Simba Sports Club Thread

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Simba: Tunahujumiwa.​

FJ84_yUXMAIBtYW.jpg

MMOJA wa mabosi wakubwa wa Simba ametamka kwa hasira jijini Dar es Salaam: “Tunahujumiwa.” Kisha akatangaza kufanya maamuzi magumu ndani ya siku tatu kuanzia Alhamisi.
Hiyo ni kufuatia matokeo mabovu ya Simba katika mechi tatu mfululizo zilizopita, yaliyowafanya wawe nyuma ya Yanga kwa tofauti ya pointi 10 huku timu zote zikiwa zimecheza michezo sawa.
Kigogo huyo ambaye hakutaka kuanikwa na ambaye alisema habari hiyo ni siri, alilinyetisha Championi Ijumaa kuwa uongozi wa Simba umejipanga kufanya maamuzi magumu kabla ya Jumatatu juu ya mwenendo wa timu hiyo.
Simba imevuna pointi moja tu katika michezo yao mitatu iliyopita ambapo ilipoteza kwa kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Mbeya City kabla ya kutoka suluhu na Mtibwa Sugar, kisha ikapoteza kwa bao 1-0 juzi Jumatano dhidi ya Kagera Sugar.
Simba haijapata ushindi katika mechi tatu mfululizo zilizopita ambazo ni sawa na dakika 270 na kupelekea timu hiyo kubakia katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 25, nyuma ya wapinzani wao wa jadi Yanga wanaoongoza ligi hiyo kwa tofauti ya pointi kumi wakiwa na pointi 35.
Bosi huyo ameeleza kuwa uongozi haufurahishwi na mwenendo wa timu na umedhamiria kufanya maamuzi magumu kabla ya siku ya Jumatatu kwa lengo la kurejesha makali yake kwenye michuano ya Ligi Kuu Bara.
“Uongozi umesikitishwa na aina ya matokeo ambayo yamepatikana katika mechi tatu tulizocheza na ukweli ndani ya timu hali siyo nzuri kwa sababu siyo jambo la kawaida kupata pointi moja katika mechi tatu ambazo zilikuwa wazi kupata matokeo mazuri.
“Tunahisi kuna hujuma tunafanyiwa. Kilichopangwa na mikakati ilivyo kwa sasa ni kwamba uongozi utakutana ndani ya hizi siku tatu kuanzia leo (jana) Alhamisi, yaani haitafika Jumatatu watakuwa wamefanya maamuzi magumu ambayo hakuna anayejua kitu ambacho kinaweza kutokea,” alisema bosi huyo.
Bosi huyo hakuwa tayari kutaja kwa undani wanahisi wanahujumiwa kivipi, na kama hujuma hizo zinatoka ndani au nje ya Simba, kwa wachezaji au makocha, kwa viongozi au marefa.
Hata hivyo, alipotafutwa Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Abdallah, alisema anaamini wamefanya vibaya kutokana na sababu za kiufundi, akisisitiza: “Hayo mambo mengine mi siyajui.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pablo Ajitibulia Mwenyewe Simba SC.​

pablo.jpg

KOCHA Mkuu wa Simba, Mhispania, Franco Pablo, ameweka rekodi ya kucheza michezo mitatu mfululizo ya Ligi Kuu Bara, sawa na dakika 270 bila ya kupata bao katika msimu huu.
Kocha huyo aliyebeba Kombe la Mapinduzi, ameweka rekodi hiyo tangu ajiunge na timu hiyo msimu huu akichukua nafasi ya Didier Gomes aliyesitishiwa mkataba.
Simba msimu huu inaonekana ni butu kwenye ushambuliaji, ikiwa kwa ujumla haijafunga bao lolote katika mechi sita za ligi kati ya 13 ilizocheza hadi sasa.
Timu hiyo iliyorejea juzi ikitokea mkoani Bukoba kucheza dhidi ya Kagera Sugar mchezo wa ligi, keshokutwa Jumapili inatarajiwa kuvaana na Dar City kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC).
Katika mechi hizi tatu mfululizo ambazo Simba haijapata bao lolote, ni dhidi ya Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya ambao walifunga 1-0, aliyewaliza akiwa ni Paul Nonga.
wake wa pili ni dhidi ya Mtibwa Sugar uliomalizika kwa suluhu kwenye Uwanja wa Manungu, kisha Jumatano pale Kaitaba, Bukoba wakachapwa 1-0, bao likifungwa na Mganda, Hamis Kiiza ‘Diego’.
Katika mchezo huo dhidi ya Kagera, Pablo aliwaweka benchi washambuliaji wote huku akitumia viungo pekee katika safu ya ushambuliaji huku Mghana, Bernard Morrison akimpanga namba tisa.
Morrison tangu ajiunge na timu hiyo katika msimu uliopita akitokea Yanga, hajawahi kucheza nafasi hiyo ya ushambuliaji lakini Jumatano alipangwa.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Barbara Aitwa Polisi, Asota Saa Nzima.​

bvrbvra_245534676_895030654768265_2654446010686184596_n.jpg

MTENDAJI Mkuu (C.E.O) wa Simba, Barbara Gonzalez jana Ijumaa alilazimika kusota kwa saa zima kwenye Kituo Kikuu cha Polisi (Central) Dar, baada ya kuitwa kwa ajili ya kesi yake inayomkabili dhidi ya Ofisa wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jackline Kamwamu.
Championi Jumamosi ambalo lilikuwepo kituoni hapo lilimshuhudia Barbara akifika kituoni hapo saa 9:10 alasiri akiwa kwenye gari lake kabla ya kushuka nje ya kituo hicho na kuingia ndani kisha kutoka saa 10:15 jioni, akitumia saa moja kituoni hapo.
Barbara alifunguliwa kesi ya udhalilishaji na ofisa huyo wa TFF kwa madai ya kumdhalilisha wakati akijaribu kumzuia asiingie kwenye eneo VVIP katika mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya Simba na Yanga Desemba 11, mwaka jana.
Hii ni mara ya pili kwa Barbara kuitwa polisi kutokana na kesi hiyo baada ya mara ya kwanza wiki iliyopita kushikiliwa katika kituo cha polisi Alhamisi iliyopita na kumfanya ashindwe kuwepo kwenye mechi ya Simba dhidi ya Mtibwa Sugar.
CEO huyo baada ya kutoka kituoni humo hakutaka kuzungumza na vyombo vya habari bali alipanda kwenye gari lake na kuondoka.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mastaa Simba Wapigishwa Tizi Kwenye Jua Kali.​

SIMBA-3-1.jpg

PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba Ijumaa aliwafanyisha mazoezi wachezaji wake kwenye mchana wa jua kali ikiwa ni maandalizi ya mchezo wao wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC) dhidi ya Dar City unaotarajiwa kuchezwa kesho Jumapili, Uwanja wa Mkapa.
Kocha huyo sambamba na msaidizi wake, Selemani Matola waliwafanyisha mazoezi hayo mida ya saa nane mchana mastaa hao ambapo mazoezi hayo yalifanyika Uwanja wa Mo Simba Arena, Bunju jijini Dar.
Miongoni mwa mastaa waliopo katika mazoezi hayo ni Chris Mugalu, Pascal Wawa, Gadiel Michael, Kenedy Juma, Yusuph Mhilu, Erasto Nyoni, Meddie Kagere, Hassan Dilunga, Aishi Manula, John Bocco na Pape Sakho.
Kwenye mazoezi hayo, Pablo alikuwa akiwasisitiza wachezaji wake hasa safu ya ushambuliaji kuwa makini katika kutumia nafasi ambazo wanazipata. Mabao aliyokuwa akisaka Pablo ilikuwa ni kupitia pembeni kwa Gadiel ambaye alikuwa na kazi ya kupiga krosi kati.
Bernard Morrison, Mohamed Hussein, Henock Inonga, Jonas Mkude na Rally Bwalya hawakuwa sehemu ya wachezaji waliohudhuria mazoezi hayo.
Katika hatua nyingine mastraika wawili wa Simba, John Bocco na Chris Mugalu jana walitoa gundu la kutofunga kwa siku 193.
Wawili hao walifunga mabao kwenye mazoezi ya timu hiyo ya kujiandaa na mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Dar City kwenye Uwanja wa Simba Mo Arena, Bunju.
Bocco alifunga bao moja kwa kichwa akitumia krosi iliyopigwa na Pape Sakho na Mugalu pia alifunga bao kwa pasi ya Pape kwa kichwa ndani ya 18.
Pia Mugalu alifunga bao akiwa kwenye mwendo baada ya kukokota mpira akiwa nje ya 18 na kufunga kwa shuti lililomshinda kipa Aishi Manula.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mzee Dalali Awashukia Mabosi Simba.​

mdalali-data.jpg

KUKOSA matokeo mazuri kwa timu ya Simba kumemuibua mwenyekiti wa zamani wa timu hiyo, Mzee Hassan Dalali ambapo amewashukia viongozi wa timu hiyo akitaka majibu ya chanzo cha hali hiyo.
Dalali ameongeza kuwa kutokana na hali hiyo yeye pamoja na wazee wenzake wanatarajia kukutana kesho Jumapili kwa ajili ya kutafakari hali hiyo inayowaandama timu yao.
Mzee Dalali alisema kwenye kikao hicho wameagiza na kuwataka viongozi wote wa juu wa Simba akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Salim Abdallah ‘Try Again’ na Mtendaji Mkuu, Barbara Gonzalez kuwepo kutoa majibu.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Mzee Dalali alisema haiwezekani timu yao ikose matokeo kwenye mechi tatu jambo ambalo wao wanahisi kutakuwa na shida mahali na wenye kujua hayo ni viongozi hao.
“Tunataka watuambie pindi tutapokutana nao kesho kwa nini timu ikose matokeo kwenye mechi tatu mfululizo jambo ambalo siyo kawaida yetu. Waje watuambie shida ipo wapi.
“Tumewaambia lazima mwenyekiti wa bodi na C.E.O wawepo. Wao ndiyo wenye majibu sahihi ya haya maswali ambayo sisi wazee wa Simba tunataka kuyajua kutoka kwao,” alisema.
Simba haijapata matokeo kwenye mechi zao tatu za Ligi Kuu Bara wakichapwa 1-0 na Mbeya City na Kagera Sugar huku wakienda suluhu na Mtibwa Sugar.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pablo Franco Atetea Mfumo wa Guardiola Simba.​

SIMBA-9-1.jpg

KOCHA Mkuu wa Simba, Pablo Franco, ametetea uamuzi wake wa kucheza bila straika halisi katika mchezo wao wa Jumatano iliyopita dhidi ya Kagera Sugar, mfumo ambao umekuwa ukitumiwa sana na kocha wa Man City ya England, Pep Guardiola.
Katika mchezo huo wa Jumatano iliyopita, Simba hawakuanza na straika yeyote wa asili huku wakianza na viungo sita ambao ni Sadio Kanoute, Rally Bwalya, Clatous Chama, Pape Sakho, Mzamiru Yassin na Bernard Morrison ambaye alicheza kama mshambuliaji.
Guardiola alianza kuwa maarufu kutumia mfumo huo wa straika kivuli akiwa na kikosi cha Barcelona ya Hispania.
Akizungumza na Championi Jumamosi, kocha Pablo alisema: “Kama kocha, wajibu wangu mkubwa ni kutafuta suluhisho inapotokea tunapitia changamoto fulani. Kabla ya mchezo dhidi ya Kagera Sugar hatukuweza kufunga bao lolote kwa dakika 180 za michezo miwili mfululizo iliyopita na niliamini tulipaswa kufanya maamuzi ya utofauti.
“Hapo ndipo tulikuja na wazo la kutumia namba tisa kivuli kwa kujaza viungo wengi na kumtumia Morrison kama straika wetu, kila mmoja ni shuhuda kuwa kwa kiasi fulani tulifanikiwa kutengeneza nafasi lakini kwa bahati mbaya hatukufanikiwa kupata mabao.
“Yote kwa yote kwa sasa tunapaswa kuangalia mbele na kurejesha hali yetu ya kujiamini ili kuwapa furaha mashabiki wetu.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Straika Mkongo Aanza Nyodo Simba.​

mugaluchris07_243701390_1005591420225378_7844867719325901672_n.jpg

MARA baada ya kufunga bao lake la kwanza tangu kuanza kwa msimu huu, mshambuliaji Mkongomani ndani ya kikosi cha Simba, Chris Mugalu, ameibuka na kutamka kuwa sasa hivi kasi ya mabao ndiyo imeanza, hivyo watamtambua.
Kauli hiyo aliitoa mshambuliaji huyo mara baada kufunga bao moja katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Dar City katika mchezo wa hatua ya 32 bora ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports, juzi Jumapili.
Katika ushindi huo, mabao mengine ya Simba yalifungwa na Meddie Kagere aliyefunga mawili, huku Clatous Chama,
Rally Bwalya na Pascal Wawa kila mmoja akifunga moja.
mugaluchris07_244271520_937896000095714_1815605476186806358_n.jpg

Kwa mujibu wa Mugalu, bao hilo litamuongezea hali ya kujiamini baada ya kukaa muda mrefu bila ya kufunga.
“Nina furaha kubwa leo (juzi) kufunga bao langu la kwanza tangu kuanza kwa msimu huu ambao kwangu nauona
mgumu tofauti na msimu uliopita.
“Lakini ninashukuru kuona nikifunga, bao hili litaniongezea hali ya kujiamini na kufunga mengi zaidi. “Kikubwa niendelee kuomba ushirikiano na umoja kutoka kwa wachezaji, viongozi na mashabiki wetu kuendelea kuvumilia hiki kipindi kigumu tunachokipitia,” alisema Mugalu
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mangungu: Simba Hali ni Shwari.​

simbasctanzania_148252560_244695397183703_4745773412771480422_n.jpg

MWENYEKITI wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu, amesema licha ya timu yao kukosa matokeo mazuri katika michezo mitatu iliyopita ya Ligi Kuu Bara, lakini bado wapo imara na hakuna mgogoro wowote unaoendelea klabuni hapo, kila kitu ni shwari.
Kwenye mechi hizo tatu, Simba imepoteza mbili dhidi ya Mbeya City na Kagera Sugar, huku ikitoka
suluhu na Mtibwa Sugar. Juzi Jumapili ilishinda 6-0 dhidi ya Dar City kwenye Kombe la Shirikisho la
Azam Sports hatua ya 32 bora.
Akizungumza na Spoti Xtra, Mangungu alisema: “Hakuna mgogoro wowote baina ya benchi la ufundi na wachezaji wala bodi, naweza kukiri hayo yanayosemwa ni propaganda za watu wa mataani tu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

CAF yairuhusu Simba mashabiki 35, 000.​

caf pic

SHIRIKISHO la Soka Barani Afrika (CAF) limeruhusu mashabiki 35, 000 kuhudhuria mchezo wa kwanza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Simba dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast utakaopigwa Februari 13 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Meneja wa habari na mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally alisema kuwa wamepokea barua kutoka CAF ya kuwaruhusu kuingiza mashabiki katika mchezo huo kwa sharti la kutoingiza namba inayozidi watu 35,000.
"Kuelekea mchezo huo, hii leo tumepokea taarifa rasmi kutoka Caf likituruhusu kuingiza mashabiki 35,000 katika mchezo huo kwa hiyo tuwaambie mashabiki wetu wa Simba popote walipo kwamba siku ya mchezo wetu huo ni mashabiki 35,000 pekee ndio watakaoruhusiwa kuingia katika mchezo huo.
Tulitamani kuwa na mashabiki wote 60,000 lakini mamlaka husika kwa maana ya Caf wameturuhusu mashabiki 35,000," alisema Ally.
CAF imeitaka klabu hiyo kufuata taratibu zote za kujikinga na ugonjwa wa corona kama kukaa kwa nafasi baina ya mtu na mtu, kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa maji safi na vitakasa.
Aidha CAF imesisitiza taratibu hizo kuzingatiwa hivyo kila shabiki anapaswa kuchukua hatua na kumlinda mwenzake aliye karibu yake kwa muda wote wa mchezo huo.
Katika hatua nyingine uongozi wa klabu hiyo umepanga kuhakikisha maandalizi yote yanakamilika huku ukiwataka mashabiki kununua tiketi mapema ili kuondoa usumbufu siku ya mchezo.
Simba imepangwa kwenye kundi D katika michuano hiyo ikiwa na timu za RS Berkane (Morocco), Asec Mimosas (Ivory Coast) na US Gendarmerie Nationale ya Nigeria.
Baada ya mchezo na Ases Mimosas, Simba itasafiri kucheza michezo miwili ugenini na US Gendarmerie Nationale Februari 20 kisha RS Berkane Februari 27, kabla ya kurudiana na Berkane Machi 13 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Michezo miwili iliyosalia itasafiri Ivory Coast kucheza na Ases Mimosas Machi 20, kisha kumaliza hatua hiyo ya makundi dhidi ya US Gendarmerie Nationale Aprili 3 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Matawi Simba yacharuka.​

matawi pic

KLABU ya Simba imetumia zaidi ya saa tatu kujadili mwenendo mbovu wa timu yao kwenye Ligi Kuu, kisha kuchimba mkwara mzito wakitaka mambo yabadilike ili kuweza kula sahani moja na watani wao, Yanga inayoongoza msimamo.
Simba imeachwa kwa pointi 10 na Yanga licha ya kila timu kucheza mechi 13, kwani watetezi hao wamekusanya pointi 25, wakati watani wao wana 35 na kuwapa presha mashabiki ndipo juzi Jumamosi matawi ya klabu hiyo wakaitisha mkutano.
Mkutano huo maalumu wa ndani uliwakutanisha viongozi wa matawi ya klabu hiyo na Mwenyekiti wa Klabu, Murtaza Mangungu na ulifanyika kwenye majengo ya Shule ya Sekondari Jamhuri, iliyopo eneo la Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.
Mwanaspoti lililotinga kwenye mkutano huo lilishuhudia viongozi hao wa matawi wakiandika majina yao katika orodha ya waliohudhuria kuanzia saa 2 asubuhi na mkutano kuanza saa 4:30 hadi saa 7:48 mchana, lakini gazeti hili lilizuiwa kuingia ndani kusikiliza kilichojadiliwa.
Licha ya kikao hicho kuwa ni cha siri kubwa lakini Mwanaspoti ilipenyezewa ajenda kubwa katika mkutano huo kuwa ni matokeo mabovu ya timu yao na mjumbe mmoja alidokeza kuwa, kukosa matokeo mazuri yanawaumiza mno.
“Kumekuwa na hisia za kuwepo kwa hujuma na tumemtaka mwenyekiti wetu, Mangungu akalifanyie kazi na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, ili kuweka mambo sawa, wakati sisi tunafanya yetu kuwashughulikia wahusika,” alisema mjumbe huyo aliyeomba kuhifadhiwa jina.
“Haiwezekani timu inacheza, lakini haipati matokeo katika mechi tatu mfululizo, hii sio sawa na mbaya baadhi ya wachezaji hawaonyeshi kujituma uwanjani,” alisema mjumbe huyo aliyedai mashabiki kukosa raha kutokana na kero za Yanga.
“Yanga kuongoza tu pale kelele nyingi, lakini timu yao inacheza na inafunga, sasa tunaoumia ni sisi, tumemwambia mwenyekiti waliangalie hilo.”
Mangungu alipoulizwa na Mwanaspoti kuhusu mkutano huo wa matawi, alisema kikao hicho kiliwahusu wao tu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pablo apiga kijembe Yanga.​

simba pic

KAMA ulikuwa unaamini Simba imesalimu amri kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu, basi pole yako, kwani wenyewe wamesisitiza bado wamo sana na hii inatokana na jeuri ya mechi zilizosalia kabla ya msimu haujamalizika.
Watetezi hao wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wakiwa na pointi 25 baada ya mechi 13 ikizidiwa pointi 10 na vinara Yanga wenye alama 35 kwa idadi sawa ya mechi na kuwafanya mashabiki wa Jangwani kuanza kuhesabu ubingwa.
Hata hivyo, kocha Pablo Franco licha ya kukiri pointi walizoachwa na watani wao ni nyingi na ni mara ya kwanza kwa historia kwa timu hizo zikiwa zimelinga michezo, lakini bado haiwaondoi Simba kuwepo kwenye mbio za ubingwa.
Pablo alisema, Simba haina presha na kelele za watani wao kuanza kujihesabia ubingwa, kwa vile ligi imesaliwa na mechi 17 ambazo ni nyingi kuliko zilizochezwa hadi sasa na anaamini watatetea ubingwa mwisho wa msimu.
“Hakuna aliyejua kama Simba ingecheza mechi tatu bila ushindi, vivyo hivyo hata kwa timu nyingine mambo yanaweza kutibuka, bado naamini tuna uwezo wa kuikuta na kuipita Yanga,” alisema na kuongeza;
“Katika michezo 17 tuliyobaki nayo kuna mmoja tutacheza nao (Yanga), hivyo hatuna presha na mashabiki na wapenzi wasikate tamaa, bado tuna nafasi kubwa ya kutetea ubingwa wetu na kuweka rekodi.”
Pablo alisema hata hivyo anawaheshimu wapinzani wao wote wa Ligi Kuu na michuano ya ASFC, lakini kama timu wana malengo waliyojiwekea ikiwamo kutetea mataji yao na ndilo wanalolifikiria na kujipanga kutimiza hilo.
“Niwatoe hofu wanasimba, ni kweli kazi bado ni ngumu, kama benchi la ufundi hatutaacha kufanya kazi ya kutosha kutoa maelekezo na kuweka mipango sahihi katika kikosi chetu ili kuwa na matokeo mazuri katika michezo ijayo,” alisema.
Juu ya kupitwa pointi 10 alisema ni nyingi, lakini bado zinaweza kufikiwa kama watashinda mechi zao na wapinzani wao wakipata matokeo tofauti na waliyozoea.
“Kuwania ubingwa ni kama mbio za marathoni kuna wakati unaweza kuanza vibaya, njiani ukakutana na vikwazo, lakini mwishowe ukajipanga na ukamaliza kinara, hatuamini kama hatumo kwenye ubingwa. Subirini muone!”
Kwa misimu minne mfululizo iliyopita, Yanga ilikuwa ikiongoza msimamo kwa muda mrefu, lakini ikajikuta ikizidiwa ujanja mwishowe na Simba kutokana na misimu hiyo kuwa na mechi nyingi za viporo na pia Yanga kuwa na kikosi dhaifu.
Kwa msimu huu Yanga inaonekana kuwa na kikosi bora chenye wachezaji wenye viwango vya juu kulinganisha na wale wa Simba, lakini pia Bodi ya Ligi (TPLB) imepanga ratiba ambayo haitoi nafasi ya kuwepo kwa viporo vingi.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pablo Aitisha Kikao ghafla Juzi Simba.​

simba-12.jpg

UNAAMBIWA muda mfupi baada ya Simba kuibuka na ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Dar City, Kocha Mkuu
wa Simba raia wa Hispania, Pablo Franco, ameitisha kikao ghafla Juzi Simba iliibuka na ushindi huo mnono katika mchezo wa hatua ya 32 bora ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports uliochezwa Uwanja wa Mkapa,Dar.
Kwa siku za karibuni, Simba imekuwa haina matokeo mazuri katika ligi kuu hali inayotishia kulikosa taji wanalolitetea kutokana na kuachwa pointi kumi na vinara Yanga baada ya timu zote kucheza mechi 13.
Chanzo chetu kutoka Simba, kimeliambia Spoti Xtra kuwa, baada ya mchezo wa juzi dhidi ya Dar City, Kocha Pablo ambaye hakuwepo kwenye benchi kutokana na kufungiwa mechi tatu, aligoma kuzungumza lolote na wachezaji.
“Ushindi wetu wa jana (juzi Jumapili), umeongeza morali kwa wachezaji kuanza kuona mwelekeo katika mechi zijazo tukianza na Prisons.
“Kutokana na ushindi huo na mchezo ulio mbele yetu, ndiyo kisa cha Kocha Pablo kuwataka wachezaji wawahi kambini leo (jana Jumatatu), ili kupata muda wa kukaa kikao na uongozi kabla ya kuanza mazoezini kujiandaa
kuwakabili Prisons,” kilisema chanzo hicho.
Alipotafutwa Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, alisema: “Kikao kilipangwa kufanyika baadaya mazoezi ya jioni (jana Jumatatu) ambapo ni kawaida ya kocha na wachezaji kuzungumza kukumbushanamambo.”
Katika mechi tatu zilizopita za Ligi Kuu Bara, Simba imekuwa na matokeo yasiyoridhisha ambapo imekusanya alama moja kati ya tisa kutokana na kupata suluhu dhidi ya Mtibwa Sugar na kupoteza mbele ya Mbeya City na Kagera Sugar.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mastaa Simba watoa azimio zito, Chama aeleza.​

mastaa pic

HAINA kufeli, ndiyo tamko walilotoka nalo Simba katika kikao cha wachezaji peke yao walichokaa chini ya manahodha wao kikilenga kubadili hali ya mambo na kutetea taji lao la Ligi Kuu Bara kwa mara ya tano mfululizo.
Kabla ya ushindi wa 6-0 dhidi ya timu ya Daraja la Pili ya Dar City katika mechi ya hatua ya 32-Bora ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), Simba ilikuwa haijafunga bao hata moja katika mechi tatu zilizopita mfululizo za Ligi Kuu Bara ambazo waliambulia pointi moja na kupitwa pointi 10 dhidi ya vinara, Yanga.
Vipigo viwili na sare moja katika mechi tatu hizo za Ligi Kuu, vimewastua sio mashabiki peke yao bali pia wachezaji ambao wamekutana na kuamua kuanza upya ligi chini ya kauli mbiu kwamba kila mechi sasa ni fainali.
Kwenye kikao hicho kilichokaa kabla ya mechi ya juzi usiku, baadhi ya wachezaji waliongea ikiwemo manahodha, John Bocco na Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ kisha wakatoka na jibu moja kuwa kila mechi iliyokuwa mbele yao ni fainali.
Wachezaji walimueleza kocha wao kuwa huu si wakati tena wa kuangalia yaliyopita ila watayachukua kama fundisho katika mechi zijazo na hakuna mpinzani watakayemuacha salama kuanzia sasa.
“Ebwana eehh, wachezaji wa Simba sasa tumekubaliana hakuna kuangalia tunacheza na nani, wapi, bali kikubwa ni kama fainali na tunataka ushindi sasa kwani heshima yetu kama imeshuka na kuchukulia wa kawaida,” alisema mmoja wa wachezaji waandamizi kwenye kikosi hicho.

CHAMA AELEZA
Wakati hayo yakijiri, kiungo wa Simba, Clatous Chama amepiga stori na Mwanaspoti na kueleza yanayomzunguka tangu aliporejea Msimbazi katika dirisha dogo la usajili, wachezaji wa timu hiyo.
Chama ambaye anatazamwa na mashabiki wengi wa timu hiyo kama mtu sahihi anayekuja kuamsha morali iliyopungua klabuni, amesema ana muda mfupi tangu amejiunga na kikosi hicho ambacho kina mabadiliko kwahiyo si rahisi kuingia na kuanza kucheza katika kiwango cha juu moja kwa moja hadi apate muda zaidi.“Wakati nikiendelea na hilo huku mechi za ligi na mashindano mengine zinaendelea kwahiyo natakiwa kujituma zaidi ya vile ilivyokuwa mchezo uliopita na kuipa Simba mafanikio ya ushindi,” alisema Chama na kuongeza;
“Ukiangalia mechi mbili zilizopita ni tofauti kabisa na ambavyo nimetumika na Dar City kuna vitu vimeongezeka ikiwemo kuelewana vizuri na wenzangu na ninaamini baada ya muda mfupi kama mwezi mmoja tu itakuwa vizuri zaidi.
“Unajua wakati huu ligi ina ushindani mkubwa na kila timu inayokutana na Simba inatamani kupata matokeo mazuri kutokana na mafanikio tuliyokuwa nayo sasa hilo wachezaji tumelichukua kama changamoto na muda si mrefu mambo yatabadilika na kuwa mazuri.”
Alisema kikosi cha Simba kina uwezo wa kutetea mataji mawili Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho (ASFC), kutokana na kiu ya mafanikio waliyonayo. Amewataka pia kubeza kejeli za washindani wao na kwamba sasa ni muda wa kuwa kitu kimoja.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Wawa afunguka shangilia yake.​

wawa pic

BEKI Pascal Wawa wa Simba juzi Jumapili alifunga bao lakini kilichovutia ni namna alivyoshangilia kitofauti na wenzake wote baada ya kwenda moja kwa moja kwa Henock Inonga ‘Varane’ na kumkumbatia kisha alipita kwenye benchi zima la timu yake na kuwapa mkono.
Wawa aliingia katika dakika ya 45 akichukua nafasi ya Varane na dakika 47 alifunga bao la tano la Simba kwa shuti ndani ya boksi wakati Wekundu wa Msimbazi wakishinda 6-0 dhidi ya Dar City kwenye mchezo wa hatua ya 32-Bora ya Kombe la Shirikisho Azam (ASFC).
Akizungumza na Mwanaspoti, Wawa kwa kifupi alisema; “Inonga wakati naingia uwanjani aliniambia “kila la kheri kaka.” Kauli ile ilinipa moyo. Kushangilia kwa kuwafata benchi zima ni kwa sababu sisi ni familia, sisi ni kitu kimoja, nawapenda mashabiki pia.”
Wawa hajawa na uhakika wa kuanza kikosi cha kwanza kwasasa mbele ya mabeki Inonga na Joash Onyango ambao wamekuwa kwenye kiwango bora kwasasa timu ikiwa chini ya kocha Pablo Franco.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kiiza amtetea Bocco.​

bocco pic

STRAIKA wa Kagera Sugar, Hamis Kiiza anawashangaa Watanzania wanaomshauri nahodha wa Simba, John Bocco, 32, kwenda kusomea ukocha kwa madai ya kwamba umri umemtupa na ameshashuka kiwango wakati bado anahitajika uwanjani.
Kauli ya Kiiza imekuja baada ya kuona Bocco anasakamwa kila kona, kutokana na ukame wa mabao anaoupitia msimu huu, jambo analoliona ni kama wanamkosea.
Kiiza anaamini Bocco atafanya jambo kubwa na kuwashangaza watu msimu huu kwani mechi bado nyingi na anaweza akaibuka kinara wa mabao.
“Hali anayoipitia Bocco imewahi kunikumba, kwanza nilivyojiunga na Kagera Sugar walinisema nimeisha kwasababu hawakujua nilikuwa nafanya nini,”
“Angalau nilivyoifunga Simba kejeli zao za kuwa nina kitambi zinaishia, ndio maana namtetea Bocco kwamba naamini ana kitu kikubwa anachoweza kukifanya msimu huu,” alisema Kiiza na kuongeza:
“Hicho anachopitia ni kipindi cha mpito na kinaweza kumtokea mchezaji yeyote hivyo si sawa kwa watu kumuandama kama ilivyo sasa.
“Bocco anastahili heshima kwani ni mshambuliaji mzuri na namkubali sana. Naamini kabisa akitulia na aache kabisa kufikiria watu wanasema nini atarudi kwenye ubora wake kwani bado ana nafasi ya kufunga mabao mengi tu kwa sababu mechi bado zipo na anaweza hata kuibuka mfungaji bora na kuwashangaza watu.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MZEE WA UPUPU: Kuna mtoto anachezea simu ya Mo Dewji?​

mo pic

Mara zote Simba inapopitia kipindi kigumu, mwekezaji wao Mo Dewji huibuka na maneno fulani ya mafumbo kupitia mitandao ya jamii. Hii huongeza taharuki kwa wana Simba ambao wakati huo wanahitaji faraja kutoka kwa mtu kama yeye.

Mafumbo ambayo huwa anatumia husababisha maswali mengi ambayo kila mtu huibuka na majibu yake na kuongeza sintofahamu. Baada ya kucheza mechi tatu za Ligi Kuu Bara bila kufunga hata bao moja, wakipoteza mbili na suluhu moja, wazee wa klabu hiyo ambao kimsingi hawatambuliki kikatiba wakafanya kikao chao chini ya Hassan Dalali, mwenyekiti wa zamani wa Simba.

Siku hiyohiyo, Januari 30, 2022, Mo akaibuka na mafumbo kupitia mitandao ya kijamii. Alianza kwa kukiri kwamba hali si shwari ndani ya Simba. Kweli kuna tatizo!

Licha ya kubaini kwamba kuna shida klabuni, lakini akaonyesha kwamba hata yeye mwenyewe hajui shida hiyo iko wapi? Tatizo liko wapi?

Kama ilivyo kawaida yake, huwa hawezi kumaliza posti zake kuhusu Simba bila kuwakumbusha mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kuhusu pesa anazotumia. Simba hii pesa hazina thamani. Hapa ni kama alikuwa akimaanisha kwamba kuna watu wanamdharau ndani ya klabu yao licha ya kuwa na pesa na kuzitoa kwa ajili ya maendeleo ya klabu.

Itakumbukwa kwamba siku chache zilizopita kulikuwa na taarifa kwamba Mo ndiye tajiri namba moja Tanzania, namba moja Afrika Mashariki na namba kumi na tano Afrika. Sasa tajiri kama huyu kudharauliwa na watu anaowazidi pesa kwa kiwango cha usingizi na kifo, ni tusi kubwa.


Mwisho kabisa akatoa wito wa kuhoji mchakato wa mabadiliko ulipofikia. Kwa heshima na taadhima tuulize transformation imekamilika? Mtiririko huu wa maoni ya Mo kupitia mitandao ya kijamii unaonyesha aidha kuna kitu hakiko sawa ndani ya Simba au ndani ya fikra zake mwenyewe kuhusiana na klabu hiyo.

Kitendo cha kila mara kuwakumbusha watu pesa anazotumia kwa ajili ya Simba huku akisema hapati faida, ni ishara kwamba pesa zake zinamuuma. Na kama kweli ishara hiyo inaakisi picha halisi, maana yake siku za Mo ndani ya Simba zinahesabika.

Mashabiki wa Simba wajiandae kisaikolojia. Siku yoyote watarajie kusikia ‘breaking news’ kwamba Mo kaachana na Simba. Mo amekuwa na tabia ya kuegemea kwa watu wa kuwalaumu kisha kujitoa pale anapohisi alilotarajia halijawa.

Hiki ndicho kilichotokea alipokuwa Singida United, timu ambayo aliibadilisha jina kutoka Mto Singida. Hiki ndicho kilichotokea alipokuwa African Lyon, timu ambayo aliibadilisha jina kutoka Mbagala Market. Mara zote alitafuta kichaka cha kujifichia na akatoka nduki kimoja. Sasa yuko Simba na dalili zimeshaanza kujitokeza.

Alijiuzulu kama mwenyekiti wa bodi baada tu ya kufungwa na Mtibwa Sugar kwenye fainali ya Kombe la Mapinduzi, Januari 2020. Katika mambo aliyoyataja ni pamoja na pesa anazotumia kwa ajili ya Simba. Akapigiwa magoti na kutengua uamuzi wake, lakini baadaye akajiuzulu tena na hakurudi.

Ameibuka tena kwenye mitandao na kuleta mjadala wa pesa. Hii inawaweka roho juu mashabiki na wanachama wa klabu hiyo ambao wamewekeza nyoyo zao klabuni. Ukimsikiliza mwenyewe anapoongea kuhusu Simba unapata hisia kwamba huyu jamaa ni Simba hasa na siyo mtu wa kutoka leo wala kesho.

Sasa kama hiyo ndiyo iko hivyo kweli, basi labda kuna mwanaye mmoja huchezea simu yake. Haiwezekani mtu mwenye mapenzi mema na Simba kiasi kile awe anayumbisha vichwa vya wana Simba wenzake wanaomtegemea. Na kama siyo mtoto kuchezea simu, basi akaunti yake imedukuliwa. Lakini binafsi naamini Mo anaelekea kuikimbia Simba, kwa hiyo anawaandaa kisaikolojia mashabiki wake.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Chama, Bwalya Wampa Jeuri Mpya Pablo.​

SIMBA-2.jpg

UWEZO mkubwa ambao umeonyeshwa na kikosi cha Simba hususani viungo wao raia wa Zambia, Clatous
Chama na Rally Bwalya kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam dhidi Dar City umemuibua kocha mkuu, Pablo Franco ambaye ameweka wazi kuwa hawatakata tamaa kuhusu ubingwa wao na watapambana kushinda kila mchezo ulio mbele yao.
Simba Januari 30, mwaka huu wakiwa katika Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam walifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Dar City katika mchezo wa hatua ya 32 ya michuano ya Kombe la Shirikisho laAzam ambapo walifanikiwa kutinga hatua ya 16 Bora huku Chama na Bwalya wakionyesha uwezo mkubwa.
Ushindi huo ni wa kwanza kwa Simba katika michezo yao minne mfululizo iliyopita ambapo michezo mitatu ya Ligi Kuu Bara walipoteza michezo miwili na kutoa sare mchezo mmoja.
Akizungumza na Championi Jumatano, Kocha Pablo alisema: “Ni jambo zuri kuweza kupata ushindi huu muhimu dhidi ya Dar City, hususani baada ya kupitia kipindi kigumu cha kukosa matokeo katika michezo mitatu mfululizo ya ligi kuu.
“Lakini kama ambavyo nilieleza hapo awali, kwetu yaliyopita yamepita na tunawekeza katika michezo yetu ijayo, hatukati tamaa kwa kuwa hakuna anayeweza kutabiri nini kitatokea mwishoni mwa msimu, hivyo la muhimu kwetu ni kushikamana na naamini tutajitahidi kushinda kila mchezo ujao.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Matola aihofia Prisons, Kibu nje.​

matola pic

KOCHA msaidizi wa Simba Seleman Matola amesema timu yoyote itakayotumia vyema dakika 90 katika mchezo wa kesho ndiyo itapata pointi tatu.
Simba kesho ni mwenyeji wa Tanzania Prisons mchezo wa raundi ya 14 wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaopigwa katika uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam.
Matola amesema kila timu imejipanga na kutokana na ushindani uliopo yoyote atakayezitumia vyema dakika hizo ndiye atapata pointi katika mchezo huo.
Aidha Matola amesema haijalishi wapinzani wao kuburuza mkia katika msimamo wa Ligi kutawafanya wabweteke bali watahakikisha wanapambana dakika zote.
"Tanzania Prisons ni miongoni mwa timu nzuri japokuwa wanashika mkia katika msimamo ila ni mchezo ambao tunatakiwa kupambana mwanzo mwisho kupata matokeo, "
Matola amesema katika mchezo wa kesho atakosekana mshambuliaji wao Kibu Denis ambaye ana majeruhi mpaka sasa bado hajarejea uwanjani isipokuwa Jonas Mkude yeye ameanza mazoezi jana.
Simba inashika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi ikiwa na pointi 25 ikishinda mechi saba sare nne na kupoteza michezo miwili huku Prisons pointi 11 kashinda tatu sare mbili na kupoteza michezo nane.