Yanga Thread

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Huyu Chico ni Balaa.​

chico-ushindi-yanga.jpg

CHICO Ushindi, ingizo jipya ndani ya Yanga, ameanza kwa ushindi kwenye mchezo wake wa kwanza dhidi ya Mbuni FC mbele ya Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi.
Juzi, Chico alicheza kwa mara ya kwanza mchezo wa kirafiki na ubao wa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid ulisoma Mbuni 0-2 Yanga na mabao yote yalifungwa kwa penalti na mtupiaji alikuwa ni Tonombe Mukoko.
Chico alianzia benchi na aliingia dakika ya 64 akichukua nafasi ya Deus Kaseke na katika dakika 64 aliweza kufanya makeke yake yaliyoonyesha kwamba ikiwa ataendelea na kasi hiyo, atakuja kuwa ni chaguo la kwanza. Alisababisha penalti moja dakika ya 81 baada ya kuchezewa faulo na nyota wa Mbuni ndani ya 18 na iliweza kufungwa na Mukoko, ilikuwa dakika ya 82.
Pia alikuwa na uwezo wa kupiga pasi zenye uhakika kwa kuwa pasi zake zote alizopiga ziliwafikia wachezaji kwa asilimia 100 na aliweza kupiga jumla ya pasi 13.
Hakuwa mnyonge kwenye eneo la kumiliki mpira na kutembea nao kwa kuwa aliweza kufanya ‘dribble’ 7 huku mguu anaopenda kuutumia ni ule wa kulia na ameonekana kuwa siyo winga mchoyo kwa kuwa hata akiwa ndani ya 18, anatoa pasi.
Mkongomani huyo alitambulishwa rasmi na Yanga Jumapili iliyopita kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga, ambapo Yanga walikuwa na mchezo wa ligi ugenini dhidi ya Coastal Union uliomalizika kwa Yanga kushinda mabao 2-0.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Kocha Msaidizi wa Yanga, Cedric Kaze alisema: “Matokeo ya ushindi kwenye mchezo wetu dhidi ya Mbuni yamekuwa muhimu kwa ajili ya kuwaandaa wachezaji wetu kisaikolojia, hasa wale ambao wamekuwa hawapati nafasi ya kucheza mara kwa mara kuelekea michezo yetu ijayo ya Ligi Kuu Bara.
“Kuhusiana na uwezo wa Chiko Ushindi, alichokionyesha Jumatano ni sehemu ndogo tu ya ubora wake, ameanza vizuri na kuonyesha maelewano mazuri na wenzake na hii inaonyesha ni wazi kuwa atawahi kuingia kwenye mfumo na kutoa changamoto kwa Saido Ntibazonkiza na Jesus Moloko kwenye kikosi cha kwanza.”
Naye kiungo wa zamani wa Simba, Amri Kiemba amefungukia kiwango cha nyota huyo huku akikiri kuwa anajua.
Kiemba alisema kwa dakika chache ambazo amemshuhudia winga huyo akicheza, amebaini kuwa ni mchezaji mzuri ambaye ataongeza kitu ndani ya klabu hiyo. “Ushindi ni mchezaji mzuri, kwa dakika chache nilizomuona nimegundua kuwa ana uwezo mzuri wa kupiga krosi zenye macho, lakini pia ana uwezo mzuri wa kupiga pasi zenye macho.
“Mbali na hapo ni mchezaji mwenye uwezo wa kukokota vizuri mpira, hivyo naamini ataongeza kitu ndani ya Yanga, japo bado unahitajika muda mwingi zaidi kuthibitisha kama yeye ni bora,” alisema kiungo huyo.







 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Saido Milioni Moja Kila Mechi Yanga.​

SAIDO.png

IMEFAHAMIKA kuwa mshambuliaji mkongwe, raia wa Burundi, Said Ntibazonkiza ‘Saido’, anaingiza Sh milioni moja katika kila mchezo atakaoucheza akiwa akiwa amevaa jezi namba 60 Yanga kwenye mashindano yote na mechi za kirafiki.
Kiungo huyo tangu ametua hapo, amefanikiwa kubeba mataji mawili, lile la Kombe la Mapinduzi, mwaka jana na Ngao ya Jamii msimu huu.
Mrundi huyo ameonekana kurejea kwa kasi kubwa katika msimu huu kutokana na kujihakikishia namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza chini ya Mtunisia, Nasreddine Nabi.
Taarifa ambazo imezipata Championi Ijumaa, kiungo huyo anapata kiasi hicho kwa makubaliano waliyokubaliana katika mkataba wake huo ambao unamalizika mwishoni mwa msimu huu.
Mtoa taarifa huyo alisema kuwa kabla ya kusaini mkataba huo katika msimu uliopita, aliomba apewe jezi namba 10 aliyomkuta anaivaa Yacouba Songne lakini Mburkinabe huyo alikataa, ikabidi Mrundi akubali kuvaa namba 60 baada ya kutangaziwa dau.
Alisema kuwa Yacouba aligoma kuiachia jezi hiyo kabla ya viongozi kumbembeleza na kushikilia msimamo wake wa kutoiachia namba hiyo 10 anayoendelea kuivaa.
Aliongeza kuwa baada ya Yacouba kuendelea kugoma, wadhamini wa timu hiyo, GSM walimshawishi kumuahidi kumpa kiasi hicho cha fedha kila atakapocheza mechi akiwa amevalia jezi hiyo namba 60 na ndipo Saido akakubali.
“Wengi walikuwa hawafahamu kilichokuwa kinaendelea juu ya jezi namba 10 ambayo anaivaa Yacouba, ilizua utata mkubwa kutokana na Saido kuitaka ambayo alikuwa anaivaa tangu akiwa anacheza Ulaya na nyumbani kwao Burundi.
“Saido mwenyewe alikuwa tayari kumpa Yacouba dola 10, 000 (zaidi ya Sh 2OMil) ili amuachie jezi hiyo namba 10, lakini alizikataa na kushikilia msimamo wake.
“Jezi hiyo namba 60 anayoivaa Saido imeonekana kumnufaisha, kwani katika makubaliano yake na viongozi ambayo yapo katika mkataba, wamekubaliana kumlipa shilingi milioni moja katika kila mchezo atakaoucheza kuanzia alipojiunga na Yanga hadi hivi sasa,” alisema mtoa taarifa huyo.
Yanga kwa kupitia Makamu Mwenyekiti wa timu hiyo, Frederick Mwakalebela, hivi karibuni alisema: “Mkataba ni siri kati ya mchezaji na uongozi, hivyo ngumu kuweka wazi kila kitu kilichopo katika mkataba.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Yanga Yaifunika Simba kwa Rekodi ya Dk 2,520.​

yanga-9.jpg


KLABU ya Yanga imekuwa ikitengeneza rekodi na kuzitikisa timu pinzani ikiwemo Simba, Azam na nyingine, kwani kwa sasa ndiyo timu pekee ambayo haijaonja kipigo kwenye ligi msimu huu.
Yanga wanatamba na rekodi ya kucheza michezo mingi zaidi msimu huu kuliko timu yoyote tangu msimu huu kuanza, wamecheza jumla ya mechi 31, wakishinda 24, sare nne na kufungwa mechi tatu. Wakifunga mabao 53, wao wakiruhusu 14 tu.
Huku rekodi wanayowatesea Simba ni ile ya kucheza mechi 28 sawa na dakika 2,520 bila kupoteza. Tena kubwa zaidi wakiwa wao pekee hawajafungwa kwenye ligi msimu huu wakati Simba wenyewe wamefungwa juzi tu.
Yanga wamecheza mechi 12 za ligi kuu, wakishinda mechi tisa, sare kwenye mechi mbili, wakifunga mabao 20, wakiruhusu manne. Wamecheza mechi 12 za kirafiki wakishinda zote, mechi tatu za Mapinduzi Cup walishinda moja, sare kwenye mechi mbili, na moja ikiwa ya nusu fainali wakitolewa kwa matuta na Azam FC.
Wamecheza mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika, wakifungwa zote na Rivers United ya Nigeria, mchezo mmoja wa Ngao ya Jamii dhidi ya Ihefu wakishinda 4-0.
Mechi za kirafiki 12, wameshinda 11 na kufungwa mechi moja tu, dhidi ya Zanaco ya Zambia mabao 2-1 kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi huku wakiwa hawajatoka sare kwenye mechi hata moja ya kirafiki.
Hivyo Yanga walifungwa na Rivers mara mbili na kufungwa na Zanaco mara moja ndani ya dakika 90. Sare za Yanga ni ile ya 1-1 na Namungo, pamoja na suluhu dhidi ya Simba na kule Mapinduzi Cup sare ya 2-2 na KMKM.
Kwa upande wa Simba wao wamecheza jumla ya mechi 20, mechi 11 za ligi kuu, mechi nne za kimataifa na michezo mitano ya kirafiki. Simba Ligi ya Mabingwa walicheza mechi mbili.
Walikipiga dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana mechi mbili kwenye hatua za kwanza za mashindano hayo, walishinda ugenini 2-0 na kufungwa nyumbani 3-1.
Kisha wakacheza na Red Arrows Kombe la Shirikisho. Wakafungwa ugenini 2-1 mechi ya pili, wakati mechi ya kwanza walishinda 3-0 nyumbani. Kwa ujumla kwenye mechi zote msimu huu Simba wamefunga mabao 28, wakifungwa mabao 16.
Simba wamefungwa mechi nyingi zaidi msimu huu kuliko Yanga, walifungwa na TP Mazembe 1-0, wakapigwa na Yanga kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii 1-0. Wakatandikwa na Jwaneng Galaxy 3-1. Wakafungwa pia na Red Arrows 2-1.
Rekodi yao ya kucheza bila kupoteza ikiwa ni ya dakika 1,350 sawa na michezo 15, michezo 10 ya ligi kuu, michezo minne ya Kombe la Mapinduzi na mechi moja ya FA.
Walitoka sare ya 2-2 na Far Rabat, kisha 1-1 na Olympique De Khouribga zote za Morocco. Wakaenda sare ya 2-2 na Cambiaso, Sare na Coastal Union, sare na Biashara United kisha kwenda suluhu na Yanga yote kweli ligi kuu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mayanga, Mayele Wana Vita Yao.​

yangasc_271892792_662952828229685_5039591577653457978_n.jpg

UKIWEKA kando ile vita ya kusaka pointi tatu leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo Arusha kati ya Polisi
Tanzania inayonolewa na Malale Hamsini dhidi ya Yanga inayonolewa na Nasreddine Nabi, kuna bato ya ufungaji bora.
Bato hiyo ya kibabe inatarajiwa kuwashuhudia washambuliaji wawili ambao ni namba moja kwenye timu zao ambapo ni Vitalis Mayanga kwa upande wa Polisi Tanzania na Fiston Mayele kwa upande wa Yanga.
Mayanga ametupia mabao matano kibindoni kati ya11 na ametoa pasi tatu za mabao na kumfanya ahusike kwenye mabao nane, huku Mayele akiwa ametoa pasi moja ya bao na kufunga mabao sita na kumfanya ahusike kwenye mabao saba.
Ni mechi 11 kati ya 12 Mayanga ameanza kikosi cha kwanza ndani ya Polisi Tanzania, huku Mayele akiwa amecheza mechi zote 12.
Katika mchezo huo wa leo, wawili hao wanatarajiwa kuziongoza timu zao kusaka ushindi kwani wana uhakika wa kuanza kila wanapokuwa fiti.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Chico Apewa Majukumu ya Moloko Yanga.​

YANGA-6-1.jpg

KOCHA Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Polisi Tanzania, amempa Chiko Ushindi majukumu ya Jesus Moloko.
Chico anatarajiwa kuwa miongoni mwa wachezaji watakaoonekana kwenye kikosi cha Yanga kinachotarajia kucheza mchezo huo utakaopigwa leo Jumapili kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.
Chanzo kutoka ndani ya Yanga, kimeliambia Spoti Xtra, kuwa: “Chico amesajiliwa kwenye kikosi cha Yanga kutokana na kuwa na uwezo wa kutumia miguu yote miwili jambo ambalo ni nadra kwa wachezaji wengi wanaocheza nafasi ya winga.
“Kwa sasa Kocha amekuwa haridhishwi na kiwango cha Moloko kwani alisajiliwa kuwa mbadala wa Tuisila Kisinda, lakini aina ya uchezaji wake sio kama ule aliotarajiwa licha ya kufunga mabao na kutoa asisti.
“Tuisila alikuwa akipata mipira anakimbia kuingia ndani ya boksi tofauti na Moloko, ukimwangalia Chico
katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Mbuni FC alikuwa akipata mipira anaingia ndani ya boksi mpaka akasababisha
penalti.
“Huenda Chico akachukua nafasi ya Moloko kwa sababu kocha amefurahishwa na kiwango chake kwani anapopata mpira anatengeneza nafasi tofauti na Moloko ambaye anarudisha mipira nyuma na kuifanya timu kupunguza kasi ya
kushambulia.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MUKOKO AACHANA NA YANGA, ATUA MAZEMBE.​

AVvXsEjq-XEj3v27S0IjdDWYxwd7n4jmWKcqlnpm7NICUjFgXCD9g-AsHyom3R0W8hTdkrXM1WPcGZQUGXEQr17X5dYKUwf3PGjoGAuXJNPzkCpS22srqWZ7YK2Lj4_UrpECE4L324GRj-42bZhGD4x3mZLpbckXCrlf7Aqq82pUkYMYdu5-NwFyDreTCszv=w584-h640

KIUNGO Tonombe Mukoko ameachana na klabu ya Yanga na kujiunga na TP Mazembe ya kwao, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Taarifa ya Yanga jioni hii imemshukuru Mukoko kwa mchango wake kama Nahodha Msaidizi kwa kipindi cha msimu mmoja na nusu tangu awasili kutoka AS Vita ya kwao, Kinshasa.
Mukoko anakwenda Mazembe wiki moja baada ya Yanga kumsajili Mkongo mwingine, winga Chico Ushindi kutoka klabu hiyo ya Lubumbashi.
AVvXsEhf9BSKTN6oLQGZP6np2i14REmQajTnZmnYdzmMu98p1soRNi74BOLDnQZOhUKqUnp-2K1Q-Z0UfainMg-e-N05dRm8HHQoinGV9gz19nje0LL1pVCINBTU7bnhJTfso2gWMuySakzSt_p1h76ligIHBOo1dizeAzai4IjCDTfiwWx2grxMe_YdtE-H=w640-h622
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Makambo Ataja Siku Atakayofunga.​

makambo.jpg

HERITIER Makambo, mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa ipo siku atafunga kwenye ligi kwa kuwa ni suala la muda hana mashaka nalo.
Kwenye ligi Yanga ikiwa imefunga mabao 22 katika mechi 12 ambazo imecheza, nyota huyo raia wa DR Congo hajafanikiwa kufunga wala kutoa pasi ya bao.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Makambo alisema kuwa anatambua kwamba mashabiki wanapenda kuona akifunga ila muda bado haujafika.
“Mashabiki wanapenda kuona nafunga hata mimi pia ninapenda kufanya hivyo lakini ni suala la kusubiri kwani bado kuna mechi za kucheza na mechi zipo nyingi hivyo ipo siku nitafunga,” alisema.
Nyota huyo amecheza mechi 10 kati ya 12 na kuyeyusha dakika 279 kwenye mechi za ligi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Ntibazonkiza Ampagawisha Nabi Yanga.​

YANGA.jpeg

BIG bosi wa benchi la ufundi la Yanga, Nasreddine Nabi ameonekana kukoshwa vilivyo na kiwango cha staa wake, Saidi Ntibazonkiza ‘Saido’ huku akiwaambia viongozi wa timu hiyo wampe mkataba mpya.
Saido amekuwa na kiwango cha juu ndani ya kikosi hicho msimu huu akiwa amefunga mabao manne na asisti moja katika ligi. Nyota huyo pia anakaribia kumaliza mkataba wake mwisho wa msimu huu.
Chanzo cha ndani kutoka Yanga kimeliambia Championi Jumamosi, kwamba uwezo wa nyota huyo umefanya kocha huyo awaambie mabosi wake wampe mkataba.
“Tangu Saido aanze kucheza kwenye kikosi amemshawishi sana kocha Nabi kutokana na kiwango kikubwa alichokionesha ambapo ameutaka uongozi kumuongezea mkataba.
“Ukiangalia Saido amehusika kwa asilimia kubwa katika mabao ya Yanga, kitu ambacho Nabi ameonekana kuvutiwa nacho na kwa sasa huwezi kumwambia kitu chochote kuhusu Saido yaani anamkubali sana.”
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakalebela ameliambia Championi Jumamosi kuwa: “Saido amekuwa na kiwango kizuri lakini kwa sasa tunafikiria kumuongezea mkataba.
“Ukiangalia katika michezo ya hivi karibuni amekuwa na kiwango kizuri sana hata wewe ungeacha kumpa mkataba sasa.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Yanga Yafungukia Ishu ya Djuma Shaban.​

djuma.jpg

BAADA ya jana Januari 23 Yanga kuweza kusepa na pointi tatu mazima mbele ya Polisi Tanzania,Ofisa Habari wa Yanga, Haji Manara amefungukia kuhusu sakata la beki wao Djuma Shaban kuonekana akimpiga kiwiko mchezaji wa Polisi Tanzania.
Katika mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Djuma dakika ya 89 alionekana akimchezea faulo mchezaji wa Polisi Tanzania na mwamuzi wa kati hakuweza kuona tukio hilo ambalo lilikuwa ni baya.
Manara amesema kuwa kitendo ambacho amekifanya sio kizuri na wenyewe wanakikemea.
“Yes sio kitendo kizuri na Yanga tunakikemea hata kama kulikuwa na provocations,(hasira)”.
Baada ya kitendo hicho, Djuma alifanyiwa mabadiliko kwenye mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa.
Yanga inaongoza ligi ikiwa na pointi 35 baada ya kucheza mechi 13 za ligi na haijapoteza mchezo hata mmoja.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Hizi Hapa Sababu za Mukoko Kuondoka Yanga.​

kidanistars_272644635_337833768192404_7789918297120667803_n.webp.jpg

RASMI uongozi wa Yanga umethibitisha kwamba kiungo Tonombe Mukoko hatakuwa sehemu ya kikosi hicho kwa msimu wa 2021/22 kwenye mechi ambazo zimebaki.
Kiungo huyo anakwenda kujiunga na kikosi cha TP Mazembe kwa ajili ya kuendelea kufanya kazi ya mpira ambayo ameichagua.
Sababu kubwa ya kiungo huyo kuondoka ni makubaliano ya pande zote mbili kati ya TP Mazembe na Yanga.
Yanga wamemchukua Chico Ushindi ambaye ni kiungo na TP Mazembe wao wamemchukua kiungo Mukoko.
Mchezo wa mwisho wa Mukoko kucheza akiwa na jezi za Yanga ilikuwa mbele ya Mbuni FC ambao ulikuwa ni wa kirafiki ulichezwa Uwanja wa Sheik Amri Abeid na Yanga ilishinda kwa mabao 2-0.
Mabao yote yalikuwa ni mapigo ya penalti na aliyefunga alikuwa ni Mukoko pia Chico aliweza kucheza kwenye mchezo huo na alisababisha penalti moja ilikuwa ni Januari 19,2022.
Yanga wamesema:”Tunashukuru sana kwa mchango wako nahodha msaidizi wa klabu yetu ya Yanga. Tunakutakia kila la kheri na mafanikio kwenye klabu yako mpya ya TP Mazembe,”.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Chico Ampa Kiburi Nabi Yanga.​

Chico-Ushindi-2.jpg

KOCHA Mkuu wa Yanga, raia wa Tunisia, Nasreddine Nabi, amesema kuwa ujio wa kiungo mshambuliaji,
Mkongomani, Chico Ushindi, umeongeza ubora na ushindani wa namba katika kikosi chake.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Nabi alisema kuwa licha ya kuwepo hatihati ya kumtumia Fei Toto, lakini yupo Chico ambaye anamudu kucheza nafasi hiyo namba kumi.
Nabi alisema kuwa anaamini uwezo mkubwa alionao Chico kutokana na kumfahamu baada ya kumfuatilia tangu akiwa klabu ya TP Mazembe ya DR Congo.
Aliongeza kuwa Chico ana uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja namba 7, 10 na 11 hivyo uwepo wake katika timu, unampa nafasi kubwa ya kuwepo katika kikosi chake cha kwanza.
“Chico ana faida kubwa katika timu, hiyo ni kutokana na uwezo wake wa kucheza nafasi zaidi ya moja katika timu, hivyo ninaamini atatoa mchango mkubwa katika timu.
“Hivyo ushindani utaongezeka katika timu baada ya Chico kuja, hivi sasa kilichobakia kwake ni kuingia
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mukoko: Nitamiss Ugali na Samaki.​

mukoko.png

Baada ya kuthibitishwa ameondoka Young Africans na kusajiliwa TP Mazembe ya nchini kwao DR Congo, Kiungo Mkabaji Mukoko Tomombe ametoa ya moyoni.
Mukoko ameondoka Young Africans akisisitiza kuipenda klabu hiyo iliyomsajili mwanzoni mwa msimu uliopita akitokea AS Vita ya ya mjini Kinshasa-DR Congo.
Kiungo huyo amesema daima klabu hiyo Kongwe katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati itaendelea kubaki moyoni mwake, kufuatia maisha mazuri aliyoishi klabuni hapo.
Amesema aliishi vizuri na wachezaji wenzake, viongozi, mashabiki na wanachama, hivyo alijihisi yupo nyumbani katika kipindi chote alichokaa Young Africans.
Maneno hayo ya mapenzi ya dhati kwa Mukoko dhidi ya Young Africans, ameyaandika kwenye ukurasa wake wa Instagram usiku wa kuamkia leo, ambapo dili lake la kuondoka Young Africans lilishika hatamu kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
“Yanga ni kama familia kwangu. Siku zote itabaki moyoni. Nitaikumbuka Tanzania hasa kwa ugali na samaki wa baharini.“ Teacher Mukoko Tonombe.
Mukoko amelazimika kuondoka Young Africans, kufuatia kukosa nafasi ya kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza, baada ya kusajiliwa kwa viungo Khalid Aucho na Yanick Litombo Bangala msimu huu 2021/22.
Dili lake la kwenda TP Mazembe limechagizwa na usajili wa Chiko Ushindi Wakubanza aliyetokea klabu hiyo ya Lubumbashi hadi Young Africans, wakati wa Dirisha Dogo la Usajili lililofungwa rasmi Januari 15.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kocha Yanga Afunguka Diarra Kusotea Benchi Afcon.​

djiguidiarraofficial_272234099_3080964722168531_3277925330781385411_n.jpg

KUENDELEA kusugua benchi kwa mlinda mlango namba moja wa Yanga, Djigui Diarra, akiwa na kikosi cha timu ya Taifa ya Mali inayoshiriki mashindano ya Afcon huko Cameroon, kumemuibua kocha wa makipa wa Yanga, Mbrazili, Milton Nievov ambaye ameweka wazi kuwa huenda ikaleta athari katika kiwango chake.
Diarra hajaanza katika mchezo wowote wa Mali katika hatua ya makundi kwenye Afcon, ambapo kikosi cha timu hiyo tayari kimefuzu hatua ya 16 bora na wanatarajia kuvaana na timu ya Taifa ya Equatorial Guinea keshokutwa Jumatano saa 4 usiku majira ya Afrika Mashariki.
katika kikosi cha Yanga, Diarra ndiye mlinda mlango namba moja huku Aboutwalib Mshery akiwa ndiye namba mbili na Erick Johora ambaye ni mlinda mlango namba tatu wa kikosi hicho.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Milton alisema: “Nilikuwa nikimtazama Diarra wakati nikiwa na Simba, naweza kusema huyu ni miongoni mwa makipa bora zaidi ndani ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa sasa na hili linathibitishwa na kuitwa kwake kwenye kikosi cha timu ya Taifa kubwa kama Mali.
“Najua hajapata nafasi ya kucheza kutokana ushindani mkubwa wa namba anaokutana nao kwenye kikosi hicho na kwa upande wetu hilo sio jambo jema, tunatamani kuona anacheza kwa sababu mara zote mchezaji anakuwa bora zaidi kadiri anavyopata nafasi ya kucheza na kukaa benchi kunaweza kuhatarisha kiwango chake japo hatuwezi kuthibitisha hilo kwa sasa mpaka atakaporejea.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Ambundo Aahidi Makubwa Yanga.​

yangasc_272285981_684213372744416_8925370667724190717_n.jpg

WINGA wa Yanga, Dickson Ambundo, amefunguka na kuelezea matumainiyake ndani ya kikosi hicho baada ya juzi Jumapili kufunga bao la ushindi dhidi ya Polisi Tanzania.
Yanga ambao ni vinara wa Ligi Kuu Bara wakikusanya alama 35, juzi Jumapili kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, iliibuka na ushindi wa bao 0-1 dhidi ya Polisi Tanzania.
Ambundo alifunga bao hilo dakika ya 64 akimalizia pasi ya Fiston Mayele. Hilo ni bao la kwanza kwa Ambundo tangu ajiunge na Yanga msimu huu akitokea Dodoma Jiji.
Akizungumza na Spoti Xtra Ambundo, amesema kuwa: “Nimejisikia furaha kufunga kwa mara ya kwanza kwenye
mchezo muhimu kama ule. “Malengo yangu ni kuhakikisha ninaisaidia timu kutwaa ubingwa, siwezi kusema nitafunga mabao mangapi, ila nitajitaidi kuhakikisha timu yangu ninaisaidia kuchukua ubingwa.
“Mashabiki wa Yanga wawe na imani na timu yao, Mungu akipenda tutabebea ubigwa msimu huu.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Djuma, Bangala Watimka Yanga.​

wadoldjuma_officiel__265189717_1586901598340337_5234136936641486476_n.webp.jpg

MASTAA wa Yanga, Djuma Shaaban na Yannick Bangala jana Jumanne saa tisa kamili alfajiri walipanda ndege kurejea nyumbani kwao DR Congo tayari kwa kujiunga na timu ya taifa ya nchini kwao.
Hiyo ikiwa ni saa chache tangu mastaa warejee jijini Dar es Salaam wakitokea Arusha walipokwenda kuvaana na Polisi Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa Sheikh Amri Abeid mkoani huko.
Katika mchezo huo wa ligi, Yanga ilifanikiwa kuwafunga Polisi Tanzania bao 1-0 ambalo lilifungwa na Dickson Ambundo akipokea pasi ya Fiston Mayele kabla ya kufunga.
Djuma na Bangala wamerejea nyumbani kwao Congo kwa ajili ya kujiunga na kambi ya timu ya Taifa ya
DR Congo inayojiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Bahrain.
ybangalaa4_270059626_1113318229500859_3795380467250545417_n.jpg

Sasa rasmi timu hiyo itakawakosa wachezaji wake hao wawili katika mchezo ujao wa Kombe la FA watakaocheza dhidi ya Mbao FC utakaochezwa Jumamosi hii kwenye
Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.Wachezaji hao Jumamosi iliyopita walitangazwa kuwepo katika orodha
ya wachezaji 25 wa timu hiyo wataokwenda kucheza mchezo huo wa kirafiki.
Nyota hao wawili watakwenda kucheza mchezo huo maalum wa kujiandaa kutafuta nafasi ya kufuzu
Kombe la Dunia. Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Februari Mosi, mwaka huu na wachezaji hao watakuwepo sehemu ya kikosi hicho.
Wachezaji hao tangu wajiunge na Yanga wamekuwa tegemeo na uhakika wa kuanza katika kikosi cha Nabi
kinachowania Ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Kikosi kimewasili Mwanza tayari kwa maandalizi ya mchezo wetu wa Kombe la ASFC dhidi ya Mbao Fc, Jumamosi kwenye Dimba la CCM Kirumba.
Image
Image
Image
Image
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mastaa Yanga Wakomba Mamilioni.​

yanga-6.jpeg

USHINDI wa 11 walioupata Yanga, umewapa wachezaji wa timu hiyo bonasi ya Sh 265Mil katika michezo ya Ligi Kuu Bara tangu kuanza kwa msimu huu. Hiyo ikiwa ni siku chache tangu watoke kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Tanzania, mchezo uliopigwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.
Ushindi huo umewafanya waendelee kukaa kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 35 wakicheza michezo 13 ya
ligi, huku watani wao Simba wakifuatia wakivuna pointi 25 wakibakiwa na mchezo mmoja mkononi.
Yanga tangu kuanza kwa msimu huu, wameshinda michezo 11 huku wakitoka suluhu miwili dhidi ya Simba iliyochezwa Uwanja wa Mkapa, Dar nyingine na Namungo FC nayo ilichezwa Uwanja wa Ilulu, Lindi.
Ipo hivi, wadhamini wa Yanga ambao ni GSM mara baada ya kuanza kwa msimu waliwaahidi wachezaji kuwapa Sh 20Mil katika katika kila ushindi wa mchezo wa ligi.
yanga-5.jpeg

Lakini katika michezo miwili ambayo ilikuwa migumu dhidi ya Coastal Union iliyochezwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga matajiri hao waliongezewa bonasi na kufikia sh 35Mil kama wakiwafunga, ikaja kuongeza na kufikia Sh 50Mil walipowavaa Polisi Tanzania ambayo yote walifanikiwa kushinda na kuchukua Sh 85Mil.
Mastaa hao wakishinda michezo hiyo 11 ya ligi walijikuta wakichukua Sh 265Mil zilizogawiwa kwa wachezaji na benchi la ufundi la timu hiyo, linaloongozwa na Kocha Mkuu Mtunisia, Nasreddine Nabi.
Hivyo wachezaji hao katika michezo 11 waliyocheza na kushinda, tisa walivuna Sh 180Mil kutokana na bonasi ya Sh 20Mil kabla ya kuongezewa dhidi ya Coastal na Polisi Tanzania ambazo zilifikia Sh 265Mil. Wadhamini hao, huenda wakaendelea kutoa bonasi ya Sh 50Mil katika michezo miwili ya mwisho ya kumaliza mzunguko wa kwanza wa ligi watapocheza dhidi ya Mbeya City na Geita Gold.
Wachezaji hao wameahidiwa kupewa bonasi ya ushindi pekee, kama wakitoa sare hakutakuwa na bonasi, umewekwa utaratibu huo kwa ajili ya kuongeza hamasa ya wachezaji kupambana kupata ushindi pekee utakaowafanya
watwae ubingwa mwishoni mwa msimu.
Mkurugenzi Uwekezaji wa GSM ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Injinia Hersi Said,
hivi karibuni alizungumzia hilo la bonasi na kusema kuwa: “Bonasi ipo kwa wachezaji wetu ambayo
maalum kwa ajili ya kuongeza hamasa wakiwa uwanjani.
“Bonasi hiyo imekuwa ikibadilika kwa kuongezeka kutokana na aina ya timu tunayokutana nayo. Na bonasi ni siri kati ya uongozi na wachezaji.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

GSM Wamuita Mayele Fasta.​

YANGA-1-2.jpg

YANGA kweli safari hii imepania kuhakikisha kuwa inawalinda mastaa wake hiyo ni baada ya uongozi wa klabu hiyo chini ya wadhamini wao, GSM kumuita fasta mshambuliaji hatari wa timu hiyo, Fiston Mayele kwa ajili ya mazungumzo.
Fiston Mayele ndani ya Yanga kwa sasa ndiye kinara wa upachikaji mabao akiwa na jumla ya mabao 6 huku akiwa wapili kwenye orodha ya wafungaji bora. Kinara wa jumla ni Reliants Lusajo wa Namungo mwenye 7.
Chanzo cha ndani kutoka Yanga kimeliambia Championi Jumatano kuwa, uongozi wa GSM umefanya
kikao na Mayele ambaye amekuwa ni msaada wa timu na hiyo ni katika kuhakikisha kuwa anaendelea kusalia ndani ya timu hiyo kwa muda mrefu zaidi.
YANGA-6-1.jpg

“Ni kweli Mayele leo Jumanne (jana) alikutana na uongozi wa GSM ambao walikuwa na kikao na kubwa zaidi lilikuwa ni kuzungumza ni kwa namna gani mshambuliaji huyo anaendelea kusalia ndani ya timu kwa muda
mrefu licha ya kuwa tayari ana mkataba wa miaka miwili ambao alisaini wakati anajiunga na timu hiyo.
“Unajua kuna mambo mengi kwenye mpira, unapokuwa na wachezaji wazuri lazima ufahamu jinsi ya kuishi nao na ndio maana vitu kama hivi uongozi kukaa kufanya vikao na mchezaji ni kawaida kwa ajili ya manufaa ya
pande zote mbili yaani mchezaji na timu,” kilisema chanzo hiko.
Alipotafuta Mayele kuzungumzia juu ya ishu hiyo alisema: “Ni kweli nilikuwa na kikao na uongozi jambo
ambalo sio geni kwa wachezaji na yalikuwa ni mambo binafsi ambayo nisingependa kuyaweka hadharani.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Senzo: Ubingwa Yanga ni Suala la Muda Tu.​

senzo.png

OFISA Mtendaji Mkuu (CEO) wa klabu ya Yanga, Senzo Mbatha ameweka wazi kuwa kwa moto ambao kikosi chao kinaendelea kuuwasha kwenye Ligi Kuu Bara, wanaamini kuwa ni suala la muda tu kabla hawajatangazwa kushinda ubingwa msimu huu.
Yanga ndiyo vinara wa msimamo wa Ligi Kuu Bara mpaka sasakwa tofauti ya pointi 10 ambapo wamefanikiwakujikusanyia pointi35 katika michezo yao 13 waliyochezampaka sasa, huku wakiwa wamesaliwa na michezo miwili tu kukamilisha mzunguko wa kwanza ambayo ni dhidi ya Mbeya City na Mtibwa Sugar.
Akizungumzia mipango yao ya ubingwa msimu huu, Senzo alisema:“Tunajivunia mwenendo ambao kikosi chetu kimekuwa nao kwa michezo yote 13 ya kwanza, ni wazi tumefanya kazi kubwa kufikia hapa na binafsi kuona tunaweza kupata matokeo katika michezo migumu ugenini kama vile dhidi ya Coastal Union na Polisi Tanzania tofauti na ilivyokuwa msimu uliopita.
“Hili linanionyesha wazi kuwa kwa kiasi kikubwa tuna nafasi kubwa ya kuibuka mabingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu, nadhani ni suala la muda tu na tunapaswa kuendelea na kasi hii mpaka mwishonimwa msimu.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Manara Kuhama Nchi.​

manara-4.jpg

MSEMAJI wa Klabu ya Young Africans, Haji Sunday Ramadhani Manara ameweka nadhiri ya kuhama nchi, endapo klabu hiyo itashindwa kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu 2021/22.
Manara ameweka nadhiri hiyo akiwa kwenye kipindi cha Sports Arena cha Wasafi FM leo Alhamis (Januari 27), ambapo amesema hakuna la kuwazuia kufanya hivyo, baada ya kusubiri kwa miaka minne.
Amesema Young Africans ina kikosi cha kutimiza dhamira ya kutwaa ubingwa msimu huu na hana shaka na hilo, ndio maana ameweka nadhiri hiyo hadharani.
“Tukikosa ubingwa msimu huu mimi nitahama nchi, nitachana passport yangu na kila kitu, yaani Yanga hii ikose ubingwa? tufungwe michezo minne sisi ili tupoteze sifa hii ya kuwa mabingwa wa msimu huu? Haiwezekani!”
“Huwa ninafurahishwa sana na vichekesho vinavyoendelea huko, kuna watu wanasema Yanga imekua kawaida yao kuongoza halafu sisi tunakuja kuchukua ubingwa, hivi ni vichekesho jamani, watu wanaishi kwa mazoea, yaani kwa Yanga hii usubiri hilo litokee, kweli mimi nitahama nchi,”
amesema Manara.
Young Africans inaongoza msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kufikisha alama 35, baada ya kucheza michezo 13, ikiwaacha Simba SC kwa tofauti ya alama 10.