AFCON Thread

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

CAMEROON NA BURKINA ZATINGA NUSU FAINALI AFCON.​

WENYEJI, Cameroon wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Gambia jana Uwanja Douala.
Mabao ya Cameroon jana yalifungwa na mshambuliaji wa Lyon ya Ufaransa, Karl Brillant Toko Ekambi yote mawili dakika ya 50 na 57 na sasa watakutana na Brukinha Faso, ambayo imeitoa Tunisia kwa kuichapa 1-0, bao pekee la Dango Ouattara dakika ya 45 na ushei Uwanja wa Roumde Adjia, Jijini Garoua.


Image
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Jeshi Laamuru Wachezaji Kurudisha Posho Baada ya Kushindwa AFCON.​

Doumbouya.jpg

Serikali ya taifa la Afrika la Magharibi la Guinea imewataka wachezaji wa timu ya taifa ya mchezo wa kandanda waliokuwa huko nchini Cameroon kurejesha pesa za marupurupu walizokuwa wamepewa endapo wangetwaa ubingwa wa AFCON 2021.
Hatua hiyo ya serikali ya Guinea inayo ongozwa na Kanali Mamady Doumbouya imekuja baada ya Wachezaji hao kutakiwa kulitwaa kombe la fainali za mataifa ya Afrika na mwishowe kushindwa kufanya hivyo.

Mambo yalivyokuwa kabla
Mwishoni mwa mwezi Disemba 2021, akiiaga timu ya taifa ya Guinea, Kiongozi mkuu wa taifa la Guinea,
Kanali Mamady Doumbouya aliwataka wachezaji wa timu ya taifa iliyokuwa ikienda kushindana katika fainali za AFCON 2021, kulitwaa taji hilo na wakishindwa, basi wazirejeshe pesa za posho walizokuwa wametengewa.
Kanali Mamady Doumbouya aliitetea kauli yake kwa kudai kuwa, serikali ya taifa hilo imewekeza pesa nyingi katika timu ya taifa, hivyo matokeo ya uwekezeji huo ni lazima yaonekane kwa kikosi hicho kulileta kombe la AFCON 2021 nchini Guinea.

Baada ya kufika nchini Cameroon
Mara baada ya kufika nchini Cameroon, timu ya taifa ya Guinea ilifanikiwa kupenya katika hatua ya 16 bora baada ya kushika nafasi ya pili katika jedwali la msimamo wa kundi B. Guinea ilipenya 16 bora pamoja na timu ya taifa ya Senegal huku Zimbabwe ikifungashwa virago na timu ya taifa ya Malawi kupita kama mshindwa bora.

Mchezo wa hatua ya 16 bora
Katika mchezo wa hatua ya 16 bora, Guinea ilipangwa kucheza na timu ya taifa ya Gambia. Kwa bahati mbaya, Guinea ilitolewa na Gambia kwa kufungwa bao moja kwa bila na timu ya taifa ya Gambia. Kushindwa kwa Guinea dhidi ya Gambia kulitamatisha agizo la Kanali Mamady Doumbouya kukitaka kikosi hicho kulipeleka kombe la AFCON 2021 nchini Guinea.

Wachezaji waparanganyika
Baada ya kutolewa na Gambia katika mchezo wa hatua ya 16 bora, Mara moja wachezaji wa timu ya taifa ya Guinea walisambaratika kwa kila mchezaji kurejea katika klabu yake bila ya kurejea nchini Guinea.

Kanali Mamady Doumbouya atangaza kuwasemehe
Baada ya kutolewa katika hatua hiyo ya 16 bora ya makala ya 33 ya fainali za mataifa ya Afrika huko nchini Cameroon, Kanali Mamady Doumbouya ametangaza kuwasemehe wachezaji wake wa timu ya taifa.
Pia, Kanali Mamady Doumbouya alieleza kuwa, kauli yake ya awali ya kukishurutisha kikosi hicho kulileta kombe la AFCON 2021 ililenga kukihamasisha kikosi cha timu ya taifa.
Azitaka pesa walizokuwa wamepewa za kufika hatua ya ¼ fainali, ½ fainali na fainali. Mbali na kutoa msamaha huo, Kanali Mamady Doumbouya amewataka viongozi wa timu ya taifa kuzirejesha hazina posho walizokuwa wamepewa endapo timu ya taifa ingetwaa taji hilo.
Kanali Mamady Doumbouya ameachana na pesa za kushiriki mchezo na zile za kufika hatua ya 16 bora na sasa anazitaka zile za ¼ fainali, ½ fainali na fainali (kutwaa taji) hatua ambazo timu ya taifa ya Guinea haikuweza kuzifikia.
Ikumbukwe kuwa, Kanali Mamady Doumbouya alitwaa madaraka mwezi Septemba 2021, baada ya kumpindua aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Bwana Alpha Conde.

Kiasi cha pesa ambacho kinatakiwa kurejeshwa
Endapo wangefika hatua ya ¼ fainali, kila mchezaji wa timu ya taifa ya Guinea angelipwa shilingi milioni 23.
Wangefika hatua ya ½ fainali, kila mchezaji angelipwa shilingi milioni 28 na nusu.
Na wangefika hatua ya fainali na kutwaa taji, kila mchezaji angelipwa kitita cha shilingi za Kitanzania milioni 69.
Pesa zote hizo zikizidishwa kwa idadi ya wachezaji 30 wa kikosi hicho, kikosi cha timu ya taifa ya Guinea kinatakiwa kurejesha zaidi ya shilingi za Kitanzania bilioni 3. 66 za posho na marupurupu.




 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MISRI NA SENEGAL ZAKAMILISHA NUSU FAINALI AFCON.

TIMU ya taifa ya Senegal imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya Equatorial Guinea usiku huu Uwanja wa Ahmadou Ahidjo Jijini Yaoundé, Cameroon.
Mabao ya Simba wa Teranga yamefungwa na Famara Diedhiou dakika ya 28, akimalizia pasi ya Sadio Mane, Cheikhou Kouyate dakika ya 68 na Ismaila Sarr dakika ya 79, wakati la Equatorial Guinea limefungwa na Jannick Buyla dakika ya 57.
Awali ya hapo, Misri ilitangulia Nusu Fainali kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Morocco hapo hapo Ahmadou Ahidjo katika mchezo uliodumu kwa dakika 120.
Sofiane Boufal alianza kuifungia Morocco kwa penalti dakika ya sita na Mohamed Salah akaisawazishia Misri dakika ya 53, kabla ya nyota huyo wa Liverpool kumsetia Mahmoud Ahmed Ibrahim Hassan ‘Trezeguet’ kufunga la ushindi dakika ya 100.
Sasa Misri itakutana na wenyeji, Cameroon Alhamisi baada ya Senegal kumenyana na Burkina Faso katika Nusu Fainali ya kwanza Jumatano.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Klabu ya Pyramids Fc
🇪🇬
imekamilisha usajili wa kiungo wa Burkina Faso
🇧🇫
Ibrahim Blati Toure (27) kama mchezaji huru
Toure alienda kwenye michuano ya AFCON 2021 akiwa hana timu tangu alipoachana na AFC Eskilstuna ya Sweden
🇸🇪

Siku ya jana alikuwa mchezaji bora wa mechi dhidi ya Tunisia
🇹🇳
.
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Kampuni ya Quick Point Constr. ya Malawi imemzawadia Kit Manager wa timu yao ya Taifa Richard Justin zawadi ya kiwanja chenye ukubwa Mita 15 kwa 30, matofali 2,000 na mabati 50 kutokana na kazi nzuri aliyoifanya kabla na baada ya kutolewa kwenye michuano ya AFCON 2021.
Image
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Morocco waliwasili Cameroon kwa ajili ya AFCON wakiwa jumla ya watu 86 wakiwemo wachezaji 28.
Walikuwa na;
wapishi wao
Vyakula na maji yao
Magodoro yao
Wafanyakazi wa hoteli
Wanarudi kama walivyoondoka, hakuna kombe.
Image
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

SADIO MANE AIPELEKA SENEGAL FAINALI AFCON.​


TIMU ya taifa ya Senegal imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuichapa Burkina Faso 3-1 katika mchezo wa Nusu Fainali usiku wa Jumatano Uwanja wa Ahmadou Ahidjo Jijini Yaoundé nchini Cameroon.
Mabao ya Senegal yamefungwa na Abdou Diallo dakika ya 70, Bamba Dieng dakika ya 76 akimalizia kazi nzuri ya Nahodha, Sadio Mane ambaye naye alifunga la tatu dakika ya 87.
Bao pekee la Burkina Faso limefungwa na Blati Toure dakika ya 82 na sasa Senegal itakutana na mshindi kati ya wenyeji, Cameroon na Misri wanaomenyana leo katika Nusu Fainali ya pili.



Image
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

NI MISRI YA SALAH NA SENEGAL YA MANE FAINALI AFCON 2021.​


TIMU ya taifa ya Misri imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa penalti 3-1 kufuatia sare ya bila kufungana na wenyeji, Cameroon ndani ya dakika ya 120 usiku wa Alhamisi Uwanja wa Paul Biya Jijini Yaoundé.
Kipa wa klabu ya Zamalek, Mohamed Abou Gaba ‘Gabaski’ ndiye aliyeibuka shujaa wa Mafarao kwa kucheza penalti mbili za nyota wa Simba Wasiofungika, Harold Moukoudi na James Lea Siliki, wakati mkwaju wa zamani wa Tottenham Hotspur, Clinton N'Jie uliota mbaya.
Waliofunga penalti za Misri ni
Ahmed Mostafa Mohamed ‘Zizo’, Mohamed Abdelmonem na Mohanad Lasheen na sasa Mafarao watakutana na Senegal katika Fainali tamu ya AFCON 2021 Jumapili hapo hapo Paul Biya .
Kocha wa Mreno wa Misri, Carlos Queiroz alitolewa kwa kadi nyekundu na refa Mgambia, Bakary Papa Gassama baada ya kupingana na maamuzi kipindi cha pili.
Utakuwa usiku mzuri wa kuwashudia washambuliaji wawili nyota wa Liverpool, Mohamed Salah wa Misri na Sadio Mane wa Senegal wakiyapigania mataifa yao baina yao uwanjani.
Cameroon watajaribu kupoza machungu kwa kumenyana na Burkina Faso katika mechi y kuwania nafasi ya tatu, ambayo itachezwa Jumamosi.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
MSHINDI WA TATU
Burkina Faso
🇧🇫
3-3 Cameroon
🇨🇲

Penati [3-5]
⚽
Yago
⚽
Onana (OG)
⚽
Sufian

⚽
Stephane
⚽
Abubakar
⚽
Abubakar
Wanasema It's not Over Until It's Over, Cameroon
🇨🇲
kutoka 3-0 hadi 3-3 na kushinda katika mikwaju ya penati
🙌

#AFCON2021


Image
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Vincent Aboubakar ndiye mchezaji wa kwanza kufikisha magoli 8 katika kampeni moja wa AFCON ndani ya miaka 48! (Ndaye Mulamba, mabao 9 mwaka 1974).

ImageImageImage
Image
 
Last edited:

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
CEO wa klabu ya Simba SC, Barbara Gonzalez pamoja na Rais wa As Vital Club Bestine Kazadi siku ya jana walihudhuria mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu wa AFCON2021 kati ya Burkina Faso
🇧🇫
dhidi ya Cameroon
🇨🇲

Hii leo wanatarajia kuhudhuria mchezo wa fainali kati ya Senegal
🇸🇳
dhidi ya Egypt
🇪🇬

#AFCON2021
Inaweza kuwa picha ya Watu 7 na watu wanasimama

 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

SENEGAL BINGWA AFCON, YAIPIGA MISRI KWA MATUTA.​


TIMU ya taifa ya Senegal imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mara ya kwanza katika historia yake baada ya ushindi wa penalti 4-2 kufuatia sare ya bila kufungana na Misri ndani ya dakika 120 usiku huu Uwanja wa Paul Biya Jijini Yaoundé nchini Cameroon.
Shujaa wa Simba wa Teranga ni kipa wa Chelsea ya England, Édouard Mendy aliyeokoa mkwaju wa penalti wa nne wa Mafarao uliopigwa na Mohanad Lasheen baada ya awali, Mohamed Abdelmonem kugongesha mwamba shuti lake.
Waliofunga penalti za Misri ni Ahmed Mostafa Mohamed Sayed 'Zizo' na Marwan Hamdy pekee.
Upande wa Senegal waliofunga ni Kalidou Koulibaly, Abdou-Lakhad Diallo, Cheikh Ahmadou Bamba Mbacke Dieng na Sadio Mane, wakati mkwaju wa Bouna Junior Sarr uliokolewa na kipa Mohamed Abou Gabal 'Gabaski '.
Mapema tu katika dakika ya tatu mchezo, Senegal walipata penalti baada ya Mohamed Abdelmonem kumuangusha kwenye boksi beki mwenzake, Saliou Ciss lakini Gabaski akaokoa mkwaju wa Mane baada ya kupewa maelekezo na Nahodha wake, Mohamed Salah.
Salah na Mane wote wanacheza Liverpool na hilo linakuwa taji la kwanza la AFCON kwa Senegal katika fainali ya tatu baada ya mwaka 2002 na 2019.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kushere Ubingwa wa AFCON, Rais wa Senegal Atangaza Mapumziko ya Kitaifa.​

Macky-Sall-senegal-1.jpg

Rais wa Senegal, Macky Sall ametangaza kuwa leo Jumatatu Februari 7, 2022 ni mapumziko kitaifa ili watu washerehekee ushindi wa timu ya taifa ya Senegal baada ya kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON 2021.
Macky-Sall-senegal-2.jpg

Rais huyo ambae alifuatilia fainali akiwa nje ya nchi, ameahirisha pia safari yake nje ya nchi ili awakaribishe Mabingwa hao Ikulu ambapo nyota hao wa soka watarejea nchini kwao leo Jumatatu, Februari 7. “Tumeongoja ushindi huu kwa miaka 60,” amesema Rais Sall.
Senegal waliishinda Misri 4-2 kwa mikwaju ya penalti na kupata ushindi wao baada ya fainali kumalizika bila kufungana iliyofuatiwa na muda wa nyongeza.