AFCON Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Aboubakar Aingia Levo za Samuel Eto’o.​

Vincent-640x360-1.jpg

NYOTA wa timu ya taifa ya Cameroon, Vincent Aboubakar kwenye mashindano ya Afcon 2021 nchini Cameroon yeye anakiwasha tu kwa kucheka na nyavu.
Mpaka sasa yeye ni namba moja kwa utupiaji ambapo amefunga jumla ya mabao matano kibindoni. Timu ya Cameroon ambao ni wenyeji wa mashindano hayo wamekuwa kwenye mwendo mzuri ambapo tayari wametinga hatua ya 16 bora.
Kwa mwendo ambao anakwenda nao anaingia anga za mshambuliaji mahiri wa zamani wa timu hiyo Samuel Eto’o ambaye aliwahi kufanya maajabu kwenye fainali za Afcon.
Nyota huyo wa Cameroon, amwfunga mabao matano katika mechi tatu za makundi kwenye Afcon 2021 na hakuna mchezaji mwingine wa Cameroon amefunga mara nyingi zaidi katika msimu mmoja wa fainali za Afcon sawa na Samuel Eto’o ambaye naye alifunga mabao matano kwenye mechi tatu.
Eto’o alifanya hivyo mwaka 2006 kwenye mechi tatu na akarudia tena mabao matano 2008.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Milovan Atimuliwa Ghana.​

Milovan-Rajevac.jpg

BAADA ya kupata matokeo mabaya ya Ghana katika michuano ya AFCON inayoendelea, Wizara ya Michezo ya nchi hiyo katika mkutano wa dharura siku ya Ijumaa iliagiza Chama cha Soka cha Ghana kumfukuza kazi kocha wake Mserbia, Milovan Rajevac.
Licha ya kusitasita kwa FA kumtimua Rajevac, wizara hiyo inaonekana kushinda mzozo kuhusu mustakabali wa Mserbia huyo.
Katika kipindi chake cha kwanza akiwa na Black Stars Rajevac aliiongoza Ghana kutinga fainali za AFCON 2010 na Robo fainali ya Kombe la Dunia la 2010.
Kipindi chake cha pili hakikwenda kama ilivyotarajiwa kwani Ghana walitoka AFCON 2021 bila ushindi, wa kwanza wa aina yake katika historia ya Black Stars.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Mechi za leo AFCON.
Burkina faso vs Gabon saa moja usiku
Nigeria vs Tunisia saa nne usiku
Image
 
Last edited:

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

TUNISIA YAITUPA NJE NIGERIA AFCON.​


BAO la Nahodha, Youssef Msakni dakika ya 47 limeipa Tunisia ushindi wa 1-0 dhidi ya Nigeria katika mchezo wa Hatua ya 16 Bora Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika usiku wa Jumapili Uwanja wa Roumdé Adjia Jijini Garoua, Cameroon.
Mechi nyingine ya 16 Bora usiku huo, Burkina Faso ilitoa Gabon kwa penalti 7-6 kufuatia sare ya 1-1 Uwanja wa Limbe.


Image
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

CAMEROON NA GAMBIA ZATINGA ROBO FAINALI AFCON.​


WENYEJI, Cameroon wamefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Comoro usiku wa Jumatatu Uwanja wa Paul Biya Jijini Yaoundé.
Mabao ya Cameroon yamefungwa na Karl Toko Ekambi dakika ya 29 na Vincent Aboubakar dakika ya 70, wakati la Comoro limefungwa na Youssouf M'Changama dakika ya 81.

Comoro ilipata pigo la mapema kufuatia kiungo wake, Jimmy Abdou kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja dakika ya sita.
Comoro iliingia kwenye mchezo huo bila wachezaji wake nyota 12 kwa sababu ya majeruhi na kukutwa na virusi vya corona, wakiwemo makipa wote watatu, ambao ni Salim Ben Boina majeruhi, wakati Ali Ahamada na Moyadh Ousseini wana COVID.

Lakini beki wa kushoto wa Ajaccio ya Ligie 2 Ufaransa, Chaker Alhadhur aliyesimama langoni alifanya kazi nzuri mno.
Katika mchezo uliotangulia, Gambia iliitupa nje Guinea kwa kuichapa 1-0, bao pekee la mshambuliaji wa Bologna ya Italia, Musa Barrow dakika ya 71 Uwanja wa Bafoussam. Sasa Cameroon itakutana na Gambia katika Robo Fainali Jijini Douala Jumamosi.

Image
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
☑️
Mara yao ya kwanza kushiriki AFCON
☑️
Wameingia hatua ya 16 bora baada ya kuwafunga Ghana
🇬🇭

☑️
Beki wao wa kushoto amecheza nafasi ya Golikipa na kucheza kwa kiwango kikubwa
☑️
Wamepata kadi nyekundu dakika ya 7 lakini wamefanikiwa kupata goli mbele ya Cameroon
🇨🇲

Hawa ni mashujaa Comoros
🇰🇲
What a team!
#AFCON2021
272684015_5031601496899760_5448560880481214824_n.jpg
272630674_5031601493566427_8108670213149179004_n.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Mlinzi wa kushoto wa Comoros
🇰🇲
Chaker Alhadhur alianza kama golikipa katika mchezo dhidi ya Cameroon
🇨🇲
kutokana na kukosekana kwa magolikipa wao waliokumbwa na janga la virusi vya COVID-19.
Takwimu za Mlinzi wa kushoto wa Comoros
🇰🇲
Chaker Alhadhur hii jana akicheza kama golikipa dhidi ya Cameroon
🇨🇲

Inaweza kuwa picha ya Mtu 1
comoros.PNG
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MOROCCO NA SENEGAL ZATINGA ROBO FAINALI AFCON.​


MOROCCO imetoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya Malawi katika mchezo wa Hatua ya 16 Bora Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika usiku huu Uwanja wa Ahmadou Ahidjo Jijini Yaoundé nchini Cameroon.
Malawi ilitangulia kwa bao la mshambuliaji wa Orlando Pirates ya Afrika Kusini, Hellings Frank ‘Gabadinho’ Mhango dakika ya saba, kabla ya mshambuliaji wa Sevilla ya Hispania, Youssef En-Nesyri kuisawazishia Morocco dakika ya 45 na ushei na beki wa Paris-Saint Germain, Achraf Hakimi Mouh kufunga la ushindi dakika ya 70 kuwapeleka Robo Fainali Simba wa Atlasi.

Katika mchezo uliotangulia, Senegal ilikwenda Robo Fainali pia baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Cape Verde, mabao ya washambuliaji, Sadio Mané wa Liverpool dakika ya 63 na Cheikh Ahmadou Bamba Mbacke Dieng wa Marseille dakika ya 90 na ushei Uwanja wa Bafoussam.
Cape Verde ilicheza pungufu kwa muda mrefu, kufuatia wachezaji wake wawili kutolewa kwa kadi nyekundu,kiungo Patrick Andrade dakika ya 21 na kipa Josimar José Évora Dias ‘Vózinha’ dakika ya 57.
Morocco itakutana na mshindi kati ya Ivory Coast na Misri na Senegal itakutana na mshindi kati ya Mali na Equatorial Guinea zinazokamilisha Hatua ya 16 Bora.


Image
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

SITA WAFARIKI WAKIGOMBEA KUINGIA UWANJANI CAMEROON.​


WATU wasiopungua sita wamefariki na wengine zaidi ya 40 kujeruhiwa katika vurugu zilizotokea nje ya Uwanja wa Olembe Jijini Yaounde wakigombea kuingia kutazama mechi baina ya wenyeji wa Fainali za AFCON, Cameroon dhidi ya Comoro jana – Serikali ya nchi hiyo imethibitisha na kusema kwamba idadi ya vifo inaweza kuongezeka.
Maafisa wa hospitali ya Messassi wamesema wamepokea kiasi cha watu 40 waliojeruhiwa, ambao walikimbizwa hospitalini hapo na Polisi na wasamaria wema – na chanzo cha vurugu hizo imeelezwa ni walinzi ‘Stewards’ kufunga mageti kuzuia watu zaidi kuingia uwanjani – na baada ya tafrani hiyo ilishuhudiwa viatu, kofia na mawigi vikizagaa chini.
Katika mechi hiyo ya Hatua ya 16 Bora, Cameroon ilishinda 2-1 na kwenda Robo Fainali.
Pamoja na hayo, Hatua ya 16 Bora ya AFCON inaendelea leo kwa mechi mbili, washindi wa pili wa 2019 Senegal wakimenyana na Cape Verde Saa 1:00 usiku na Morocco dhidi ya Malawi Saa 4:00 usiku.
Kocha wa Morocco, Vahid Halilhodzic amesema kambi yake imetikiswa mno na janga la COVID kuelekea mchezo wake na Malawi, japokuwa beki Achraf Hakimi alifanya mazoezi jana baada ya siku nzima ya Jumapili kupumzika tu hotelini.
Lakini bado haijulikani kama mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 atakuwa sehemu ya mchezo wa leo Uwanja wa Ahmadou Ahidjo Jijini Yaounde.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Golikipa wa timu ya Taifa ya Cape Verde
🇨🇻
Vozinha alienda kumjulia hali hospitalini nahodha wa timu ya Taifa ya Senegal
🇸🇳
Sadio Mane mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa raundi ya 16 bora ya AFCON 2021 wakati timu hizo zilipokutana
Vozinha aligongana na Mane dakika dakika ya 57 na kupelekea kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Inaweza kuwa picha ya Watu 2, watu wanasimama, hospitali na ndani
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Winga wa timu ya Taifa ya Malawi
🇲🇼
Peter Banda akiwa pamona na mlinzi wa kulia wa timu ya Taifa ya Morocco
🇲🇦
Achraf Hakimi mara baada ya mchezo wa raundi ya 16 bora ya AFCON 2021 uliozikutanisha timu hizo kumalizika.
Inaweza kuwa picha ya Watu 3 na watu wanasimama
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kisa Kuondolewa Afcon, Mastaa Nigeria Watishiwa Kuuwawa.​

iwobi-maduka.jpg

WACHEZAJI wa timu ya taifa ya Nigeria, Maduka Okoye ambaye ni golikipa na kiungo Alex Iwobi wametishiwa kuuwawa baada ya timu yao ya taifa kuondolea kwenye mashindano na Tunisia siku ya jumapili.
Kutokana na vitisho hivyo golikipa wa timu ya taifa ya Nigeria Okoye alifunga sehemu ya wafuasi wake kuweza kuacha ujumbe kwenye machapisho yake (comment), huku Iwobi ambaye alitolewa dakika ya 66 kwa kupewa kadi nyekundu nae alipokea vitisho vya kuwawa, sababu ni timu yao kufungwa kwenye michuano hiyo ya AFCON 2021.
Iwobi baada ya kupata vitisho hivyo nae aliiweka akaunti yake “archived” kwa muda ili asiweze kuona vitisho ambavyo wanaigeria walikuwa wanamtishia na kuonekana kuwa wao ndio sababu ya timu hiyo kutofuzu hatua ya 16 bora.
Mashabiki wengi wa Nigeria baada ya mchezo kuisha walitumia mitandao ya kijamii kuelezea hisia zao za kutoridhishwa na matokeo ambayo timu ya taifa lapp waliweza kuvuna kwenye michuano ya AFCON 2021, pia baadhi ya wachezaji walitumia mitandao ya kijamii kuweza kuwasihi mashabiki wasiwatishe baadhi ya wachezaji kupitimia mitandao.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MISRI YATINGA ROBO FAINALI AFCON, IVORY COAST NA MALI NJE.​


MABINGWA wa kihistoria, Misri wamefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa ushindi wa penalti 5-4 dhidi ya Ivory Coast kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 Uwanja wa Douala nchini Cameroon.
Waliofunga penalti za Misri ni Ahmed Mostafa Mohamed Sayed ‘Zizo’, Amr El Soleya, Omar Kamal, Mohamed Abdelmonem na Mohamed Salah.
Upande wa Ivory Coast waliofunga ni Nicolas Pépé, Ibrahim Sangaré, Gnaly Cornet na Wilfried Zaha, wakati mkwaju wa Eric Bailly ulipanguliwa na kipa Mohamed Abou Gabal aliyeingia dakika ya 88 kufuatia Mohamed El Shenawy kuumia.
Mechi ya mwisho ya Hatua ya 16 Bora, Equatorial Guinea pia ilitinga Robo Fainali kwa ushindi wa mikwaju ya penalti 6-5 baada ya sare ya bila kufungana na Mali Uwanja wa Limbe.
Robo Fainali zitaanza Jumamosi, wenyeji Cameroon wakimenyana na Gambia, Burkina Faso na Tunisia, Jumapili Misri na Morocco Na Senegal dhidi ya Equatorial Guinea, wakati Nusu Fainali zitafuatia Februari 2 na 3 na Fainali ni Februari 6.


Image
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Wachezaji Wote Ligi Kuu Bara Watolewa AFCON.​

Prince-Dube.jpg

Kuanzia Januari 9, 2022, mashabiki wa soka Barani Afrika na waliopo sehemu mbalimbali nje ya Afrika walianza kuelekeza umakini wao nchini Cameroon hii ni kutokana na kuwepo kwa mashindano ya kombe la Mataifa ya Afrika (AFRIKA) nchini humo mashindano ambayo kwa sasa yamefikia hatua ya robo fainali hii ni baada ya michezo ya hatua ya kumi na sita bora kutamatika usiku wa siku ya jumatano ya tarehe 26 mwezi huu wa kwanza.
Wakati mashindano hayo yanaanza mashabiki wa soka hapa nchini Tanzania walijikuta wanavutiwa sana kufuatilia mashindano hayo hii sio kwa sababu tu ya ukubwa wa mashindano yenyewe ambayo yanajumuisha wachezaji ambao wanacheza soka katika vikubwa zaidi duniani bali pia kwa kuwa wachezaji kadhaa kutoka katika vilabu vya soka hapa nchini Tanzania walikuwepo katika mashindano hayo wakiziwakilisha nchi zao.
Azam FC ndio timu iliyoongoza kwa kutoa wachezaji wengi kwa vilabu vya hapa nchini Tanzania hii ni baada ya wachezaji Bruce Kangwa, Prince Dube pamoja na Never Tigere kujumuishwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Zimbabwe ambacho kilishiriki mashindano hayo huku Simba ikitokea mchezaji mmoja ambae ni Peter Banda kwenda katika timu ya taifa ya Malawi na wakati huo Yanga ikitoa mchezaji mmoja pia yaani Djugui Diarra ambae aliitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Mali.
Huenda ni kwa sababu ya ukubwa na ushindani mkubwa uliopo katika mashindano hayo au ndio sehemu ya mchezo wa soka ambao una matokeo matatu kwa timu husika lakini katika hali ambayo mashabiki wengi wa soka hapa nchini Tanzania hawakuitarajia wachezaji wote kutoka ligi ya Tanzania bara wamejikuta wako nje ya mashindano hayo baada ya timu zao za taifa kufungwa na wapinzani wao.
Katika hatua ya makundi walianza wachezaji watatu wa Azam FC kutolewa yaani Dube, Kangwa na Tigere wakiwa na timu ya taifa ya Zimbabwe ambayo katika hatua ya makundi tu hali ikawa mbaya sana kwao na wakaaga mashindano hayo baada ya kushindwa kupata alama ambazo zingeifanya timu hiyo kutinga hatua ya kumi na sita bora ya mashindano hayo.
Peter Banda mchezaji wa timu ya soka ya Simba akiwa na timu ya taifa ya amejikuta akiaga mashindano hayo na timu yake ya Malawi baada ya kukubali kichapo cha magoli 2 kwa moja kutoka kwa timu ya taifa ya Morocco licha ya wachezaji wa timu ya Malawi kupambana sana lakini wakajikuta wanazidiwa maarifa na kufungwa katika hatua hiyo ya kumi na sita bora.
Djugui Diarra akiwa na timu ya taifa ya Mali na yeye usiku wa kuamkia Alhamisi akaungana na wachezaji wengine wanne kutoka katika timu za ligi kuu soka Tanzania bara kuaga mashindano hayo hii ni baada ya timu yake ya taifa ya Mali kufungwa na kutolewa na timu ya taifa ya Equatorial Guinea kwa mikwaju ya penati 5 kwa sita hii ni baada ya dakika 120 za mchezo huo kuisha bila ya kufungana.