Ligi Kuu Thread

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

HERSI AONYWA, MASHABIKI WAIPONZA COASTAL.​

AVvXsEguhHJGRofg71DAL34fKGcucLqElOBge0GQFt23TXtvRVK6B5XZscJb4d-OwZbFfn_JT5ZGv4GMm0Z8HmP7NcAfpjpNQi__Ya8U_74-G8WkcjnQAkz8N3Q61LU3e-NXEBcLn7YvIx-35ZM1SwOsgDcByC7LSs9eiUyqqKDEmsy4S1bBkW-OOHhvgetV=w640-h578

KIONGOZI wa klabu ya Yanga, Hersi Said amepewa onyo kali kwa kosa la kuingia uwanjani kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Taarifa ya Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TPLB) imesema kwamba nayo Coastal imetozwa faini ya Sh. Milioni 1 baada ya mashabiki wake kumtupia chupa mchezaji wa Yanga wakati akishangilia.
AVvXsEgzYq2-b3vF_lwGTFGFp9EEEwMsJfdJBCHHsxe-ad9-6O7zqX3fARWmacrk95Rubi-qRXs36pDuRyfWqIPcKwIqgMFJ1lwwxUcraLuXRr8rV0Nv4XN-DiS46yEx1_02GkqUfSUZjlw3kcGOnBkVLk3QYvAPbH8LJVEkZTgjWwamNLlnr7yW32EESB5p=w512-h640
AVvXsEgisryU-yFGO5GmRtCOfBx00o5eH1_RV9-esqJFDZSzi8o44IrghhDWLpeVYmmGCGAM3SDChaTP0OeKgYwHwt1u8g9jnQfvp8NDe-Xm-tjKgu3c0sNK3ZsTE_viN1nFbr5YPejb6-CH7-IV-uhrQamzSDI43Yx3rXhnBqbbmhbdwN7IaREkn22WqSJt=w512-h640
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

YANGA SC YAPUNGUZWA KASI, 0-0 NA MBEYA CITY DAR.​


WENYEJI, Yanga SC wamelazimishwa sare ya bila kufungana na Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku wa jana Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Sare inayoiongezea alama moja kila timu, inaifanya Yanga ifikishe pointi 36 na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi nane zaidi ya mabingwa watetezi, Simba SC baada ya wote kucheza mechi 14.
Mbeya City yenyewe inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 14, ingawa inabaki nafasi ya tatu ikizidiwa pointi moja na Azam FC.
Mechi nyingine ya Ligi Kuu , Kagera Sugar imeibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Mabao ya Kagera Sugar yamefungwa na Erick Mwijage dakika ya 20 na 73, wakati la Coastal Union limefungwa na Vincent Abubakar dakika ya 54.
Kagera Sugar inafikisha pointi 19 na kusogea nafasi ya tano, wakati Coastal Union inabaki na pointi zake 17 katika nafasi ya nane baada ya wote kucheza mechi 14.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SIMBA SC YAILAZA MBEYA KWANZA 1-0 BAO LA CHAMA.​

AVvXsEjDr_3qWqTHQFlpG6CwAnFKrda2x4SmPNsOSzd_Er45aqlG9oaF3NeBRv7HQTvTOpcrAOpz9paqUEqFZ-r0J7mZfN_r7x6JwrhdZlPerR-PnD8qhMZ9W8TTvr4Sohj8HlDjEdgHgaDHj6isetE1JzsmZqx8dmScEDameMGvPXDjuAV8m8N51Qbnh2Sl=w640-h416

BAO pekee la kiungo Mzambia, Clatous Chama dakika ya 80 limetosha kuipa Simba SC ushindi wa 1-0 dhidi ya Mbeya Kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Sifa zimuendee mshambuliaji Mnyarwanda, Meddie Kagere aliyevunja mtego wa kuotea wa mabeki wa Mbeya Kwanza na kuendeleza shammbulizi lililozaa bao hilo.
Kwa ushindi huo, mabingwa hao watetezi wanafikisha pointi 31 katika mchezo wa 14, ingawa inabaki nafasi ya pili, ikizidiwa pointi tano na watani wa jadi, Yanga ambao pia wana mechi moja mkononi.
Mbeya Kwanza wanabaki na pointi zao 13 za mechi 14 pia katika nafasi ya 12.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

NAMUNGO NA GEITA ZAWAPIGA MTIBWA NA POLISI 3-1.​

AVvXsEhXFDTSwPw_ci6OFKi_VU5lghQBBVr-l_1B9sh9nZcIwSxLS4NkLGwHgG_XMxSDcaRRuMkLhFejTrH06Bk6YMjVCUO2fsokgaD-qeEbQLw0nFzSEovPDRidCmbbJ_iIEiS-KqrxgCj38Sfy3I0xtc_sjQhKxu6DGtBHmi_3LV0pscZTz1ey1YfvBU4a=w580-h640

WENYEJI, Namungo FC wameibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
Mabao ya Namungo FC yamefungwa na Ibrahim Mkoko dakika ya 33 na Relliant Lusajo mawili, dakika ya 18 na 52, wakati la Mtibwa limefungwa na Muludi Mayanja dakika ya 45 na ushei.
Kwa ushindi huo, Namungo inafikisha pointi 20 na kusogea nafasi ya tano, wakati Mtibwa inabaki na pointi zake 12 katika nafasi ya 14 kwenye ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi 14.
Nayo Geita Gold imetumia vyema Uwanja wa nyumbani, Nyankumbu kwa kuichapa Polisi Tanzania 3-1.
Mabao ya Geita yamefungwa na Kelvin Nashon dakika ya 20, George Mpole dakika ya 24 na Amos Charles dakika ya 46, wakati la Polisi limefungwa na Vitalis Mayanga dakika ya 70.
Kwa ushindi huo, Geita inafikisha pointi 17 na kusogea nafasi ya nane, wakati Polisi inabaki na pointi zake 18 na kuteremka kwa nafasi moja hadi ya saba baada ya wote kucheza mechi 14.
Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitateremka moja kwa moja na mbili zitamenyana na timu za Championship kuwania kubaki Ligi Kuu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

TANZANIA PRISONS YARAJESHA MECHI ZAKE MBEYA.​

AVvXsEi3y1JwyjuywUwX-GOGrHkCR0D6gmLpXIfuiVuQxqS38ns-7u5gXujvM9PMXm9WLwubMw27QFeTdEvvDafruFxsr8qWsK5T8QPQBJUQIxbIV0HJjUzztXLAibmqDaBE-72zF59p--xF2OKelD9fkrM4zeV7NQ2nf6j8n3tGAs4aZho2GD6CnqEiB816=w640-h414

KLABU ya Tanzania Prisons imeamua kurejesha mechi zake za nyumbani Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya kuanzia hatua iliyobaki ya msimu.
Hatua hiyo inafuatia mwenendo mbaya katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa msimu wa pili mfululizo sasa tangu ihamie Uwanja wa Nelson Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.
Kwa sasa Tanzania Prisons inashika mkia katika Ligi Kuu, ikiwa imeambulia pointi 11 tu katika mechi 14.
AVvXsEjaTQJ_TiyIbvct6IdSfvTlKSj5GlyJh-NXbmrEeazETX4U8wyylcLsQNR9r89taOWlvdXVP-r6JaFPZVRwQpe3We5KbtPADXOjWKjY7cKPXsXkdYL0mkHkJLT9AxM56W_LC3hNzZvxwWbCiCu35hQvjxrAo-5cxL1NBOGpcBMIs9QtyYR9DymFd0VM=w640-h640
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kocha Mbeya City: Tulikuja Kuwavuruga Yanga.​

yanga-4-1.jpg

MATHIAS Lule, Kocha Mkuu wa Mbeya City, amesema kuwa waliingia uwanjani kuwavuruga Yanga baada ya kujua kwamba wamewasoma kwenye mechi zao ambazo wamecheza.
Juzi, Mbeya City iliweza kusepa na pointi moja mbele ya Yanga ambao ni vinara wa ligi wakiwa na pointi 36 baada ya kucheza mechi 14 msimu wa 2021/22 na hawajapoteza mchezo.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Lule alisema kuwa alikuwa anatambua ubora wa Yanga ulipo na namna bora ya kuwavuruga jambo ambalo limewafanya wapate pointi moja ambayo kwao ni muhimu.
“Yanga ubora wake ni eneo la kati na ukiwaacha wacheze wao wanacheza kwa kujiamini, hivyo tulichokifanya ni kuwavuruga kwenye kila kitu, hiyo ilikuwa ni mpango kazi wetu, ndiyo maana unaona kwamba hata mipira iliyokufa tulikuwa tunaitumia bila kuleta hatari kwao.
“Kikubwa ilikuwa ni kuanza na mfumo wa kujilinda kisha kushambulia kwa kushtukiza na kuwabana kwenye eneo la viungo ambalo limekuwa likitumika kupata ushindi. Wao walitusoma kwenye mechi zetu tukabadili mbinu wakakutana na kitu cha tofauti,” alisema Lule.
Mbeya City imesepa na pointi nne mbele ya vigogo Simba na Yanga msimu wa 2021/22 baada ya kuwatungua Simba bao 1-0 Uwanja wa Sokoine kisha ikawa ni sare ya bila kufungana na Yanga, Uwanja wa Mkapa, juzi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

GSM YAJITOA LIGI KUU, GHARIB AJIUZULU STARS.​

KAMPUNI ya GSM imejitoa katika orodha ya wadhamini wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa kile ilichokieleza Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi (TPLB) kushindwa kutekeleza makubaliano.
Aidha, Mwenyekiti wa kampuni hiyo, Gharib Said Mohamed amejiuzulu Uenyekiti wa Kamati ya Taifa Stars kuanzia leo.

8DD02A55-4C99-4A8D-ADB6-044C2BB56F95.jpeg
 
Last edited:

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MAYELE MCHEZAJI BORA LIGI KUU FEBRUARI.​

MSHAMBULIAJI Mkongo wa Yanga SC, Fiston Kalala Mayele ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara mwezi Januari, huku Francis Baraza wa Kagera Sugar akiwa Kocha Bora.
47E92D15-935D-4654-8DC5-9496789E3FC6.jpeg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

TFF YAITAFUTIA MAJIBU GSM KUJITOA LIGI KUU.​

8C35EE2F-F37D-4876-BFC6-FA6A234B8358.jpeg

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limekiri kupokea barua ya kampuni ya GSM kujitoa katika orodha ya wadhamini wa Ligi Kuu, lakini imesema itaifanyia kazi aria hiyo kabla ya kutoa majibu.
Jioni ya leo GSM imetangaza kujitoa katika orodha ya wadhamini wa Ligi Kuu kwa kile ilichokieleza TFF na Bodi ya Ligi (TPLB) kushindwa kutekeleza makubaliano.
Aidha, Mwenyekiti wa kampuni hiyo, Gharib Said Mohamed amejiuzulu Uenyekiti wa Kamati ya Taifa Stars kuanzia leo.
4A7A0229-DA43-4FBC-8995-71B1A03129D9.jpeg
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Manara, Bumbuli wawakalia kooni waamuzi.​

Wakizungumza na wanahabari leo kwenye makao makuu ya klabu hiyo, Bumbuli amesema waamuzi wamekuwa na matukio tata hali iliyowafanya leo watoe ya moyoni.
“Tunawataka waamuzi wetu wajitafakari kwa matukio haya, wanaosimamia wachukue hatua juu ya jambo hili kwa sababu watu wanawekeza pesa nyingi kwenye mpira,” amesema Bumbuli na kuongeza;
“Ligi ikiwa na ubora thamani ya Ligi yetu itazidi kuwa kubwa na mpira wetu kiujumla utazidi kukuwa.”
Upande wa Manara amesema upande wa waamuzi kwenye mechi za Simba wapo watu wanalalamika juu maamuzi yanayotolewa.
Manara aliyataja matukio matata ambayo yalitokea ikiwepo mchezo wa Biashara Utd dhidi ya Simba mwamuzi hakuwa na ubora.
Manara alifunguka na kusema wenzao (Simba) waliomba mechi ihairishwe lakini sisi kesho yake tukacheza mechi huku wachezaji wetu wakiumwa na kula panadol.
“Lazima tuwe na usawa kwa timu zote, hata upande wa viongozi kuhukumiwa wanabidi wawe na usawa, mpira unagusa hisia za watanzania”amesema Manara na kuongeza;
“Sisi hatutaki kupendelewa bali tunataka usawa wa ndani ya uwanjani kwa timu zote.”
Manara amesema wao wanakumbusha waamuzi kutambua majukumu yao na hawalalamiki bali wanafanya kwa ajili ya mashabiki zao.
“Mashabiki wetu wanaona kabisa kinachoendelea na sisi hatuwezi kukaa kimya, mimi binafsi siwezi kunyamaza kusemes mpira,” amesema Manara.
Naye Bumbuli alirejea kuzungumza na amesema kuna matukio ambayo yanatokea kwenye mechi za watani wao (Simba) na yana maswali mengi.
Bumbuli ametaja mechi na kinachowashangaza akisema;”Dakika zilizoongezwa kwenye mechi 14 zetu ni 34 huku Simba wameongezwa dakika 75 kwenye mechi 15,”
Bumbuli aliongeza akisema upande wa wapinzani Simba wamepewa kadi nyekundu sita na kupata penalti nane.
“Kadi na penalti hizi sio zote hazifai hapana bali zipo ambazo sio halali ndio maana tunaongea, hii huwezi kukuta ikiwa Simba wanaongoza, sanasana mechi ya sare wataongezwa na watapata bao dakika 94,” amesema Bumbuli na kuongeza;
“Waamuzi wajitafakari maana mpira umebeba hisia za mashabiki wengi sana.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kisa GSM, Musukuma amshambulia Rais TFF.​

pic-msukumka-data.jpg

Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku Musukuma amemshukia Rais wa Shirikisho la soka nchini TFF Wallace Karia kwa kumtuhumu kuwa adui namba moja wa kuua soka la Tanzania, kufuatia kujiondoa kwa Mdhamini Mwenza wa Ligi Kuu Tanzania Bara Kampuni ya GSM.
Musukuma ametoa tuhuma hizo kwa ujumbe wa sauti aliousambaza katika mitandao ya kijamii, huku akionesha kusikitishwa na hatua zilizochukuliwa na Kampuni ya GSM juzi Jumatatu (Februari 07).
Musukuma amesema Karia ameshindwa kuongoza soka la Tanzania na anapaswa kujiuzulu, kutokana na baadhi ya mambo kufanywa hadharani kwa makusudi na yeye kama kiongozi anayakalia kimya.
Mbali na tuhuma kwa kiongozi huyo, Musukuma amelaani vitendo vya baadhi ya waamuzi wanaochezesha michezo ya Ligi Kuu kwa kushindwa kusimamia sheria 17 za mchezo wa soka na kujikuta wakizionea baadhi ya timu ambazo zinajiandaa kwa gharama kubwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Kampuni ya GSM ilitangaza kuondoa udhamini wake kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es salaam kwa kigezo cha baadhi ya vipengele vya mkataba uliosainiwa Mwezi Novemba mwaka jana dhidi ya TFF havijafuatwa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Klabu zagawanyika GSM kujitoa udhamini.​

gsm pic

Dar es Salaam. Uamuzi wa Kampuni ya GSM kujiondoa katika udhamini mwenza wa Ligi Kuu Bara umepokewa kwa hisia tofauti na klabu mbalimbali huku Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) likikiri kuondoka kwa wadhamini hao.
Jana jioni, GSM kupitia kwa Ofisa Biashara Mkuu, Allan Chonjo ilisema kuwa wameamua kujiondoa kutokana na TFF pamoja na Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) kushindwa kutekeleza vipengele vya kimkataba wa miaka miwili ambao pande hizo mbili zilikubaliana.
“Haya hayajawa maamuzi rahisi kwa kampuni ya GSM kwani tunatambua zipo baadhi ya klabu za mpira zitaumizwa pamoja na wadau mbalimbali na hatua hii haikuwa dhamira yetu kufikia uamuzi huu mgumu,” alisema Chonjo.
“Upande wa klabu udhamini wa tutaendelea kuwa kwenye mkataba wetu kama kawaida bali tumejitoa upande huu wa ligi.”
Mbali na kujitoa katika udhamini wa ligi, mmiliki wa kampuni hiyo, Gharib Said naye amejiondoa kwenye kamati ya ushindi ya timu ya taifa ‘Taifa Stars’.
Muda mfupi baada ya GSM kutangaza kujitoa, TFF ilithibitisha kupokea barua ya uamuzi huo na kuahidi kuufanyia kazi.
“Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linathibitisha kuwa leo Februari 7, 2022 limepokea barua ya kuvunja mkataba wa mdhamini mwenza (co - sponsorship) wa Ligi Kuu ya NBC kutoka kampuni ya GSM.
“TFF inafanyia kazi barua hiyo na itatoa taarifa kwa wadau wa mpira wa miguu kuhusu suala hilo,” ilisema taarifa ya TFF.
Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, viongozi wa klabu za soka wameonyesha kutofautiana kwa kilichotokea.
Mwenyekiti wa Mtibwa Sugar, Nassor Abubakar alisema timu yao inaendeshwa kitaasisi na haitegemei sana wadhamini, hivyo kujitoa kwa GSM hakuwezi kuwayumbisha.
“Sina maana kwamba pesa za udhamini hazitusaidii, ila kuondoka kwa GSM hatuwezi kuyumba kwani ni tasisi inayojitegemea.” alisema Abubakar.
“Kuhusu nembo ya GMS kwenye jezi tunasubiri Bodi ya Ligi na TFF ambavyo ni vyombo makini kutupa taarifa rasmi na mwongozi wa nini tufanye baada ya hapo.”
Kwa upande wake, Ofisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwile alisema kitendo cha GMS kujitoa udhamini mwenza wa ligi ni maumivu makubwa kwao, kwani walitarajia pesa hizo kuwasaidia kiuendeshaji.
“Japokuwa bado hatujapokea taarifa rasmi, nimeona kupitia mitandao ya kijamii, inaumiza kwani tayari tulianza kuweka mabango uwanjani, nembo kwenye jezi na sijui sababu haswa za maamuzi yao ni nini,” alisema Masau.
Makamu Mwenyekiti wa Polisi Tanzania, Robert Munisi alisema wamepokea kwa masikitiko taarifa za GSM kujiondoa udhamini mwenza wa ligi, kwani tayari walishauingiza kwenye bajeti yao.
“Kuondoka kwao kumevuruga bajeti yetu. Mbaya zaidi ni katikati ya msimu, jambo ambalo litaumiza vichwa vyetu,” alisema Munisi.
Naye Katibu wa Kagera Sugar, Masoud Ally alisema kujiondoa kwa GSM kutayumbisha timu kiuchumi kwa kuwa tayari walishawasaidia.
Mkataba wa GSM na TFF ulisainiwa Novemba mwaka jana hivyo umedumu kwa siku 76.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Dawa ya waamuzi ligi kuu hii hapa.​

Marefa PIC

WADAU wa soka nchini wamependekeza dawa ya makosa yanayojirudia ya uamuzi kwenye Ligi Kuu Bara hasa mechi zinazohusisha Simba, Yanga na Azam.
Bao lililozua mjadala zaidi mpaka mitandaoni ni lile la Simba dhidi ya Mbeya Kwanza juzi, huku wengi wakidai lilikuwa la kuotea na waamuzi wasaidizi wakirushiwa lawama kushindwa kutekeleza wajibu.
Wachezaji, makocha, waamuzi na viongozi wa zamani wametoa maoni yaliyotaka kuwepo na umakini kwa waamuzi ikibidi kufutwa kabisa na kulipa faini wanapokosea.
Mchezaji wa zamani Simba, Yanga na Taifa Stars, Zamoyoni Mogela alisema wapo marefa wanaokosea kwa bahati mbaya lakini wengine kwa makusudi lengo likiwa kuwanufaisha watu wa upande mmoja na wanahitaji kupewa adhabu kali ili iwe fundisho.
Mshambuliaji wa zamani Yanga, Hery Morris alisema waamuzi wanaoyumba wafutwe kwenye ratiba kwa sababu wakifungiwa miezi mitatu halafu wakarudi wanakuwa hawajajirekebisha vizuri.
“Unamfungia miezi mitatu halafu kwa mfano kuna mtu kampa pesa nzuri ni ngumu kuumia kwa sababu anakaa nyumbani huku akiwa ameingiza kitu mfukoni. Wakifutwa kabisa haya makosa hayawezi kuwepo,” alisema Morris.
“Hili la waamuzi kwa namna moja ama nyingine linawafanya wachezaji wakicheza mechi za kimataifa wanashindwa kufanya vizuri kwa sababu wamezoea kubebwa.”
Kocha wa zamani Ruvu Shooting na Mbao, Abdulmutic Haji alisema: “Inabidi wafungiwe na kulipa faini kali kama ambazo wachezaji na makocha wanapewa, hii itapunguza haya ambayo yanaendelea kwa sasa.”
Katibu mkuu wa zamani wa TFF, Angetile Osiah anadhani suala la waamuzi kukosea lisiwe kama mazoea kwani kuna tiba sahihi ambayo inatakiwa kufanyika.
“Waamuzi hawawezi kubadilika na kuacha kufanya makosa kutokana na kuwafungia au wakishajadiliwa na Kamati ya Saa 72 ndio iwe basi au fundisho kwao, hiyo si njia sahihi,” alisema Osiah.
“Matukio ya wakati huu kwanza Kamati ya Waamuzi inatakiwa kutoa tamko, lakini tuwatengenezee njia sahihi waamuzi kuacha haya makosa, kwa mfano wenzetu Uingereza wana kundi lenye waamuzi 22 ambao 18 kati yao ni wale wazoefu na waliobaki wanapewa mafundisho kila wakati, lakini kuna waamuzi wa zamani nao hutoa mafundisho kila nyakati.”
Mchezaji wa zamani wa Azam FC, Philip Alando alisema waamuzi wengi wa soka nchini sio kama hawajui kuchezesha mpira, bali wanakosa umakini kutambua majukumu yao na kuna uzembe unawaingia ndani yake.
“Muda mwingine ambalo nimeliona kumekuwa na shida ya kuelewana kati ya mwamuzi wa kati na wasaidizi wake wa pembeni, ndio maana kuna shida nyingi zimekuwa zikitokea eneo hilo,” alisema Alando.
“Wakati mwingine nadhani watu wengi hawafuatilii soka katika mechi kama Geita Gold huko au Polisi Tanzania muda mwingine kumekuwa na makosa mengi kuliko mechi za Simba, Yanga na Azam zinazofuatiliwa na wengi.”
Mwamuzi wa zamani wa kimataifa, Omary Abdulkadir pia amezungumzia malalamiko ya mechi ya Simba dhidi ya Mbeya Kwanza aksiema: “Ni kweli aliotea (mchezaji wa Simba), lakini kabla hajacheza ule mpira ulichezwa na mpinzani wake hivyo akawa ameunawa.”
“Sheria inasema kama mtu wa mwisho aliyecheza mpira alikuwa kwenye nafasi ya kuotea basi ndiyo offside, hivyo kabla mpira haujamfikia Kagere tayari mchezaji wa Mbeya Kwanza alishaiua.”
Akizungumzia kuhusu malalamiko ya mara kwa mara alisema, “inategemea na uzoefu na presha ya mashabiki.”
Isihaka Shirikisho, mwamuzi mkongwe alisema: “Nafikiri ni uzoefu wengi siku hizi wanatoka ligi za chini na kupanda haraka haraka kwenye Ligi Kuu, hivyo wanakosa uzoefu na kukabiliana na presha ya ligi japo wapo baadhi wamefanikiwa lakini wengi wao wanafeli. Walipaswa kuchezesha ligi za chini muda mrefu, hadi wakifika levo ya Ligi Kuu wameiva.”
Mwenyekiti wa zamani wa Yanga, Imani Madega alisema Ligi Kuu inakidhi viwango vya kuweka teknolojia itakayoondoa utata na maswali kwa mashabiki huku akitaja matumizi ya VAR.
Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almas Kasongo alisema: “Mwamuzi ni mtu muhimu hivyo tuna kazi kubwa ya kufanya kuhakikisha tunatoa elimu ya kutosha, ufiti wao kuondoa changamoto zilizopo, waamuzi wanatakiwa kutumia elimu wanayoipata kwa kuwaelimisha wadau ambao ndio mashabiki wa soka, kinachoendelea sasa ni ukosekanaji wa elimu.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

MZEE WA UPUPU: Manungu wameenda sasa ni zamu ya saa nane mchana.​

Manungu P[IC

Mwaka 1976, Bob Marley aliachia albamu yake ya Rasta Man Vibration iliyokuwa na nyimbo kadhaa ukiwemo WAR (Vita) ambao uliakisi hotuba ya Mfalme Haile Selassie I wa Ethiopia kwenye Umoja wa Mataifa mwaka 1963.
Katika wimbo huo, Bob Marley aliimba kwamba dunia itaendelea kuwa na vita hadi pale usawa utakapokuwepo.
Until the philosophy that holds one race superior and another inferior (Ni hadi pale falsafa inayokumbatia tabaka moja kuwa juu na jingine kuwa chini). Is finally and permanently discredited and abandoned (Itakapofikia mwisho na kuachwa jumla).
That until there is no longer first class and second class citizens of any nation (Ni kwamba ni hadi pale patakapokuwa hakuna raia wa daraja la kwanza na daraja la pili wa nchi yoyote).
Hapa Bob Marley alitangaza vita duniani hadi mambo hayo na mengine mengi kama hayo yatapopatiwa ufumbuzi.
Kiasili maneno hayo yalisemwa na Haile Selassie I kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa, Oktoba 4, 1963, akihutubia kama mwenyekiti wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU). Hamishia maneno haya kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Kwa miaka na mikaka ligi yetu imekuwa na falsafa inayokumbatia tabaka moja juu na jingine chini. Tabaka la juu ni Simba na Yanga na tabaka la chini ni wengineo. Yaani ligi yetu imekuwa haina tofauti ni nchi yenye raia wa daraja la kwanza na daraja la pili. Simba na Yanga ni raia wa daraja kwa kwanza wengine ni daraja la pili.

KIVIPI?
Mambo mengi yanafanyika au yanatokea kwa faida ya Simba na Yanga yakiwakandamiza wengine. Kwa miaka na mikaka, Simba na Yanga hazikuwa zikilazimika kwenda kucheza kwenye baadhi ya viwanja eti kwa sababu zina mashabiki wengi.
Eti mashabiki wengi wanaweza kufanya fujo na kuwadhibiti itakuwa vigumu. Hivi ni shabiki gani angeweza kwenda kufanya fujo Mlandizi kwenye uwanja wa Ruvu Shooting ndani ya kambi ya jeshi?
Baada ya kilio cha muda mrefu cha hao raia wa daraja la kwanza, hao watu wanaokumbatiwa na falsafa na kuwaweka juu hatimaye wameenda kucheza huko. Wameanzia Manungu, wataenda Mlandizi, wangeenda Mwadui kama timu yao ingekuwepo...na kila sehemu kama hizo.
Kilichobaki sasa ni mechi za saa nane. Kama huo muda haufai, basi usifae kwa wote. Na kama unafaa basi na ufae kwa wote. Siyo wengine wakumbatiwe na falsafa kama raia wa daraja la kwanza na wengine daraja la pili.
Nilishawahi kuandika hapa, madhara ya mechi za saa nane mchana katika vita endelevu ni kubwa kuliko mchezo husika. Kucheza saa nane mchana kutamlazimu mchezaji kutumia nguvu nyingi zaidi ya kawaida kutoka akiba yake ya nguvu mwilini.
Matokeo yake atachoka sana siku zijazo, siyo katika mchezo husika pekee. Katika mbio za ubingwa zile timu ambazo hazikutani na hiyo adha wachezaji wake wanabaki na akiba ya nguvu na kuitumia mwishoni. Hii ni sayansi kwa hiyo kama imewezekana kwa raia hawa wa daraja kwanza kwenda Manungu na iwezekane pia kucheza saa nane au mechi za saa nane ziondolewe.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

HISIA ZANGU: Kutoka Bocande mpaka Mane, Tanzania ijipange.​

Mane PIC


NILIWAHI kwenda Barcelona mara kadhaa. Nilikutana na watu warefu, weusi, wakiwa kando za fukwe nzuri za Barcelona. Ni Wamachinga. Wanauza viatu kwa machale. Kwa sababu hawalipi kodi basi mara nyingi wanakuwa katika purukushani na Polisi.
Wanauza viatu, shanga, nguo na vitu kadhaa vinavyobebeka mkononi. Wanauza kwa Euro bei rahisi. Mara zote wanahamahama kutegemea tu ni wapi polisi wameweka kambi. Nilimuuliza rafiki yake mwenyeji hawa watu walikuwa wanatoka wapi. “Wengi wanatoka Senegal wengine wanatoka Mali”. Naam, inaonekana ni maisha yao. Wamezaliwa Ulaya kwa miaka mingi lakini pia wanaonekana wameizoea Ulaya. Umbali wa kutoka Dakar mpaka Ulaya ni kilomita 4,206. Wameachanishwa na bahari. Hapo hapo kumbuka kwamba umbali kutoka Mtwara hadi Kigoma zinakaribia kilomita 2000.

Juzi Senegal wamechukua ubingwa wa Afrika nikakumbuka mambo mengi. Nikawakumbuka wale Wamachinga wa Senegal waliopo Barcelona ambao pia niliwahi kuwakuta Milan. Nikakumbuka jinsi ambavyo wameizoea Ulaya. Nikakumbuka kwamba Senegal ni taifa la watu milioni 17 tu wakati Tanzania ina watu milioni 60. Kwanini Taifa la Senegal linatoa vizazi vya wachezaji wazuri? Nadhani inachangiwa pia na Jiografia yao. Kabla hatujajadili namna gani tunaweza kuwa Senegal kuna vitu inabidi tujikumbushe na kuumeza ukweli mchungu kama ulivyo.

Jiografia haitupi nafasi ya kuwa Senegal. Tunaweza hata kutambika lakini sidhani kama tunaweza kuwa Senegal. Wana watu wachache lakini wametapakaa Ulaya. Sisi tuna watu wengi lakini ambao hawajatapakaa Ulaya. Jiografia. Achilia mbali Jiografia lakini pia wenzetu walitawaliwa na Wafaransa. Wafaransa waliwapenda watu wao kupitia ile sera ambao iliwafanya watawaliwe wajione wao kama ni Wafaransa. Assimilation policy. Ni kama ambavyo Wacongo na watu wengine waliotawaliwa na Wafaransa wajione kuwa Wafaransa zaidi.

Najaribu kuwakumbuka mastaa wa Senegal. Tuanzie kwa Jules Bocande. Nenda google kamtazame vizuri Bocande. Niliwahi kumfuatilia nikiwa kijana mdogo., mwamba huyu ametamba na PSG, Metz, Nice, Lens na kwingineko. Kati ya mwaka 1984 mpaka mwaka 2002, Bocande alifunga mabao zaidi ya 100 katika Ligi Kuu ya Ufaransa. Kuna Mtanzania wa miaka hiyo amewahi kufanya hivyo? Bocande kwa sasa ni marehemu na alifia huko huko Ufaransa.

Ukiachana na Bocande jaribu kuangalia mastaa wengine. Watazame mastaa wenye asili tu ya Senegal ambao walicheza kwingine. Watazame Patrick Vieira na Patrice Evra ambao walizaliwa Senegal kabla ya kuvuka bahari na kwenda Ulaya. Nakukumbusha kwamba walikuwa Wasenegal asilia kama wale Wamachinga wa Barcelona. Na baada ya hapo kumbuka vizazi vyao vya kuanzia akina Khalilou Fadiga, El Hadji Diouf, Henry Camara, Tony Silva, Aliou Cisse na wengineo. Wote hawa wamezurura Ulaya wakiwa vijana wadogo. Yaani ni kama vile wamekwenda Ulaya katika umri wa Kelvin John.
Hawa ndio waliipeleka Senegal kombe la dunia kwa mara ya kwanza mwaka 2002. Na walipoipeleka walikwenda moja kwa moja katika robo fainali. Nadhani wakati huo idadi ya watu wao ilikuwa watu milioni 10. Sisi inawezekana tulikuwa watu milioni 40. Baada ya hapo kikaja kizazi cha kina Demba Ba, Demba Cisse, Mamadou Niang na wengineo ambao hawakufanya vizuri sana. Na sasa wana kizazi kinachoongozwa na Sadio Mane. Wote wanacheza Ulaya halafu ni katika klabu kubwa. Nadhani katika timu zote ambazo zimeshiriki Afcon mwaka huu, Senegal ndio taifa ambalo lilikuwa na wachezaji wengi wanaocheza katika Ligi Kubwa tatu za Ulaya. Matumaini ya Tanzania kuwa kama Senegal ni finyu. Pengine Jiografia inatubana lakini hata watu wake pia hawana kitu ya mafanikio. Kwa mfano, mataifa yenye idadi kubwa ya watu huku mchezo wa soka ukiwa ni namba moja inakuwa rahisi kwa watu wake kuondoka na kusaka mafanikio nje ya nchi kwa sababu mgao wa keki ya taifa unakuwa adimu.

Haishangazi kuona nchi kama Nigeria na Brazil zikiwa na wachezaji wengi Ulaya hata kama Jiografia inaonyesha hawapo karibu na Ulaya. Kisa? Raia wake wengi wanatoka kwenda kusaka mafanikio nje. Na kwa sababu soka ni mchezo namba moja katika mataifa hayo, inakuwa rahisi kuwapata vijana wenye kiu ambao wanakwenda nje kusaka maisha. Baadaye inakuwa faida kwa taifa.

Tanzania haipo hivyo. Tuna watu milioni 60 wakiwemo vijana wengi wenye vipaji vikubwa vya soka lakini hawana kiu. Mpaka leo sioni kiini ni nini. Labda ni sera zetu za ujamaa ambazo zimesababisha Watanzania wengi kuwa na uhakika wa kula na kunywa hata kama hawana pesa.

Matokeo yake taifa lenye watu milioni 60 limemtwisha kijana mmoja tui kutoka Mbagala anayeitwa Mbwana Samatta ndiye awe tegemeo la taifa. Na kwa sasa tumeanza safari nyingine ndefu ya kuanza kumtegemea kinda Kelvin John ambaye nyota yake imeanza kung’ara Genk. Hili ni tatizo la kimsingi.

Unapofikiria mafanikio ya Senegal huku wakiwa wametwaa Afcon kwa mara ya kwanza unapata ganzi pale ambapo unafahamu kwamba tuna safari ndefu isiyoonekana kuwafikia walipo. Na wanachofanya wao ni kitu kile kile ambacho kinafanywa na mataifa ya Mali, Burkina Faso, Guinea na wengineo.

Bahati mbaya pia tatizo hili la Kijiografia inawezekana sio la Tanzania pekee ingawa Tanzania ipo chini zaidi. huu ukanda wetu wenye Rwanda, Burundi, Kenya na Uganda pia unakabiliwa na matatizo haya haya ya Watanzania.

Rafiki zetu Burundi na Rwanda wametawaliwa na Wafaransa lakini nadhani Jiografia imewatenga. Waganda na Wakenya wana vipaji maridhawa na watu kama akina Victor Wanyama wameonyesha kwamba wanaweza kwenda mbali zaidi lakini nadhani kuna ukosefu wa kiu na mipango.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

KARIA, WAKUTANA NA BALOZI WA UTURUKI NCHINI.​

AVvXsEj5CtccjbrJhPaJcBtR4-lMcqJk5MUeqt0PHzGQaiwPGmetIpgDGeMmj7w861o2s6xbcCT-djamYOPllUPrgE0paVqaYAz__L7Pe892KXN24Qtc0oXMgP9nsNr1fYluAjd4RRQtdDMOOMqQ5AimnrgWxcrdPOPAfceWLvDWbUFmmJ0bkWN4Zu_PLeIi=w640-h602

RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia na Katibu Mkuu wake, Kidao Wilfred leo wamekutana na Balozi wa Uturuki hapa nchini Dk. Mehmet Gulluoglu ofisini kwake, Oysterbay, Dar es Salaam kuzungumzia juu ya ushirikiano katika maendeleo ya mchezo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Bodi ya Ligi Kuu Bara Yafungukia Hatma ya GSM.​

DtVHO_8WkAEfRlY.jpg

MWENYEKITI wa Bodi ya Ligi Kuu Bara, Steven Mnguto, ameibuka na kusema licha ya wadhamini wenza Kampuni ya GSM kutangaza kujiondoa katika udhamini lakini hakuna klabu yoyote iliyolipwa.
Kauli hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tangu GSM watangaze kujiondoa kudhamini klabu za ligi ambazo awali waliingia mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya Sh 2.1Bil.
Akizungumza na Championi Jumatano, Mnguto alisema kuwa, hilo suala wamepanga kulizungumza hivi karibuni
mara baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) watakapokutana.
Mnguto alisema kuwa, wanasubiria wanasheria wao walipitie suala hilo na mwisho wa siku watalitolea ufafanuzi
kwa undani.
“Kiukweli tangu tuliposaini mkataba na GSM nikiri klabu hazijapata chochote. Klabu zimeitangaza GSM kwa muda wa miezi mitatu sasa, kwa hiyo tunasubiri wanasheria walipitie suala hilo tujue tunafanyaje.
“Hata suala la zile nembo kwenye mabega sijui kama zinaweza kutolewa haraka lakini hata hilo litafanyiwa
kazi kisheria,” alisema Mnguto.
Naye Mkurugenzi wa Habari na Masoko wa TFF, Boniface Wambura, akizungumzia hilo alisema: “Sisi
baada ya kupata barua kutoka GSM, suala la mkataba ni Bodi ya Ligi na ni vema akatafutwa Mnguto lakini
kwa upande wa sisi TFF hatuwezi kuzungumzia kila jambo.
“Tayari tumetoa tamko letu jana (juzi) kuhusiana na hilo baada ya kupata barua GSM.” Juzi TFF ilitoa taarifa
kuwa, Februari 7, mwaka huu walipokea barua ya kuvunja mkataba wa udhamini mwenza wa Ligi Kuu Bara
ya NBC kutoka Kampuni ya GSM, hivyo Shirikisho hilo linafanyia kazi barua hiyo na litatoa taarifa kwa wadau.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

BODI YA WADHAMINI TFF YAKUTANA BUNGENI DODOMA.​

AVvXsEiCo7IlPPXy-X6zjy5pF7Oqka4bVT8WaKWYYBDao0jTF2Skgp7I9huprEKfrffUBJdCv0QKi0rHNlUgGn3H8q6J-ctsCBugHoVkz16RTI_e45fKqvbaOouuVbKhZRQBSh4kSsamDejcvXlwwNPQJtNidRWZ-qzXt1KlgKqs-0S8365hzxIh1nqPIP-j=w640-h640

MWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mohamed Abdulaziz akimkabidhi fulana ya shirikisho hilo, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson kwenye Ofisi yake iliyopo Bungeni Jijini Dodoma leo.
Dk. Tulia pia ni Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini TFF.
AVvXsEjWdbOzZ6CPwhwu_y_E0kE0A1hUc2Yk0Fdp7d0cspz6juHpm0Pw7xGtPvDhUg5xSGpiArNgiPcDmYKg7WTBGHhnLMmQvjpC7QItFCw4CGYUKG_1jjblpUUDVIRg3rncn4-8pDsyVVQUSZhKoS01i3y6M01peH9VZ86s3XnUyMVf11DOlO9VREqN1GKq=w640-h640

Dk. Tulia Ackson amekutana na Wajumbe wenzake Bodi ya Wadhamini ya TFF, mbali na Mwenyekiti Mohamed Abdulaziz (wa kwanza kushoto), wengine ni Mjumbe wa Bodi Said Meckysadick (wa pili kutoka kulia) na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji TFF, Mohamed Aden ambao walimtembele Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kaseja: Silogi mtu ni uwezo tu.​

kaseja pic

MIAKA 20 kwenye Ligi Kuu Bara, Juma Kaseja anajua siri nyingi za soka la Bongo na utamdanganya nini kuhusu mpira wa nchi hii? Huyu ni gwiji.
Tanzania One, Mikono Mia, mfano wa kuigwa, kipenzi cha wengi ni kati ya sifa nyingi ambazo amekuwa akipambwa nazo supastaa huyu wa soka nchini. Kiufupi, Juma K. Juma si mtu wa mchezo mchezo
Amekipiga kwa kiwango cha juu katika klabu kubwa nchini za Simba na Yanga, pia akizitumikia Moro United, Mbeya City, Kagera Sugar na sasa KMC huku pia akijenga heshima kubwa kwenye timu ya taifa, Taifa Stars, ambako alifahamika kwa jina la Tanzania One.
Ukibahatika kukaa na supastaa huyu, utagundua ni mcha Mungu, mcheshi, mkarimu, anajali utu kuliko vitu, nidhamu na bidii ni silaha ya mafanikio yake.
Mwanaspoti ilifunga safari kutoka Tabata Relini hadi Bunju kwenye kambi ya KMC ambako timu hiyo ya Manispaa ya Kinondoni imejichimbia na kubahatika kuongea na staa huyo ili kufahamu mengi ndani ya maisha yake ya soka.
Ukisikia maneno ya watu nje na kumtazama mwonekano wake, unaweza kudhani ni mtu wa majivuno lakini kumbe sivyo hata kidogo na ndio maana wahenga walisema usihukumu kitabu kwa kuangalia kava, kisome ndani.
Kama haujui ndivyo ninavyokujuza Kaseja, ni moja ya wachezaji wanaojua nini wanatakiwa kukifanya na kwa wakati gani ili kuepuka kukwazana na nyota wenzake pamoja na viongozi.
Kaseja anasema, jina kubwa alilonalo mpaka sasa, sio fimbo ya kujivunia kuwachapia wenzake bali anaamini alipo hivi sasa ni mapenzi ya Mungu.
“Mimi kwanza sipendi kumdharau na kumchukia mtu japokuwa mimi wananidharau na kunichukia lakini wanaofanya hivi ni kwa sababu hawanijui mimi Juma nikoje na wengine wananunua chuki bila sababu,” anasema.

SILOGI UWEZO TU

Mkongwe huyo aliyecheza kwa mafanikio makubwa na ameweka wazi changamoto alizokutana nazo huku imani za kishirikina akitaja kuwa ndio ishu iliyomsumbua zaidi na kusema lakini haikumuumiza sana kwani hakuwahi kufanya vitu alivyokuwa anahusishwa navyo.
Anasema alikuwa akihusishwa mara kwa mara kwenye imani hizo huku akitaja Mungu kuwa ndio alikuwa kimbilio lake kwenye kazi yake hiyo japo lawama zilikuwa nyingi kwake hakuzipa nafasi majibu yake yalikuwa kwa maandishi na sio mdomo.
“Unaweza kufanya kitu na watu wasione, na mimi nilikuwa naandika ujumbe kwenye fulana yake kwamba Kaseja atabaki kuwa Kaseja kwa hiyo zile jumbe zilikuwa za watu ili kuheshimu wenzao kutokana na juhudi wanazoonyesha kwa kuachana na kashfa ambazo hazikuwa na maana,” anasisitiza.
Kaseja anasema alikuwa anavaa nguo nyeupe zenye ujumbe ndani ya jezi akifanya vizuri mpira unapoisha anavua jezi anabaki na ujumbe wake uliokuwa ukisomeka kuwa yeye atabaki kuwa yeye miaka yote kutokana na juhudi zake na sio imani za kishirikina wanazomtwisha.
“Mpira wetu wa Tanzania una changamoto nyingi kwa upande wangu nimeweza kupambana nazo na kufanikiwa kufika hapa nilipo kama ningekuwa mtu wa kuka tamaa nadhani ningekuwa nimeshastaafu soka, halafu ishu ya ushirikina ingekuwa na maana basi mimi ningedaka hadi Barcelona,” anasema.

DALADALA FRESH TU

Kwa upande wa wachezaji wa Tanzania wakitaka kuonyesha kama wamefanikiwa basi ni kumiliki dinga, lakini unaambiwa kwa upande wa Kaseja yeye anaona kujionyesha ni ulimbukeni akisisitiza yeye ni sawa na binadamu wengine hivyo hana sababu za kujitofautisha na ndio maana usafiri wake mkubwa ni daladala.
“Nimeanza kumiliki gari 2002 lakini sioni maajabu japo nimekuwa nikichukuliwa tofauti na wachezaji wengi kwa kuniona natumia usafiri wa umma. Kwani mimi nina utofauti gani na wengine hadi nijiweke mtu wa juu zaidi yao,” anasema, Kaseja ambaye anamiliki nyumba kadhaa na magari kadhaa amba-yo mwenyewe hataki kuyazungumzia akisema hayo ni maisha yake binafsi sana.
Anakiri kuchukizwa na watu wanamuita na kumuona staa wakati yeye hana ustaa wowote na ni binadamu wa kawaida kama ambavyo binadamu wengine wanaishi.
“Mimi sipendi kabisa, sijui ustaa ndio nini na unanisaidia nini naishi maisha ya kawaida kama ambavyo wengine wavyoishi sio kwamba gari sina hapana, sina tabia za kupanda bodaboda wala mwendokasi hapana naamua tu na napenda sana kusema ukweli,” anasema Kaseja.
Kaseja anasema, licha ya watu kumshangaa na wengine kumuona amefulia yeye anaona ni sawa tu kwa kuwa maisha yake anayeyajua ni Mungu pekee lakini mwanadamu ni ngumu.

LAKI 2 MORO UTD

Anasema ulikuwa usajili wake wa kwanza katika maisha yake ya mpira, ambapo aliipokea pesa hiyo akiwa na majonzi kutokana na msiba wa baba yake mzazi.
Anasema wakati wanaondoka kumbe nyuma jamaa wa Moro United walipishana wakawafuata mpaka Magomeni, kwenye moja ya baa maeneo hayo wakati huo inaitwa Zaragoza ambayo sasa Moro United.
“Nilisaini laki 2 mwaka 2000 Novemba ikiwa daraja la kwanza, nakumbuka kaka alivyowaambia nimefiwa wakaniongezea Sh50,000 nakumbuka hiyo pesa yote nilimpa mama yangu baada ya kwenda msibani kumzika baba,” anasema Kaseja.