Yanga Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MTU WA MPIRA: Nani alimsajili Fiston Mayele pale Yanga?​

mayele pic

KUNA Fiston Mayele mmoja tu mtu anayeifanya kazi ya kufunga kuwa rahisi kama vile kutafuna karanga. Mwanaume wa shoka kweli. Wakati anatua Yanga ilionekana kama ni mchezaji wa kawaida. Wengi walimbeza kutokana na rekodi zake za kawaida pale AS Vita ya DR Congo. Mayele hakuwahi kuwa tishio sana pale DR Congo.
Hata hivyo, tangu ametua Yanga amebadilika na kuwa mchezaji hatari. Anajua kufunga. Ana kasi na utulivu wa kutosha. Ni kiwango hiki cha Mayele kimetufanya tumuone Heritier Makambo kama mchezaji wa kawaida. Mayele anakupa kila kitu ambacho straika halisi anapaswa kutoa. Muda wote ananusa hatari.
Anakwenda na mikimbio ya timu. Anawapa viungo washambuliaji wigo mpana wa kumpasia mpira. Yupo imara kwenye mipira ya juu na chini. Ni mastraika wachache wenye uwezo huo.
Kwa sasa kwenye ligi yetu hakuna kazi ngumu kama kumkaba Mayele. Hata kama hatafunga, basi atawaacha mabeki wa timu pinzani wakiwa hoi.
Utakumbuka namna ambavyo Joash Onyango aliteseka kumkaba wakati wa pambano la watani mwishoni mwa mwaka jana. Onyango alilala hoi kwelikweli siku ile. Nadhani hatamani kukutana na Mayele katika siku za karibuni. Kama kuna lulu kubwa ambayo Yanga imejipatia katika eneo la ushambuliaji msimu huu ni nyota huyo kutoka DR Congo. Kwa bahati nzuri zaidi ni kombinesheni nzuri aliyotengeneza na Saido Ntibazonkiza siku za karibuni. Mayele anazitendea haki pasi za Saido. Anaifanya Yanga kuwa hatari katika eneo la mbele.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Yanga yarejea Dar, kituo kinachofuata KMC
yanga dar pic

TIMU ya Yanga imewasili leo asubuhi saa 3:50 katika uwanja wa ndege wa JK Nyerere Terminal 2 wakitokea Mwanza.
Yanga jana walicheza na Geita Gold na kushinda 1-0 mchezo uliochezwa katika uwanja wa CCM Kirumba.
Baada ya kuwasili Mwananchi Digital lilifanya mazungumzo na kocha mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi na amesema walikuwa na mchezo mgumu licha ya kupata pointi tatu.
Nabi amesema licha ya kupata ushindi mechi yao na Geita Gold haikuwa nyepesi kutokana na wapinzani wao walivyokuwa wamejipanga.
Kocha huyo akizungumzia upande huo huo wa mchezo amesema; ”Walikuwa wanatumia nguvu sana, mchezaji mmoja anafanya faulo mara mbili iwa wachezaji tofauti lakini anapewa kadi ya njano.”
Nabi amesema amewapa mapumziko wachezaji wake kwa siku mbili tatu wakijiandaa na mchezo dhidi ya KMC Machi 16.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Zahera: Asikuambie Mtu, Msimu Huu ni Mayele Tu​

PPJaT3QdUXAhd.jpg

MKURUGENZI wa Soka la Vijana wa Yanga, Mwinyi Zahera, amesema straika wa timu hiyo, Fiston Mayele, ana kila sababu ya kuwa mfungaji bora msimu huu, labda tu azembee mwenyewe.
Zahera alisema suala la kuwa mfungaji bora kwake lipo kwa asilimia kubwa, kwa sababu amekuwa na uwezo wa kufunga kwenye kila mchezo uliopo mbele yake na kama akishindwa basi itakuwa ni uzembe wake mwenyewe.
Zahera aliliambia Championi Jumatatu kuwa Yanga ina wapishi wengi sana kwa sasa ambao wanaweza kumpikia mabao ya kutosha Mayele na yeye akawa anafunga kirahisi, kwa hiyo ni yeye tu kuweka juhudi kwenye kila mchezo.
“Yanga ina wapishi wengi wa mabao na Mayele naona kabisa ana kila sababu ya kuchukua tuzo hiyo na hata mwenyewe niliwahi kumueleza hivyo.
“Mayele amekuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza anayecheza zaidi ya dakika 80, kila mechi tena kwenye timu iliyoimarika kuanzia kipa hadi mbele, kazi ni kwake mwenyewe ila hakuna sababu ya kumzuia na kushindwa kufanya hivyo,” alisema Zahera.
Mayele alikuwa na mabao tisa kabla ya mchezo wa jana dhidi ya Geita Gold FC, akiwa nyuma kwa bao moja dhidi ya Reliant Lusajo wa Namungo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Shikalo azungumzia Yanga, Dube amliza​

Shikalo PIC

UKIANZA kutaja majina ya makipa ambao walikuwa na wakati mzuri ndani ya Yanga huwezi kuacha kulitaja jina la Faruk Shikhalo ambaye alicheza kwenye kikosi hicho kwa misimu miwili mfululizo akitafuta ugali wake na maisha mengine yaendelee.

Shikhalo aliondoka mwishoni mno kwenye kikosi hicho na kusajiliwa, Diara Djigui na kuwafanya mashabiki wengi wajiulize namna alivyoachana na timu hiyo huku wengi wao wakitarajia kuona akiendelea kuitumikia Yanga kwa msimu wa tatu.

Kwasasa kipa huyo yupo katika kikosi cha KMC akiendelea kufanya yake licha ya kukutana na ugumu wa namba mbele ya mkongwe, Juma Kaseja ana uhakika wa kucheza kutokana na uwepo wake kwa misimu mitatu mfululizo pamoja na unahodha.

Mwanaspoti lilimfuata Shikhalo hadi kambi ya timu yao iliyopo Bunju A na kupiga naye stori nyingi juu ya namna ambavyo aliondoka kwenye kikosi cha Yanga, maisha ambayo aliishi katika timu hiyo na malengo yake ya sasa akiwa KMC.

MISIMU MITATU MICHUNGU
Shikhalo anasema kwenye misimu yake mitatu ambayo amecheza Tanzania hawezi kusema alikuwa kwenye urahisi bali alikumbana na ugumu mkubwa wa kuzoea mazingira kwa uharaka kwa sababu upande wa Ligi ya Tanzania hakuna utofauti mkubwa.

Kipa huyo anasema kucheza Tanzania lazima ujue utamaduni ili upate nafasi, pia ilikuwa ni ngumu kujua viwanja bora na timu nzuri, lakini kwasasa anajua kila kitu kutokana na kukaa kwa muda mrefu nchini.

“Safari yangu haikuwa nzuri wala mbaya sana naweza kusema hivyo, kiukweli kwasasa najua viwanja vyote lakini awali ilikuwa ngumu, kwasasa najua hata Tanzania Prisons mshambuliaji fulani hatari kwahiyo inanisaidia kupambana uwanjani,” anasema na kuongeza;

“Tanzania mpira ni mgumu sababu kuna mazingaombwe mengi kwenye maisha ya mpira, ukikaa kawaida na wenzako kuna vitu unajifunza na kujionea kwenye ‘stori’, kikubwa namshukuru Mungu kwa kunisimamia mpaka leo naendelea kuwa Tanzania nikiwa naenda mwaka wa tatu.”

YEYE NA MNATA FRESHI TU
Kama unazani makipa Metacha Mnata na Shikhalo walikuwa kwenye sintofahamu wakati wanaitumkia Yanga basi unajidanganya kwa sababu majamaa hao walikuwa wanashirikiana vya kutosha kuhakikisha timu yao inashinda na kujiweka sehemu nzuri.

Shikhalo anasema anamshukuru sana Mnata kwa misimu miwili waliyokuwa wote kwa sababu walipitia kwenye wakati mgumu na mzuri na hayo yote yalikuwa katika harakati za kuipambania timu yao ipate ushindi kwenye mechi zao.

“Mnata ni mtu ambaye tulipeana changamoto vizuri sana bila kumsahau Kabwili (Ramadhan) alikuwa akitusapoti, changamoto kwenye timu kubwa ni kawaida kwa sababu kuna muda yapo mabaya na muda mwingine unapitia mazuri,” anasema na kuongeza;

“Yanga ni timu kubwa na namshukuru mwenyezi Mungu nimecheza kwenye kiwango kikubwa, presha yake imenijenga kwa sababu unapozungumzia kuhusu mchezaji mzuri basi ni yule ambaye anaweza kuendana kwenye mazingira ya kucheza kwa presha.”

Shikhalo anaongeza na kusema;”Kabwili naye sio kipa mbaya ni mzuri na kwa baadaye atakuja kuwa kipa mzuri kama ataendelea.”

DUBE AMLIZA
Shikhalo anasema kwa misimu yote miwili ambayo amecheza Tanzania akiwa na Yanga hawezi kusahau kabisa bao alilofungwa na mshambuliaji wa Azam, Prince Dube Aprili 25, 2021 kwani lilimfanya amwage chozi uwanjani baada ya kuona amewaangusha wenzake.

Yanga kwenye mchezo huo ilifungwa 1-0 na mchezo ulimalizika Azam ikiibuka na ushindi huku wakiweka pointi tatu mfukoni.

“Nilijihisi kabisa nimewaangusha wenzangu kwa sababu tulipambana sana licha ya kukosa mabao mengi, kwa muda ule kuruhusu bao dah sikuwa poa, hakuna mtu ambaye anapenda kuwaangusha wenzake na nashukuru Mungu baada ya mchezo wenzangu waliniambia imeshaisha maana huu mpira leo kwangu kesho kwao,” anasema na kuongeza;

“Nashukuru Mungu upande wa mashabiki sikuwahi kuwa nao kwenye shida kabisa, muda wote ambao nimekuwa nao Yanga wa miaka miwili sikuwahi kuwa nao kwenye shida kabisa kiukweli nisiwe muongo na nashukuru kwa hilo.

BOCCO AMTESA DERBY
Shikhalo anasema kila wakati wanakuwa wanakutana na mechi ya watani wa jadi mtu ambaye alikuwa anamfikilia ni mshambuliaji wa Simba, John Bocco kwa sababu hakuwahi kabisa kukutana naye lakini baada ya kucheza naye mechi mbili basi alimjua vizuri.

Kipa huyo anasema Bocco ni mzuri sana kwenye mipira ya vichwa na sizani kama ana udhaifu bali kwenye upande niliokuambia basi ni hatari zaidi na hiyo ipo hata sisi kwetu makipa yupo ambaye anaweza kucheza uso kwa uso na mwingine anacheza mbali, mwingine krosi.

“Upande wa kina Kagere, Kahata nilishacheza nao Kenya lakini tofauti na Bocco, yeye pia baada ya kukutana naye mara mbili nilimjua vizuri, mimi nimecheza mechi nne za debi na Metacha nne kati ya nane kwahiyo nilimsoma vizuri.”

KOMBE LAMUUMIZA
Hapa Shikhalo anainama kisha anainuka na kusema licha ya kucheza misimu miwili Yanga na kumaliza nafasi ya pili hawezi kujipiga kifua kwa sababu hajafanikiwa kabisa kutoka na kombe la Ligi Kuu kwa sababu yalikuwa malengo yake yeye mwenyewe wakati anasajiliwa na Yanga.

Shikhalo anasema kama mchezaji alikuwa anatamani abebe ubingwa na Yanga lakini jambo hilo halijafanikiwa na baadaye alijitahidi kuhakikisha anawapa furaha mashabiki wa Yanga kwa kuwapa ubingwa wa Kombe la Mapinduzina alifanikiwa.

“Tulibeba ubingwa wa Mapinduzi na nilikuwa kipa bora, hivyo sikuwaacha watupu kabisa, mashabiki walikuwa na furaha kisha matunda niliyaona baada ya kupewa shilingi kadhaa na wao baada ya kuona nimewapa kitu fulani, nashukuru sana.”

Hali ya kukosa ubingwa inawatesa mpaka sasa mabosi wa Yanga wanahangaika kuhakikisha wanapata kombe msimu huu mbele ya Simba ambao wameanza ligi kwa kusua sua.

AACHWA MATAA YANGA
Shikhalo anapatwa na kigugumizi alipoulizwa namna ambavyo aliondoka Yanga, kipa huyo aliinama kisha anasema; “Kutokana na kufanya vizuri kwangu nikiwa na Yanga kiukweli sikutarajia kabisa kama naweza kuondoka Yanga na nilikuwa na ubora wakati mkataba wangu unaenda kuisha.”

Kipa huyo anafunguka zaidi na kusema kocha Nasreddine Nabi tayari alikuwa na pendekezo lake la Diara (Djigui) na mkubwa siku zote hakosei hivyo aliheshimu uamuzi wa kocha na kutakiana naye kheri kwa sababu mpira ni mchezo wa kuonana.

“Nilikuwa nasubili lolote ujue maana mkataba wangu ulikuwa unaenda ukingoni, tulivyomaliza msimu niliondoka kwenda nyumbani kwa ajili ya mapumziko na suala langu lipo kwa kocha lakini siku chache CECAFA ilipokuwa inaendelea Rama (Kabwili) alipata kadi nyekundu na mwalimu aliniomba nirudi,” anasema Shikhalo na kuongeza;

“Niliporudi nilicheza mechi moja wakataka niendelee kucheza lakini mimi nikawaambia hapana nitakuwa simtendei haki Kabwili kwa sababu yeye alikuwa ameshaanza, basi mwenzangu aliendelea na bahati mbaya tukatolewa kwenye mashindano.”

Shikhalo anaongeza na kusema; “Baada ya kama wiki akatambulishwa Diara huku mimi nikiwa sijaambiwa lolote lile, baadaye nikaitwa ofisini viongozi wakaniambia mwalimu amemtaka waliomsajili basi nikachukua mizigo yangu, nilipokea vizuri kwa sababu kwenye mpira huwa inatokea.”

APATA OFA NJE, DANTE AMVUTA KMC
Kipa huyo baada ya kuchukua mabegi yake na kuondoka Tanzania anasema alipata ofa tatu kutoka nchi ya Ethiopia na Zambia lakini alipoziangalia aliona Ligi ya Ethiopia ipo chini na upande wa Zambia kwenye kipengele cha pesa hawakuwa vizuri.

Wakati akiwa anazidi kuchang anua alipokea simu kutoka kwa bosi wa KMC na yeye aliangalia ubora wa Ligi pamoja na ofa akaona bora arejee nchini Tanzania kwa ajili ya kucheza na kuendelea kuonekana kama ilivyokuwa wakati anacheza Yanga.

“Unajua hata kama unapokea kidogo hapa lakini ligi ni nzuri na inafatiliwa na watu wengi, baada ya kupigiwa simu na kiongozi wa KMC basi nilikata simu na moja kwa moja nilimtafuta Dante (Andrew Vicent) nikamuuliza kuhusu timu na suala zima namna ambavyo inaenda, alinielelezea na mimi nikasema basi naweza.”

Shikhalo anasema baada ya kutua KMC haoni tofauti yoyote kutokana na yeye ni mtu wa watu hivyo anachukulia maisha kama kawaida na hakuna tofauti yoyote ile ambayo anakutana nayo isipokuwa mashabiki mtaani wanapokuona lazima waanze kukushangaa.

“Mtaani kidogo ilitaka kuwa changamoto lakini uzuri ni kwamba hawakuzungumzii kwa ubaya, upande wa wachezaji Dante alinipokea vizuri sana na niliwahi kufanya naye kazi kwa mwaka mmoja Yanga, nashukuru Mungu naendelea vizuri.”

HAJAKATA TAMAA
Shikhalo baada ya kuingia KMC alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kupoteza mechi kadhaa na baadhi ya mashabiki wakiona kama vile tayari ameshapoteza muelekeo lakini mwenyewe anasema yeye hakuwahi kukata tamaa na ndio maana timu yao imerejea kwenye mstari kidogo kidogo. “Nashukuru kwanza kwa uzoefu wangu mdogo wa miaka 10 kucheza Ligi Kuu imenisaidia kujua kuna nyakati ngumu na nyepesi kwenye mpira, kikubwa ni kuendelea kuweka bidii na kuomba sana kwa Mungu ili azidi kunifanyia wepesi kwenye kazi yangu,” anasema Shikhalo.

Kipa huyo anasema yapo magoli ambayo amefungwa na anayajutia lakini siku zote yeye ana amini kipa mazuri anafungwa mabao ya ajabu kwa sababu mabao magumu lazima ahakikishe anayacheza na hiyo sio kwake bali ni kwa makipa wote.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Nabi Ataja Mambo Mawili Yanga​

nabi-pic-data.jpg

ACHANA na mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Bara, Kocha Mkuu wa Yanga SC, Nasreddine Nabi, amewaambia wachezaji wake anataka kuona mambo mawili yakifanyika katika kila mchezo watakaoucheza.
Hiyo ni baada ya kuongoza katika msimamo wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 45, wakifuatiwa na mabingwa watetezi, Simba SC wenye 34 kabla ya jana kucheza dhidi ya Dodoma Jiji kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.
Msimu huu Yanga imepania kuivua ubingwa Simba baada ya kuukosa kwa misimu minne ambapo mara zote Simba wametawala.
Akizungumza na Spoti Xtra, Nabi alisema jambo la kwanza ambalo analitaka likifanywa na wachezaji wake ni kucheza soka safi la kuvutia lenye mchanganyiko wa pasi nyingi kwa ajili ya kuwapa burudani mashabiki.
Nabi alisema jambo la pili ni timu kupata ushindi mnono katika kila mchezo uwe wa ligi au Kombe la Shirikisho la Azam Sports. Aliongeza kuwa, anaamini wachezaji wake watafuata maagizo yake na kufanikisha hayo yote, licha ya kikosi chake kuandamwa na majeruhi wengi.
“Lipo wazi ligi ni ngumu, lakini hiyo isitufanye kupoteza malengo yetu tuliyojiwekea msimu huu ambayo ni kubeba makombe yote.
“Lengo langu la kwanza katika timu kuona inacheza soka safi, lingine kupata ushindi na siyo kujilinda, katika hilo nashukuru nimeanza kuliona.
“Mfano mchezo wetu wa ligi dhidi ya Geita, tulicheza soka safi la kutojilinda ambalo liliwavuruga wapinzani wetu na kufanikiwa kupata matokeo mazuri.
“Tuliwaheshimu Geita lakini sio kwamba wametuzidi baada ya kucheza katika kiwango bora, ubora wao umetokana na sisi kikosi chetu kuwa na majeruhi wengi ambao hivi karibuni wataanza kuonekana baada ya kupata nafuu baadhi yao.
“Kila siku ninaendelea kuwaongezea mbinu wachezaji wangu zitakazotufanya tuendelee kuwa bora na kucheza katika kiwango kizuri zaidi ya sasa wanachokionesha,” alisema Nabi.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Makipa Yanga wamweka mtu kati Manula.​

manula pic

Yanga imeendelea kuweka rekodi nyingine ya ubora ikitoa makipa bora wawili katika makipa ambao lango lao lipo salama.
Katika takwimu ambazo zimetoka Bodi ya Ligi Kuu zinaonyesha kipa wa Yanga Diara Djigui na Aishi Manula wa Simba kwasasa wako katika nafasi moja wakiwa na mechi 9 ambazo hawajaruhusu bao 'clean sheets kwenye mechi 17 ambazo timu zote zimecheza mpaka sasa ligi ilipofikia.
Hata hivyo makipa hao wawili ambao ni chaguo la kwanza katika klabu zao wametofautiana katika idadi ya mabao waliyoruhusu ambapo Manula ameruhusu mabao 5 huku Diara akiruhusu mabao 4.
Nyuma ya makipa hao yupo kipa Aboutwalib Mshery ambaye ni kipa chaguo la pili katika kikosi cha Yanga ambaye ana mechi 8 bila kuruhusu bao.
Katika mechi hizo Mshery amefanikiwa kumaliza mechi tatu bila kuruhusu bao akiwa na jezi ya Yanga huku 5zilizobaki akihama nazo akitokea Mtibwa Sugar.
Kipa huyo kijana alisajiliwa na Yanga katika dirisha dogo la usajili msimu huu akitokea Mtibwa akija kusaidiana na Diara katika lango la vinara hao wa Ligi.
Nyuma ya makipa hao wapo makipa wa zamani wa Yanga Metacha Mnata ambaye sasa anaichezea Polisi Tanzania na Mussa Mbisa wa Coastal Union aliyewahi kuichezea Yanga ya vijana ambao wote wawili wana mechi 6 kila mmoja bila kuruhusu bao.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Yanga: Sisi Bado Tupo Sana Kileleni​

yanga-mayeleee.jpg

UONGOZI wa Yanga umeweka wazi kwamba bado upo nafasi ya kwanza na kwa wale ambao wanafikiria kwamba watapoteza kwenye mechi za hivi karibuni hilo walisahau.
Ikiwa imecheza mechi 17 kibindoni imekusanya pointi 45 haijapoteza mchezo hata mmoja zaidi ya kuambulia sare kwenye mechi tatu pekee na moja kati ya sare hizo ni ile iliyopata mbele ya Simba.
Ofisa Habari wa Yanga,Hassan Bumbuli alisema kuwa bado wapo nafasi ya kwanza jambo ambalo litawafanya wadumu hapo mpaka ligi itakapokamilika.
“Sisi tupo nafasi ya kwanza na tunazidi kupambana kwa ajili ya mechi zijazo kikubwa ni kuona kwamba tunaendelea pale ambapo tuliishia mzunguko wa kwanza na hilo linawezekana.
“Malengo yetu ni kuona kwamba tunatwaa ubingwa lakini sio kazi nyepesi kwa kuwa kila timu inapambana kuona kwamba inashinda mechi zake hasa inapokutana na sisi ila hilo la ufundi linafanyiwa kazi na benchi la ufundi,” amesema.
Kinara wa utupiaji ni Fiston Mayele akiwa ametupia mabao 10 kibindoni na pasi zake ni tatu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA NA SOMALIA 1-1 MECHI YA HISANI CHAMAZI​

AVvXsEhgO1EgKwfMo5xi2iet9zXYeoNdD7F2IQeomuEBKew2SRw7s-tAna1A-VmoGeYL42wA7jgUTKaNiqc616P9HJ5fZmiUYqe1bJ56jHn-f85doGD2sn-esgjYuBhB43eHrsQOMTdj6d4N7zJXsxl_IvY41Iw3p7xon1227Sr2H3L04W8x32C-aT9ISw9D=w640-h468

VIGOGO, Yanga SC wamelazimishwa sare ya 1-1 na timu ya taifa ya Somalia katika mchezo wa kirafiki leo Uwanja wa Azam Comolex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Zakaria alianza kuifungia Somalia dakika ya 18, kabla ya Mkongo Chico Ushindi kuisawazishia Yanga dakika sita baadaye.
Huo ulikuwa mchezo maalum kuchangia taasisi ya Ally Kimara Foundation, kijana anayesumbuliwa na maradhi adimu aliyeanzisha mfuko huo kusaidia watoto wengine wote wnaosumbuliwa na maradhi hayo.
Mapema kabla ya mchezo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan alipiga simu na kuahidi kuchangia Sh. Milioni 15.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Mayele Aandaliwa Pacha Mpya Yanga​

yangasc_275284244_282803377325722_9114847024602308163_n.jpg

NASREDDINE Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga, amesema anaamini kwamba ipo siku atawaanzisha washambuliaji wake wawili kwenye mechi za ushindani ambao ni Fiston Mayele na Heritier Makambo.
Nyota hao wawili raia wa DR Congo, kwenye mechi za Ligi Kuu Bara msimu huu wakati Yanga ikishuka dimbani mara 17, hawajafanikiwa kucheza pamoja kutokana na mfumo wa mwalimu huyo ambaye anapenda kutumia mshambuliaji mmoja halisia.
Katika mechi zote 17, Mayele amekuwa chaguo la kwanza, huku Makambo akitokea benchi akipishana na Mkongomani mwenzake huyo.


274480447_373713300869546_3870057394497176153_n-1.jpg

Kwa sasa Mayele amekuwa akicheza sambamba na Saidi Ntibazonkiza kwenye eneo la ushambuliaji na kuonekana pacha yao imeanza kuiva.
Akizungumza na Spoti Xtra, Nabi alisema: “Unaona kwa sasa ni Mayele anaanza kikosi cha kwanza kwenye mechi zetu, lakini yupo na mshambuliaji mwingine Makambo, hawa wote ni washambambuliaji wazuri na wanatimiza majukumu yao.
“Ipo wazi kwamba kuna siku wote watacheza pamoja kulingana na mchezo utakavyokuwa, ni suala la kusubiri kwani ambacho tunahitaji kwenye mechi zetu zote ni ushindi na si kingine.”
Mchezo ujao kwenye Ligi Kuu Bara, Yanga itacheza dhidi ya KMC unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Dar, Machi 19, mwaka huu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Siri 2 za msako wa ubingwa Yanga SC zafichuka​

yanga-mayeleee.jpg

KAMA unafikiri Yanga wana mpango wa kushuka kutoka nafasi ya kwanza katika msimamo wa ligi kuu, basi umejidanganya na ndio kwanza wameweka wazi kuwa wanahitaji kupata matokeo katika michezo yote ili waweze kutwaa ubingwa msimu huu, hasa kwa kupata ushindi dhidi ya KMC katika mchezo unaofuata.

Lakini Injinia Hersi Said amefichua siri mbili ambazo wanazitumia kusaka ubingwa msimu huu waliodhamiria ni lazima wabebe taji la Ligi Kuu Bara kwa namna yoyote ile.

Hersi ametaja siri ya kwanza kuwa ni kuhangaika na mchezo unaofuata, yaani wanachowaza inakuwa ni mchezo unaofuata tu. Hesabu za mchezo mmoja baada ya mwingine.

Pili, wamezungumza na wachezaji wao na kuwaambia wauchukulie kila mchezo kama fainali. Yanga ambao ndio vinara wa ligi kuu kwa sasa, watacheza dhidi ya KMC katika Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, Machi 19 wakiwa na kumbukumbu ya kushinda mchezo wa kwanza katika mzunguko wa awali kwa mabao 2-0.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Mkurugenzi wa Mashindano wa Yanga, Injinia Hersi Said, alisema kuwa malengo yao kwa sasa ni kuhakikisha wanapata alama katika kila mchezo unaofuata kutokana na mzunguko wa pili kuwa mgumu, jambo ambalo tayari wameshazungumza na wachezaji kwenye michezo hii ya mzunguko wa pili kuhakikisha wanaondoka na ushindi hasa katika mchezo unaofuata dhidi ya KMC.

“Kwa sasa hatufikirii kuwa tutacheza michezo mingapi iliyobaki na kuanza kuhesabu mechi ya ubingwa, ambacho tumewaambia wachezaji ni kwamba kila mchezo ni kama fainali kwetu katika huu mzunguko wa pili, hivyo ambacho tunatakiwa kufanya ni kushinda katika mchezo ambao upo karibu yetu.

“Mfano kwa sasa tunafikiria kuhusu mchezo wetu unaofuata dhidi ya KMC na wala hakuna kingine ambacho tunawaza, tunahitaji kupata matokeo mazuri katika mchezo huo ili tuendelee kukaa kileleni,” alisema kiongozi huyo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

AISHA WA YANGA PRINCESS ASAJILIWA LIGI KUU SWEDEN​



MSHAMBULIAJI wa timu ya wanawake ya Yanga, Yanga Princess, Aisha Masaka amesajiliwa na klabu ya BK Hacken FF ya Ligi Kuu ya Sweden.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA WAMPA POLE MFADHILI WAO GSM​



UONGOZI wa Yanga umempa pole mfadhili wao, Gharib Said Mohamed (GSM) kwa kuunguliwa na kiwanda chake cha kutengeneza magodoro cha GSM Foam mwishoni mwa wiki.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Nabi Ataja Siri Tano za Mayele​

yangasc_275284244_282803377325722_9114847024602308163_n.jpg

KOCHA Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi ametaja mambo muhimu ya Fiston Mayele yanayofanya aweze kuanza moja kwa moja kikosi cha kwanza.
Mayele ni mtupiaji namba moja ndani ya Yanga akiwa ametupia mabao 10 na pasi tatu katika mechi 17 ambazo Yanga imecheza ikiwa na pointi 45 kibindoni.
Akizungumza na Championi Jumatano, Nabi alisema kuwa Mayele ana mambo mengi ya muhimu ambayo anayafanya kabla ya mechi na kwenye mechi ikiwa ni pamoja na nidhamu pamoja na juhudi katika mazoezi.
“Mayele ni mchezaji mzuri unaona kwamba anaanza kikosi cha kwanza kwenye mechi nyingi kwa sababu ana nidhamu pia amekuwa akitoa ushirikiano kwa wachezaji pamoja na juhudi mazoezini na hata kwenye mechi pia.
“Akianza kwenye mechi amekuwa akiweza kufunga na wakati mwingine amekuwa akitoa pasi za mabao hivi ni vitu alivyonavyo na kila mchezaji ni muhimu kwenye kikosi hilo kila mmoja analitambua,” alisema Nabi.
Mchezo ujao wa Yanga ni dhidi ya KMC timu ambayo ilikuwa ya kwanza kufungwa na Mayele mchezo uliochezwa Uwanja wa Majimaji, Songea.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA WAMUENZI MAGUFULI KWA NA NAMNA HII​

74C6CFFC-4A19-4F6B-81FB-E8A0C53C3379.jpeg

VIONGOZI wa benchi la Ufundi na wachezaji leo waumeungana na Watanzania wote katika kumbukizi ya Mwaka mmoja wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliekuwa Rais wa Awamu ya Tano kwa kuwatembelea Wagonjwa katika Hospitali ya Ocean Road Jijini Dar es Salaam.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Saido, Moloko Wavuruga Mipango Yanga
Ntibaa.jpg

KOCHA Mkuu wa Yanga, Mtunisia, Nasreddine Nabi, amepanga kuliboresha eneo la winga ndani ya kikosi chake ambalo limeonekana kuwa na upungufu mkubwa.


Kauli hiyo aliitoa Jumamosi iliyopita mara baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara kumalizika kwa Yanga kushinda 2-0 dhidi ya KMC, uliochezwa Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.


Yanga hivi sasa inakosa huduma ya viungo washambuliaji, Saidi Ntibazonkiza ‘Saido’ na Jesus Moloko ambao wapo nje ya uwanja wakiuguza majeraha, wakitarajiwa kurejea kabla ya mchezo dhidi ya Azam FC, Aprili 6, mwaka huu.


Akizungumza na Spoti Xtra, Nabi alisema katika kikosi chake, eneo la winga ambalo hivi sasa linachezwa na Chico Ushindi na Denis Nkane, limeonekana kutotimiza majukumu yake vizuri ya kutengeneza mabao.


Nabi alisema mawinga hao waliocheza dhidi ya KMC, walishindwa kutimiza majukumu yao ya kupiga krosi kwa mshambuliaji, Fiston Mayele.


ushindi-pic-data.jpg



Aliongeza kuwa, anaamini katika mchezo ujao dhidi ya Azam eneo hilo litacheza vizuri ambalo amepanga kuliboresha mara baada ya timu hiyo kuingia kambini.

“Tulichelewa kuingia mchezoni na wenzetu walitumia udhaifu huo dakika 20 za mwanzo. Bahati haikuwa upande wao la sivyo wangepata si chini ya mabao mawili.

“Lakini umakini mkubwa wa golikipa wetu Diarra (Djigui) na mabeki uliweza kutuokoa kufungwa kipindi cha kwanza ambapo hatukuwa na utulivu mzuri hususani eneo la kiungo na winga.

“Nimeliona tatizo hilo, hivyo nitalifanyia kazi mazoezini mara baada ya timu kuingia kambini kujiandaa na mcheo ujao dhidi ya Azam ambao huenda nikawatumia baadhi ya mawinga niliokuwa ninawatumia akiwemo Saido ambaye amepona majeraha ya goti,” alisema Nabi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MAYELE AKIMPA DARASA CHIPUKIZI WA YANGA​

D4DE797A-81DA-4B34-863D-912F6214BC0D.jpeg

KINARA wa mabao Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Mkongo wa Yanga, Fiston Kalala Mayele akimpa maarifa ya kiushambuliaji na ufungaji mshambuliaji chipukizi wa timu hiyo, Yussuf Athumani katika mazoezi ya timu hiyo kambini kwao, Avic Town, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Yacouba Rasmi Yanga SC​

yangasc_273981881_4154637584638908_8217086733076312454_n-1.jpg

HABARI njema kwa Wanayanga ni kwamba, mshambuliaji wao, Yacouba Songne muda wowote kuanzia sasa atarejea ndani ya uwanja kuanza kuitumikia timu hiyo mara baada ya kuwa nje kwa kipindi cha takribani miezi mitano akiuguza majeraha ya goti.
Yacouba aliumia katika mchezo dhidi ya Geita Gold Oktoba 2, mwaka jana ambao Yanga waliibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Jesus Moloko ambapo yeye alitoa pasi ya bao hilo.
Akizungumza na Spoti Xtra, Daktari wa Yanga, Youssef Amar, alisema Yacouba kwa sasa yupo sawa na kuanzia Aprili 1 ataanza mazoezi.
“Yacouba kwa sasa yupo salama na anaendelea vizuri tofauti na hapo awali ambapo hali ilikuwa mbaya zaidi, kwa sasa tunasubiri mpaka Aprili 1 ndio aanze rasmi mazoezi ya ufiti ambayo ni pamoja na gym.
“Baada ya hapo ataanza mazoezi na wenzake kwa ajili ya kujiandaa kucheza mechi za ushindani ambazo zitakuwa zimesalia msimu huu, tuna imani ataanza kupatikana mapema sana kwa kuwa maendeleo yake ni mazuri,” alisema daktari huyo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA YAMPONGEZA KIONGOZI WAKE KWA UTEUZI​

94C72D38-6F75-474B-97A6-6D2C30E65394.jpeg

KLABU ya Yanga imempongeza Mwanasheria wake, Wakili Simon Patrick kwa kuteuliwa kwake kuwa mmoja wa Mawakili Wasaidizi wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).
2320B40D-A33E-4FD3-A65E-8295098D6192.jpeg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MASATU KATIKA KUNDI LA WACHEZAI WA YANGA​

maktaba%20ya%20bin%20zubeiry.jpg

BEKI wa Simba SC, George Magere Masatu katika kundi la wachezaji wa Yanga wakati wa mazoezi ya kupasha misuli moto kabla ya mchezo baina ya watani wa jadi mwaka 1993 Uwanja wa Taifa, sasa Uhuru Jijini Dar es Salaam.