Ligi Kuu Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

KIIZA ATOKEA BENCHI KUIUA SIMBA KAITABA.​

AVvXsEgYSUf05o3K8lRqZrna6CoTCsceoFQsitnKdHVKpS1BgCc8qs5TV4x5a5V7Om5j88LnMTN3nqSBFknIbjNtZSxruLKy8B7vTKOS9IGkxWL9tUqCuEmaiGSTCAVuq7WWZFE6zZpw3JcQSjG82gt6y7vp3xUO3bKLk7mLLIFaEWI8KUm3Wv4iaBYpn3DO=w640-h640

MSHAMBULIAJI mkongwe wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ ametokea benchi kuifungia bao pekee Kagera Sugar ikiibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya mabingwa watetezi, Simba SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba mkoani Kagera.
Kiiza aliingia dakika 56 kuchukua nafasi ya Ally Ramadhani na akafunga bao hilo dakika ya 70 akimalizia pasi nzuri ya Ally Nassor ‘Ufudu’, kabla ya Mganda huyo kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 90 kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.
Kagera Sugar inafikisha pointi 17 na kupanda hadi nafasi ya nane, wakati Simba inabaki na pointi zake 25 katika nafasi ya pili, ikizidiwa pointi 10 na vinara, Yanga SC baada ya timu zote kucheza mechi 13 za msimu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kizza: Inonga, Onyango ni Mabeki Bora.​

kizza.jpg

Baada ya kupeleka msiba mzito katika mitaa ya msimbazi, mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Burundi Hamis Kizza anayekipiga katika klabu ya Kagera Sugar amefunguka mambo mazito juu ya walinzi wa klabu ya Simba Sc Hennock Inonga pamoja na Joash Onyango.
Hamis Kizza alikua ni nyota wa mchezo wa jana ambao Kagera Sugar walipata ushindi wa goli moja kwa sifuri dhidi ya klabu ya Simba Sc katika dimba la Kaitaba. Kizza ndiye aliyetenganisha matokeo katika mchezo huo baada ya kufunga goli safi na pekee kwa upande wa Kagera Sugar ambao walikua katika uwanja wao wa nyumbani.
Baada ya mchezo huo kumalizika Hamis Kizza alipata nafasi ya kufanya mahojiano na waandishi wa ambao walijitokeza kushuhudia mchezo huo ambao ulikua ni mgumu kwa timu zote mbili. Kizza katika mazungumzo yake aligusia uwezo na kiwango cha walinzi wa klabu ya Simba Sc ambao ni Inonga na Onyango.
Kizza ameweka wazi kwamba walinzi hao ni wachezaji wazuri na imara sana licha ya kwamba alifanikiwa kufunga goli moja dhidi yao. Kizza amesema kwamba alitumia akili nyingi kuwatoroka kabla ya kufunga goli lake lakini hii haifanyi kuona kwamba Inonga na Onyango ni wachezaji wa kawaida sana.
Kizza ni mchezaji mkongwe ndani ya ligi kuu Tanzania bara ambapo miaka kadhaa ya nyuma nyota huyu aliwahi kupita katika vilabu vya Simba Sc na Yanga katika nyakati tofauti tofauti. Kizza kwa bahati nzuri sana ameweza kucheza kwa mafanikio makubwa sana akiwa na timu zote mbili na hivyo basi mashabiki wa Simba Sc na Yanga wamekua na kumbukumbu nzuri juu ya nyota huyu.
Kizza ni mshambuliaji hatari sana na mpaka sasa akiwa na Kagera Sugar tayari amefunga magoli mawili ikiwa ndio kwanza amejiunga na timu hii siku chache zilizopita. Kagera Sugar wamepata mshambuliaji mzuri na hatari sana ambaye anaweza kuwasaidia kufanya vizuri msimu huu ikiwa ni pamoja na kumaliza katika nafasi za juu katika msimamo wa NBC Premier League.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

SHABANI NA MAREFA YANGA NA POLISI WAFUNGIWA.​


BEKI Mkongo wa Yanga SC, Djuma Shabani amefungiwa mechi tatu za kutozwa faini ya Sh. Milioni 1 kwa kumpiga kiwiko mchezaji wa Polisi Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu baina ya timu hizo.
Taarifa ya Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TPLB) imesema kwamba pamoja naye, refa Hance Mabena na wasaidizi wake, Paschal Joseph na Jackson Samuel wote wameondolewa kwenye orodha ya waamuzi kadhaa wa Ligi Kuu kwa mechi tatu hadi tano kwa kutochukua hatua dhidi ya tukio hilo.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

KOCHA WA SIMBA AFUNGIWA NA FAINI MILIONI 2.​


KOCHA Mspaniola wa Simba SC, Pablo Franco Martin ametozwa faini ya Sh. Milioni 2 jumla kwa makosa mawili yanayofanana na kufungiwa mechi tatu kwa kupiga chupa chini kwenye mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mtibwa Sugar.
Taarifa ya Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TPLB) imesema kwamba Pablo ametozwa faini ya Sh. Milioni 1 kila mchezo dhidi ya Mtibwa na dhidi ya Kagera Sugar kwa kukataa kufanyiwa mahojiano na Waandishi wa Habari baada ya mechi hizo za ugenini.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kiiza Aweka Rekodi ya Ajabu Ligi Kuu.​

kizza.jpg

HAMIS Kiiza (Diego) ndiye aliyebaki kwenye kumbukumbu mbaya kwenye vitabu vya Simba baada ya kuwafungia Kagera Sugar bao 1-0 na Simba kukosa alama tatu kwenye mechi tatu mfululizo.
Kiiza aliingia dakika ya 58 kuchukua nafasi ya Ally Ramadhan na ilimchukua dakika 12 pekee kuweza kuweka utofauti wa matokeo kwenye mchezo huo.
Kwa bao lake hilo mbele ya Simba, Kiiza ameweka rekodi ya kuzifunga timu zote mbili akiwa anazitumikia timu hizo kwa nyakati tofauti. Septemba 20, 2015 Kiiza akiwa na jezi ya Simba, aliwapiga Kagera Sugar ‘hat trick’ kwenye Uwanja wa Mkapa.
Kisha Januari 26 amewafunga Simba akiwa na jezi ya Kagera Sugar. Kiiza kwenye mechi hiyo aliweka rekodi ya kucheza dakika chache na kisha kutolewa nje kwa kadi nyekundu kufuatia kadi mbili za njano alizopewa kwa makosa tofauti.
Huu ni mchezo wa pili kwa Kiiza tangu atue Kagera Sugar, mchezo wake wa kwanza ilikuwa ni dhidi ya Dodoma Jiji akitoa pasi ya bao lililowapa ushindi Kagera wa mabao 2-1.
Hii ni mara ya tatu Kiiza anakuja Tanzania akitokea kwao Uganda, mara ya kwanza ilikuwa 2011- 15, akiwa anaitumikia Yanga. Alipotemwa akaenda kwao Uganda.
Kisha wakati wa dirisha dogo la msimu wa 2015-16 akasajiliwa na Simba. Simba alicheza msimu mmoja tu kisha akaondoka akiwa mfungaji bora klabuni hapo, akifunga mabao 19 katika mechi 30 za ligi.
Akiwa anaitumikia Yanga alicheza mechi 80 na kufunga mabao 56, alishawahi kucheza Free State ya Afrika Kusini, URA ya Uganda, El Hilal SC El Obeid ya Sudan, Vipers na Fasil Kanema ya Ethiopia.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mtibwa Sugar: Yanga Wanaletwa Manungu.​

yanga-7.jpeg

OFISA Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru ameweka wazi kwamba hawafikirii kuacha kuutumia Uwanja wa Manungu kwa wakati huu kwenye mechi za Ligi Kuu Bara ambazo zipo mbele yao ikiwa ni pamoja na ile dhidi ya Yanga.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Kifaru alisema kuwa uwekezaji ambao wameufanya unawapa nguvu ya kutumia uwanja wao bora ambao upo kwenye viunga vya miwa Morogoro.
“Sisi tumefanya uwekezaji bora na imara na mashabiki wa Mtibwa Sugar wanatambua kwamba tupo imara na baada ya Simba kucheza Uwanja wa Manungu hata Yanga nao tutawaleta hapa.
“Hatufikirii kuondoka hapa zaidi ya kuendelea kuuboresha uwanja wetu, hatujiendeshi kwa kutegemea mapato ya uwanjani bali uwezo upo na tupo imara,” alisema.
Mtibwa Sugar ipo nafasi ya 13 ikiwa imekusanya pointi 12 baada ya kucheza mechi 13 na safu yake ya ushambuliaji imefunga mabao saba. Walipocheza na Simba uwanjani hapo walitoshana nguvu ya bila kufungana.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mbeya City Yaichimba Mkwara Yanga.​

lule.jpg

KOCHA Mkuu wa Mbeya City, Mathias Lule, ameitahadharisha Yanga, kuwa isitarajie kupata mteremko katika mchezo ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, watakapokutana Februari 5 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
Mbeya City, wapo nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 22 kibindoni huku wakiwa wameshuka uwanjani mara 13 wakiwa juu ya Azam FC kwa pointi moja malengo yao mwakani ni kushiriki michuano ya Shirikisho barani Afrika.
Lule amesema kuwa malengo yao ni kucheza michuano ya Shirikisho mwakani ili kuwapa uzoefu wa michuano ya kimataifa wachezaji wake kama ilivyokuwa kwa Namungo na Biashara ambazo kwa misimu ya karibuni zimeiwakilisha nchi pamoja na Simba.
“Tunapaswa kuwa na muendelezo mzuri katika michezo minne ijayo ili kujiwekea katika mazingira mazuri yakutimiza malengo yetu ambayo yatatimia kama tutapata ushindi kwenye michezo yetu,” alisema Lule.
Mbeya City watakuwa kibaruani Februari 5, kuwakabili vinara Yanga, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam, katika muendelezo wa kuzisaka alama tatu ambazo zitawasaidia kusogea juu katika msimamo wa Ligi kuu Tanzania Bara.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Prisons: Tupo Tayari Kuwakabili Simba.​

prisons-1.jpg

KOCHA Msaidizi wa Tanzania Prisons, Shaban Kazumba, amebainisha kuwa kwa sasa wamewekeza nguvu na umakini kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Simba ili kuhakikisha wanapata ushindi na kujitoa kwenye nafasi ya mwisho ya msimamo wa Ligi Kuu Bara.
Mchezo huo wa ligi unatarajiwa kupigwa Februari 3, mwaka huu ambapo Prisons watakua wageni wa
Simba kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
prisons-2.jpg


Akizungumza na Spoti Xtra, Kazumba alisema: “Baada ya kupata ushindi kwenye mchezo wetu wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Rhino Rangers, wachezaji wamefanikiwa kurudisha morali yao kwa sababu tulikuwa na mwenendo usioridhisha kwenye michezo iliyopita ya ligi.
“Simba ni timu nzuri, tunawaheshimu lakini na sisi pia tuna kikosi bora, tutahakikisha tunawapa ushidani, matokeo yatajiweka wazi ndani ya dakika 90.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Simba? Wanafungika mbona.​

FUNGIKA PIC

KOCHA Mkuu wa Tanzania Prisons, Patrick Odhiambo amesema vipigo walivyopata katika mechi mbili mfululizo vinatosha na sasa shughuli inahamia dhidi ya Simba kuhakikisha wanafanya kweli, huku akiwataka matraika wake kubadilika.
Odhiambo alitua kwa ‘Wajelajela’ hao hivi karibuni akichukua mikoba ya Salum Mayanga aliyejiunga na Mtibwa Sugar na katika mechi mbili alizosimamia zote amekumbana na vichapo huku wakifungwa jumla ya mabao 6-0.
Timu hiyo inatarajia kuwa kibaruani kuwakabili Wekundu wa Msimbazi, Februari 6 kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam ukiwa wa raundi ya 14 kwa timu hizo.
Hata hivyo, timu hizo zinakutana huku kila upande ukiuguza majeraha ya kupoteza mechi iliyopita, baada ya Simba kulala 1-0 dhidi ya Kagera Sugar huku Prisons wakila kisago cha mabao 4-0 mbele ya Azam.
Odhiambo aliliambia Mwanaspoti kuwa matokeo waliyopata katika mechi mbili nyumbani hayakuwa mazuri, hivyo mchezo ujao na Simba lazima kieleleweke.
Alisema makosa yaliyofanywa na vijana wake haswa sehemu ya kipa na ushambuliaji ameifanyia kazi huku akiwataka washambuliaji kuwa makini katika kumalizia mipira ya mwisho.
“Siyo matokeo mazuri, lakini nimeona wapi tuliteleza na nimefanyia kazi tangu mechi na Azam, kwa sasa tunajipanga kumalizia hasira kwa Simba, naamini tutarejesha furaha kwa mashabiki,” alisema Odhiambo.
Straika na kinara wa mabao kikosini humo, Jeremia Juma alisema licha ya kwamba mchezo huo utakuwa mgumu, lakini lolote linaweza kutokea.
“Tumepoteza mechi mbili lakini si kwamba hatuwezi kushinda mchezo unaofuata, dhidi ya Simba, tunafahamu ugumu wake ila lolote linawezekana na hii ni ligi, tunaenda kwa umakini na tahadhari,” alisema Juma.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Wababe wa Simba watua kwa Yanga.​

WABABE PIC


HADI sasa ni Yanga pekee ambayo haijapoteza mchezo wowote kwenye Ligi Kuu Bara lakini unaambiwa Mbeya City wanataka kuweka rekodi na historia ya kuwazima vigogo wote wa soka nchini kuhakikisha vinara hao nao wanakaa.
Mbeya City licha ya kutovuma, lakini imekuwa ya moto msimu huu baada ya kutembeza vipigo ikiwamo dhidi ya bingwa mtetezi, Simba na Februari 5 watawavaa Yanga kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Nahodha wa timu hiyo, Paul Nonga alisema wao msimu huu kila mechi ni vita ya pointi tatu na hawaangalii wanacheza na nani kwani wanafahamu timu yoyote ya Ligi Kuu ni ngumu.
“Sisi kila mechi tunataka pointi tatu na msimu huu tumeweka malengo, tunashirikiana wachezaji wote kuhakikisha tunapata ushindi, Yanga tunawaheshimu ila hatuwaogopi,” alisema Nonga.
Naye kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ alisema wanafahamu mchezo utakuwa mgumu kutokana na rekodi waliyonayo wapinzani, lakini Mbeya City hawana presha na matarajio ni ushindi.
“Mchezo utakuwa mgumu na ushindani, kila mmoja anataka ushindi, tunajua Yanga ni timu kubwa na wachezaji wake, lakini hatuna hofu binafsi nimejipanga kuendeleza rekodi ya kutofungwa,” alisema Dida.
Kocha mkuu wa timu hiyo, Mathias Lule, alisema Yanga ni kama timu nyingine na mchezo huo ni wa kawaida kama zilivyopita nyingine na kwamba vijana wake wako fiti.
“Hii ni ligi hakuna cha Yanga au nani, kimsingi vijana wangu wako fiti kisaikolojia na kiufundi.”
na wako tayari kwa mchezo huo tukiamini tutashinda,” alisema Lule.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SIO ZENGWE: Simba, Yanga wanapokuwa wenyeji ugenini.​

wenyeji pic

KATIKA miaka ya hivi karibuni nguvu ya klabu za Simba na Yanga inazidi kuwa kubwa, huku klabu nyingine zinazoshindana nazo zikionyesha nguvu yake ndani ya dakika tisini tu.
Hivi sasa Yanga na Simba kwenda hata Morogoro ni kitu kikubwa kama vile kwenda Nigeria au Cameroon kucheza mechi za Ligi ya Mabingwa wa Afrika au Kombe la CAF.
Ni kama vile klabu nyingine 14 zinazoshindana nazo kwenye Ligi Kuu hazina shabiki hata mmoja zaidi ya kutegemea mashabiki wa moja ya timu hizo kuwashangilia wanapocheza na moja ya klabu hizo kongwe.
Hata Coastal Union ambayo ina historia ya muda mrefu katika soka nchini, bado inahaha kuwa na mashabiki wake yenyewe, hali kadhalika Mtibwa Sugar, Kagera na hata Azam ambazo zina muda wa kutosha kwenye soka nchini.
Nini kinasababisha klabu hizo kutokuwa na mashabiki wafia timu licha ya kuwa na muda mrefu kwenye soka?
Ni kweli kwamba Yanga na Simba zina historia kubwa si tu kwenye soka nchini, bali hata kwenye katika historia ya nchi hivyo si ajabu kwao kuvuna mashabiki kiasilia bila ya hata kutumia nguvu kubwa.
Pengine tatizo kwao ni kutumia mtaji mkubwa wa mashabiki wao kugeuza kuwa fedha. Bado hazina vyanzo vizuri vya mapato vitokanavyo na uwingi wa mashabiki wao.
Lakini nimeona katika siku za karibuni Yanga ikianzisha kitengo cha ushirikishaji mashabiki (fans engagement), ambacho kwanza kilikuwa kinaongozwa na Antonio Nugaz na sasa kimewekwa chini ya Haji Manara.
Pengine ni kutokana na uwezo wake mkubwa wa propaganda ndio maana amepewa kitengo hicho pamoja na kile cha habari, lakini sidhani kama kimetengenezewa vipimo vya ufanisi wake.
Ni vigumu kwa klabu kujiendesha bila ya kuwa na mashabiki wake kindakindaki. Na ni ajabu kwa klabu kuwepo mchezoni kwa zaidi ya miaka kumi lakini haijajenga wigo mpana wa mashabiki kiasi kwamba hata inapocheza mechi za nyumbani dhidi ya timu kama Simba au Yanga, ndio kwanza inaonekana iko ugenini.
Hili ni jambo ambalo haliji kwa bahati tu kama inavyodhaniwa kwa Simba na Yanga, bali kwa mipango ya kisayansi. Watafiti wanasema moja ya mambo yanayoweza kugeuza mashabiki kuwa kindakindaki ni ushindi wa uwanjani.
Ni lazima kwanza klabu iwe na matokeo mazuri uwanjani ndipo ianze kuvutia mashabiki. Lakini wanasema matokeo pekee hayavutii sana mashabiki, hasa kwa nchi kama hii ambayo ni kama imegawanyika nusu kwa nusu kwa kuziangalia Simba na Yanga.
Mashabiki pia huangalia ni jinsi gani wanahusiana na timu zao, hapa ni kuangalia uimara wa klabu na utamaduni wake. Yaani leo klabu inapata matokeo haya, zengwe linaanza hadi uongozi unang’oka, keshokutwa tatizo jingine hadi mashabiki hawaelewi kinachoendelea.
Wataalamu hao wanaona kuwa ushirikishaji mashabiki lazima uangaliwe katika mambo manne; siku za mechi, siku zisizo za mechi, mazoezini na nje ya mazoezi. Mashabiki wanashirikishwaje?
Kuna program gani za kushirikisha mashabiki siku za mechi, siku zisizo za mechi, mazoezini na nje ya mazoezi? Kuna tiketi maalum kwa ajili ya mashabiki kuungana na viongozi na wachezaji nyota siku za mechi?
Labda kwa sababu huku viwanja ni vya wazi, mashabiki huweza kuhudhuria mazoezi ya timu yao. Kwa wenzetu, siku za mashabiki kuhudhuria mazoezi ya timu ni maalum, na hasa siku ambazo kocha hafundishi mbinu. Huku tunashirikishaje mashabiki siku za mazoezi?
Lakini kitu kingine kikubwa ambacho kinaendana na wakati ni kushirikisha mashabiki kwa kutumia mitandao ya kijamii kupeleka habari muhimu na za kufurahisha mashabiki. Simba, Yanga na Azam zimeanza kwa nguvu, lakini zimeishia kutoa taarifa tu, lakini si kushirikisha mashabiki.
Inakuwaje klabu kama Mtibwa Sugar, Kagera, Coastal Union, Prisons hazina akaunti za mitandao ya kijamii kwa ajili ya kushirikisha mashabiki wao?
Tunategemea mashabiki waje kwa bahati au tunaridhika kushangiliwa na mashabiki wa Yanga wakati timu tukicheza dhidi ya Simba?
Hatukasirishwi na hali ya viwanja kuwa tupu tunapocheza dhidi ya timu nyingine, ukiondoa Yanga na Simba?
Bila ya kuanza program maalum za kushirikisha mashabiki, Yanga na Simba wataendelea kuwa wenyeji ugenini.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

JICHO LA MWEWE: Mapokezi ya wakubwa mikoani na hatima ya 'Leeds' wetu.​

mwewe pic

MAISHA yanahama na mbwembwe zake. Siku hizi imezuka fasheni ambayo zamani haikuwepo. Wakubwa wa soka letu wamekuwa wakipokewa kwa mbwembwe nyingi wanapokwenda mikoani. Zamani wakubwa walikuwa wanaingia kimya kimya.
Labda kwa sababu walikuwa wanaingia na mabasi, lakini siku hizi wakubwa wetu Simba na Yanga huwa wanaingia mikoani kwa ndege. Umati wa mashabiki unawasubiri wakubwa wetu. Wengine wanajipanga barabarani.
Zamani hali kama hii ilikuwa inatokea pale tu wakubwa wakichukua taji nje ya nchi au nje ya mkoa. Kama vile Yanga walivyotwaa taji la Afrika Mashariki na kati pale Kampala Uganda mwaka 1993. Kama vile Simba walipoitoa Zamalek na kusonga mbele katika michuano mabingwa wa Afrika mwaka 2003 pale Cairo Misri.
Siku hizi watu wa mikoani wamechangamka. Wanashindana kuwapokea wakubwa wetu. Nini hatima yetu? Unajiuliza, majuzi Yanga walikwenda Mwanza kucheza dhidi ya Mbao katika michuano ya FA wakapokewa kwa mbwembwe zote. Huu ni mkoa ambao hauna timu ya Ligi Kuu. Bahati mbaya au nzuri sidhani kama wenyewe wanajali.
Kama ilivyokuwa zamani ndivyo tunavyorithisha vizazi vyetu. Nchi nzima imegawanyika kuwa Simba na Yanga, basi. Hata watoto wadogo wa mikoani nao wameingia katika mkumbo wa kufuata hisia za baba na mama zao. Hakuna anayetaka kuwa shabiki wa Prisons wala Mbeya City wala Geita Gold. Ni mwendo wa Simba na Yanga tu.
Nini matokeo yake? klabu zao zinakosa hamasa ya mashabiki wa nyumbani. Mashabiki ni roho. Simba na Yanga zinasonga mbele kwa sababu ya hamasa za mashabiki. Mikoani hatuna timu za namna hii. Labda kidogo Tanga ambako wamebakia mashabiki wachache wa asili wa Coastal Union na African Sports.
Lakini zaidi klabu hizi zinakosa pesa. Zinashindwa kujiendesha kwa sababu hazina mashabiki wala wanachama wanaojitolea kuziendesha klabu hizi. Bahati mbaya zaidi hata uwanjani mashabiki hawaendi. Siku pekee ambayo Mbao inaweza kupata mashabiki ni pale inapocheza na Yanga. Watajitokeza mashabiki waTATIZO
Siku hizi mashabiki hawaendi katika mechi za mikoani kwa sababu wanaangalia Simba na Yanga katika televisheni.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Azam ya Moallin unapigwa na yeyote.​

azam pic

KAMA unadhani kuwazuia washambuliaji wa Azam wasipate bao utakuwa umefanikiwa sahau! Maana unaambiwa mikakati mipya ya kocha mkuu wa kikosi hicho, Abdihamid Moallin ni kuona kila mchezaji anafunga mabao.
Moallin alisema kuwa wachezaji aliokuwa nao wana uwezo mkubwa wa kufunga hivyo licha ya jukumu la kutupia nyavuni kuwa ni la washambuliaji, atahakikisha anaandaa mikakati imara itakayofanikisha dhamira yake ya kila mmoja uwanjani kuwa mfungaji.
“Kuna siku washambuliaji wanakuwa hawako kwenye kiwango kizuri ,sasa ukiwa kama kocha ni lazima uangalie njia mbadala ya kukuwezesha kupata ushindi, hivyo ninachokifanya ni kuwatengenezea uwezo kila mmoja wao kufunga,” alisema Moallin.
Katika hatua nyingine uongozi wa timu hiyo chini yake Ofisa Mtendaji Mkuu, Abdulkarim Amin ‘Popat’, umemtangaza Omar Abdikarim Nasser kuwa kocha wao msaidizi baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu kwa ajili ya kushirikiana na kocha mkuu Moallin.
Akizungumzia ujio wa kocha huyo, Moallin alisema kuwa yalikuwa ni mapendekezo yake ya kuongezewa nguvu kwenye benchi la ufundi hivyo ni wakati wa kufanya kazi kwa kushirikiana ili kufikia malengo ya klabu.
“Tulikuwa naye kipindi chote cha michuano ya Mapinduzi ila kulikuwa na taratibu kadhaa ambazo zilikuwa hazijakamilika, ila kwa sasa kila kitu kimewekwa wazi na uongozi hivyo jukumu lililopo mbele yetu ni kufanya kazi,” alisema Moallin.
Nasser na Moallin ni kama wanaendana kwenye mambo mbalimbali ya soka kwani licha ya kuwa ni watu wenye asili ya Somalia, wana uwezo mkubwa wa kuchambua mechi (match analyst) ambapo hapo kabla ya Moallin kuteuliwa kuwa kocha mkuu alikuwa akiifanya kazi hiyo.
Naye Nasser amewahi pia kufanya hivyo akiwa na timu ya vijana ya umri wa chini ya miaka 23 (U-23) ya Al Sadd ya nchini Qatar kabla ya kufanya majukumu hayo pia akiwa na klabu ya Al Duhail ya huko huko.
Al Sadd ni moja ya timu kubwa nchini Qatar iliyokuwa ikifundishwa na gwiji wa zamani wa Hispania, Xavi Hernandez ambaye kwa sasa amerejea Barcelona akiwa kocha mkuu.
Licha ya kuwa na asili ya Somalia, Nasser alichukua uraia wa England na anahudumu kama kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Somalia kuanzia mwaka jana hadi sasa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Rafu hatari Ligi Kuu.​

rafu pic

KUNA haja sheria 17 za soka kukumbushwa mara kwa mara kwa wachezaji ili kuepuka kufanyiana vitendo vya utovu wa nidhamu vinavyoweza kuhatarisha maisha yao.
Madhara ya kucheza kwa utovu wa nidhamu yaliwahi kumuathiri aliyekuwa straika wa Yanga, Amissi Tambwe baada ya kukabwa na beki wa Ruvu Shooting, George Michael.
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ilimfungia mechi tatu Michael kutokana na tukio hilo lililohatarisha maisha yake na tukio hilo lilikuwa Februari 2015.
‘Fair play’ ni moja ya kanuni za soka ambazo zinatakiwa kufuatwa ndani ya dakika 90 za mchezo kwa kila timu na mchezaji mmojamoja.
Licha ya sheria hiyo kuwepo, yapo baadhi ya matukio yanayojitokeza makusudi yakifanywa na wachezaji wenyewe kwa wenyewe yanayoonekana kuhatarisha maisha.
Kuna matukio manne ya ajabu msimu huu yamefanywa na wachezaji kwenye viwanja mbalimbali nchini. Mwanaspoti linakuletea baadhi ya matukio ya kushangaza yaliyofanywa na wachezaji na kuzigharimu timu zao.

SIMBA vs COASTAL UNION
Oktoba 31, 2021, katika Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, Simba ilikuwa mwenyeji wa Coastal Union katika mchezo uliomalizika kwa sare ya bila kufungana.
Katika mchezo huo ilimlazimu mwamuzi Raphael Ikambi kutoka Morogoro kutoa kadi nyekundu kwa Henock Inonga wa Simba kwa kosa la kinidhamu alilomfanyia Issa Abushee.
Abushee alimvuta jezi Inonga akiwa katika harakati za kupambania mpira, kitendo kilichomfanya nyota huyo kumpiga kichwa na kutolewa kwa kadi nyekundu iliyoigharimu timu yake.
Mbali na Inonga katika mchezo huo Jacob Junior alilimwa kadi nyekundu kutokana na faulo kwa kosa la kujitakia akipiga mpira kwa hasira kabla ya mwamuzi kuamuru ikawa kadi ya pili ya njano baada ya awali kuonywa kwa kushindwa kucheza mchezo wa kiungwana kwa Sadio Kanoute.

POLISI TANZANIA vs YANGA
Mchezo uliokuwa na upinzani mkali kwa timu zote mbili ulipigwa Januari 23 Uwanja wa Sheikh Amir Abeid, Arusha huku Yanga ikish-inda bao 1-0.
Katika mchezo huo beki wa Yanga, Djuma Shaaban
alimchezea rafu ya makusudi nyota wa Polisi Tanzania, Yahya Mbegu akimpiga kiwiko usoni na kugalagala chini.
Licha ya uwepo wa waamuzi wanne ndani ya mchezo, lakini hawakuliona tukio hilo hadi baada ya video ya mchezo huo kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zikionyesha tukio hilo. Djuma amefungiwa mechi tatu na faini ya Sh1 milioni.

SIMBA vs NAMUNGO
Novemba 3, mwaka jana, Simba ilicheza na Namungo katika Uwanja wa Mkapa ambapo Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0.
Katika mchezo huo mwamuzi Nassoro Mwichui alitoa kadi nyekundu kwa beki wa Namungo, Abdlulaziz Makame aliyemchezea rafu Shomary Kapombe ambayo huenda ingemsababishia madhara makubwa kwenye mguu wake.
Ilikuwa dakika ya 50 ya mchezo huo ambapo Makame aliigharimu timu yake ikicheza pungufu ingawa baadaye aliomba msamaha kwa Kapombe.

BIASHARA UNITED vs SIMBA
Mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Bara ambao Simba ilitoka sare ya bila kufungana, beki wake Kennedy Juma alionyesha mchezo usiokuwa wa kiungwana kwa Christian Zigah.
Baada ya tukio hilo ilimlazimu mwamuzi Emmanuel Mwandembwa kumpa kadi ya njano kwa kumpiga mwenzake teke la mgongoni.
Tukio hilo lilitokea dakika za nyongeza za mchezo huo baada ya John Bocco kukosa mkwaju wa penalti iliyosababishwa na Pape Sakho aliyechezewa rafu na Salum Kipaga.
Staa wa zamani wa Mecco ya Mbeya, Abeid Kasabalala anasema wachezaji wanapokuwa uwanjani damu zao zinakuwa zinachemka, hivyo anaweza akafanya lolote na kinachokuwa kinatakiwa kufanywa ni wenzake kumtuliza.
“Mchezaji akiwa amechemka na akafanyiwa kitu kitakachomkasilisha anakuwa nusu mtu na nusu jini. Anaweza akafanya lolote baadaye akitulia anajuta. Kikubwa ni wachezaji waepuke vitendo vya utovu wa nidhamu,” anasema.
Samuel Mpenzu, mwamuzi wa zamani wa soka anasema muda mwingine unakuta mchezaji hajaonwa na mwamuzi, lakini ikaonekana kwenye runinga na wachezaji huwa wajanja kuvizia mwamuzi jicho lake liko upande gani ili kufanya tukio wanalokusudia.
“Wachezaji wajanja sana kusema kweli. Unakuta mwamuzi muda mwingine hajaona tukio...wajitahidi kujirekebisha hizi tabia sio nzuri hata kidogo, maana mchezaji anaweza kuhatarisha maisha ya mwenzake,” anasema.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Prisons Wapo Tayari Kuwakabili Simba.​

prisons-1.jpg

LIGI Kuu ya NBC Tanzania Bara, inatarajiwa kuendelea jioni ya leo Alhamasi kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam ambapo wenyeji Simba watapambana na Tanzania Prisons.
Timu hizo zinakutana huku zote zikiwa zimetoka kupoteza michezo yao iliyopita katika ligi kuu, Simba walifungwa 1-0 na Kagera Sugar, wakati Prisons walitembezewa kipigo cha mabao 0-4 dhidi ya Azam FC.
Akizungumza na Spoti Xtra, Ofisa Habari wa Prisons, Jackson Mwafulango, amesema: “Maandalizi yetu yamekamilika na wachezaji wako tayari kwa ajili ya mapambano yaliyo mbele yetu.”
Prisons mpaka sasa wako katika nafasi ya 16 ambayo ndiyo ya mwisho katika msimamo wa ligi hiyo wakikusanya alama 11, huku Simba wakishika nafasi ya pili na alama zao 25.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SIMBA SC YAIKALISHA PRISONS KWA BAO LA TUTA.​

AVvXsEgQX1eKIOx2bL9IIA1bjx19BNnulKEBl-1_qsfmc66WhJNXaDcBw6OMf_VIpcFAEE9M4sfhL2kJJhhYnHHmGgLBbf-8yq6j5FUG3mdMUzOsj650uYnBOHZmgdvwydFDrdeqBsAu1hzBym9fEjmvtoNmqCTW-u3JEnN6iV9V7o8VdFbFnbky6B19iu2H=w640-h498

BAO la mshambuliaji Mnyarwanda mzaliwa wa Uganda, Meddie Kagere dakika ya 78, limetosha kuipa Simba SC ushindi wa 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo, mabingwa watetezi wanafikisha pointi 28 katika mchezo wa 14, ingawa wanabaki nafasi ya pili wakizidiwa pointi saba na vinara, Yanga SC ambao pia wana mchezo mmoja mkononi.
Tanzania Prisons hali inazidi kuwa mbaya baada ya kichapo cha leo, wakibaki na pointi zao 11 baada ya mechi 14 na kuendelea kuzibeba timu nyingine zote 15 kwenye ligi hiyo.
Katika mchezo uliotangulia, wenyeji, Ruvu Shooting walilazimishwa sare ya 1-1 na Mbeya Kwanza Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.
Saadat Mohamed alianza kuifungia Ruvu Shooting dakika ya 36, kabla ya Habib Kyombo kuisawazishia Mbeya Kwanza dakika ya 51.
Kwa matokeo hayo, Ruvu Shooting inafikisha pointi 12 na kusogea nafasi ya 14 na Mbeya Kwanza wanatimiza pointi 13, ingawa wanabaki nafasi ya 12 baada ya tlmu zote kucheza mechi 14.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Ligi ya Tanzania Yaingia Top 10 Afrika.​

Shirikisho la Kimataifa la Historia na Takwimu za Mpira wa Miguu (IFFHS) limetangaza orodha ya Ligi Bora duniani kwa mwaka 2021, ambapo Ligi Kuu ya Brazil (Serie A) imeshika nafasi ya kwanza.
Ligi Kuu Tanzania imepanda kwa nafasi tisa (9) kutoka nafasi ya 71 (2020) hadi nafasi ya 62 (2021) duniani huku kwa Afrika ikishika nafasi ya 10 na kusalia kuwa Ligi pekee kwenye 10 Bora ya Afrika kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
ligi.jpg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Mechi ya Yanga dhidi ya Mbeya City itakayopigwa Jumamosi Februari 5 kwenye Uwanja wa Mkapa itachezwa saa 1:00 usiku na sio saa 2:30 usiku kama ilivyokuwa inaeleza awali.
yangasc_272956522_621035745676948_9039599249652413405_n.jpg
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

AZAM FC YAJISOGEZA NYUMA KABISA YA SIMBA.​


WENYEJI, Azam FC wameibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Mabao ya Azam FC yamefungwa na washambuliaji wake wa kigeni, Mzambia Rodge Kola dakika ya tano na Mkongo, Idris Mbombo dakika ya 64.
Kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 24 katika mchezo wa 14 na kupanda nafasi ya tatu, ikiizidi pointi mbili Mbeya City ambayo hata hivyo ina mechi moja mkononi.
Dodoma Jiji inabaki na pointi zake 17 za mechi 14 sasa baada ya kucheza mechi 14 pia katika nafasi ya nane.