Yanga Thread

Mkwavinyika

Administrator
Staff member
Dec 2, 2021
49
9
26
Dar es Salaam
𝗡𝗘𝗫𝗧 𝗠𝗔𝗧𝗖𝗛
🏟


Timu ya Wananchi Jumatano tarehe 15/12/2021 inashuka dimbani kwenye mchezo wetu wa kwanza Kombe la #ASFC dhidi ya Ihefu Sc, kuanzia saa 1 Usiku kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

267841836_4726725307348831_8736970523333235827_n.jpg
 
  • Like
Reactions: Brenda

yangadaima

Mgeni
Dec 14, 2021
3
1
5
Tiketi za mchezo wetu wa kesho dhidi ya Ihefu Sc, utakaochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, zinapatikana katika vitu tajwa.
Twende kwa wingi tukaipe sapoti timu yetu
💛
💚
💪🏾


268100144_4729836040371091_3811651419738082099_n.jpeg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
FULL TIME
Yanga Sc 4-0 Ihefu Sc
⚽
6': Makambo
⚽
23': Makambo
⚽
45+1': Aucho
⚽
66': Makambo
 

Attachments

  • yanga1.PNG
    yanga1.PNG
    594.3 KB · Somwa: 0

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA YAZIMA GWARIDE SUMBAWANGA, PRISONS CHALI​

VIGOGO, Yanga SC wametoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya wenyeji, Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara hapo jana Uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga mkoani Rukwa.
Tanzania Prisons iliyokuwa inaongozwa na Kocha Msaidizi na mchezaji wa zamani wa timu hiyo ilitangulia kwa bao la Samson Mbangula kwa kichwa dakika ya 12 akimalizia mpira wa Kona wa Lambert Sabiyanka kutoka upande wa kushoto.
Kiungo Mzanzibari, Feisal Salum ‘Fei Toto’ akaisawazishia Yanga dakika ya 23 kwa shuti kali baada ya kazi nzuri ya kiungo Mganda, Khalid Aucho ambaye yeye mwenyewe alifunga bao Lila ushindi dakika ya 43 kwa kichwa cha kuchupia mpira chini chini kufuatia krosi ya kiungo Mrundi, Said Ntibazonkiza.
Kwa ushindi huo, Yanga SC inayofundishwa na kocha Mtunisia, Nasreddine Nabi akisaidiwa na Mrundi, Cedric Kaze inafikisha pointi 23 baada ya kucheza mechi tisa sasa na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi tano zaidi ya mabingwa watetezi, Simba SC ambao wamecheza mechi nane.
Hali ni mbaya kwa Tanzania Prisons inayobaki na pointi zake nane za mechi tisa katika nafasi ya 13 kwenye ligi ya timu 16, ambayo mwisho wa msimu mbili zitashuka na mbili zitakwenda kucheza na timu za Championship kuwania kusalia Ligi Kuu.
 

mhindi

Mgeni
Nov 29, 2021
17
6
5
Tanzania

Saido kapindua meza Yanga​

saido-pic.jpg


STRAIKA wa Yanga, Said Ntibazonkiza ‘Saido’ mwishoni mwa msimu ulioisha jina lake lilianza kutajwa miongoni mwa watakaopitiwa na panga, lakini mchezaji huyo ameonekana kupindua meza mbele ya kocha wake, Nasreddine Nabi na sasa ni nguzo muhimu ya mauaji kikosini.

Yanga iliinasa saini ya Saido kwa mkataba wa miaka miwili kupitia usajili wa dirisha dogo Oktoba 2020 muda mfupi akitokea kuifunga Taifa Stars katika mchezo wa kirafiki akiwa na timu yake ya taifa ya Burundi.

Alianza maisha Jangwani kwa kishindo akihusika katika mabao sita kwenye mechi nne za Ligi Kuu Bara, akifunga mawili dhidi ya Dodoma Jiji na Prisons na kutoa asisti nne, mbili katika mechi waliyoshinda 3-0 dhidi ya KMC na asisti nyingine moja kila mechi waliposhinda 3-1 dhidi ya Dodoma Jiji, walipoichapa Ihefu mabao 3-1.

Hata hivyo, baadaye majeraha ya muda mrefu yalimsumbua huku matatizo ya kinidhamu ikiwamo kutaka kutoka uwanjani baada ya kufunga bao wakati mechi ikiendelea kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa akipingana na uamuzi wa aliyekuwa kocha wa wakati huo Juma Mwambusi wa kumuanzishia benchini, vikaanza kumfuta Saido katika ramani za Yanga.

Lakini baada ya kuomba radhi kwa tukio hilo ambalo lilishuhudiwa ‘live’ na kocha Nabi ambaye alikuwa jukwaani siku hiyo baada ya kuwasili kupewa ajira Yanga, Saido sasa amekuwa mtu mpya. Amerejeshwa kikosini baada ya kuumia kwa Yacouba Songne na anakiwasha ile mbaya. Msimu huu tayari amefunga mabao mawili na kutoa asisti mbili.

Straika wa zamani wa timu hiyo, Said Bahanunzi alisema Saido alifunga mabao mawili timu ikiwa na uhitaji na presha kubwa na kwamba ni fundi wa mbinu na kucheza kwa akili. “Angekuwa mchezaji muoga angekosa, lakini alijivika ujasiri akapiga,” alisema.

Mchezaji wa zamani wa Kagera Sugar, George Kavila alisema uzoefu wa straika huyo ni faida kwa timu yake hasa wakati wa mechi ngumu za kupata matokeo.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Nabi atawaua mwaka huu​

1640166832557.png
HII Yanga ya mwaka huu itawaua watu kwa presha, ndio tambo za mashabiki kwenye vijiwe na mitandao ya kijamii baada ya mabingwa hao wa kihistoria kupindua meza na kushinda 2-1 ugenini dhidi ya Tanzania Prisons juzi, na sasa mastaa wa timu hiyo wamesema kwa mbinu za mwalimu Nasreddine Nabi na msaidizi wake Cedric Kaze, ndoo inaenda Jangwani.
Yanga imerejea jana jioni ikitokea mkoani Rukwa ikipitia Mbeya, ambako walivuna ushindi wao wa nne ugenini, lakini kuna mambo mawili yamemshtua kocha wao timu hiyo huku akifichua kwamba wachezaji wake wanayataka hasa makombe.
Kocha Nabi ameliambia Mwanaspoti kwamba hatua ya Yanga kutokea nyuma kisha kushinda ugenini huo ni ukomavu mkubwa kwa timu yake.
Nabi alisema ushindi huo wa Prisons ambao waliupata katika mazingira magumu unathibitisha kwamba msimu huu wana kila dalili ya kuwa mabingwa.
Yanga ikitokea nyuma baada ya kutanguliwa kwa bao 1-0 ilisawazisha na hatimaye kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wanajeshi hao wa Magereza katika mchezo wa juzi uliopigwa kwenye Uwanja wa Nelson Mandela mkoani Rukwa.
Rekodi zinaonyesha huu ulikuwa mchezo wa pili kwa Yanga kutokea nyuma kwa bao 1-0 kisha kushinda baada ya awali kutanguliwa 1-0 dhidi ya wanajeshi wengine wa Ruvu Shooting ambao baadaye waliwashushia kipigo cha mabao 3-1.
“Angalia tunatoka nyuma kwa bao moja tunapofanya makosa yetu lakini vijana wanatulia na kusawazisha na kupata bao la ushindi,” alisema Nabi.
“Hii ni ishara kwamba tuna kila kitu kuweza kuwa mabingwa msimu huu, najivunia sana wachezaji wangu na wasaidizi wangu wamewapa heshima kubwa uongozi na mashabiki wetu ambao wako na sisi kila mchezo.”
Nabi aliongeza kuwa alishtuka mara baada ya wachezaji wake kusimama imara wakizuia taratibu zote za kuahirisha mchezo kufuatia idadi ya wachezaji wake nane kuugua mafua makali, kichwa na kukohoa lakini bado walicheza mechi na kuibuka na ushindi.
Nabi alisema kuugua kwa wachezaji wake kulianza kabla ya safari yao ya kutokea Dar na kulazimika kumwacha staa wao Yannick Bangala ambaye hali yake ilikuwa mbaya.
“Tuliugua kabla hatujaondoka Dar es Salaam hata Bangala tulimrudisha Uwanja wa Ndege akapumzike wapo pia wengine walionyesha kuvumilia tu,” alisema.
“Tulipokuwa tunaenda kwenye kikao cha mchezo idadi ya wagonjwa iliongezeka zaidi, ilinitisha sana na viongozi walianza kuchukua hatua za kuangalia kama mchezo unaweza kusogezwa mbele,” alisema.
Nabi aliwataja wachezaji waliokumbana na maradhi hayo kuwa ni kipa Diarra Djigui, mabeki Djuma Shabani, nahodha mkuu Bakari Mwamnyeto, Dickson Job, viungo Mukoko Tonombe, Feisal Salum na mshambuliaji Fiston Mayele ambao wote walicheza mchezo huo kwa nyakati tofauti.
“Wachezaji waliposikia walinifuata na kukataa wakasema watacheza hawataki kusogeza mechi mbele, kama kocha lazima utashtuka lakini angalia walivyopambana.
“Huu ni ukomavu mkubwa kwa wachezaji hawa hii pia inaonyesha kwamba wako tayari kwa vita ya ubingwa kwa mazingira yoyote.”
Mayele, Fei, Aucho ni kati ya wachezaji waliokuwa mstari wa mbele kuhakikisha mechi hiyo haisogezwi mbele wakisema kuwa wana jambo lao msimu huu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
OFFICIAL: Kiungo wa kati Salum Abubakary "Sure Boy" amejiunga na Yanga Sc baada ya kuvunja mkataba wake na waajiri wake wa muda mrefu Azam Fc
Zawadi ya Christmas
🤶
kwa Wananchi
1640450822976.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
𝗠𝗔𝗧𝗖𝗛 𝗗𝗔𝗬
Leo Saa 1 usiku Young Africans Sc wanashuka dimbani kwenye mchezo wetu wa 10 Ligi Kuu NBC dhidi ya Biashara United ndani ya Dimba la Benjamin Mkapa.
1640522510273.png
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

YANGA YATOKA NYUMA TENA KUILAZA BIASHARA 2-1​

1640611155898.png

WENYEJI, Yanga SC wametoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya Biashara United katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Biashara walitangulia kwa bao la Atupele Green Jackson dakika ya pili tu, kabla ya mshambuliaji Fiston Kalala Mayele kuisawazishia Yanga SC dakika ya 40 kwa bao zuri la til-tak akimalizia krosi ya Mkongo mwenzake, beki Djuma Shabani kutoka upande wa kulia.
Kiungo mkongwe Mrundi, Said Ntibanzokiza akaifungia bao la ushindi Yanga dakika ya 79 kwa penalti baada ya beki Abdulmajid Mangaro kumsukuma winga Mkongo, Jeses Moloko Ducapel upande ule ule wa kulia.
Yanga inafikisha pointi 26 katika mchezo wa 10 na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi tano zaidi ya mabingwa watetezi, Simba SC ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi.
Biashara United yenyewe baada ya kipigo cha leo ambacho ni cha tatu mfululizo ikitoka kufungwa 2-0 na Mtibwa Sugar Morogoro na 1-0 na Coastal Union nyumbani, Musoma inabaki na pointi zake nane za mechi 11 sasa katika nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Msheri aanza vizuri, Yanga ikiichapa Dodoma​

yanga-pic.jpg

MWANZO mzuri kwa kipa wa Yanga, Abuutwalib Mshery baada ya kumaliza dakika 90 za mchezo wake wa kwanza bila kuruhusu bao.

Mshery alikuwa langoni akiiongoza Yanga wakati wakiichapa Dodoma 4-0 mchezo uliochezwa katika uwanja wa Mkapa.

Katika kipindi cha kwanza Yanga walianza kwa kushambulia na kuonyesha hawataki utani zaidi ya kupata

Dakika 19 Yanga ilitaka kupata bao kupitia kwa Fiston Mayele ambaye aliwazidi mbio mabeki wa Dodoma na kupiga shuti na kupanguliwa kisha kuwa kona isiyokuwa na faida.

Dakika 22 Jamal Mtegeta alionyeshewa kadi ya njano baada ya kumfanyia madhambi Saido Ntibazonkiza na kuwa faulo isiyokuwa na madhara.

Dakika 30 Yanga ilitaka kupata bao baada ya Emmanuel Martin kumfanyia madhambi Ntibazonkiza ambaye alipiga faulo nje kidogo ya goli lakini kipa wa Dodoma Jiji, Hussein Masalanga aliucheza.

Yanga ilifanya shambulizi lingine dakika 32 baada ya mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele aliyefyatuka shuti kali na kupanguliwa na kipa Masalanga na kuwa kona isiyokuwa na faida.

Dakika 38 Masalanga alifanya sevu nyingine baada ya Mayele

Dakika 40 Dodoma Jiji na wao walifanya shambulizi kupitia krosi fupi iliyopigwa na Khamis Mcha na Anuary Jabir alionganisha lakini uliishia mikononi kwa kipa.

Yanga ilipata bao dakika 42 baada ya Yassin Mustapha kupiga krosi na Mayele aliunganisha na kwenda wavuni.

Dakika 43 Dodoma walijibu shambulizi kupitia kwa Jamal Mtegeta baada ya kucheza pasi za haraka na Jabir ndani ya boksi na kufyatuka shuti kali liliopanguliwa na Mshery kisha mabeki waliokoa hatari.

Dakika 45 Dodoma walifanya shambulizi lingine baada ya kiungo Cleofas Mkandala kumipigia pasi Khamis Mcha aliyefyatuka shuti pa chinichini na kuishia mikononi kwa kipa Mshery.

Kwenye kipindi cha pili Yanga waliendelea kufanyw mashambulizi na kuonyesha kuhitaji mabao zaidi kwenye mchezo huu.

Yanga ilitaka kupata bao dakika 48 baada ya Ntibazonkiza kupiga pasi kwa Feisal ambaye alimchungulia kipana kupiga mpira mfupi uliombaa ambaa karibu na gori.

Dodoma walifanya mabadiliko dakika 54 ya kuingia Waziri Junior, Erick Nkosi na Joram Mgeveke wakichukua nafasi za Khamis Mcha, Mbwana Bakari na Hassan Nassor.

Dakika 56 Yanga ilipata bao la pili kupitia kwa Jesus Moloko baada ya Yanick Bangala kupiga mpira mrefu na Moloko aliuwahi na kuingia ndani ya boksi kidogo na kuupiga kwa juu na kwenda wavuni.

Dakika 62 Dodoma walifanya mabadiliko mabadiliko ya kumtoa Jamal Mtegeta na kuingia Seif Karihe.

Mabadiliko ya Dodoma yalionekana kuhitaji kusogeza mashambulizi mbele zaidi licha ya kuwa nyuma kwa mabao mawili.

Dakika 70 Feisal aliipata Yanga bao la tatu baada ya kupiga krosi akiwa upande wa kulia na beki wa Dodoa Jiji, Justine Bilary akiwa kwenye harakati za kuokoa alijifunga.

Wakati huo Yanga walifanya mabadiliko ya kuingia Heritier Makambo na Mukoko Tonombe wakichukua nafasi ya Fiston Mayele na Feisal Salum huku upande wa Dodoma walimtoa Emmanuel Martin na kuingia Agustino Nsata.

Dakika 81 Yanga ilipata bao la nne baada ya kupigwa pasi za haraka haraka na kiungo Khalid Aucho aliupiga mpira na kwenda wavuni.

Baada ya bao hilo mabadilio ya Mayele, Ntibazonkiza na Aucho huku wakiingia Deus Kaseke, Farid Mussa na Salum Abubakari ‘Sure Boy’, mabadiliko hayo yalionekana kushangiliwa na mashabiki.

Dakika 89 Dodoma Jiji nusura wapate bao la kufutia machozi baada ya Waziri Junior kumtoka Dickson Job na kupiga pasi kwa Mkandala aliyefyatuka shuti na kupita nje kidogo ya goli.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mukoko ampa jezi Waziri Jr​

mukoko-pi.jpg


KIUNGO wa Yanga, Mukoko Tonombe amempa jezi mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo, Waziri Junior kabla ya mchezo kuanza.

Yanga huwa na kawaida ya kugawa jezi kwa mashabiki wake kila mchezo unapokuwa unaanza.

Katika mchezo huo wakati wachezaji wa Yanga wakiwa wanaenda kugawa jezi kwa mashabiki, Mukoko yeye alimfuata Junior kisha alimnyanyua na kumpa jezi hiyo.

Junior alipoipokea alipiga picha na Mukoko huku akiishika jezi hiyo kisha akakaa na Mukoko akarudi kwenye benchi lake.

Mukoko na Junior msimu uliopita walikuwa pamoja katika kikosi cha Yanga kabla ya mmoja kuondoka kwenye timu hiyo.