AFCON Thread

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
FULL TIME
Comoros
🇰🇲
0-1 Gabon
🇬🇦

⚽
Aaron Boupendza
No Auba No Problem
😜

#AFCON2021
1641878433326.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Ratiba ya mechi za leo za Kombe la Mataifa ya Afrika:
Saa 10:00 jioni, Algeria
🇩🇿
vs. Sierra Leone
🇸🇱

Saa 1:00 usiku, Nigeria
🇳🇬
vs. Egypt
🇪🇬

Saa 4:00 usiku, Sudan
🇸🇩
vs. Guinea Bissau
🇬🇼

#AFCON2021
1641890550518.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

NIGERIA YAICHAPA MISRI 1-0, ALGERIA YASHIKWA AFCON.​

1641964645006.png
TIMU ya taifa ya Nigeria imeanza vyema Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Misri leo, bao pekee la mshambuliaji wa Leicester City, Kelechi Iheanacho dakika ya 30 katika mchezo wa Kundi D Uwanja wa Roumdé Adjia Jijini Garoua.
Nao mabingwa watetezi, Algeria wamelazimishwa sare ya bila kufungana na Sierra Leone katika mchezo wa Kundi E Uwanja wa Japoma Jijini Douala.
Mechi nyingine ya Kundi D, Sudan imetoka sare ya bila kufungana na Guinea-Bissau Uwanja wa Roumdé Adjia Jijini Garoua.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Baadhi ya Wananchi wa Sierra Leone
🇸🇱
walivyokusanyika kwa pamoja kuishuhudia timu yao ya Taifa ikivaana na Algeria
🇩🇿
katika mchezo wao wa kwanza wa AFCON2021
Mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bila kufungana.
1641965094397.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Ratiba ya mechi za leo za Kombe la Mataifa ya Afrika:
Saa 10:00 jioni, Tunisia
🇹🇳
vs Mali
🇲🇱

Saa 1:00 usiku Mauritania
🇲🇷
vs. Gambia
🇬🇲

Saa 4:00 usiku Equatorial Guinea
🇬🇶
vs. Ivory Coast
🇨🇮

#AFCON2021
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

IVORY COAST, MALI NA GAMBIA ZASHINDA 1-0 AFCON.​

1642052725825.png

TIMU ya taifa ya Ivory Coast imeanza vyema Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Equatorial Guinea usiku wa Jumatano bao pekee la kiungo wa Sivasspor ya Uturuki, Max-Alain Gradel dakika ya tano katika mchezo wa Kundi E Uwanja wa Douala Jijini Douala, Cameroon.
Nayo Gambia imeichapa Mauritania 1-0, bao pekee la kiungo wa RFC Seraing ya Ubelgiji, Abdoulie Jallow mchezo wa Kundi F Uwanja wa Limbe Jijini Limbe.
Mechi nyingine ya Jumatano, bao pekee la mshambuliaji wa Sarpsborg 08 ya Norway, Ibrahima Koné kwa penalti dakika ya 48 limeipa Mali ushindi wa 1-0 dhidi ya Tunisia katika mchezo wa Kundi F hapo hapo Limbe.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Refa Janny Sikazwe
🇿🇲
kwenye mchezo wa AFCON2021 kati ya Tunisia
🇹🇳
vs. Mali
🇲🇱

🇿🇲
Ametoa faulo: 28
🇿🇲
Ametoa kadi za njano: 4
🇿🇲
Ametoa kadi nyekundu: 1
🇿🇲
Ametoa penati: 2
🇿🇲
Amemaliza mpira dakika ya 85' akarudisha uendelee akamaliza tena dakika ya 89'
Mchezaji bora wa mechi
😂
😂
😂

#AFCON2021
1642053149783.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

CAMEROON YASONGA MBELE AFCON BAADA YA KUIPIGA ETHIOPIA 4-1​

1642136787121.png
WENYEJI, Cameroon wamekuwa timu ya kwanza kuingia hatua ya mtoano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) baada ya ushindi wa 4-1 dhidi ya Ethiopia katika mchezo wa Kundi A leo Uwanja wa Paul Biya Jijini Yaoundé.
Mabao ya Cameroon yamefungwa na Karl Toko Ekambi mawili dakika ya nane na 67 na Vincent Aboubakar mawili pia dakika ya 53 na 55, baada ya Wahabeshi kutangulia kwa bao la Dawa Hottesa dakika ya nne.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
BURKINA FASO YAILAZA CAPE VERDE 1-0
1642136932554.png
Burkina Faso imeilaza Cape Verde 1-0, bao pekee la Boureima Hassane Bandé dakika ya 39 hapo hapo Paul Biya.
Kwa matokeo hayo, Simba Wasiofungika wanafikisha pointi sita baada ya mechi ya mbili na kuendelea kuongoza Kundi A wakifuatiwa na Burkina Faso na Cape Verde wenye pointi tatu kila moja, wakati Ethiopia inaendelea kushika mkia ikiwa haina pointi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Ratiba ya mechi za leo za Kombe la Mataifa ya Afrika
🔥

⏰
16:00
Senegal
🇸🇳
v Guinea
🇬🇳

⏰
19:00
Malawi
🇲🇼
v Zimbabwe
🇿🇼

Morocco
🇲🇦
v Comoros
🇰🇲

⏰
22:00
Gabon
🇬🇦
v Ghana
🇬🇭

Mechi gani hujapanga kuikosa?
1642168160653.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MOROCCO YASONGA MBELE AFCON, SENEGAL YASHIKWA​

1642229076540.png
TIMU ya taifa ya Morocco imeendeleza wimbi la ushindi katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuichapa Comoro mabao 2-0 usiku wa Ijumaa katika mchezo wa Kundi C Uwanja wa Ahmadou Ahidjo Jijini Yaoundé.
Mabao ya Morocco yamefungwa na kiungo wa Standard Liège ya Ubelgiji, Selim Amallah dakika ya 16 na mshambuliaji wa
Alkmaar Zaanstreek ya Uholanzi, Zakaria Aboukhlal dakika ya 89 na kwa ushindi huo, Simba wa Atlasi wanafikisha pointi sita na kufuzu Hatua ya mtoano ya michuano hiyo mbele ya Gabon yenye pointi nne, Ghana moja na Comoro ambayo haina pointi.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
FULL TIME
Gabon
🇬🇦
1-1 Ghana
🇬🇭

⚽
18': Andre Ayew
⚽
88': Allevinah
Ghana wanalazimika kutoa sare katika dakika za lala salama
1642232193448.png
 
Last edited:

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Ratiba ya mechi za leo za Kombe la Mataifa ya Afrika:
19:00 Nigeria
🇳🇬
vs. Sudan
🇸🇩

22:00 Guinea Bissau
🇬🇼
vs. Egypt
🇪🇬

Baada ya kutandaza soka safi dhidi ya Egypt na kuondoka na alama zote tatu, leo The Super Eagles
🦅
wanaendelea na burudani yao
🙌