AFCON Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Wananchi wa Senegal
🇸🇳
walivyokuwa wanaisubiri timu yao ya Taifa ikirejea na kombe la Mataifa ya Afrika
🔥
kutoka Cameroon
🇨🇲

Hapa ni Airport
🤔

#AFCON2021
273596903_5082442048482371_3223669154048171458_n.jpg
273508826_5082442041815705_4160670941184850046_n.jpg
273612916_5082442045149038_3247195934470704596_n.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Golikipa wa Misri, Mohammed Abou Gabal amezua gumzo baada ya kutumia chupa inayosemekana ina michoro ya wachezaji na aina yao ya upigaji penalti iliyomsaidia kuokoa penalti 6 katika michuano ya Afcon 2021 ikiwemo ya mchezaji bora Sadio Mane.
Image
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
RASMI: Mlinzi wa zamani wa timu ya Taifa ya Cameroon
🇨🇲
Rigobert Song (45) amepewa mikoba ya kukinoa kikosi cha timu ya Taifa hiyo
Song atasaidiana Sebastien Migne.
Samuel Eto'o ameanza kazi
🤔

Inaweza kuwa picha ya Mtu 1 na maandishi
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Shirikisho la soka la DR Congo (FECOFA)
🇨🇩
limetoa siku 15 kwa Tp Mazembe kurudisha medali, kombe na pesa walizopewa kama mabingwa wa Ligi Kuu nchini humo msimu uliopita wa 2020/21
Ikumbukwe Mazembe walitwaa ubingwa huo baada ya As Vita Club kukatwa alama tisa kutokana na kutumia mchezaji Zao Mututala ambaye Mazembe walifungua kesi na kudai amesajiliwa kinyume na sheria akitokea Don Boscow.
Baada ya hukumu hiyo, As Vita Club walikata rufaa CAS na baadae wakashinda kesi hiyo.
Inaweza kuwa picha ya Watu 3, watu wanasimama na maandishi yanayosema 'BCDC 28 S0'
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SONG KOCHA MKUU MPYA CAMEROON​

AVvXsEi3QLJ5hDyi-RmYBBMh1aqM31YbK3IEqQP8MHc-5EswC4MWC-FhT0C2L6Nd9ZFr16shjvuaIXh8BNKy8-bEnYLUDVuinPMn3eyOU4Y1dMPvACZS3xj4U4pxjDf2MLlMTu6TFF4vIsvD_g3G2iT4PIZE3PzrRGVPGoB-VBy8A8bFS1mrKCvPro3U3voD=w638-h640

BEKI wa zamani wa Liverpool na West Ham United, Rigobert Song (45) amethibitishwa kuwa kocha mpya Mkuu wa Cameroon kwa agizo la Rais wan chi hiyo, Paul Biya nyota huyo wa zamani wa Simba Wasiofungika, akichukua nafasi ya Toni Conceicao, aliyeshindwa kuipa timu taji la AFCON nyumbani mwezi uliopita, ikimaliza nafasi ya tatu.
Song ndiye mchezaji aliyeichezea mechi nyingi aidi Cameroon, 137 na amewahi kuwa kocha muda wa timu hiyo mwaka 2018.
Conceicao amesaidia Cameroon kufika hatua ya mwisho ya mchujo wa kuwania tiketi ya Kombe la Dunia na watamenyana na Algeria katika mechi mbili za nyumbani na ugenini kuwania tiketi ya Qatar baadaye mwaka huu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Mkongwe Seydou Keïta (42) amejitolea kununua tiketi 5000 kwaajili ya mashabiki wa timu yao ya Taifa ya Mali
🇲🇱
kuelekea kwenye mchezo wa hatua ya mtoano ya kuwania tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia 2022 dhidi ya Tunisia
🇹🇳
Machi 25
Mchezo wa Marudiano utapigwa Tunisia
🇹🇳
Machi 29
Inaweza kuwa picha ya Watu 3
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0
Kikosi cha timu ya Taifa ya Senegal
🇸🇳
kimeanza mazoezi hii leo tayari kwa mechi mbili dhidi ya Egypt
🇪🇬
za kutafuta tiketi ya kufuzu Kombe la dunia 2022
Machi 25, Egypt
🇪🇬
🆚
Senegal
🇸🇳

Machi 29, Senegal
🇸🇳
🆚
Egypt
🇪🇬

#WCQ2022






 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0
"Nilipokuwa mdogo, ilinibidi nifiche ukweli kwamba nilikuwa nikicheza mpira kwa sababu mambo yalikuwa hayaendi vizuri shuleni,"
“Nilikuwa nadanganya kuwa naenda shule, kumbe nacheza soka, nikaonekana ni mtoto msumbufu ndani ya familia"
"Kuna Wakati familia yangu ilisikia jina langu kwenye redio. Walifikiri kwamba huenda kuna watu wengi wanaoitwa Ibrahima. Lakini nilipoanza kuchezea timu ya wakubwa katika Klabu ya Olympique Bamako, ambapo nilikuwa mfungaji bora, waliniona kwenye televisheni.”
"Hapo ndipo ndoto zangu zilipoanza kutimia"
🗣
Ibrahima Kone (22)
Mshambuliaji wa Lorient
🇫🇷
na Mali
🇲🇱

Chanzo: Breton Le Telegramme
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1 na anacheza kandanda

 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0
Golikipa wa Ajax na timu ya Taifa ya Cameroon
🇨🇲
Andre Onana amepata ajali akiwa njiani kuelekea kambini tayari kwa maandalizi ya kuwakabili Algeria
🇩🇿
katika mchezo wa kuwania tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia 2022
Onana (25) ni mzima na tayari amewasili kambini.



 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0
"Nimesikitishwa na kushindwa kujiunga na timu yangu ya Taifa inayojiandaa na mchezo wa kufuzu Kombe la dunia dhidi ya Morocco kutokana na majeraha niliyonayo, lakini tutakuwa pamoja kwa kila jambo kuhakikisha tunafanikisha lengo letu"
🗣️
Samuel Moutoussamy (25)
Kiungo wa Nantes
🇫🇷
na CONGO DR
🇨🇩

Inaweza kuwa picha ya Mtu 1, anacheza spoti na amesimama

 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
MAPEMA TU
Kikosi cha timu ya Taifa ya Morocco
🇲🇦
kimeanza safari ya kuelekea Kinshasa tayari kwa mchezo wa kuwania tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia 2022 Machi 25 dhidi ya wenyeji wao CONGO DR
🇨🇩

276322800_5204997449560163_1350017790005519120_n.jpg
277003181_5204997456226829_5637397653844703804_n.jpg
276321188_5204997442893497_5692926084636707252_n.jpg
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Kwa mara ya kwanza Mshambuliaji wa RB Leipzig Ademola Lookman (24) ambaye anakipiga Leicester City kwa Mkopo amefanya mazoezi na kikosi cha timu ya Taifa ya Nigeria
🇳🇬
kinachojiandaa na mchezo wa kufuzu Kombe la dunia 2022 dhidi ya Ghana
🇬🇭

Awali Lookman alikuwa akiitumikia England
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿



 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Senegal
🇸🇳
walishawasili nchini Egypt
🇪🇬
tayari kwa mchezo wa mzunguko wa kwanza wa hatua ya mtoano wa kuwania tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia 2022 leo Machi 25 saa 4:30 usiku

Inaweza kuwa picha ya Watu 3 na watu wanasimama
Inaweza kuwa picha ya Watu 4 na watu wanasimama
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Thomas Partey ataongoza timu ya Taifa ya Ghana
🇬🇭
kama nahodha katika mechi mbili za kutafuta tiketi ya kufuzu Kombe la dunia 2022 dhidi ya Nigeria
🇳🇬
kutokana na Andre Ayew kushindwa kucheza mechi hizo kwasababu ya kadi nyekundu aliyoipata dhidi ya Comoros
🇰🇲
kwenye mechi ya AFCON 2021 nchini Cameroon
🇨🇲

#WCQ2022
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1

 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
"Taifa liko nyuma yenu, kufika Kombe la Dunia ni mafanikio ya kubadilisha mchezo wa soka kwa taifa letu, nyinyi wenyewe pamoja na familia zenu.
Ingieni uwanjani kama simba wa ajabu ili muende kuweka historia kwa mara nyingine tena"
🗣️
Ujumbe wa Asamoah Gyan kwa Wachezaji wa timu ya Taifa ya Ghana
🇬🇭
kuelekea kwenye mchezo wa leo wa kufuzu Kombe la dunia 2022 dhidi ya Nigeria
🇳🇬

#WCQ2022
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania Emmanuel Amunike (51) atakuwa kibaruani hii leo Ijumaa Machi 25 wakati timu yake ya Taifa ya Nigeria
🇳🇬
itakapovaana na Ghana
🇬🇭
katika mchezo wa kuwania tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia 2022
Amunike yupo kwenye timu hiyo kama kocha Msaidizi.
Inaweza kuwa picha ya Watu 2
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

QATAR 2022 NI CAMEROON, SENEGAL, GHANA, MOROCCO NA TUNISIA​

55976863-10663877-image-a-37_1648595861469.jpg

MABALOZI wa Afrika kwenye Fainali za Kombe la Dunia baadaye mwaka huu nchini Qatar ni Cameroon, Ghana, Morocco, Senegal na Tunisia.
Cameroon imefuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia kwa mara ya nane baada ya ushindi wa 2-1 ndani ya dakika 120 dhidi ya wenyeji, Algeria usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Mustapha Tchaker mjini Blida.
Mshambuliaji wa Bayern Munich ya Ujerumani, Erick Choupo-Moting alianza kuifungia Cameroon dakika ya 22, hilo likiwa sawa na bao la kusawazisha baada ya Algeria kushinda 1-0 kwenye mchezo wa kwanza Younde bao pekee la mshambuliaji wa Sporting Lisbon ya Ureno Islam Slimani dakika ya 40.
Mchezo ukahamia kwenye dakika 30 za nyongeza baada ya kutimua dakika 90 Cameroon ikiongoza 1-0 na mshambuliaji wa RKC Waalwijk ya Uholanzi, Ahmed Touba akaisawazishia Algeria dakika ya 118 likiwa sawa na bao la ushindi kwao kwa matokeo ya jumla.
Lakini wakati refa Bakary Papa Gassama wa Gambia anajiandaa kupuliza kipyenga cha kuhitimisha mchezo huku mashabiki wa nyumbani wakishangilia tiketi ya Qatar 2022, mshambuliaji wa Lyon ya Ufaransa, Karl Louis-Brillant Toko-Ekambi akazima kelele hizo kwa bao la dakika ya nne ya muda wa fidia baada ya kutimia dakika 120 za mchezo.
Ni Cameroon ya kocha Rigobert Song inakwenda Qatar baadaye mwaka ikiungana na Senegal, Ghana, Morocco na Tunisia kukamilisha idadi ya wawakilishi watano wa Afrika.

Mechi nyingine jana, Senegal walifuzu kwa ushindi wa penalti 3-1 dhidi ya Misri baada ya sare ya jumla ya 1-1.
Mechi ya kwanza Misri walishinda 1-0 Cairo, bao la kujifunga la Saliou Ciss dakika ya nne na jana Uwanja wa Me Abdoulaye Wade mjini Diamniadio, Senegal wakashinda 1-0 pia bao la kujifunga pia la Hamdi Fathi dakika ile ile ya nne.
Ni mshambuliaji wa Liverpool, Sadio Mane aliyefunga penalti ya mwisho baada ya Ismaila Sarr na Cheikh Ahmadou Bamba Mbacke Dieng kufunga mbili zilizotangulia kufuatia Kalidou Koulibaly na Saliou Ciss kukosa mbili za mwanzo.
Kwa upande wa Misri, Mohamed Salah, Ahmed Mohamed Sayed 'Zizo' na Mostafa Mohamed wote walikosa huku Amr El Soleya pekee akiwafungia Mafarao.

Nayo Ghana imefuzu baada ya sare ya 1-1 na wenyeji, Nigeria jana Uwanja wa Taifa wa Abuja, hivyo kufuzu kwa faida ya bao la ugenini kufuatia sare ya 0-0 nyumbani kwenye mechi ya kwanza.
Ni Black Stars waliotangulia kwa bao la kiungo wa Arsenal, Thomas Partey dakika ya 10, kabla ya beki wa Watford ya England, William Paul Troost-Ekong kuisawazishia Super Eagles kwa penalti dakika ya 22.

Nayo Morocco ikaitandika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo 4-1 na kufuzu kwa ushindi wa jumla wa 5-2 kufuatia sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Kinshasa.
Mabao ya Morocco yalifungwa na Azzedine Ounahi mawili, dakika ya 21 na 54, Tarik Tissoudali dakika ya 45 na Achraf Hakimi dakika ya 69, wakati la DRC lilifungwa na Ben Malango Ngita dakika ya 77.


Tunisia ililazimishwa sare ya 0-0 na Mali Uwanja wa Olimpiki mjini Rades na kufuatia ushindi wa 1-0 ugenini kwenye mchezo ya kwanza nayo inakwenda Qatar.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Wachezaji wa timu ya Taifa ya Ghana
🇬🇭
wamekutana na Rais wa Nchi hiyo Nana Addo na kupongezwa kwa kazi kubwa waliyoifanya na kufanikiwa Kufuzu Kombe la dunia 2022
277557687_5226279084098666_1177949349793766047_n.jpg
277536136_5226279087431999_5008583686726542864_n.jpg