Simba Sports Club Thread

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
OFFICIAL: Wachezaji walioondoka Simba Sc
🇹🇿
katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo:
✅
Ibrahim Ajibu
✅
Duncan Nyoni
✅
Abdulsamad Kassim
✅
Jeremiah Kisubi (Mkopo)
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Bocco: Tulieni, bado mawili
1642167977958.png
NAHODHA wa Simba, John Bocco amesema wamefungua mwaka vizuri kwa kutwaa taji la Mapinduzi wanatarajia kutetea mawili yaliyobaki.
Simba wametwaa taji hilo baada ya kumfunga Azam FC bao 1-0 iliwa ni fainali yao ya tatu kukutana na wao kuibuka na ubingwa baada ya kushindwa mara mbili.
Bocco anasema baada ya kushindwa kuwafunga ndani ya misimu miwili waliyokutana fainali walikuwa na mbinu nyingine kuhakikisha wanatwaa taji.
“Haikuwa rahisi lakini ubora na uzoefu umetubeba na kufanikisha hili tunaangalia mipango mingine ya mataji yaliyobaki kwa kuhakikisha tunayatetea,” anasema.
“Azam FC walicheza vizuri lakini hawakuwa bora kama tulivyokuwa bora kitu kilichosaidia sisi kupata matokeo ambayo yametupa taji la nne,” anasema na kuongeza kuwa;
“Habari za taji sasa tumelisahau tunaangalia namna ya kutetea taji la ligi kuu ambalo tumelitwaa mara nne mfululizo na tunaimani tunaweza kutokana na matarajio na morali kwa wachezaji,” anasema.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

CHAMA AONGOZA MSAFARA WA SIMBA KUIFUATA MBEYA CITY.​

AVvXsEhG45Wbm8nIWpZku4RBCn4gJBGd_I9iwIb7UD8jB6_et3D6xLJlbMiuuLvFqFHAEWfFG8z5Elp3hS0CPy1HbqAx-k8kDYr9hrt4fp29K7bW7leXscxm3p3x30-_OAsSucSDgOi-_UcVzeS1lqkX5PXBejGQSTQi2IRAkgZCL-zocAv8Cubuus8iow6V=s16000


KIUNGO Mzambia, Clatous Chama akiongoza msafara wa Simba SC kwa safari ya Mbeya kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Mbeya City Jumatatu Uwanja wa Sokoine.
AVvXsEgnqW6uicp2ztHbAigYKGw9STuAZxexNeF61ShW7JE599jIOyAm_TeNiLxa-LJnErRw2IWKwcvWnfinKQa-M5tu1EjoH_wUlnjfyP-zXMxNik7LHk5NQAS-fJWjm1AIO8ADxxSmbxYG_rN6fNqO6GGhpawd1D8dGFhxc3iAEwm4m2ADCGO0D7EYKdlH=s16000

AVvXsEjf4TP_4FYSwdcceOOUoiUa0uvuwKsd-olhDxAC7ilVAyR4EDqbsaOAv4_dzHq52eLRKfNSgsN2zuC1awyPzQ3t0cRgMCWQ0nLiIBSxu6lI-L59q3T8XrYSjEp4sblu1XmSGIzOQnn_LF-4KqumDBByZKVBWCfl1CY_trHaYqJMsPPtJDWgjH-loFF9=s16000


AVvXsEg17n95IvpntCYLbFFkMfIbaEOyLcFbzuDNT89dcyxvBMzxP8-0WzNUIT33VARsCPcgObIsxw6O4N4asBE8Cbs18QGUhd8J1VwVlMuglQ22o0twZtqE0d1uPPNAXcrgJOYjX0N8AU8x7IFoKySSuCLzv-spBLmkw3vE_TGncb07BU3lKyaqtzpLKCxu=s16000

AVvXsEjajEQiLMaNTHhpiXOda-dgLlzuyjAf3KtLXvJLOxc0TJqIuOa0Iyi3IhtRfx2OMG2_HhapgbYwcz4wN48xK0OWLDwSjpS_TGjTw45pmZrjTyY4E3TRsRLIa7gT5iQLQmtjYLSQuYwkJdAldB3xdAsIWGdKthUci1fd6pNXMjSPo7Kirq-bUpoHE4Xx=s16000
 

Attachments

  • 1642405178657.png
    1642405178657.png
    248.1 KB · Somwa: 0

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Lwanga Yuko Fiti, Kurejea Soon.​


20210925_233726.webp

Baada ya mwishoni mwa mwaka jana taarifa kusambaa kuwa Klabu ya Simba ina mpango wa kuvunja Mkataba wake na Kiungo Mganda Taddeo Lwanga baada ya kupata majeraha na taarifa zilidai atakaa nje kwa muda mrefu.
Sasa ukweli ni kwamba kiungo huyo mkata umeme, anarejea Uwanjani mwishoni mwa Januari hii kwa mujibu wa Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Wekundu wa Msimbazi, Ahmed Ally.
“Thadeo Lwanga ilikuwa tusitishe mkataba wake mwezi huu kutokana na jeraha lake kuchelewa kupona na tulikuwa tayari kutafuta mbadala wake ila daktari ametuhakikishia atakuwa amepona kufikia mwisho wa mwezi huu (January)” amesema Ahmed Ally.
Urejeo wa Lwanga ni faida kubwa kwa Simba ambayo ratiba yake ni ngumu kwa miezi miwili ya hivi karibuni, wakiwa na mfululizo wa mechi nyingi katika muda mfupi.
Hivyo urejeo wa Kiungo huyo utatoa nafasi kwa Mwalimu Pablo kuwa na machaguo mengi uwanjani, na kufanya mabadiliko ya wachezaji hivyo kuwaepusha nyota wake na uchovu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Ahmed: Yanga Wanatamani Kuwa na Mtu Kama Mimi.​

ahmed-ally.jpeg

OFISA Menaja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amesema klabu ya Yanga wanatamani kuwa na mtu kama yeye ndio maana alipochukuliwa na Simba wakaanza kufukua mafaili yake ikiwemo picha alizopiga na Yanga.
Ahmed amesema hayo jana, Jumatano, Januari 19, 2022 wakati akifanya mahojiano na Kituo cha Radio cha WASAFI FM jijini Dar es Salaam.
“Yanga wanatamani kuwa na mtu kama mimi, ndiyo maana baada ya uteuzi wangu wakawa wanahaha kuanza kutafuta mafaili kuonyesha kwamba huyo pia ni Yanga, hii ni ishara kwamba hata wao wanatamani kuwa na mtu kama mimi.
“Angeteuliwa hafisa habari wa kawaida kawaida pale simba, wasingehangaika kufukua mafaili, wasinge hangaika kutafuta taarifa zangu, lakini kwa kuwa nimeteuliwa mimi ambaye wananipenda, wananihitaji niwe pale kwao ndio maana wakaanza kuhangaika,”
amesema Ahmed Ally.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Chama Aanza Vibaya Simba.​

SIMBA-10-1.jpg

MARA baada ya kipyenga cha mwisho cha mchezo wa Ligi Kuu Bara kupulizwa, haraka mabosi wa Simba walifanya kikao cha dharura na benchi la ufundi la timu hiyo na wachezaji wote.
Hiyo ikiwa saa chache mara baada ya timu hiyo kutoka kufungwa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City katika mchezo wa ligi uliopigwa juzi Jumanne kwenye Uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.
Kikao hicho kiliwashirikisha wachezaji wote akiwemo kiungo mpya wa timu hiyo, Mzambia Clatous Chama
aliyejiunga na timu hiyo wikiendi hii.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya benchi la ufundi la timu hiyo, viongozi wa timu hiyo waliitisha kikao hicho cha dharura kwa ajili ya kufanya tathimini ya mchezo wao dhidi ya Mbeya City.
Chanzo hichokilisema kuwa kikao hicho kilifanyika saa mbili usiku kabla ya chakula cha usiku huko Mbeya ambako mchezo huo ulipigwa. Kiliongeza kuwa mabosi wa timu hiyo waliwataka wachezaji hao kupambana katika michezo inayofuatia ili kuhakikisha wanapata ushindi utakaowawezesha kutetea taji lao la ubingwa wa ligi.
SIMBA-9-1.jpg

“Unaambiwa mara baada ya timu kupoteza mchezo wa ligi dhidi ya Mbeya City, uongozi wa timu hiyo uliokuwepo katika msafara, ulilazimika kukaa kikao cha dharura na wachezaji na benchi la ufundi.
“Kikubwa ni kuwaelekeza juu ya hatima ya matokeo hayo huku wakimtaka kocha kuhakikisha anasoma alama za nyakati kabla ya mchezo husika.
“Kikao hicho kilimtaka kocha huyo kujieleza na kutoa sababu ya kupoteza mchezo huo ambao ulikuwa ni muhimu kupata ushindi ili kuwaondoa kileleni wapinzani wao Yanga,” kilisema chanzo hicho.
Alipotafutwa Mtendaji Mkuu wa timu hiyo, Barbara Gonzalez kuzungumzia hilo, kama kawaida yake simu yake ya mkononi iliita bila ya mafanikio kupokelewa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Tatizo la Bocco Limepata Dawa.​

simba-bocco-pic-data.jpg

IWAFIKIE mashabiki wa Simba kwamba tatizo la nahodha wa Simba kuwa kwenye kipindi kigumu cha kushindwa kufunga wala kutoa pasi ya bao kwenye ligi kwa msimu wa 2021/22 limepata dawa baada ya mshikaji wake Clatous Chama kurejea.
Chama alikuwa na maelewano mazuri na Bocco kabla ya kusepa msimu wa 2021/22 ambapo kwenye pasi mbili ambazo alitengeneza Bocco kwenye ligi mtu wa kwanza kuitumia na kujaza mpira kimiani alikuwa ni Chama.
Bocco alifanya hivyo msimu wa 2021/22 wakati Simba iliposhinda mabao 2-0 dhidi ya Polisi Tanzania na washkaji wote wawili walitokea benchi na kuweza kuipa pointi tatu timu ya Simba zama za Sven Vandenbroeck.
Kwa sasa Bocco ambaye anapambania tuzo yake ya ufungaji bora ambapo alifunga mabao 16 msimu uliopita bado hajafunga bao wala kutoa pasi na kinara wa kucheka na nyavu ni Fiston Mayele mwenye mabao sita na pasi moja ya bao.
Leo Bocco anatimiza siku ya 187 bila kufunga bao kwenye mechi za ligi na mara ya mwisho kufanya hivyo ilikuwa ni Julai 18,2021 alipofunga mbele ya Namuno FC.