Yanga Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Aucho Jeuri Nyie! Atupa Kijembe Simba​

yanga-2-1.jpg

BAADA ya kumaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara bila ya kufungwa huku wakiwa kileleni katika msimamo wakiwa na pointi 39, kiungo fundi wa Yanga, Mganda, Khalid Aucho ameibuka na kutamka ligi wataianza rasmi Februari 27, mwaka huu.
Yanga tarehe hiyo ambayo ni keshokutwa Jumapili wanatarajiwa kucheza mchezo wa kwanza wa raundi ya pili ya ligi dhidi ya Kagera Sugar, Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam, na kauli hiyo ya Aucho ni kama anawaambia Simba wasahau suala la ubingwa msimu huu kwani kazi ndio kwanza inaanza.
Kauli ya Mganda huyo imekuja baada ya kufanikiwa kuwafunga Mtibwa Sugar mabao 0 2-0 nyumbani kwao kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani mkoani Morogoro.

yangasc_265180616_1064414541016915_1049622209843011182_n.jpg


Ushindi huo umewawezesha timu hiyo kuwaacha watani wao, Simba kwa tofauti ya oint inane. Kwa mujibu wa Aucho, baada ya mchezo dhidi ya Mtibwa nguvu na akili zao wanazielekeza katika mchezo ujao wa ligi dhidi ya Kagera ambao ni muhimu kwao kupata matokeo mazuri.
Aucho alisema kuwa katika kuelekea mchezo huo wataingia uwanjani kusaka pointi tatu kama vile ndiyo wanaanza ligi.
. “Wachezaji wote tumesahau matokeo tuliyoyapata katika mzunguko wa kwanza wa ligi, badala yake tutaingia kutafuta pointi tatu Februari 27.
“Hivyo mchezo wetu ujao wa ligi (Kagera) tutaingia uwanjani kwa lengo moja pekee kupata ushindi. Na tutauchukulia mchezo huo kama vile tunaanza ligi.
“Nafikiri nitakuwa nimeeleweka vizuri nina maana gani, kama inavyojulikana malengo yetu katika msimu huu ambao kwetu tunahitaji kuchukua makombe yote, nimalizie kwa kuwaambia nawapenda mashabiki wa Yanga” alisema Aucho.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MAYELE ATETEMA MARA MBILI, YANGA YAITANDIKA KAGERA 3-0​

AVvXsEgXnTrOMRwFe87Aa1psZ2-Gb13Ctjjdl5Agdb8bm4v4WGHOvcMbcnw6uOM33jVVxMTrlMV064WMU6_qP3iW2AULjlP-ws8PkvVyKOFB8anhdYK33lt30wQlAUbs_9TrvztpHF3a_tZM8vPrte0UpZ2RTxdSU3RbjO9EFi-jggCUQjNMesSCuxiBrHFw=w640-h578

VINARA, Yanga SC wameuanza vyema mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Kagera Sugar usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga SC leo yamefungwa na mshambuliaji Mkongo, Fiston Kalala Mayele mawili dakika ya 30 na 50 na kiungo Mrundi, Saido Ntibanzokiza dakika ya 64.
Yanga ingeweza kuondoka na ushindi mnoni zaidi kama si wachezaji wake, Mayele, Ntibanzokiza na mtokea benchi, mshambuliaji Mkongo mwingine, Heritier Makambo kupoteza nafasi nzuri za kufunga.
AVvXsEgyvq-xiXZ4EVm1WZAY46OhTVNvlCrs_PwD1iVWYteQEHSEUkv36NSbhyx2qA9D9RKzEaSjikZgrSS6WQ4P5E5obYwifobKnjWn8it0Id6JNZp-_BB7y_QnhsPcmnZJ0ip1Cy5mMbBXNt-TLSlTabZqLPx9Nmx5uS01HSoRLzaR1swuVknWY1GByQKq=w640-h568

AVvXsEhLdrkursv07cyx74fRThFkPp9fX5vJQWd7JRIt8iNrEGKmCG94AhaeZhenOJTDEOPLTvdGXRuN0vTJs2IYP9mVag59r2ztzTJbISudCielwLq4aTdSR6hembO0xpwzEmAti1XLKM0-8sHCwgSvDYLNBqvKWm-KX3Dxyb7CtqIZ6r49g06Q7Efot8Iw=w640-h448

Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 42 katika mchezo wa 16 na kutanua uongozi wake kwa pointi 11 zaidi ya mabingwa watetezi, Simba SC ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi.
Kagera Sugar baada ya kupoteza mechi ya leo, wanabaki na pointi zao 20 za mechi 16 sasa katika nafasi ya nane.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

ZA NDANI KABISA: Kaseke ndo basi tena Yanga SC​

Kaseke PIC

ZA NDAANI kabisa ambazo hazina chembe za shaka yoyote ni juu ya safari inayotarajiwa kumkuta, Deus Kaseke ndani ya Yanga kwa msimu ujao.
Ni kwamba hatma ya kiungo mkongwe wa Yanga Deuse Kaseke italazimika kusubiri mpaka mwisho wa msimu kuangalia kama ataweza kuongezewa mkataba wa kuendelea msimu ujao.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Yanga zinasema Kaseke ambaye mkataba wake unafikia tamati mwisho wa msimu bado hakuna uhakika wa moja kwa moja kusalia katika kikosi hicho.
Wasiwasi huo umeongezeka zaidi kufuatia kiungo huyo kupoteza nafasi ya moja kwa moja kuanza katika kikosi cha kwanza cha Kocha Nasreddine Nabi anayemtumia mara chache akitokea benchi.
Inaelezwa Kaseke inabidi afanye maombi sana ili kumlainisha Nabi kwani ni yeye tu kwa sasa aliyeshikilia hatma yake kwa msimu ujao.
Nabi ndiye atakayeamua kubaki au kuondoka kwa Kaseke, huku utitiri wa viungo wa pembeni ukiiweka nafasi ya kiungo huyo wa zamani wa Mbeya City na Singida United kusalia kuwa finyu.
Kwa sasa Yanga ina mawinga 6 akiwamo Kaseke, Farid Mussa, Jesus Moloko, Chico Ushindi, Denis Nkane na Dickson Ambundo wanaotumika kila mara na kuonyesha uwezo mkubwa kikosini.
Taarifa zinasema, Nabi ameweka msimamo wake akisema anataka wasalie viungo watano kati ya waliopo sasa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kuna namna tunamkosea heshima Saido Ntibazonkiza​

Saido PIC

Saido Ntibazonkiza. Mtangazaji wa Azam TV, Baraka Mpenja hupenda kumuita ‘Godfather wa Bujumbura’. Ni mchezaji kweli kweli.
Jumatano iliyopita aliibeba Yanga katika mabega yake pale Manungu. Akaiamua mechi kupitia miguu yake. Akaifanya Mtibwa Sugar kile anachojisikia.
Saido alifunga goli la kwanza na kutoa pasi ya goli la pili Yanga ikinawiri pake katikati ya mashamba ya miwa. Ni sehemu ngumu kucheza. Tuliona kilichomkuta Simba pale.
Yanga ilikuwa ikirejea Manungu baada ya miaka Zaidi ya 20. Mtibwa Sugar huwa wanapaita Machinjioni lakini Saido alipageuza kuwa sebuleni kwake. Mechi ikawa nyepesi kwa Yanga.
Wengi tunaweza kumzungumza Saido baada ya mechi hiyo pale Manungu. Lakini ukweli ni kwamba tangu Saido amerejea katika kikosi cha kwanza cha Yanga hakuna mchezaji aliyefanya vizuri Zaidi yake. Labda Fiston Mayele tu.
Saido amekuwa na wastani mzuri wa magoli ya kufunga. Ndio mchezaji anayeamua Yanga ishambulie vipi. Ule ushawishi aliokuwa nao Feisal Salum mwanzoni mwa msimu sasa umehamia kwa Saido.
Anaisukuma timu mbele kwa kasi ya ajabu. Anatengeneza nafasi kwa wachezaji wenzake. Anakaa kwenye nafasi na kuifanya Yanga kuwa na utulivu wa kutosha katika eneo la kushambulia. Halafu ana utulivu mkubwa ndani ya eneo la hatari.
Kuanzia mwishoni mwa Novemba Saido amefunga magoli matano na kutoa pasi moja ya goli kwenye Ligi Kuu. Katika kipindi hicho Feisal amefunga goli moja tu na pasi moja ya goli.
Hii ndiyo sababu nasema kuna namna tunamkosea heshima Saido. Kwa sasa pale Yanga amekuwa na mchango mkubwa sana. Ni tofauti na anavyozungumzwa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kisinda Akubali Kurudi Yanga​

KISINDA-1.jpg

MZEE wa spidi 120, Tuisila Kisinda ambaye kwa sasa yupo ndani ya RS Berkane amesema kuwa anaweza kuja kucheza Tanzania tena ikiwa Yanga watahitaji huduma yake.
Kisinda alikuwa anacheza Yanga alijiunga na RS Berkane mwanzoni mwa msimu huu wa 2021/22 na jana alikuwa katika kikosi cha kwanza kilichoshinda mabao 2-0 dhidi ya Simba katika mchezo wa Kombe la Shirikisho, hatua ya makundi ambapo Simba ipo kundi D.
Kisinda amesema:”Naongea tu Yanga ni nyumbani kama bosi ananitaka ninarudi kucheza fresh, tutaongea tu fresh.
“Kwenye mpira hapa tunacheza na Tanzania tunaweza kucheza kwenye mpira fresh tu kila kitu kinawezekana,”.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

GSM, Mabosi Yanga Waweka Kikao Kizito Kujadili Pointi Za Ubingwa​

gsm.jpg

KATIKA kuhakikisha wanaendeleza moto wao wa ushindi mfululizo kwenye mzunguko huu wa pili na kufanikisha malengo yao ya kushinda ubingwa, uongozi wa Yanga
Jumamosi jioni ulikuwa na kikao kizito cha wadhamini, Kamati ya Utendaji, benchi la ufundi na wachezaji kilichofanyika katika kambi yao ya Avic Town, Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Yanga walimaliza mzunguko wa kwanza wakiwa vinara wa msimamo na pointi zao 39, ambapo jana Jumapili walivaana na Kagera Sugar kwenye mchezo wao wa kwanza wa mzunguko wa pili uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Yanga, Senzo Mbatha, alisema: “Tumefanya kazi kubwa katika michezo yetu ya mzunguko wa kwanza, tumekuwa na kiwango bora na hili linathibitishwa na rekodi mbalimbali ambazo tumeziandika, kuelekea mzunguko wa pili tunafahamu kuwa tutakutana na wakati tumedhamiria kutimiza malengo yetu.”
Akizungumzia maandalizi yao ya michezo ya mzunguko wa pili, Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli, alisema: “Kwanza uongozi unajivunia mafanikio ambayo tumekuwa nayo katika michezo yetu ya mzunguko wa kwanza, ambapo tumemaliza kama vinara wa msimamo tena tukiwa na pengo kubwa kati yetu na wale ambao wanatufuatia.
“Lakini tunajua kuwa mzunguko wa pili utakuwa mgumu maradufu, hivyo kwa kutambua hilo uongozi wa wadhamini wetu, Kamati ya Utendaji, benchi la ufundi na wachezaji kwa umoja Jumamosi jioni tulikutana kuweka mkakati wa pamoja kukusanya pointi tatu katika michezo ya mzunguko huu wa pili ili kushinda ubingwa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mayele kumbe 60% tu Yanga​

Yanga PIC

Mshambulia wa Yanga na kinara wa mabao, Fiston Mayele aliyetupia tisa katika Ligi Kuu katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar, akiwa ameiteka asilimia kubwa ya nchi kwa staili yake ya kushangilia, eti kocha wake Nesreddine Nabi ametoa tathmini ya kazi yake akisema ni asilimia 60 tu.Akizungumza na Mwanaspoti, kocha Nabi alisema mpaka sasa Mayele amefanya kazi yake kwa asilimia 60 tu, licha ya mashabiki kuzidi kupagawa na mabao yake na staili yake ya kushangili kwa kupiga mkono na kutetema.
Nabi alisema bado Mayele anaweza kufikia asilimia 40 ya kazi yake, lakini kuna vitu ambavyo ataendelea kuboreshwa taratibu.
“Mimi ndio nimemleta Mayele nilipomuona nilijua kwamba ni mtu atakayefanya makubwa sio tu Yanga, bali kwa ligi kwa ujumla kwa vile nilikuwa hapa msimu uliopita na kuona ni aina gani ya mshambuliaji atakayefanya kazi bora hapa.
“Hadi sasa naweza kusema amefanya kazi kwa asilimia 60 tu, ingawa bado kuna nafasi ya kufikia hata asilimia 100 yapo mambo anayotakiwa kumboresha zaidi,” alisema Nabi na kuongeza;
“Jambo kubwa ni kujiweka katika mazingira ya kufunga zaidi mara nyingi anakuwa anapokea mpira akiwa anaangalia eneo letu.”
Nabi alisema Mayele sasa anatakiwa kuboreshwa kupokea mipira mingi akiwa anaangalia lango la wapinzani hapo atafunga kirahisi.
Aliongeza kwamba kitu kingine ambacho kimesalia ni viungo wa pembeni kuwa na ubora wa kumtengenezea mashambulizi mazuri kwa kuwa na krosi rafiki.
“Tuna changamoto ya viungo wanaocheza pembeni bado hawajajua ni aina gani ya mipira ya ya kumpa Mayele, angalia krosi aliyopiga Saido (Ntibazonkiza) wakati tunacheza na Mtibwa mipira kama ile ya chini na juu inatakiwa iwe mingi.”

Marefa na mabao kukataliwa
Aidha Nabi aliongeza, Mayele bado amekuwa akikumbana na changamoto mbili nje ya ufundi wa timu yao kwa kuchezewa vibaya na mabeki, pia mabao yake ya wazi yakikataliwa.
“Wachezaji wakubwa wanalindwa kila mtu anaigiza shangilia ya Mayele hata wapinzani wetu, lakini jina lake linafanya mabeki kumkamia ila waamuzi hawaoni hilo,” alisema Nabi na kuongeza;
“Wachezaji wakubwa Ulaya wanalindwa angalia Messi (Lionel) na hata Ronaldo (Cristiano) yapo mazingira ya kulindwa.
“Pia kuna mabao yake mazuri tu yanakataliwa kwa sasa angekuwa na mabao hata 11 ingempa nguvu zaidi za kukimbia kufunga zaidi.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MFADHILI, GHALIB WA YANGA AFIWA NA BABA MZAZI​

AVvXsEgFtRQ71Iv-8p3ihXUZoc2u_xBP3SBRyVXxy9aO5Zr7kZoDzDhs0SkjuMgz0b-ypEWZdOYgC1UGoB6GZNMOyyBQkW3id_OxjBkxYyIX6gaEIE_4bnccKFEUsJvht68k5-f17hrgNJkPPbxlrHgaI6X98tSo3LQ033Pup5_vjby9efCS0W6chNhxHX44=w640-h424

MFADHILI Mkuu wa klabu ya Yanga na Mwenyekiti wa Makampuni ya GSM Tanzania, Gharib Said Mohammed amefiwa na baba yake mzazi, Sheikh Said Mohamed leo Jijini Dar es Salaam.



AVvXsEh2sFArdeQaOFok8CmCZbSJhF5JlesC3JKQE2-Y7Als2zwUSynOUczASrNfKEYUEApivnz8NkTNriojJWkj--gRZwgKpbh_rPIXNNJWOgqOwcgTctMTya5UTL7J6AAeSwUrWhw1jZOuGTToy1sWcQPigPSC1QxMekiqQ5P2vQnVL5Quvu_NTVRj62L8=w640-h640
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Siri nzito Yanga, Bangala, Aucho watajwa​

siri pic

YANGA imetoa tathimini ya mzunguko wao wa kwanza wa ligi lakini ndani yake yakatajwa mambo manne mazito yaliyoibeba timu hiyo huku mastaa Khalid Aucho na Yannick Bangala wakitajwa.
Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Yanga Mhandisi Hersi Said ameliambia Mwanaspoti kwamba mzunguko wa kwanza umeakisi mipango bora ya uwekezaji ndani ya kikosi chao.
Alisema mambo yaliyowabeba kwanza ni ubora wa wachezaji waliobaki na wapya waliosajiliwa katika kikosi chao msimu huu akisisitiza wengi wana ubora mkubwa kulinganisha na wengi wa timu nyingine.
“Timu hii tulianza kuijenga tangu misimu miwili iliyopita haikuwa kwa msimu mmoja ila kilichotokea msimu huu tuliboresha zaidi tukiwabakiza wachezaji wachache na kuongeza wengine bora zaidi, nafikiri hapa ndipo mafanikio ya msimu huu yalipoanza,” alisema Hersi ambaye alihusika kwa asilimia 100 katika usajili huo kupitia wadhamini wao GSM.
“Ukomavu ambao timu yetu umeonyesha ni mkubwa nimeona kuna takwimu mbalimbali za ligi katika mzunguko wa kwanza zimetolewa katika kila ubora Yanga tuko juu wengine wakifuatia, hiki ndicho ambacho klabu imelenga.
Jambo la pili ambalo Hersi alilitaja ni upana wa kikosi chao ambapo mbali na kuwakosa wachezaji wao wanane walio majeruhi lakini bado wengine waliweza kuziba nafasi zao.
“Kikosi chetu kina majeruhi wanane kwasasa, wengi hapo ni wale ambao walikuwa kikosi cha kwanza lakini kitu bora ni pale waliokuja kuziba nafasi zao hawakuonyesha tofauti kubwa, bado timu iliendelea kupata matokeo yaleyale ya ushindi au labda sare hii inaonyesha tulikuwa na daraja zuri la ubora kati ya wale wanaoanza na wanaokuja kuingia baadaye.
“Unaweza kuangalia mfano pale golini tukiamua kuanza na Diara (Djigui) kama chaguo la kwanza kipa aliyekuja kuingia badala yake ana mechi tano bila kuruhusu bao ambaye ni Mshery (Aboutwalib) ambaye ubora wake ni mkubwa.”
Hersi aliongeza kwamba jambo la tatu ni uwekezaji ambao waliufanya katika kikosi chao ambapo ukiacha mazingira bora ya kikosi chao kuishi pia walikuwa na maboresho makubwa ya posho mbalimbali kulingana na ugumu wa mchezo.
“Wachezaji walikuwa wanapambana sana kwasababu kuna kitu kikubwa wanajua wanakipata mchezo unapokwisha, posho zimekuwa zikijieleza, unajua kuna kile kiasi ambacho tumekuwa tukiwapa.
“Lakini inapokuja mechi ngumu kuna mambo yanabadilika, mfano ni mchezo wa Mtibwa Sugar tulipowatajia kiasi cha fedha ambacho tutawapa tulishtuka kumuona mtu kama Bangala (Yannick) akiwaambia wenzake kwa Kiswahili ‘jamani twendeni tukachukue fedha zetu’ wakati wakiwa wanaenda uwanjani.”
Aliongeza jambo la nne kuwa ni ubora wa kiungo wao Khalid Aucho na kiraka Bangala ambao wamekuwa na nguvu kubwa ndani ya kikosi chao cha kwanza msimu huu.
“Watu wanamuona Aucho juu ya ubora wake uwanjani ambacho ndio kikubwa lakini tulio ndani tunajua mambo bora zaidi ya hayo ya Aucho, akiwa mazoezini kuna wakati amekuwa akisimamisha mpaka mazoezi akiwahimiza wenzake kupambana kama anaona kasi ya mazoezi ni ndogo.
“Ukomavu wake umekuwa mpaka kwenye mechi amekuwa msaada mkubwa katika kuwaunganisha wenzake na kuongeza ubora na juu ya yote ubora wake mwenyewe umekuwa ujieleza huyu ni mchezaji mwenye thamani kubwa ambaye tulipambana kumleta hapa.
“Kuna Bangala nakumbuka wakati namsajili kocha Ibenge (Florent) aliniambia Yanga tumepata wachezaji bora wawili walio ndani ya mtu mmoja, tunapomkosa mtu pale nyuma anaweza kucheza kokote na ubora ukawa mkubwa, angalia pia akicheza katikati amekuwa kiraka mwenye ubora mkubwa.
“Mwisho ni umati wa mashabiki wetu wanatubeba sana,” alisema.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Nabi Ataja Kinachomnyima Mabao Makambo Yanga
Heritier-Makambo-2.jpg

KWA mara ya kwanza Kocha Mkuu waYanga, Mtunisia Nasreddine Nabi ameibuka na kutaja sababu inayomfanya mshambuliaje wake Heritier Makambo kushindwa kufunga mabao.
Nyota huyo ameonekana kutokuwa na msimu mzuri kwake kutokana na kukosa nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Tangu kuanza kwa msimu huu mshambuliaji huyo hajafanikiwa kufunga bao katika ligi huku akipata ugumu wa namba kutoka kwa Mkongomani mwenzake, Fiston Mayele aliyekuwepo katika ubora mkubwa.
Akizungumza na Championi Jumatano, mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar, Nabi alisema ukame wa mabao unamfanya atoke mchezoni, apoteze umakini na kujikuta kukosa nafasi nyingi za wazi za kufunga.
Nabi alisema kuwa mshambuliaji huyo anatakiwa kutuliza akili yake na kupunguza presha anayoipata kutoka
kwa mshambuliaji mwenzake Mayele mwenye mabao tisa katika ligi.
Aliongeza kuwa anaamini kama akituliza akili zake, basi atafunga idadi kubwa ya mabao kutokana na kiwango kizuri alichonacho hivi sasa ambacho anakionyesha uwanjani.
“Kisaikolojia Makambo hayupo sawa, hiyo ni kutokana na presha kubwa anayoipata kutoka kwa mshambuliaji mwenzake Mayele aliyekuwa katika kiwango bora hivi sasa.
“Hiyo inaweza kumkuta mchezaji yeyote mwenzake anapofanya vizuri pale anapopata nafasi ya kucheza, Makambo anatakiwa kupunguza presha itakayomfanya acheze kwa kujiamini.
“Siku zote mshambuliaji unapopoteza nafasi za wazi za kufunga, hali ya kujiamini inapungua na kujikuta mchezaji akitumia vibaya nafasi ya kufunga kama ilivyokuwa kwa Makambo ambaye leo (Jumapili) tulipocheza dhidi ya Kagera alishindwa kutumia nafasi zaidi ya moja za wazi za kufunga, hiyo imetokana na presha aliyokuwa nayo
hivi sasa anatamani kufunga lakini anashindwa kutokana na kupania,” alisema Nabi na kuongeza kuwa.
“Ninaamini atatulia na kucheza vizuri ikiwemo kufunga mabao mara baada ya kumtengeneza kisaikolojia, kama kocha hilo ndiyo jukumu langu nitajitahidi kumbadilisha na kumuweka sawa.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

UBISHI WA MZEE WA KALIUA: Unawajua au unawaskia wachezaji wa Kikongo?​

Kaliua PIC

YANGA walitakata kwa Mkapa kisha Simba wakapoteana kule Morocco. Yanga wanazidi kupaa kileleni mwa msimamo wakizidi kukaribia kumaliza safari ya kuusaka ubingwa walioukosa kwa muda mrefu.
Simba wao walikufa Morocco na kuwaruhusu RS Berkane kushikilia usukani katika kundi lao. Niliandika hapa wiki iliyopita Simba walipaswa kusaka walau alama moja Morocco kwa sababu matokeo ya ASEC na USGN yanaweza kuliathiri kundi zaidi kama mechi yao haitaisha kwa sare.
Bahati mbaya nilichotabiri na kukihofia kilitokea, USGN wamepata alama tatu na kundi limezidi kuwa wazi kwa yoyote. Hili suala la kundi kuwa wazi limezidi kuwaumiza mashabiki wa Simba.
Mashabiki wa Simba wanaumia kwa sababu kuu mbili, kwanza ni hii niliyoieleza ya matokeo ya kipigo yanayozidi kuifanya njia ya robo fainali kuwa nyembamba zaidi. Pili ni wapinzani wao wa karibu Yanga wanafanya vizuri kwenye Ligi Kuu na wanatishia kuwanyang’anya ubingwa wanaoushikilia.
Kibaya zaidi ni tambo wanazokutana nazo kutoka kwa Yanga, utawaambia nini Yanga wakati wanacheza soka safi la kitabuni linalomruhusu Fiston Mayele kutetema kila mechi?
Jumapili alitetema mara mbili na kufikisha mabao tisa yaliyomweka bao moja nyuma ya kinara Reliant Lusajo wa Namungo. Hiki ndicho kinachowapa furaha Yanga na kuwaumiza Simba.
Yanga wana haki ya kufurahi kwa kilichotokea Jumapili lakini kipo kitu kimoja zaidi nilikiwaza kikanikatisha tamaa. Nitakueleza baadae kidogo.
Mayele alifunga bao lake la nane na tisa dhidi ya Kagera Jumapili. Ulikuwa mwendelezo wa kile alichozoea kukifanya mara zote. Pasipo ubishi Mayele ndiye mshambuliaji hatari zaidi ligi kuu msimu huu. Achilia mbali Lusajo na mabao yake, hakuna mshambuliaji anayewashughulisha mabeki kama Fiston Mayele.
Unaona kabisa sura za mabeki zina wasiwasi Mayele anapokuwa uwanjani, ni kwa sababu wana uhakika muda wowote atawapiga bao.
Mayele hafungi pasipo kusaidiwa! Anategemea pasi nzuri za mwisho na ‘krosi’ za uhakika. Moja kati ya watu ambao humpigia krosi za uhakika ni swahiba wake wa karibu Djuma Shaban.
Jumapili Djuma hakumpigia krosi yoyote ya bao lakini bado alikuwa hatari kutokea upande wa kulia wa Yanga, kando ya Djuma alikuwepo Yanick Bangala akicheza beki wa kati. Ni raia mwingine wa Congo anayewapa Yanga utawala wa mchezo akichezeshwa kama kiungo au beki kama ilivokuwa Jumapili.
Wacongo hawakuwepo mechi ya Yanga na Kagera tu, kule Morocco kwenye mechi ya RS Berkane na Simba walikuwa wakiliwakilisha taifa lao kupitia klabu zao, Simba walikuwa na Henock Inonga aliyekazana kuwaweka hai muda mwingi wa mchezo. Alilihami lango la Simba vema.
RS Berkane nao hawakuwa nyuma, walikuwa na mawinga wawili kutoka Congo, alikuwepo Tuisila Kisinda ambaye Simba wanamfahamu vyema. Upande wa pili walikuwa na Chadrack Lukombe aliyekuwa anawapa mateso mabeki wa pembeni wa Simba.
Kila aliposhika mpira uliona kabisa kwamba Simba wapo matatizoni, achana na Kisinda ambaye nina uhakika Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ atamtaja kama winga msumbufu zaidi aliyewahi kukutana nae.
Baada ya kumaliza kuvutiwa na wachezaji wacongo nilitamani kufahamu utumishi wao katika timu yao ya taifa. Huwezi kuamini! Licha ya ubora na sifa zote nilizozungumza kwa hawa wacongo hakuna hata mmoja anayetegemewa na taifa lake.
Hawa kina Djuma, Mayele, Inonga na Bangala wamewahi kuitwa timu ya taifa ya Congo lakini sio kwa sababu wanawategemea. Ni kwa sababu labda ilikuwa mechi ya kirafiki na hawakuwa na uwezo wa kuwapata wachezaji wao waliopo Ulaya au waliwaita katika mechi ya kimashindano ili kutimiza idadi ya wachezaji lakini hawakuwa sehemu ya kikosi kilichocheza mechi.
Ni hiki kitu kilinikatisha tamaa. Kumbe na ubora wote huu tunaouona kwa akina Mayele bado kwao ni wachezaji wa kawaida sana. Vipi kama wangekuwa Watanzania? Lazima wangekuwa wachezaji wanaotegemewa zaidi timu ya taifa kama tu ambavyo sasa wanategemewa kwenye klabu zao.
Vipi tungekuwa na mchezaji anayeanza RS Berkane? Lazima angekuwa staa timu yetu ya taifa. Unapokaa chini na kujihoji maswali kama haya, ndipo unagundua kuwa kumbe bado tuna safari ndefu sana ya kwenda.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Bangala, Mwamnyeto ni habari nyingine​

Bangala PIC

MSHAMBULIAJI wa Kagera Sugar, Hassan Mwaterema amesifu kiwango kinachoonyeshwa na mabeki wa Yanga, Yannick Bangala na Bakari Mwamnyeto.
Mwaterema amekuwa kwenye kiwango kizuri katika timu hiyo licha ya kupoteza mchezo wao na Yanga kwa kufungwa mabao 3-0, Februari 27, katika Uwanja wa Mkapa.
“Ni mabeki wazuri wanaostahili sifa, sio rahisi kucheza nao hata kidogo kutokana na ubora wao na isitoshe uliona kwenye mchezo wetu tuliokutana nao jinsi ambavyo nilipata shida,” alisema Mwaterema na kuongeza;
“Hadi sasa Yanga ndio timu pekee iliyoruhusu mabao machache (manne) hii tu inatosha kuonyesha ni kwa jinsi gani walivyokuwa muhimu kwenye kikosi chao.”
Akiwa na Kagera Sugar, Mwaterema amecheza michezo 16 na kufunga mabao mawili akiisaidia timu yake kushika nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi hiyo ikikusanya pointi 20.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Huyu Aucho! Bado sana​

Aucho PIC

KAMA unadhani kiungo wa Yanga, Khalid Aucho yupo kwenye kiwango kikubwa basi unajidanganya kwani mchezaji huyo ameshuka katika asilimia alizokuwa nazo wakati anaichezea timu ya Taifa Uganda ‘The Cranes’ kwenye fainali ya Mataifa Afrika (AFCON) 2019 nchini Misri.
Aliyekuwa kocha msaidizi wa timu hiyo na sasa ni kocha mkuu wa Mbeya City, Mathias Lule amefichua siri ya mchezaji huyo licha ya kufanya vizuri akiwa na Yanga bado hajarudi kwenye kiwango alichokuwa nacho AFCON.
Akizungumza na Mwanaspoti, Lule alisema siku zote Aucho ni mchezaji mzuri na bora kwenye timu lakini kwa sasa licha ya kufanya vizuri ndani ya Yanga anamwona anacheza chini ya kiwango.
“Aucho yule wa Afcon na huyu ni vitu viwili tofauti, inawezekana na maandalizi makubwa ambayo tulikuwa tumeyafanya tukijiandaa na fainali hizo ndio maana alikuwa bora,” alisema kuongeza;
“Wakati ule alikuwa na asilimia 90 hivyo alitupa vitu vyote ndani ya uwanja, huyu wa Yanga bado yupo kwenye asilimia 60-70 na ikitokea akafika asilimia zile za nyuma atawapa kitu kikubwa zaidi ya sasa, siwezi kusema kitu sana labda kwa nini amekuwa hivi kwa sababu sipo naye kwa sasa.”
Lule alisema bado ana nafasi ya kufanya makubwa na kupandisha asilimia zake kwa sababu mchezaji huyo bado umri wake ni mdogo hivyo muda anao wa kujiweka sehemu nzuri.
Aucho amesajiliwa msimu huu akiwa mchezaji huru na tangu alipoingia katika timu hiyo amejihakikishia nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kocha: Huyu Saido habahatishi​

Saido PIC

SAIDO Ntibazonkiza amewasha huko Yanga na benchi la ufundi limewaambia mashabiki hicho anachokifanya habatishi wala si moto wa kifuu.
Kwa mujibu wa Kocha Msaidizi wa Yanga, Cedrick Kaze kiwango cha Saido kimepanda kutokana na kuwa na fiziki nzuri kwa sasa ambayo imemwongezea morali na amepania kufanya jambo la tofauti.
Kocha huyo aliyekaa Barcelona kwa miaka kadhaa, ameliambia Mwanaspoti mchezaji huyo ni mzoefu wa ligi za Afrika hivyo akiwa fiti kifiziki amekuwa akifanya mambo ya tofauti sana uwanjani akishirikiana na wenzie wanaomwelewa vilivyo kuanzia mazoezini.
“Saido akiwa vizuri kwenye fiziki ni mchezaji mzuri sana, ana akili ya mpira na anajua kuamua mechi,” alisema Kaze ambaye ndiye aliyemsajili kikosini hapo.
Kocha huyo alisema kila mchezaji ndani ya timu hiyo kwa sasa ana morali kubwa ya kupigania mafanikio na kulinda hadhi ya timu, ndio maana wamekuwa wakizidi kupepea kila mara na wanatambua umuhimu wa hatua waliyopo katika mbio za ubingwa.
“Bado tuna mwendo mrefu lakini angalau njia inaonekana kufikia mafanikio,” aliongeza Kaze ambaye ni muumini wa soka la pasi.

KIWANGO CHAKE
Katika mabao sita aliyoyafunga kati ya 23 iliyonayo Yanga katupia kwa aina tatu, faulo, penalti na muvu. Mabao sita ya Saido yamefungwa katika viwanja vitano, nje na kufunga pia ametoa asisti tano.
Alifunga dhidi ya Namungo FC bao la penalti dakika ya 80 iliyotokana na beki Emmanuel Charles kumchezea rafu Feisali Salum ‘Fei Toto’ dakika ya 79, mchezo ukimalizika kwa 1-1, Uwanja wa Majaliwa, ilikuwa Novemba 20.
Bao la faulo alilopiga nje kidogo ya 18 dhidi ya Mbeya Kwanza dakika ya 17, alianza kuucheza mpira mwenyewe, kisha akampa pasi Fei Toto aliyechezewa rafu na mabeki na dakika 90 ziliamua Yanga kushinda 2-0, ilikuwa Novemba 30, Uwanja wa Sokoine.
Penalti nyingine, Saido alifunga dhidi ya Biashara United dakika ya 79 Uwanja wa Benjamin Mkapa, ilitokana Jesus Moloko kuchezewa rafu na Abdulmajid Mangaro, Yanga ikishinda 2-1, Uwanja Benjamin Mkapa, Desemba 26.
Alifunga bao kali la muvu katikati ya mabeki wa Coastal Union dakika ya 89, baada ya kupokea pasi ya Faridi Mussa, Uwanja wa Mkwakwani, Yanga ikishinda 2-0 Januari Mosi. Bao lingine la aina hiyo ni dhidi ya Mtibwa Sugar dakika 45+5, Februari 23, Uwanja Manungu, timu yake ikishinda 2-0.
Bao la tatu la muvu ni dhidi ya Kagera Sugar dakika ya 64 na alipita katikati ya mabeki wawili akiukokota mpira, huku akimhadaa kipa kutoka golini kisha akapiga shuti kabla ya kufika ndani ya 18, Yanga ikishinda 3-0, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Februari 27.
Tofauti na aina tatu za ufungaji wa Saido ambaye amekuwa akisisitiza ameiacha miguu yake izungumze, katika mabao yake sita, mawili ni ya penalti, moja faulo na matatu muvi.
Yanga imepania kubeba ubingwa msimu huu ambao imesajili mastaa ghali na wenye uzoefu kutoka kwenye nchi mbalimbali za Afrika.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA YAGAWA KADI MPYA BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR​


MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdullah akimkabidhi Kadi ya Pili ya Mwanachama wa klabu ya Yanga leo visiwani Zanzibar, Spika wa Baraza la Wawakilishi, Zubeir Ali Maulid.


MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdullah na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zubeir Ali Maulid wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Viongozi wa Yanga SC katika hafla ya utoaji wa kadi mpya za Uanachama kwenye Ukumbi wa Wawakilishi, Zanzibar.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Chico Akabidhiwa Beki Mbishi​

chico-ushindi-yanga.jpg

DAKTARI wa Viungo wa Yanga raia wa Tunisia, Yussef Ammar, amesema kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Mkongomani, Chico Ushindi ataanza kucheza mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya KMC anayocheza beki mbishi, Hassan Kessy, hivyo wawili hao kuna uwezekano mkubwa kukutana.
Mchezo huo wa Ligi Kuu Bara, utapigwa Machi 16, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.
Chico amekosa michezo minne hadi sasa kutokana na maumivu ya misuli aliyoyapata akiwa mazoezini, siku moja kabla ya mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam dhidi ya Biashara United, Februari, mwaka huu.
Michezo aliyoikosa Chico ni dhidi ya Biashara United, Mtibwa Sugar, Kagera Sugar na anatarajiwa kuukosa mchezo wa Jumapili hii dhidi ya Geita Gold utakaochezwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Akizungumza na Spoti Xtra, Ammar alisema Chico amepona maumivu hayo na wiki ijayo ataanza mazoezi magumu baada ya kumaliza program binafsi.
“Chico amepata nafuu ya maumivu yake, hivi sasa yupo katika program ya mazoezi maalum ya binafsi chini ya usimamizi wangu ambayo ataimaliza Ijumaa hii.
“Baada ya hapo ataanza mazoezi magumu ya pamoja na wenzake ya uwanjani katika kujiandaa na mchezo ujao wa ligi dhidi ya KMC tutakaoucheza Uwanja wa Mkapa,” alisema Ammar.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Saido, Aucho Wanalo​

Aucho PIC

YANGA inazidi kupasua anga ikionyesha inalitaka kombe na wakati mbio hizo zikiendelea kocha wao Nesreddine Nabi ameshusha mkwara mzito akiwachonganisha mastaa wake wakiwamo Saido Ntizbazonkiza, Fiston Mayele, Djigui Diarra, Khalid Aucho, Fei Toto na wengine kwamba hakuna mwenye uhakika wa namba kikosini, isipokuwa kwa yule tu anayefanya makubwa tu kushinda wenzake.

Vinara hao wa Ligi Kuu Bara wakikusanya jumla ya pointi 42 katika mechi zao 16 za msimu huu, wakiwa pia ndio timu pekee ambayo haijapoteza mechi yoyote hadi sasa, wanatarajiwa kuondoka kwenda jijini Mwanza kuwahi pambano lao la ligi hiyo dhidi ya Geita Gold litakalopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Jumapili hii, lakini kabla ya safari hiyo itakayofanyika kesho Ijumaa, Kocha Nabi aliamua kufunguka mambo kadhaa ikiwamo vita ya namba kwa vijana wake.

Akizungumza na Mwanaspoti, Nabi alisema wakati wakiifuata Geita Gold wikiendi hii kuna mastaa wake kama wawili au watatu wanarejea katika kikosi chake ambao wanakuja kuleta vita mpya ya nafasi.

Nabi alisema beki wake wa kati Dockson Job aliyesimamishwa mechi tatu anarejea kazini akiwa hana majeraha, kiungo Feisal Salum ‘Fei Toto’ naye anarudi kazini kufuatia kuukosa mchezo uliopita kwa kuwa na kadi tatu za njano huku pia winga Chico Ushindi akirudi kazini baada ya kupona majeraha.

Nabi alisema wakati wachezaji hao wakirejea wanakutana na wengine ambao walikuwa wanacheza huku nao wakionyesha ubora mkubwa kwa kikosi chao kusimama imara katika mechi zilizopita ambapo sasa wanatakiwa kupambana kila mmoja kuwania nafasi upya.

“Wapo wachezaji ambao wanarejea tunaweza kuwa nao katika mechi ijayo ambao wana ubora mkubwa lakini shida wanakuja kukutana na wenzao ambao katika kipindi hiki wamekuwa wakifanya makubwa,” alisema Nabi na kuongeza;

“Huu ushindani wa nafasi ndio utakaotupa nafasi ya kuwa bora zaidi kwa kuwa kila mmoja atapambana kutafuta nafasi ili acheze hakuna ambaye ana uhakika wa nafasi kwamba lazima ucheze kama makocha tutaangalia kipi bora kwetu na nani yuko sawasawa.”

Akieleza zaidi Nabi alimtolea mfano Farid Mussa akisema ameonyesha ubora mkubwa tangu alipopewa jukumu la kucheza kama beki wa kushoto ambapo mabeki wa upande huo ambao wako majeruhi wanatakiwa kujipanga kwa kuwa haitakuwa rahisi kufanya uamuzi wa kumuondoa Farid.

Alisema ushindani huo anautaka pia kuonekana kwa washambuliaji wa kati ambapo sasa wanapambana kuhakikisha mshambuliaji wao aliyepoteza makali Mkongomani Heritier Makambo naye anarudisha makali ya kuja kupambana na mfungaji bora wao mpaka sasa Fiston Mayele.

“Wakati huu tunawakosa Bryson (David) na Yassin (Mustapha) ambao ni majeruhi, tumekuwa tukimtumia Farid amefanya kazi bora sana ni lazima uwe na sababu kubwa ya kumbadilisha hata kama kuna watu wamepona, watatakiwa kuonyesha kitu tofauti na huyu anayecheza sasa.

“Hiki pia tunapambana nacho kwa Makambo (Heritier) nafikiri mliona jinsi hivi karibuni tulivyokuwa tunapambana naye mazoezini ili arudi katika ubora, kama Makambo akifanikiwa kurudi katika ubora wake kutakuwa na hesabu nzuri kwa kutumika kwake na Mayele.”

Yanga iliwakosa wachezaji 9 katika mchezo uliopita wakishinda kwa mabao 3-0 dhidi ya Kagera Sugar kati ya hao majeruhi walikuwa 7 ambao ni mabeki Abdallah Shaibu , Kibwana Shomari, Bryson, Crispin Ngushi, Yacouba Songne na mawinga Ushindi na Jesus Moloko.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

#TBT ZILITRENDI: Micho awatimua makomandoo Yanga​

Micho PIC

miaka ya nyuma na leo tunaenda hadi Machi 3, lakini mwaka 2007.
Siku hiyo buana iliripotiwa tukio la aliyekuwa Kocha Mkuu Mpya wa Yanga, Sredejovich Milutin ‘Micho’ kuamua kuwatimua makomandoo wa klabu hiyo.
Micho anafahamika kwa misimamo yake mikali na siku hiyo, aliwaonyesha jinsi alivyo baada ya bosi huyo wa benchi la ufundi kuamuru makomandoo hao washushwe kwenye basi lililokuwa limewabeba wachezaji.
Hali hiyo iliwaacha midomo wazi baadhi ya mashabiki wa Yanga kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam saa 1 usiku, dakika chache kabla ya basi lililokuwa limebeba wachezaji hao ili kuwapeleka kambini kwenye Hoteli ya Landmark baada ya kumaliza mazoezi yao.
Baada ya wachezaji kupanda kwenye basi hilo aina ya Toyota Coaster na kutaka kuondoka, Micho ambaye hutumia usafiri binafsi alichungulia dirishani na kuwaona makomandoo hao kama sita hivi.
Papo hapo akaamuru dereva kusimamisha gari haraka na kwamba kuna kitu kibaya kimetokea.
Micho alimwita kiongozi mmoja wa Yanga, Abdul Sauko kwa sauti kubwa na kumwambia bila woga hataki kuwaona makomandoo kwenye gari hilo na kuwataka wateremke haraka.
“Sauko...hilo gari ni kwa ajili ya wachezaji, sitaki kuwaona hao wanaoitwa makomandoo...waambie washuke wakapande teksi..hilo gari ni kwa ajili ya wachezaji tu,” alisema kocha huyo kwa hasira akifuta utamaduni wa kizamani wa makomandoo kupanda gari la wachezaji kwenda au kutoka uwanjani.
Baada ya kauli hiyo, makomandoo hao hawakushuka mara moja wakisubiri mazungumzo ya faragha yaliyokuwa yakiendelea pembeni baina ya Sauko na Micho, lakini baada ya kuona Mserbia huyo haelewi somo wakaanza kushuka mmoja baada ya mwingine na kutoka nje ya uwanja ili kupanda daladala.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MOLOKO AFANYIWA UPASUAJI, YANGA WATUA MWANZA​

AVvXsEgyLSy3sKnho-dPTwY_9zZZ7Zt1fmHFxTTlDsEAsB3uWwsIf29SEENXuFI3XisqTi4_jSbvoIRYrHq-n2zZVSQAMA2UKmU6NN0ppKVxzwvkVqBKQZHLReK7Oiw3f1YfjOkyJhxYdOE5_GpvoQtoZ0V3Qa69DLhdM56YmXHbnIOK_HdgMnQv-_G8Ph1W=w520-h640

WINGA Mkongo wa Yanga SC, Jesus Moloko amefanyiwa upasuaji leo Jijini Dar es Salaam baada ya kuumia mwezi uliopita na atakuwa nje kwa wiki zizisopungua tatu.
AVvXsEgMoIuFc2IOHEpzyR2HlFniaIGWiot2hGMb0q21ONklzOP_JDsLhPgid3B_spZ4uNHN1Nntqy--K9A_y6SwkNqJSPmzHAsItg1N2LwedPz968wiUb1KGzqelyp7s_AfxMfAXdnw0M6t1j5SsMnNMQrQIzM9QYRbP1b1h9-ldA2I8xbTavTlV7-DV7mk=w640-h598

AVvXsEjrX-htA5BipBaxS9Ka7LhXHfabO58rgA5KhHYHuGCP-GpHG_NvON0U_vTpvnogdvXOTzWU0BU70rdKRWRR1x7tL7VOIXbm9JC0TVelV-iq7uYuIO2k9HMQ_hXF5vAsWcg1oXI7eivILLmx2CATneKZkhZ07QBGqSXxa-5-pVvdFKx-6YmoezVMxcp4=w640-h576

Wakati huo huo, kikosi cha Yanga kimewasili Jijini Mwanza mapema leo tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya went, Geita Gold Jumapili Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MJUAJI: Kisa cha Yanga kupasuka 1976​

yanga pic

WAJUAJI tu ndio tunaolijua hili. Klabu ya Young Africans (Yanga) ilipasuka vipande viwili 1976.
Kisa na mkasa kilianza 1968. Mwaka huo Mwenyekiti wa Yanga, Kondo Kipwata alimwachia uongozi kwa hiari Mwenyekiti mpya, Mangala Tabu.
Sababu ya kumwachia. Alikuwa akitakiwa mtu msomi wa kuisimamia klabu na hata kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa jengo lake. Katika makubaliano ambayo hayakuwa rasmi, ilikubaliwa baada ya kukamilisha ujenzi Mangala arudishe uongozi wa klabu kwa Kipwata. Lakini mambo yalienda ndivyo sivyo. Hata baada ya kukamilisha ujenzi, Mangala alisimama imara na aliandaa mkutano ili kujisimika rasmi katika himaya hiyo ya Jangwani.
Wapinzani wake wakiongozwa na Kipwata na Mwambungu hawakukubali. Mgogoro ukaanza chinichini tangu 1975 japo mambo yalikuwa chinichini mwaka huo ndio Nyota Afrika ilibeba ubingwa.
Licha ya mgogoro kufukuta, Yanga ilienda kubeba ubingwa wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (sasa Kagame Cup). Katika fainali hizo za 1975, Yanga iliitungua Simba kwa mabao 2-0 na mwaka uliofuata Yanga ilikuwa inaenda Mombasa kutetea taji, tayari mgogoro ukiwa umekolea baada ya Kocha Tambwe Leya kuwashutumu baadhi ya nyota wake kuwa wanaihujumu timu hiyo.
Hii ni baada ya matokeo ya mchezo wa Klabu Bingwa Afrika (sasa Ligi ya Mabingwa Afrika) kati yao na Enugu Rangers, Yanga ikitolewa kwa faida ya bao la ugenini baada ya kutoka suluhu ugenini na sare ya 1-1 nyumbani.
Kabla ya kuondoka kwenda Mombasa, Tambwe alitaka kuwakata wachezaji wawili Sunday Manara na Gibson Sembuli, lakini uongozi wa Mangala ulipinga na kuwarudisha kundini. Katika michuano hiyo ya 1976, Yanga ilienda Mombasa na kufika fainali.
Hata hivyo, ilifika fainali na kukosa ubingwa mbele ya Luo Union ya Kenya kwa kufungwa 2-1. Huku nyumbani kulifanyika mkutano mkuu katika jengo la klabu hiyo na kina Mwambungu walimng’oa Mangala. Katika vurugu zilizotokea Mangala alitoroka klabuni kwa kuvaa baibui kupitia mlango wa nyuma kutokea Mtaa wa Nyati na Kongo na kutokomea zake.

Yanga ilibaki na wachezaji sita tu
Wachezaji wa Yanga walipotua Uwanja wa Ndege wa jijini Dar es Salaam (JNIA) walikutana na viongozi wa pande mbili. Wote wakiwa na usafiri wa mabasi ya kuwapokea. Upande mmoja alikuwa Mangala na mfadhili wa zamani wa Yanga, Shiraz Shariff na mwingine ulikuwa na Mwambungu na baadhi ya viongozi waliokuwa wakimsapoti Kipwata.
Wachezaji walitakiwa kuchagua basi la kupanda, huku viongozi hao wakitoa maneno ya ushawishi ili wapande mabasi yao. Ndipo Yanga ilipobakiwa na wachezaji sita tu. Wachezaji hao walikuwa ni Mwinda Ramadhani (Maajabu), Ahmed Omary na Juma Shaaban. Wengine ni Patrick Nyaga, Gibson Sembuli na Suleiman Said Sanga.
Wachezaji wengine wote waliondoka na Mangala ambaye alikuwa amepanga kuanzisha timu mpya. Hata hivyo, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) lilipinga kuanzishwa kwa timu mpya kipindi hicho.
Ilibidi wachezaji waliobaki wote wapelekwe Nyota Afrika ya Morogoro. Wachezaji walienda upande wa pili ni Athuman Mambosasa (aliyekuwa amejiunga Yanga akitokea Simba), Boi Idd ‘Wickens’, Leodegar Chilla Tenga, Jella Mtagwa, Kitwana Manara, Sunday Manara na Hassan Gobosi. Baadaye Juma Shaaban na Patrick Nyaga nao walirudi na kujiunga na wenzao Mseto ambayo pamoja na kuwa timu ya Morogoro, lakini ilikuwa ikifanya mazoezi Jangwani, Dar es Salaam.

Pan Africans yaanzishwa
Wachezaji wengine waliokuwa Yanga walikataa kujiunga na Nyota Afrika pamoja na kuwa upande wa Mangala. Hao ni waliotokea Yanga Kids na kupandishwa timu kubwa. Wachezaji hao ni Juma Pondamali, Jaffar Abdulrahaman na Mohammed Rishard ‘Adolf’. Wengine ni Mohammed Yahya ‘Tostao’, Kassim Manara, Said Mmanga, Ziara Mkuya, Sululu na Godwin Mapango. Hawa waliamua kujiunga na Klabu ya Breweries ya Dar es Salaam.
Hata hivyo, haikuchukua muda mrefu wachezaji hao walijiunga na wenzao wa zamani waliounda Mseto ya Morogoro na kuanzisha Pan Africans. Kwa kuwa kulikataliwa kuanzishwa timu mpya, upande wa kina Mangala walifanya ujanja na kujiunga na timu moja iliyokuwa na masikani Upanga jijini Dar es Salaam.
Timu hiyo iliyokuwa ya wachezaji wakongwe kufanya mazoezi ya kupunguza vitambi ilikuwa imesajiliwa kwa jina la Zama za Kale. Viongozi wa timu hiyo na wale wa Yanga zamani walikubaliana kufanya uchaguzi na wote kuiongoza timu hiyo ambayo waliibadili jina na kuiita Pan Africans. Jina likishabihiana na Harakati za Mapinduzi barani Afrika. Timu hii ilileta chachu kubwa ya upinzani kati yake na Yanga na hata kwa Simba. Nayo ilikuwa na masikani yake Mtaa wa Swahili na Mkunguni, Kariakoo jijini Dar es Salam ilipokaribishwa na Bendi ya Taarabu ya Egyption.
Baadaye timu hiyo ilihamia Mtaa wa Swahili na Amani, Kariakoo yalipo masikani hadi sasa na kwa jinsi ilivyoendeshwa kitajiri Pan ilitwaa ubingwa wa Bara 1982. Sio kubeba ubingwa, lakini ilisumbua nchini na kuvitoa jasho baadhi ya vigogo vya Afrika ikiwamo AS Vita ya DR Congo.
Kwa sasa timu hiyo inashiriki Ligi ya Championship ikiwa imeshasota sana ligi za madaraja ya chini kiasi cha kukimbilia kununua baadhi ya timu ili irejee Ligi Kuu bila mafanikio. Nawe sasa umeshakuwa mjuaji.