Simba Sports Club Thread

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mzungu wa Simba Awafungia Kazi Mtibwa.​

SIMBA-9-1.jpg




BAADA ya mapumziko ya siku moja, kikosi cha Simba juzi kiliingia kambini tayari kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao dhidi ya Mtibwa.
Timu hizo zinatarajiwa kuvaana katika mchezo wa Ligi Kuu Bara leo Jumamosi saa kumi kamili kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro.
Katika mchezo huo, Simba wataingia uwanjani wakiwa na hasira za kutoka kufungwa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City.
Kocha Mkuu wa Simba, Mhispania Franco Pablo, alitoa mapumziko ya siku ya Jumanne pekee mara baada ya kurejea jijini Dar es Salaam wakitokea Mbeya.
Pablo alisema kuwa kikosi chake chote kiliingia mazoezini juzi Jumatano na kufanya mazoezi jioni kwenye Uwanja wa Simba Mo Arena, Bunju Dar katika kuiandaa timu yake.
Aliongeza kuwa, atakuwa na siku mbili za kukamilisha maandalizi yake juzi Jumatano na jana Alhamisi, kabla ya kuelekea Turiani tayari kwa mchezo huo unaotarajiwa kujaa upinzani mkubwa.
“Ninauchukulia umuhimu mkubwa mchezo wetu huu wa ligi tutakaocheza dhidi ya Mtibwa Sugar wikiendi hii.
“Jana (juzi) wachezaji wote waliingia kambini tayari kwa ajili ya kuanza maandalizi ya mchezo wetu dhidi ya Mtibwa ambao ni muhimu kwetu kupata ushindi.
“Hatutaki kupoteza mchezo huu, nimepata taarifa za mazingira ya uwanja tutakaoutumia, hivyo tutaingia katika mchezo huu kwa tahadhari kubwa,” alisema Pablo.





 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pablo Awapiga Stop Mastaa Simba Kula Chipsi Zege.​

pablo-1.jpg

KOCHA Mkuu wa Simba, raia wa Hispania, Pablo Franco, amemtaka kiungo kisiki wa timu hiyo, Mganda, Thadeo Lwanga, kuepuka matumizi ya vyakula vya mafuta mengi kipindi hiki ambapo bado yupo kwenye program maalum.
Lwanga yupo nje ya kikosi hicho akiuguza majeraha ya goti lake aliyoyapata takriban miezi miwili iliyopita wakati timu hiyo ikicheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Jwaneng Galaxy FC ya Botswana, uliomalizika kwa Simba kupigwa 3-1, na kuondolewa katika mashindano hayo.
Chanzo chetu kimeliambia Championi Ijumaa kwamba, takriban wiki sasa kocha wa Simba, Pablo amemtaka Lwanga kujiepusha na utumiaji wa vyakula vyenye mafuta mengi zikiwemo chipsi mayai, ili aweze kupona mapema, maana anahitaji huduma yake kwani tangu aungane na Simba hajawahi kumuona akicheza.
“Kadiri mambo yanavyozidi kuwa magumu kikosini kocha naye ameendelea kuwasisitiza wachezaji kujiepusha na vyakula vyenye mafuta mengi kama vile chipsi, nyama nyekundu na hata utumiaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi, ili waweze kupunguza hali ya kupata majeraha.
“Tangu kocha Pablo atue kikosini amekuwa na kawaida ya kuchunguza vyakula vya wachezaji na kwamba amekuwa akikemea vikali anapoona hali ya wachezaji kupenda vyakula vya aina hiyo, hasa kwa wenye majeraha kama ilivyo kwa Lwanga ambaye kwa sasa yupo kwenye program maalum,” kilisema chanzo hicho.
Championi limethibitisha kwa Afisa Habari wa Simba, Ahamed Ally, ambaye amesema: “Kweli kocha amekuwa akifuatilia hali za wachezaji wote, ila kwa sasa Lwanga amepewa takriban wiki tatu awe amekamilisha programu na Mungu akimjalia hadi mwisho wa mwezi huu atakuwa amerejea.”







 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kocha Simba: Tuna Ratiba Ngumu, Kucheza Jumatano Tena.​

simbasctanzania_272344526_425954759267238_8709367664503329365_n.jpg

PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba, amesema wana ratiba ngumu jambo linalowafanya kutumia nguvu kubwa kusaka ushindi.
Jana Jumamosi, Simba ilitarajiwa kuwa na mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar uliochezwa Uwanja wa Manungu mkoani Morogoro.
Kabla ya mchezo huo, Simba imetoka kupoteza mbele ya Mbeya City kwa kufungwa bao 1-0.
Jumatano ijayo watakuwa mkoani Kagera kupambana na Kagera Sugar. Hizi ni mechi za ligi kuu. Kisha Januari 30,
watawakaribisha Dar City kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar, ukiwa mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam
hatua ya 32 bora.
Pablo amesema: “Tumetoka Mbeya kucheza, kisha Mtibwa Sugar, baada ya hapo bado tuna kazi nyingine, ratiba bado inaonesha kwamba wachezaji wanapaswa kucheza muda wote.
“Katika hilo wapo wachezaji ambao ilinipasa kuwapumzisha ikiwa ni pamoja na Rally Bwalya ambaye alikuwa amechoka, hivyo tuna kazi kubwa yakufanya katika mechi zetu zijazo.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Afisa TFF Amshtaki CEO Simba Polisi.​

bvrbvra_197814541_771402063550957_3631888453041136051_n.jpg

AFISA wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF Jacqueline Kamwamu amemshataki Polisi Mtendaji Mkuu wa klabu ya Simba Barbara Gonzalez.
Mashtaka hayo yamefunguliwa katika kituo Kikuu Cha Polisi Jijini Dar Es Salaam.
Siku ya Alhamisi ya Januari 20, Barbara alipokea wito wa kufika kituoni hapo ambapo baada ya kufika aliwekwa ndani kwa saa nane kisha kusomewa shtaka lake.
Shtaka linalomkabili Barbara ni kutoa lugha isiyopendeza kwa Afisa wa TFF Jacqueline Kamwamu ambae alimzuia asiingie Uwanjani katika eneo la VIP na Watoto wadogo siku ya December 11 2021 katika mchezo kati ya Yanga na Simba.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

TFF Yakana Kumfungulia Mashtaka Barbara.​

bvrbvra_245534676_895030654768265_2654446010686184596_n.jpg

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, TFF limekana kumfungulia mashataka Mtendaji Mkuu wa Simba Barbara Gonzalez.
Mapema siku ya leo kumeibuka taarifa zilizokuwa zikidai Shirikisho hilo limemfungulia Mashtaka Barbara Gonzalez kwa kitendo cha kutoa lugha Chafu wakati wa mchezo wa Simba na Yanga Disemba 11 mwaka jana, baada ya kuzuiliwa kuingia eneo la VVIP na watoto ambao kiutaratibu hawaruhusiwi.
Taarifa sahihi ni Afisa wa TFF aliyefhamaika kama Jacqueline Kamwamu, ndie aliekwenda kufungua shauri hilo kituo cha Polisi.
Tazama hapa chini sehemu ya Taarifa ya TFF wakitoa ufafanuzu.
tff.jpeg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Bosi Simba: Yanga Ubingwa Bado.​

Try-Again-1.jpg

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah Muhene ‘Try Again’, amesema kuwa licha ya kushindwa kupata ushindi katika michezo miwili mfululizo ya ligi, bado anaamini kuwa wana nafasi ya kuwa mabingwa na kuwapiku wapinzani wao ambao kwa sasa ndio vinara wa ligi kuu, Yanga.
Simba imeshindwa kupata matokeo ya ushindi katika michezomiwili mfululizo dhidi ya Mbeya City ambapo walifungwa bao 1-0 jijini Mbeya kisha kutoa sare katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani, juzi Jumamosi.
Akizungumza na Championi Jumatatu, kiongozi huyo alisema kuwa licha ya kupoteza pointi muhimu katika michezo yao miwili iliyopita, bado wanayo nafasi kubwa ya kuutetea ubingwa wao kwani bado michezo ni mingi iliyopo mbele yao.
“Wanasimba hawatakiwi kukata tamaa kwa sasa kwani bado kuna michezo mingi ya kupambania ubingwa, kupoteza pointi au kushindwa kupata ushindi katika michezo miwili iliyopita siyo sababu ya sisi kusema kuwa msimu huu hatuwezi kutwaa ubingwa.
“Kwa sasa tunatakiwa kuangalia zaidi michezo yetu inayofuata na tuhakikishe kuwa tunakusanya pointi nyingi zaidi, jambo ambalo naamini litatusaidia kuweza kuutetea ubingwa wetu ambao naamini bado upo katika mikono yetu salama,” alisema kiongozi huyo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
#AJALI: Gari lililokuwa limebeba mashabiki wa Simba Sc
🇹🇿
tawi la #WekunduWaChalinze limepinduka katika kijiji cha Mwendakulima, Kahama Shinyanga wakati wakiwa njiani kuelekea Bukoba kwaajili ya mchezo wa Kesho Jumatano wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Kagera Sugar
Poleni Wekundu wa Chalinze, wanasimba pamoja na wapendasoka wote walioguswa na ajali hii
272748755_5034276316632278_3619218996861892797_n.jpg
Inaweza kuwa picha ya Watu 6, nje na maandishi yanayosema 'PRIVATE SIMBA PLATINOM'
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kocha Pablo Aomba Radhi Mashabiki wa Simba,​

simbasctanzania_272344526_425954759267238_8709367664503329365_n.jpg

KOCHA Mkuu wa Timu #Simba, Franco Pablo Martin amewaomba radhi mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kufuatia kichapo cha 1-0 dhidi ya Kagera Sugar.
Simba ilipoteza mchezo huo mkoani Kagera, jana Jumatano bao likifungwa na Khamis Kiiza ‘Diego’. Kocha Pablo amesema imekua bahati mbaya kwa kikosi chake kupoteza mchezo huo, hivyo hana budi kuomba radhi kwa kilichotokea Uwanja wa Kaitaba.
“Ni matokeo ya kusitikisha sana, hatukutarajia kwa sababu tulijiandaa kushinda, imeniuma sana kupoteza alama tatu hapa, niwateke radhi Mashabiki ambao walikua na matumaini na timu yao leo (jana),” amesema Pablo.
Simba imepoteza mechi mbili msimu huu na sare nne, hivyo kuwa nyuma kwa pointi 10 nyuma ya Yanga wanaoongoza Ligi Kuu Bara.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mkude Akana Kumfundisha Matusi Morrison.​

simbasctanzania_145334379_704612037083018_3518866675359278426_n.jpg

Baada mchezaji wa Simba Sc, Bernard Morrison kudai kuwa mchezaji mwenzake Jonas Mkude ndiye amekua akimfundisha Lugha ya Kiswahili chenye matusi, hatimae Mkude amekanusha hilo.
Mkude amekanusha hilo kupitia show ya #LaviDavi ya Wasafi Fm, akijibu moja ya maswali ya mtangazaji @divatheebawse alietaka kujua kama ni kweli au la! Jambo ambalo Mkude amekanusha na kudai Morrison ni mtu mcheshi na alizungumza suala hilo katika hali ya ucheshi tu
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Bundi Aliyeng’ang’ania Msimbazi.​

simba-2-2.jpg

Bundi ni ndege ambaye anatajwa kua na mikosi sana ulimwengu huu, jamii nyingi zimekua na imani tofauti tofauti juu ya ndege huyu ambaye wakati mwingine amekua akitumiwa kwenye masuala ya ushirikina.
Klabu ya Simba Sc wameendelea kupata matokeo mabovu kwenye msimu huu mara baada ya kukubali kufungwa na klabu ya Kagera Sugar kwenye uwanja wa Kaitaba uliopo mkoani Kagera. Goli pekee katika mchezo huo limefungwa na aliyekua mshambuliaji wa vilabu vya Simba Sc na Yanga Hamis Kiiza raia wa Burundi.
Klabu ya Simba Sc wanapitia wakati mgumu sana siku za hivi karibuni ikiwa ni pamoja na kupata matokeo mabaya kwenye michezo yao mitatu iliyopita. Simba Sc wameambulia alama moja pekee kwenye michezo mitatu iliyopita ambapo walitoa sare dhidi ya ya Mtibwa Sugar, na wamepoteza michezo miwili dhidi ya Mbeya City na Kagera Sugar.
Takwimu hizo kwa klabu ya Simba Sc ni mbaya sana ulizingatia malengo yao msimu huu ambapo wamepanga kushinda ubingwa wa NBC Premier League. Mambo yanazidi kua magumu kwa klabu ya Simba Sc kwa sababu mpaka sasa watakua wanazidiwa alama 10 na wapinzani wa Yanga ambao wanaongoza katika msimamo wa ligi.
Simba Sc wameingia kwenye wimbi zito la mikosi kiasi kwamba wanapoteza mvuto wa timu hiyo kama ilivyokua misimu kadhaa iliyopita ambapo waliweka rekodi ya kushinda taji la ligi kuu Tanzania bara kwa misimu minne mfululizo.
Simba Sc wanapotea kwenye ramani na sasa baadhi ya mashabiki wa soka nchini Tanzania wameanza kutoa utabiri wao juu ya nafasi ya timu hii katika mbio za ubingwa.
Tatizo la kufunga magoli kwa safu ya ushambuliaji wa klabu ya Simba Sc linazidi kukua siku hadi siku na hii imekua ndio sababu kubwa kwa timu hiyo kupata matokeo mabaya kwenye michezo ya hivi karibuni.
Pablo Franco amefanya jitihada zake za kuhakikisha kwamba timu inapata matokeo lakini jitihada hizo ni kama zimegonga mwamba na sasa Simba Sc wanaendelea kusota kwa kupata matokeo mabaya.
Wachezaji wa Simba Sc wanatengeneza nafasi nyingi za wazi lakini suala la kufunga magoli imekua changamoto kubwa sana wa wachezaji wote. Bwalya, Sakho, na Mzamiru Yassin wamepata nafasi za wazi lakini wameshindwa kupata magoli kwenye mchezo wa leo ambao ulikua muhimu sana kwa upande wao.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Wafungaji Wanaoongoza kwa Mabao Simba Sc Msimu Huu.​

john-bocco-and-meddie-kagere.jpg

Licha ya klabu ya Simba Sc kuanza vibaya msimu huu wa NBC Premier League, mshambuliaji wa klabu hiyo Meddie Kagere ameendelea kuweka rekodi zake ngumu ndani ya kikosi hicho kwa kufunga magoli mengi msimu huu.
Klabu ya Simba Sc mpaka sasa wamecheza jumla ya michezo 12 ya NBC Premier League (kabla ya mchezo wa Kagera Sugar Vs Simba Sc), katika michezo hiyo Meddie Kagere amefunga jumla ya magoli manne na ndiye kinara wa magoli msimu huu ndani ya kikosi cha Simba Sc.
Nafasi ya pili ya ufungaji bora ndani ya klabu ya Simba Sc inashikiliwa na mshambuliaji mpya wa timi hiyo Kibu Denis ambaye amejiunga na klabu ya Simba Sc akitokea katika klabu ya Mbeya City ya jijini Mbeya. Kibu Denis yeye amefanikiwa kufunga jumla ya magoli matatu kwenye michezo 12 ya klabu Simba Sc msimu huu.
Wachezaji wengine kama vile Mzamiru Yassin, Kanoute, Sakho, Mohammed Hussein, Peter Banda na Rally Bwalya wamefunga goli moja moja msimu huu.
Takiwimu hizi siyo siyo mbaya sana kwa msimu huu licha ya kwamba hazina uwihano mzuri na takwimu za msimu uliopita ambapo Simba Sc walikua na uwezo mkubwa wa kufunga magoli mengi wakiwa na washambuliaji wao hatari Chris Mugalu, Meddie Kagere, na Bocco ambao msimu huu wamekua na kiwango kibovu kwa kushindwa kufunga magoli mengi.
Simba Sc wanaendelea kurudi kwenye mfumo wao haswa baada ya kurejea kwa Clatus Chota Chama ambaye ametoka katika klabu ya RS Berkane ya nchini Morocco siku chache zilizopita. Chama ni moja ya viungo bora ndani ya ligi hii ambapo tayari ameweka rekodi nyingi nzuri akiwa na Simba Sc misimu kadhaa iliyopita.
Endapo kama Chama ataendelea kucheza kwa kiwango chake kikubwa ni wazi kwamba washambuliaji wa klabu ya Simba Sc watakua kwenye nafasi ya kufunga magoli msimu huu kutokana na ukweli kwamba kiungo huyu anaweza kutengeneza nafasi nyingi za magoli akiwa katika eneo la ushambuliaji.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mkata Umeme Simba Asiye na Bahati kwa Mashabiki.​

kanoute.jpg

Licha ya Klabu ya Simba kuanza vibaya kwenye michezo ya mzunguko wa kwanza wa NBC Premier League msimu huu lakini timu hii imeonekana kua imara sana kwenye eneo lao la kiungo ambalo kwa sasa linaongozwa na wachezaji wawili matata ambao ni Jonas Mkude na Sadio Kanoute.
Baada ya kiungo mkata umeme wa klabu ya Simba Sc Taddeo Lwanga kupata majeraha ya muda mrefu mwanzoni mwa msimu huu, mashabiki wa klabu ya Simba Sc alianza kupata hofu sana na ndipo benchi la ufundi la klabu hiyo walipofanya maamuzi ya kumuibua Mkude ambaye alikua benchi kwa muda mrefu kutokana na tabia zake za utovu wa nidhamu.
Wakati Simba wanaibuka na Mkude ambaye amezoeleka katika eneo la kiungo la klabu ya Simba Sc kwa miaka mingi iliyopita, klabu hii walikua tayari wameanza kumtumia Sadio Kanoute kutoka nchini Mali ambaye alianza kucheza soka katika ardhi ya Tanzania kwenye mchezo wa Simba Sc dhdi ya Tp Mazembe siku ya Simba Sc katika dimba la Benjamini Mkapa.
Kanoute alionyesha kiwango bora sana licha ya kwamba alikua na hofu ya kucheza soka ugenini kama ilivyo kwa wachezaji wote duniani. Umati wa mashabiki wa klabu ya Simba Sc ambao walifurika katika dimba la Benjamini Mkapa siku hiyo wakizidi kumuongeza hofu kiungo huyu ambaye sasa ameongia kwenye imani ya Pablo Franco.
Kanoute ni kiungo mwenye tabia ya kuzuia mashambulizi kutoka kwa wapinzani ambapo mara nyingi amekua anaonekana kucheza juu ya Inonga na Onyango ambao wanafunga safu ya ulinzi ya Simba Sc kupitia eneo la katikati la uwanja.
Kimo cha Kanoute ni faida kwake kuweza kucheza mipira ya juu, akili kubwa iliyopo kichwani kwake inatoa nafasi kwake kuweza kuzuia mashambulizi ya mipira ya chini.
Wewe kama mdau na shabiki wa soka nchini Tanzania utakua shahidi wa Kanoute juu ya uwezo wake mkubwa ndani ya NBC Premier League licha ya kwamba jina lake halina bahati ya kuimbwa sana na mashabiki wa klabu ya Simba Sc ambao wamekua na upofu mkubwa juu ya nyota huyu mpole akiwa uwanjani.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Winga wa klabu ya Simba Sc
🇹🇿
Peter Banda
🇲🇼
anatarajia kurejea jijini Dar Es Salaam hii leo tayari kwa kuitumikia timu yake katika mechi zijazo akitokea kwenye majukumu ya timu yake ya Taifa ya Malawi
🇲🇼
iliyokuwa inashiriki AFCON 2021.
Inaweza kuwa picha ya Mtu 1 na amesimama
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kilichotokea Baada ya Simba Kufungwa na Kagera.​

simbasctanzania_272344526_425954759267238_8709367664503329365_n.jpg

Huenda walidhrika na mafanikio ya kutwaa ubingwa wa mashindano ya kombe la Mapinduzi huko visiwani Zanzibar au ndio matokeo ya mchezo wa soka ambao kuna nyakati huwashangaza mashabiki wengi wa mchezo huo hii ni baada ya kupatikana kwa matokeo tofauti na watu walivyodhani hapo awali lakini ndio hivyo Simba baada ya kurejea kutoka visiwani Zanzibar wamejikuta wakifungwa katika mchezo dhidi ya Mbeya City, kutoa sare na Mtibwa Sugar na jumatano ya wiki hii wakafungwa tena na Kagera Sugar.
Hukuwa na shabiki wa soka hususani shabiki wa Simba ambaye angeamini kuwa timu hiyo itafungwa katika mchezo wao wa dhidi ya Kagera Sugar, hii ni kutokana na matokeo mabaya ambayo Simba wameyapata katika michezo miwili ya nyuma hivyo kuamini kuwa katika mchezo huo dhidi ya Kagera, Simba ingepata ushindi ili kurejesha natumaini yao ya kuwania ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara ambao walitwaa msimu uliopita.
Dakika 90 za mchezo kati ya Kagera Sugar dhidi ya Simba mchezo ambao ulipigwa katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera uliisha kwa Simba kulala kwa goli 1 kwa bila hivyo kufanya Simba iwe imepoteza jumla ya alama 8 katika michezo 3 ya hivi karibuni na kuwapa nafasi Yanga ya kuwa juu ya Simba kwa utofauti wa alama 10 kwa sasa.
Baada ya Simba kusalimu amri na kuchapwa bao 1 kwa bila dhidi ya Kagera Sugar kuna mambo mbalimbali yamejitokeza katika ushindi huo wa Kagera Sugar dhidi ya Simba na kwa kuwa msomaji wangu napenda uwe karibu na masuala mbalimbali ya soka leo katika makala hii nimekusogezea mambo makubwa 4 ambayo yamejiri baada ya Simba kufungwa katika mchezo huo dhidi ya Kagera Sugar.
Jambo la kwanza, Simba hadi sasa imepoteza jumla ya michezo miwili ya ligi kuu huku magoli ya wapinzani katika michezo hiyo miwili yakiwa yamefungwa na wachezaji ambao wamewahi kucheza Yanga.
Simba kabla ya kuanza kufungwa katika michezo ya ligi kuu soka Tanzania bara ilifanikiwa kucheza jumla ya michezo 10 huku wakifanikiwa kushinda michezo saba na kutoa sare michezo 3 lakini katika mchezo wao wa 11 wakafungwa na Mbeya City huku goli la Mbeya City likifungwa na mshambuliaji Paul Nonga na katika mchezo wao wa kumi na tatu dhidi ya Kagera Sugar wakafungwa tena bao 1 huku bao la Kagera Sugar likifungwa na Hamisi Kiiza.
Miaka kadhaa iliyopita Paul Nonga aliwahi kucheza katika timu ya soka ya Yanga kwa msimu mmoja kabla ya kuondoka na hivyo pia kwa mfungaji wa goli la mchezo dhidi ya Kagera sugar yaani Kizza pia amewahi kucheza katika timu ya Yanga na kufanya makubwa kabla ya kuondoka nchini Uganda na kurejea nchini baada ya kusajiliwa na Simba.
Kizza na Paul Nonga wameweka historia ya kuwa wachezaji ambao waliwahi kucheza katika timu ya Yanga na kuifunga Simba katika michezo yote miwili ambayo Simba imepoteza hadi sasa.
Jambo la pili, kadi nyekundu ambayo Hamisi Kiiza ameonyeshwa katika mchezo dhidi ya Simba na kutolewa nje ndio kadi yake ya kwanza nyekundu katika historia yake katika mchezo wa soka.
Kizza Hamisi mchezaji wa Kimataifa wa Uganda katika nafasi ya ushambuliaji amekuwa akicheza soka kwa zaidi ya miaka kumi sasa katika vilabu mbalimbali ndani na nje ya Uganda huku kwa kipindi fulani alicheza Yanga na baadae Simba na sasa yuko katika klabu ya soka ya Kagera sugar ya mkoani Kagera.
Katika kipindi chote ambacho Kizza amecheza soka katika vilabu mbalimbali vya ligi kuu katika nchi mbalimbali Barani Afrika hakuwahi kutolewa nje kwa kadi nyekundu lakini katika mchezo huo, mwamuzi aliomuonyesha kadi nyekundu na kutoka nje katika dakika za nyongeza za mchezo huo na kuwa kadi yake ya kwanza nyekundu katika maisha yake ya soka.
Kizza alilisema hilo baada ya mchezo huo kuisha wakati akihojiwa na kuomba radhi mashabiki wa Kagera sugar kwa yeye kutolewa kwa kadi nyekundu licha ya kuipa goli la ushindi timu yake.
Jambo la tatu, kufungwa goli 1 na Kagera Sugar na kushindwa kupata hata bao 1 kwa timu ya Simba, kumemifanya Simba iwe imecheza jumla ya dakika 270 bila ya kupata goli katika michezo ya ligi kuu Tanzania bara.
Dakika 90 za mchezo kati ya Mbeya City dhidi ya Simba ziliisha kwa Simba kufungwa bao 1 kwa bila, dakika tisini zingine za mchezo kati ya Mtibwa sugar dhidi ya Simba ziliisha kwa sare ya bila kufungana na katika mchezo huo wa jumatano Kagera sugar walishinda goli 1 kwa bila huku Simba wakitoka bila goli.
Dakika 90 mara tatu ni sawa na jumla ya dakika 270 hivyo kuifanya Simba iwe imecheza jumla ya dakika 270 huku ikiwa na washambuliaji wake wote tegemeo bila ya kufunga hata goli 1 kitu ambacho ni adimu sana kukiona kwa Simba kwa miaka 5 ya hivi karibuni.
Ukiwa na washambuliaji kama Bocco, Mugalu na Kagere ambao msimu uliopita walifunga zaidi ya magoli 40 na sasa wamecheza kwa dakika 270 bila goli ni swala ambalo linatia mashaka sana na kuwafanya mashabiki wa timu hiyo waanze kuwa na wasiwasi juu ya hali hiyo katika timu yao.
Jambo la nne, kadi nyekundu ambayo Kizza ameonyeshwa katika mchezo huo dhidi ya Simba umeifanya Simba iwe timu ya kwanza kucheza michezo mingi ya ligi kuu Tanzania bara huku wapinzani wao wakitolewa kwa kadi nyekundu.
Hadi sasa jumla ya wachezaji watano wa timu pinzani katika michezo ya ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Simba wametowa nje kwa kadi nyekundu hivyo kuifanya Simba iwe timu ya kwanza kucheza michezo mingi ya ligi huku wapinzani wao wakiwa pungufu kwa kutolewa wakati wa mchezo baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu.
Mchezo dhidi ya Kagera sugar, mchezo dhidi ya Mbeya City, mchezo dhidi ya Coastal Union, mchezo dhidi ya Namungo FC na katika mchezo dhidi ya Dodoma jiji wachezaji wa timu pinzani walitolewa nje kwa kadi nyekundu na kumaliza mchezo wakiwa pungufu.
Huenda kwa sababu ya kucheza kwa kukamia sana au ufundi wa wachezaji wa Simba ndio inasababisha wachezaji wa timu pinzani kuonyeshwa kadi nyekundu lakini sio kadi nyekundu pekee hata adhabu ya penati msimu huu Simba ndio timu iliyopewa penati nyingi hadi sasa lakini wamekuwa na bahati mbaya ya kushindwa kufunga penati hizo.
Mashabiki, viongozi na wachezaji wa Simba kwa sasa hawapaswi kuanza kutengeneza migogoro kwa sababu ya matokeo mabaya ya timu hiyo badala yake kwa sasa wanapaswa kuendelea kuungana kwa pamoja kuhakikisha wanatafuta njia ya kutatua changamoto ya matokeo mabaya ya timu hiyo na kurudi katika njia ya kusaka ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania Bara.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kiwango cha Chama Kudaiwa Kuporomoka, Staa Simba Aanika Haya.​

chama.jpg

LICHA ya baadhi ya mashabiki wa soka kuonyesha kutoridhishwa na kiwango cha kiungo, Cleotus Chama kwenye mchezo ambao Simba ilikubali kipigo cha bao 1-0 ugenini dhidi ya Kagera, kiungo fundi wa zamani wa Simba, Mtemi Ramadhan amekuwa tofauti na kiwango alichokionyesha Chama kwenye mchezo huo.
Chama ambaye amerejea Simba msimu huu wa usajili wa dirisha dogo baada ya kuuzwa na timu hiyo mwaka 2021, jana alikuwa miongoni mwa nyota waliochapwa kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Kagera, Januari 26, 2022.
Baada ya mchezo huo, baadhi ya mashabiki wa soka walionekana kutoridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na Chama na wengine wakiamini sio yule aliyekuwa Simba kabla ya kuuzwa nchini Morocco.
Hata hivyo Mtemi amemkingia kifua nyota huyo raia wa Zambia akisisitiza kuwa kiwango cha Chama wa mechi Kagera ni kile kile alichoondoka nacho Simba mwaka jana.
“Bado yuko vizuri, hajachuja na mashabiki tutarajie pasi nzuri za mwisho na mabao kutoka kwake. Juzi alipata nafasi moja, japo viwanja vya nyasi bandia navyo huwa vina changamoto zake tofauti na vile vya nyasi halisi, vinginevyo angeweza kufunga,” amesema Mtemi na kuongeza.
Amesema Chama yule yule aliyeondoka ndiye yule yule aliyerudi kwenye kikosi cha Simba na hana shaka kuwa baada ya kucheza mechi tatu, nne mchango wake kwenye kikosi cha Simba utaonekana.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pablo Atangaza Vita Mpya Simba.​

simba-12.jpg

KOCHA Mkuu wa Simba, Pablo Franco, juizi Alhamisi alishuka na kikosi cha klabu hiyo kutokea mkoani Kagera, na kuchimba mkwara mzito kuwa wamesahau kuhusu matokeo yao mabaya kwenye michezo iliyopita na wamekuja kuanza vita mpya.
Simba Januari 26, 2022 walipata kipigo dhidi ya Kagera, Kaitaba. Baada ya kurejea Dar, Simba sasa wanajiandaa na mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC), dhidi ya Dar City kesho Jumapili kwa Mkapa.
Kocha Pablo alisema: “Kwanza kabisa niweke wazi kuwa kama kikosi tumesikitishwa na matokeo ambayo tumeyapata katika michezo yetu mitatu iliyopita, kama utaniuliza mimi ningekwambia hatukustahili kupata matokeo yale kutokana na nafasi ambazo tulitengeneza lakini wakati mwingine hivyo ndivyo mpira ulivyo.
“Tunatarajia kuwa na mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam dhidi ya Dar City, haya ni mashindano mengine ambayo tunatetea ubingwa wake hivyo tumejipanga kuhakikisha tunapata matokeo mazuri ili kurejesha hali ya kujiamini, tutapambana kama fainali kwa kila mchezo ulio mbele yetu na naamini tuna nafasi ya kufanya vizuri.”