kombe la FA Baada ya Kuichapa Geita kwa Penati​


batch_WhatsApp-Image-2022-04-10-at-9.54.15-PM.jpg

Kikosi cha Yanga kilichoanza dhidi ya Geita Gold FC
KLABU ya Soka ya Yanga imefanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho maarufu kama FA kwa kuifunga klabu ya Geita Gold FC kwa jumla ya mikwaju ya penati 7-6 baada ya mchezo kumalizika kwa kufungana bao 1-1.

Goli la Geita Gold FC lilifungwa na Paul Chikola katika dakika ya 87 na lile la Yanga likifungwa na beki wake Djuma Shabani kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 93 ya mchezo.

WhatsApp-Image-2022-04-10-at-10.48.43-PM.jpg

Mchezaji wa Yanga Jesus Moloko akiwa katika majukumu yake uwanjani
Katika mchezo Kocha Mkuu wa Yanga Nassredin Nabi alipewa kadi nyekundu kutokana na kutokubaliana na maamuzi ya mwamuzi na kwa maana hiyo anatarajiwa kukosekana katika pambano la Ligi Kuu dhidi ya watani wa jadi Klabu ya Simba.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA YAWAELEKEZA WANACHAMA WAKE NAMNA YA KUONGEZA SALIO KWENYE KADI ZAO​



KLABU ya Yanga imetoa mwongozo kwa wanachama wake juu ya namna ya kuongea salio salio kwenye kadi zao mpya za uanachama za Kidijitali.


 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA YAICHAPA NAMUNGO 2-1 , MAYELE ATETEMA TENA​


VIGOGO, wameibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga leo yamefungwa na mshambuliaji Mkongo, Fiston Kalala Mayele dakika ya 17 na kiungo Mzanzibari, Feisal Salum Abdallah ‘Fei Toto’ dakika ya 39, wakati la Namungo limefungwa na Shiza Kichuya dakika ya 33.
Yanga inafikisha pointi 54 katika mchezo wa 20 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi 13 zaidi ya mabingwa watetezi, Simba SC ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi, wakati Namungo inabaki na pointi zake 29 za mechi 21 sasa nafasi ya tatu.

 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

UCHAGUZI WA MATAWI YANGA SC WASOGEZWA MBELE​



UCHAGUZI wa viongozi wa Matawi wa klabu ya Yanga umesogezwa mbele hadi mwishoni mwa mwishoni mwa mwezi ujao, imesema taarifa ya klabu leo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

DJUMA SHABANI HATARINI KUWAKOSA SIMBA JUMAMOSI​


BEKI hodari na tegemeo wa Yanga SC, Mkongo Djuma Shabani yuko shakani kuiwahi mechi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya watani wa jadi, Simba Jumamosi Uwanja sa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Shabani aliumia kwenye mechi iliyopita dhidi ya Namungo wiki iliopita mwishoni mwa mchezo na kushindwa kuendelea nafasi yake ikichukuliwa na Dickson Job dakika ya 78, ingawa Yacouba Sogne pia ataendelea kukosekana.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

BASHUNGWA MGENI RASMI MECHI YA WATANI, MANARA MWANACHAMA YANGA​




WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Innocent Bashungwa ndiye atakuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa watani wa jadi, Simba na Yanga Jumamosi Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.





Wakati huo huo, Msemaji wa Yanga, Haji Manara leo amekabidhiwa ya uanachama wa kidijitali ya klabu hiyo.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

YANGA YATOA SARE TENA, 0-0 NA PRISONS, MAYELE...​


WENYEJI, Yanga SC wamelazimishwa sare ya bila kufungana na Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Mshambuliaji Mkongo, Fiston Kalala Mayele atalala na mawazo leo baada ya kuikosesha nafasi mbili nzuri Yanga za kupata mabao kipindi cha kwanza.
Kwanza alipewa pasi nzuri na kiungo Feisal Salum dakika ya 12, lakini akashindwa kufanya maamuzi ya haraka hadi beki wa Prisons akatokea na kuondosha kwenye hatari.
Baadaye dakika ya 39 akaenda kupiga juu mkwaju wa penalti kufuatia Feisal kuangushwa kwenye boksi.

Kwa sare hiyo ya tatu mfululizo, Yanga inafikisha pointi 57 katika mchezo wa 23 na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi 11 zaidi ya mabingwa watetezi, Simba ambao wenyewe wana mechi moja mkononi.
Tanzania Prisons inafikisha pointi 23, mechi ya 23 nafasi ya 14 kwenye ligi ya timu 16, ambayo mwisho wa msimu mbili zitashuka na mbili zitakwenda kumenyana na timu za Championship kuwania kubaki Ligi Kuu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA SC YAZINDUKA, YAICHAPA DODOMA JIJI 2-0 JAMHURI​


VIGOGO, Yanga SC wamezinduka baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Ushindi huo wa kwanza katika mechi nne umetokana na mabao ya kiungo Dickson Ambundo dakika ya 11 akiiadhibu timu yake ya zamani na kipa Mohamed Yussuf aliyeudondeshea mpira langoni mwake katika harakati za kuokoa shuti la Zawadi Mauya dakika ya 35.
Yanga inafikisha pointi 60 katika mechi ya 24 na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi 11 zaidi ya mabingwa watetezi, Simba ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi.
Dodoma Jiji inabaki na pointi zake 28 za mechi 24 nafasi ya 10 sasa.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

YANGA SC YAACHANA KWA AMANI NA NTIBANZOKIZA​




KLABU ya Yanga imeachana na kiungo mshambuliaji wa Kimataifa wa Burundi, Saido Ntibanzokiza baada ya misimu miwili ya kuitumikia timu hiyo.


 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MATOKEO YA USAILI WA AWALI UCHAGUZI YANGA SC​




KAMATI ya Uchaguzi ya Yanga chini ya Mwenyekiti wake, Malangwe Ally Mchungahela imetoa matokeo ya awali ya Usaili kuelekea uchaguzi wa klabu hiyo Julai 10, mwaka huu.




 

Brenda

Mgeni
Oct 31, 2022
489
403
5
Dar es salaam
Inasemekana TFF walitupilia mbali ombi la Yanga kusogezwa mbele mechi yao dhidi ya Geita Gold
Yanga wana kikosi kipana kwanini wanalilia mechi isogezwe mbele? Maswali yakujiuliza sana ilighali Ulaya wanacheza mechi mbili kwa wiki championi ligi na ligi za ndani sisi tuna ugumu gani wakucheza mechi 2 kwa wiki?🤷‍♀️🤷‍♀️🤷‍♀️🤷‍♀️

Reply
Report Edit Delete
 

Brenda

Mgeni
Oct 31, 2022
489
403
5
Dar es salaam
1667369259831.png

BACCA HUU NI MUDA WA VITENDO SIO MANENO.
Wakati yanga wanamtambulisha beki Ibrahim Bacca kutoka KMKM ya Zanzibar, jicho lao mashabiki wa Yanga ni kuwa sasa wamepata mrithi wa Nadir Haroub Canavaro.

Ni michezo miwili ya ligi kuu iliyopita dhidi ya KMC na Geita Golg Bacca ameonekana kuonesha uwezo wake mkubwa katika mechi hizo, Ukuta wa Yanga ukiwa chini ya uangalizi wa Ibrahim Bacca na Job ulibaki salama na Yanga kutoka na "Clean sheet"

Ni mchezaji aliyekaa benchi kwa muda mrefu ila ameonesha kuwa bora zaidi na kukiwasha kwa viwango vya juuu

Bacca anasema kuelekea mchezo wa kombe la Shirikisho la CAF, dhidi ya Club Africain, " Huu ni muda wa vitendo na sio maneno tena"
 

Brenda

Mgeni
Oct 31, 2022
489
403
5
Dar es salaam
Yanga katika mchezo wao wa kwanza leo utakaochezwa majira ya saa 10:00 jioni utakaopigwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa, wametangaza viingilio vyao dhidi ya wapinzani wao Club Africain, ambao wamekwisha wasili nchini Tanzania wakiwa 34.


1667370506316.png
 
Last edited: