Simba Sports Club Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mabosi Simba waapa sasa ni mwendo wa kugawa dozi.​

simba pic

SIMBA haina matokeo mazuri katika mechi zake tatu za Ligi Kuu Bara ingawa wikiendi iliyopita walirejesha ubabe wao nyumbani wakiipasua Dar City na kudhihirisha bado jamaa wana utamu wao.
Kama umeshtuka, Simba imeyumba mechi tatu za ligi ugenini ambako ndani ya dakika 270 hizo wamevuna pointi moja pekee iliyotokana na sare dhidi ya Mtibwa Sugar huku wakipoteza dhidi ya Mbeya City kisha Kagera Sugar.
Hata hivyo, mechi hizo sasa zitasimama kwa muda na Simba itarejea uwanja wake wa heshima wa Mkapa na katika ligi mechi yao ya mwisho kucheza hapo ni walipoichapa Azam FC siku ya kwanza ya mwaka 2022 mabao 2-1. Na wakati ikijiandaa kurudi kwa Mkapa, mashabiki wanatamba wakiwaambia wapinzani wao wajao kwamba wataona, hatoki mtu.
Walianza kwa kutuma salamu kwa kuangusha kipigo kizito kwa Dar City cha mabao 6-0 kwenye Kombe la Shirikisho la Azam.
Simba sasa itaendelea kudumu nyumbani hapo kwa Mkapa na watu wakae sawa kwani jamaa wana dakika 450 za kurudisha ubora baada ya ratiba yao kufumuliwa kidogo.
Simba watawakaribisha wachovu Tanzania Prisons kesho Alhamisi mchezo ambao awali ulipangwa upigwe Februari 6 na hapo kutakuwa na vita ya wekundu hao kutakiwa kuendelea kufuta machozi ya wanachama na mashabiki wao walioumizwa na sare na vipigo viwili.
Wakimaliza hapo watarudi katika maandalizi yao kisha kurejea uwanja huohuo dhidi ya Mbeya Kwanza Februari 6 na badaa ya hapo watahamia Kimataifa wakiwakaribisha Asec Mimosas ya Ivory Coast katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Baada ya hapo Simba itasafiri kwenda ugenini wakiwafuata Union Sportive Gendarmerie Nationale (USGN) ya Niger katika mchezo wa pili wa hatua ya makundi kisha kurejea tena nyumbani kuikaribisha Biashara United mchezo wa Ligi Kuu
Kwa upande wa viongozi wa klabu hiyo, umesema sasa wamejipanga kupata pointi tatu kila mchezo uliombele yao.
“Tumebakiza michezo miwili kabla ya kumaliza mechi za mzunguko wa kwanza. Tumejipanga kupata pointi zote sita kwenye mechi hizo na kuanza mzunguko wa pili kwa nguvu mpya,” alisema Mwenyekiti wa klabu hiyo, Murtaza Mangungu.
Alisema wamepata matokeo ya kuumiza katika mechi zao tatu mfululizo, lakini haiwezi kuwarudisha nyuma, Simba itaendelea kupambana kuhakikisha inafanya vyema mechi zijazo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kakolanya afunguka kila kitu ishu ya Simba.​

beno pic

LICHA ya kutopata nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza, kipa Beno Kakolanya wa Simba amesema suala hilo halimfanyi kuwa chini ya kiwango akipewa mechi ya kucheza.
Kakolanya ameendelea kuwa kipa namba mbili nyuma ya Aishi Manula ingawa anapopata nafasi ya kucheza hufanya viuzri.
Akizungumza na Mwanaspoti, Kakolanya alisema akiwa nje ya uwanja huwa anajifunza kutoka Manula huku akifuata kwa ukaribu maelekezo ya kocha.
“Kitu kingine nikipewa mechi huwa najiamini sinaga hofu yoyote ile kwamba sichezi basi kiwango changu kimeshuka hicho kitu hakipo kichwani kwangu, siku zote akili yangu inaniambia nipo vile vile na najitahidi kuwa bora zaidi kupitia mazoezi tunayofanya,” alisema Kakolanya.
Kuhusu kucheza bila kuruhusu bao, alisema hilo ndio jambo la muhimu ambalo kocha wao wa makipa anawasisitiza kila mmoja amalize mechi kwa namna hiyo.
“Ni kitu ambacho tunafanya kazi mazoezi na kocha wetu anapenda tusiwe tunaruhusu mabao, sisi wote huwa tunatamani tumalize kwa staili hiyo na kubwa zaidi tuongee sana na mabeki wetu na itakuwa rahisi sana kwetu kutoka bila kuruhusu bao,” alisema Kakolanya.
Kakolanya msimu huu amecheza mechi mbili, Kombe la Mapinduzi mechi moja dhidi ya Selem View uliomalizika wakishinda 2-0 baada ya hapo aliumia mazoezini na kukaa nje ya uwanja kwa muda hivyo Manula kurejea golini.
Kipa huyo alirejea uwanjani aliendelea kukaa benchi kwenye mchezo wa Ligi dhidi ya Mbeya City, Mtibwa Sugar, Kagera Sugar na kurejea mechi ya kombe la Shirikisho Azam dhidi ya Dar City ambapo alikaa golini na kupata ushindi 6-0 na Dar City.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Onyango, Morrison Wekwa Sokoni Simba.​

bm-pic-data.jpg

MAMBO ni magumu kwa sasa ndani ya Simba kutokana na mwendo wa kusuasua hasa kwenye matokeo waliyopata kwenye mechi tatu mfululizo ugenini jambo lililofanya mikataba ya mastaa wengi kuwekwa kando.
Habari kutoka chanzo cha kuaminika ndani ya Simba zimeeleza kuwa kwa sasa hakuna mchezaji hata mmoja
ambaye ameitwa kufanya mazungumzo kuhusu kuongeza mikataba yao ili waweze kuhudumu ndani ya kikosi
hicho.
Miongoni mwa mastaa ambao mikataba yao inatarajiwa kufika ukingoni pale msimu wa 2021/22
utakapomeguka ni pamoja na Bernard Morrison, Hassan Dilunga, Ibrahim Ame, Joash Onyango na Said Ndemla.
Hii ni sawa na Simba kuwaweka sokoni nyota wao ambao wamebakiza mkataba wa chini miezi sita kwani kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka la Kimataifa ‘Fifa’ mchezaji anapobakiza muda huo kwenye kandarasi yake anakuwa huru kufanya mazungumzo na timu nyingine yoyote na wakikubaliana anaweza kusaini mkataba wa awali.
Baada ya taarifa kueleza kwamba hakuna mpango wowote ambao unaendelea kwa sasa, Championi Jumatano lilimtafuta Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez ili aweze kuzungumzia suala hilo simu yake haikupokelewa.
Alipotafutwa Mwenyekiti wa Simba, Murtanza Mangungu azungumzie ishu hiyo pia hakupatikana.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pablo Aanza na Kagere, Mugalu.​

KAGERE-1.jpg

SHAUKU ya kupata mabao ya Kocha Mkuu wa Simba raia wa Hispania, Pablo Franco, imemfanya aanze kuitengeneza safu ya ushambuliaji kati ya Meddie Kagere na Chris Mugalu, ili waweze kucheza kwa pamoja katika mechi yao dhidi ya Prisons itayopigwa leo.
Simba ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara, ikiwa na pointi 25, iliyozikusanya katika michezo 13, ambapo imeshinda saba, sare nne na kufungwa miwili.
Chanzo chetu kutoka Simba, kimeliambia Championi Jumatano kwamba, pamoja na timu hiyo kufuzu hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports, dhidi ya Dar City kwa ushindi mnono wa mabao 6-0, ambapo Kagere alifunga mabao mawili na Mugalu moja, tayari kocha Pablo ameonekana kuwanoa Kagere na Mugalu ili wacheze pamoja dhidi ya Prisons.
“Kelele za mashabiki wa Simba juu ya straika wetu kutofunga kwenye ligi, nadhani tayari kocha Pablo ameamua kuzinyamazisha, ambapo katika mazoezi ya kwanza tu, ameonekana kuwahimiza Kagere na Mugalu kucheza kwa ushirikiano ili atakapowapatia nafasi ya kuanza pamoja basi waweze kufunga mabao mengi.
“Kocha Pablo nadhani anafanya hivyo baada ya kuona furaha ya mashabiki zetu, baada ya kuvuna ushindi mnene dhidi ya Dar City, hivyo ameamua kuhakikisha hasira za kutopata bao anazipeleka katika mchezo wetu wa Ijumaa hii dhidi ya Prisons,” kilisema chanzo hicho.
Kwa upande wake Pablo alisema: “Safu ya ushambuliaji bado imekuwa na umakini mdogo katika eneo la ufungaji kwa sababu bado imekuwa ikikosa nafasi nyingi za kufunga mabao kadiri muda wa mchezo unavyokwenda kitu ambacho naamini siyo kizuri kwa upande wetu kutokana na changamoto kubwa ambayo ipo mbele yetu.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mwenye namba yake Simba karudi.​

namba pic

HII ni habari njema kwa mashabiki wa Simba, lakini huenda ikawa mbaya kwa wachezaji wanaocheza nafasi moja na kiungo Mganda, Taddeo Lwanga ambaye amerejea kutoka kwenye majeraha ya muda mrefu.
Kiungo huyo mkabaji ameanza kufanya mazoezi mepesi akiwa amesaliwa na asilimia chache kabla ya kujumuika na wenzake kikosini.
Lwanga aliumia goti mwanzoni mwa msimu na ilisemekana angekaa nje ya uwanja kwa msimu mzima, lakini hali imeonekana kuwa tofauti.
Wakati anarudi Simba kwa sasa timu hiyo kiungo Sadio Kanoute yupo kwenye programu maalumu sambamba na Kibu Denis ambao juzi walikuwa kwenye mazoezi mengine ya peke yao.
Mwanaspoti lilimshuhudia kiungo huyo akiwa sambamba na kocha wa viungo, Daniel De Castro ambaye alikuwa anamsimamia kuhakikisha anarejea kwenye makali yake.
Lwanga hakumuangusha kocha huyo kwani alikuwa anafanya kila zoezi la viungo ambalo alipewa na alionyesha utimamu wa mwili aliokuwa nao tangu mazoezi yanaanza mpaka yanamalizika.
Baadhi ya mashabiki waliokuwa katika Uwanja wa Mo Simba Arena walionekana kufurahishwa na urejeo wake baada ya kumuona akifanya mazoezi bila shida yoyote.
Kurejea kwa Lwanga kunafanya eneo la kiungo mkabaji Simba kuongezewa ushindani na kuwafanya wanaocheza nafasi hiyo yaani Jonas Mkude, Kanoute na Mzamiru Yassin kukaa mguu sawa. Pia kurejea kwake kumrahisishia kazi kocha Pablo Franco namna ya kuwatumia wachezaji hao.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Banda Aandaliwa Kuwamaliza Waivory Coast.​

242581065_198100482410637_9038489158892754942_n.jpg

SIMBA imeweka wazi kuwa mara baada ya kiungo mshambuliaji wao, Peter Banda kurejea nchini akitokea Cameroon alipokuwa na kibarua cha kuiwakilisha Malawi kwenye mashindano ya Afcon, moja kwa moja atajiunga na programu za maandalizi ya michezo ijayo hususani mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast.
Katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Simba imepangwa kwenye Kundi D pamoja na timu za RS Berkane ya Morocco, USGN ya Niger na ASEC Mimosas.
Mchezo wa kwanza wa Simba katika hatua ya makundi utakuwa Jumapili ya Februari 13 dhidi ya ASEC Mimosas, mwaka huu wakianzia nyumbani kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Mkuu wa Maudhui wa Simba, Ally Shatry, alisema: “Ni kweli tunamtarajia kiungo mshambuliaji wetu Banda kujiunga na kikosi baada ya kumaliza majukumu yake ya timu ya taifa
ambapo mpaka kufikia mazoezi ya jana (juzi), Jumatano jioni alikuwa hajaripoti.
“Tunatarajia atajiunga na kikosi mara baada ya mchezo wetu dhidi ya Tanzania Prisons, ambapo atakuwa sehemu ya programu za kujiandaa na michezo yetu miwili inayofuata hususani ule wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosas.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

SIMBA YAMSIMAMISHA MORRISON KWA UTOVU WA NIDHAMU.​

KLABU ya Simba imemsimamisha winga wake Mghana, Bernard Morrison kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu ikiwemo kutoka kambini bila ruhusa.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Gadiel Michael: Sina Wasiwasi na Kukaa Benchi.​

gADIEL-MICHAEL.jpeg

LICHA ya kushindwa kupata nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza cha Simba, beki wa kushoto wa timu hiyo, Gadiel Michael, amesema kuwa hana presha kwani itafika wakati wake wa kucheza.
Gadiel amekuwa akishindwa kupata nafasi ya kuanza mara kwa mara ndani ya Simba kutokana na uwepo wa Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ ambaye wanacheza wote katika eneo la beki wa kushoto.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Gadiel alisema kuwa licha ya kushindwa kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza kwenye michezo ya ligi kuu, lakini anaamini kuwa wakati wake wa kucheza upo, hivyo hana presha ya kusugua benchi ndani ya kikosi hicho.
“Sina presha kwa kuwa sipati nafasi ya kucheza mara kwa mara kwenye kikosi cha kwanza kwani michezo ipo mingi ya kutosha na naamini kuwa nitapata nafasi ya kucheza huko mbeleni.
“Kila kitu ni mipango ya mwalimu hivyo nikipata nafasi ya kucheza huwa nashukuru lakini nikikosa nafasi ya kuanza basi huwa naamini kuwa itapatikana nafasi nyingine,” alisema beki huyo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Chama Akabidhiwa Zigo La Lawama.​

chama.jpg

KIUNGO Mzambia, Clatous Chama baada ya kurejea Simba, kocha mkuu wa kikosi hicho, Pablo Franco, amempa jukumu la kupiga penalti, faulo na kona, vitu ambavyo ndani ya timu hiyo msimu huu ni kama zigo la lawama hasa penalti.
Pablo raia wa Hispania, hivi karibuni alikasirishwa na baadhi ya wachezaji wake kushindwa kutumia vizuri kufunga penalti katika michezo ya Ligi Kuu Bara.
Simba tangu kuanza kwa msimu huu, imepiga penalti tano katika Ligi Bara pekee, kati ya hizo, moja imekuwa bao lililofungwa na Rally Bwalya dhidi ya Polisi Tanzania.
Tangu Pablo ameanza kuinoa Simba Novemba, mwaka jana, ameshuhudia vijana wake wakikosa penalti tatu dhidi ya Ruvu Shooting, Azam na Mbeya City. Penalti hizo zilipigwa na Erasto Nyoni, Bwalya na Chris Mugalu. Kabla ya hapo, John Bocco alikosa dhidi ya Biashara United.
Chama katika mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports uliopigwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa
Mkapa, Dar dhidi ya Dar City, alifunga bao kwa faulo nje kidogo ya 18.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Spoti Xtra kutoka ndani ya Benchi la Ufundi la Simba, kiungo huyo alianza majukumu hayo tangu mchezo wake wa kwanza wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar uliomalizika kwa suluhu. Mtoa taarifa huyo alisema, Chama ametakiwa kupiga faulo, kona na penalti kila anapokuwa uwanjani baada ya Pablo
kuvutiwa na aina ya upigaji wake.
“Pablo amevutiwa na Chama aina ya upigaji wake wa kona, penalti na faulo, hivyo kocha amemchagua kiungo huyo
kuendelea na majukumu hayo kila anapokuwa uwanjani,” alisema mtoa taarifa huyo.
Spoti Xtra lilithibitisha hilo katika michezo mitatu ambayo amecheza kiungo huyo dhidi ya Mtibwa Sugar, Kagera Sugar na Dar City ambapo alionekana kupiga faulo na kona. Katika faulo alizopiga, moja pekee alifanikiwa kufunga, ilikuwa dhidi ya Dar City
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pablo aitaja mbinu ya kuwaacha Yanga mbio za ubingwa Bara.​

pablo-1.jpg

PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba ameweka wazi kuwa mbinu pekee ya timu hiyo kutwaa ubingwa msimu huu na kuwafunika wapinzani wao Yanga ni kushinda mechi ambazo watacheza.
Simba ni mabingwa watetezi, wanapambana kufikia malengo yao wakiwa wamejichimbia nafasi ya pili na pointi 28 huku wakiwa wamepoteza mechi mbili kati ya 14.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Pablo alisema kuwa hana mashaka na wachezaji wa kikosi cha Simba kwa namna wanavyocheza licha ya kushindwa kupata matokeo mazuri kwenye mechi walicheza ugenini hivi karibuni.
“Bado malengo yetu ni kutwaa ubingwa kwani inawezekana na hilo lipo kwetu sisi. Jambo pekee ambalo litatupa nafasi ya kutwaa ubingwa ni kushinda mechi zetu ambazo tutacheza na hilo lipo wazi.
“Ninafurahishwa na kazi ambayo inafanywa na wachezaji uwanjani licha ya kushindwa kutumia nafasi ambazo tunazipata, hilo ni jambo ambalo tunapaswa kulifanyia kazi,” alisema Pablo.
Mchezo ujao wa Simba kwenye ligi ni dhidi ya Mbeya Kwanza unatarajiwa kuchezwa leo Jumapili.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pablo: Nitawashangaza Msimu Huu.​

mugaluchris07_244271520_937896000095714_1815605476186806358_n.jpg

KOCHA Mkuu wa Simba SC, Pablo Franco, amesema atawashangaza wengi msimu huu kwani wana imani ya kutwaa makombe yote ambayo wanayatetea licha ya kuwa katika mwendo wa kusuasua ndani ya Ligi Kuu Bara.
Simba inatetea taji la ligi na kwenye msimamo ipo nafasi ya pili ikikusanya pointi 28. Pia inatetea taji la Kombe la
Shirikisho la Azam Sports ikiwa tayari imetinga hatua ya 16 bora.
Kutokana na mwendo wao huo, wengi wamekuwa wakiitoa Simba kwenye mbio za ubingwa, huku Yanga inayoongoza msimamo kwa sasa ikiwa na pointi 35 kabla ya mechi ya jana, ikipewa nafasi kubwa zaidi ya kuwa mabingwa.
SIMBA-17.jpg

kizungumza na Spoti Xtra, Pablo alisema: “Tunakwenda kwa mwendo huu ambao haujawa mzuri, ni kweli kwani
mpira sio hisabati, ni namna ambavyo tunafanya uwanjani, hakuna tatizo, malengo yetu ni
kuchukua ubingwa wa ligi na Kombe la Shirikisho.
“Hili niliweka wazi tangu mwanzo, ligi bado inaendelea na Kombe la Shirikisho tumefika hatua nzuri, kikubwa ni kuwa na subira na wachezaji ninaamini watafanya vizuri na kuwashangaza.” Leo Jumapili, Simba inatarajiwa kucheza dhidi ya Mbeya Kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Mkapa, Dar kuanzia saa 1:00 usiku.
Hii itakuwa ni mara kwanza kwa timu hizi kukutana kwenye ligi kuu ambapo Simba inashika nafasi ya pili kwenye
msimamo huku Mbeya Kwanza inayoshiriki ligi kuu kwa mara ya kwanza, ikiwa ya 12 kabla ya
mechi za jana.
Pablo leo Jumapili, anatarajiwa kumaliza adhabu yake ya kukosa mechi tatu baada ya kufungiwa hivi karibuni ambapo tayari amezikosa mbili dhidi ya Dar City na Prisons.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kocha Prisons: Penalti ya Simba ni halali.​

simba.jpg

SHABAN Kazumba, Kocha Msaidizi wa Tanzania Prisons, amesema kuwa bao la penalti ambayo walipata Simba juzi ni halali kwa kuwa ilitolewa na mwamuzi kutokana na makosa ambayo walifanya.
Bao hilo lilifungwa na Meddie Kagere na lilionekana kuwa na utata kutokana na wachezaji wa Prisons kumfuata mwamuzi kulalamika juu ya penalti hiyo.
Kazumba aliliambia Championi Jumamosi kuwa: “Simba wamepata penalti, kwangu penati ni sehemu ya makosa, siwezi kusema kwamba tumefungwa kwa bao la penalty, hapana, siwezi kusema kwamba namlaumu mwamuzi.
“Kwangu naona liko sahihi lakini kidogo naona ilikuwa ni kwa wepesi kwetu, lakini tumefungwa, tunakubali matokeo, tumepoteza pointi tatu na timu yangu ilicheza mpira ule unaopendwa na Kocha Mkuu, Patrick Odhiambo ambaye anapenda kuona timu inacheza mpira mzuri.
“Tulikosa nafasi tatu za kufunga mbele ya Simba na tulikuwa tunajua kwamba tunacheza na mabingwa, Simba alistahili na mchezo wa mpira ni mgumu sana.”
Prisons ipo nafasi ya 16 ikiwa na pointi 11 huku Simba ikiwa nafasi ya pili na pointi 28, zote zimecheza mechi 14.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mghana wa Azam Ampa Somo Morrison.​

273129757_1293546667789867_7183809858415196594_n.jpg

KUTOKANA na winga wa Simba, Bernard Morrison kupewa adhabu ya utovu wa nidhamu, Mghana mwenzake wa Azam, Daniel Amoah, amempa somo.
Wawili hao ambao ni marafiki na wametoka kijiji kimoja, wamekuwa wakikutana mara kwa mara na kushauriana. Morrison ameadhibiwa na Simba kwa kosa la kinidhamu la kutoroka kambini na alipoambiwa asirudi mpaka atakapoongea na mtendaji mkuu pia alikaidi. Winga huyu wa Simba ambaye aliwahi kuichezea Yanga, pia alikuwa na matukio ya namna hiyo akiwa Yanga.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Amoah amesema: “Huwa naongea na Morrison mambo mengi sana na tunashauriana, namuombea aweze kupatana na timu yake na kuweza kurejea kambini. “Ni mchezaji mzuri na hata kwa hili la kusimamishwa tumeongea, nina imani watakuwa sawa,” alisema Amoah.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mastraika Simba Wachimbwa Mkwara Mzito.​

SIMBA-1.jpg


KOCHA Msaidizi wa Simba, Seleman Matola, amefunguka kuwa benchi la ufundi la klabu hiyo halijaridhishwa na mwenendo wa ufungaji mabao ndani ya kikosi chao na tayari wamekaa na mastraika wa kikosi hicho kuangalia namna ya kumaliza tatizo hilo.
Simba msimu huu wamekuwa na changamoto kubwa kwenye safu ya ushambuliaji ya timu hiyo ambapo kabla ya mchezo wa jana walikuwa wamefanikiwa kufunga mabao 15 tu, katika michezo yao 14 ya mzunguko wa kwanza waliyokuwa wamecheza.
Kwenye Ligi Kuu Bara mpaka sasa kwa Simba ni Meddie Kagere pekee ambaye amefanikiwa kuandikisha mabao msimu huu akiwa tayari amefunga mabao matano, huku John Bocco na Chris Mugalu wao wakiendelea kuwa na ukame wa mabao.
Akizungumzia changamoto ya safu yao ya ushambuliaji msimu huu, kocha Matola alisema: “Kama benchi la ufundi tunakiri kuwa ni kweli tumekuwa na changamoto katika safu yetu ya ushambuliaji msimu huu, tatizo ambalo kama benchi la ufundi tunalifanyia kazi ili kuhakikisha linamalizika na tunafunga mabao.
“Tayari tumekaa na washambuliaji wetu na kuangalia wapi tunakosea ili kurekebisha, pia kuwaweka wazi kuwa hatuhitaji kuona hali hii inaendelea.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Sakho, Bwalya waundiwa zengwe CAF.​

sakho.jpg

BAADA ya kukitazama kikosi cha Simba, Kocha Mkuu wa Asec Mimosas ya nchini Ivory Coast, Julien Chevalier, amewataja wachezaji Pape Ousmane Sakho na Rally Bwalya kuwa ni wa kuchungwa kutokana na ubora walionao, hivyo wanajiandaa kuwadhibiti kwa vyovyote vile wasilete madhara kwao.
Asec Mimosas wanatarajiwa kuwa wageni wa Simba katika mchezo wa kwanza wa Kundi D kwenye Kombe la Shirikisho Afrika utakaochezwa Februari 13, mwaka huu, Uwanja wa Mkapa, Dar. Katika kundi hilo, timu zingine zilizopo ni RS Berkane ya Morocco na Union Sportive Gerndamarie ya nchini Niger.
Akizungumzia juu ya maandalizi yao kuelekea mchezo huo, kocha huyo amesema wanapokwenda kucheza dhidi ya Simba, Sakho na Bwalya ni wachezaji wa kuchungwa kutokana na kuwa na madhara makubwa kwa wapinzani, pia wana uwezo mzuri wa kumiliki mpira.
“Simba nimewafuatilia katika baadhi ya michezo yao, wana timu nzuri na wachezaji wengi wazuri, siwezi kuwataja wote, lakini kuna kiungo wa kati Bwalya na winga Sakho, ni wachezaji wazuri.
“Ni wachezaji ambao hata sisi tunatakiwa kuwachunga kutokana na uwezo wao kwa jinsi ambavyo nimeitazama Simba, wanaweza kukokota mpira na kumiliki pia, tutafanya kile kilichobora kupata matokeo mazuri dhidi yao,” alisema kocha huyo.
Naye Meneja wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, ameliambia Spoti Xtra kwamba: “Tunajua hauwezi kuwa mchezo rahisi kwetu kwa sababu tunacheza nyumbani, hii ni michuano mikubwa na inashirikisha timu bora, hivyo ni wazi tunatarajia mchezo mgumu na tumejiandaa vizuri.
“Kocha amepata muda wa kuwasoma wapinzani wetu na malengo yetu makubwa ni kutumia faida ya kucheza kwenye uwanja wa nyumbani kupata matokeo mazuri.
“Tunataka kufuzu robo fainali na hesabu zetu ni kushinda mechi zote za nyumbani ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufikia malengo.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Simba Wanatamba! Kiko Wapi Sasa, Bado 5 tu.​

SIMBA-2.jpg


SIMBA jumapili wamepambana na kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya Kwanza katika mchezo mgumu ulioonekana ungemalizika kwa suluhu kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar, jana Jumapili. Hiyo ni siku moja tu tangu vijana wengine wa Mbeya, Mbeya City, wawabane vinara Yanga kwa suluhu pia.
Matokeo hayo yanaifanya Simba, ifikishe pointi 31 katika nafasi ya pili, ikiwa imebakiza pointi tano tu iwafikie Yanga wenye pointi 36 kileleni lakini Simba wakiwa wamecheza mchezo mmoja zaidi.
Kiungo Clatous Chama ‘Mwamba wa Lusaka’ ndiye aliyeleta tofauti kwenye mchezo huo, baada ya kufunga bao pekee dakika ya 80, ambalo lilizua utata
mkubwa kufuatia straika Meddie Kagere kuonekana kuotea lakini beki wa Mbeya Kwanza aliugusa mpira kabla haujamfikia Kagere na mwamuzi msaidizi akatafsiri alivunja offside hiyo.
Wachezaji wa Mbeya Kwanza walimzonga mwamuzi msaidizi wakilalamika kuwa hilo siyo bao halali. Msonjo akapewa kadi ya njano kutokana na tukio hilo dk ya 80.
Hii ni mechi ya pili Simba wanapata bao linaloonekana kuwa ni la utata, katika mchezo uliopita ambao pia walishinda 1-0 dhidi ya Prisons, walipata penalti iliyoonekana tata iliyofungwa na Kagere. Kwenye mchezo huo wa jana, Simba walianza na washambuliaji wawili ambao ni John Bocco na Meddie Kagere huku Clatous Chama akianzia benchi.
Dakika ya 1 tu, Bocco alifanya jaribio ambalo halikuleta matunda na dakika ya 8 na 13, Pape Ousmane Sakho alipiga mashuti yaliyolenga lango huku Rally Bwalya akiwa ni mpishi eneo la kati. Simba katika mchezo wa jana, ilitengeneza nafasi lakini ilikuwa haina ubunifu katika umaliziaji, huku wakipiga mashuti 16 nje ya lango hadi kufikia dakika ya 79.
Kwa Mbeya Kwanza mpishi wao mkuu alikuwa ni Salum Chuku ambaye amekuwa na majukumu ya kupiga kona na mipira ya kurusha. Sadio Kanoute alifanya jaribio kwa kichwa dakika ya 17 lililookolewa na kipa Hamad Kadedi ambaye alikuwa salama ndani ya dakika 15 za mwanzo chini ya beki Rolland Msonjo.
Dakika ya 13, Habib Kiyombo nusura aipatie Mbeya Kwanza bao alipofanya jaribio lililookolewa na kipa Aishi Manula. Dakika ya 28, Salum Chuku naye alifanya jaribio lakini likaokolewa na Manula.
Lakini kukosa utulivu kwa nyota wa Simba kuliwafanya washindwe kupata bao ndani ya dakika 40 za mwanzo, pongezi kubwa kwa Hamadi Kadedi kipa wa Mbeya Kwanza pamoja na Rolland Msonjo.
Hadi dakika 45 za kwanza zinamalizika, ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisomeka Simba 0-0 Mbeya Kwanza. Mashabiki wa Simba walianza kulalamika mapema walipoona orodha ya wachezaji wa mchezo ‘line up’, baada ya kuona Mwamba wa Lusaka, Clatous Chama ameanzia benchi.
Mashabiki katika ukurasa wa Instagram wa Simba, wengi walianza kumlalamikia kocha wakisema haikustahili kumuweka Chama benchi. Jana Selemani Matola ndiye aliyekuwa kocha kufuatia Mhispania, Pablo Franco kuendelea kutumikia kifungo chake cha mechi tatu.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Simba ikitengeneza mashambulizi mengi, mapema tu Simba ilimtoa Jonas Mkude na nafasi yake ikachukuliwa na Chama. John Bocco naye alitoka akaingia Chris Mugalu. Dakika ya 54, Kagere atajilaumu mwenyewe kwa kukosa nafasi ya wazi kufunga.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pablo: Sasa Ubingwa Upo Wazi.​

SIMBA-3.jpg

KOCHA Mkuu wa Simba, Pablo Franco raia wa Hispania, amefunguka kuwa anaamini ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu hauna mwenyewe, licha ya wapinzani wao Yanga kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi tano.
Pablo ametoa kauli hiyo baada ya juzi Jumapili Simba kufanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya Kwanza na kufikisha pointi 31 ikiwa ni tofauti ya pointi tano dhidi ya vinara wa ligi hiyo, Yanga wenye pointi 36.
Akizungumza na Spoti Xtra, Pablo alisema kupata matokeo hayo ya ushindi kumerudisha hali ya kuendelea kufanya vizuri katika mechi za ligi licha ya kukiri kuwa bado suala la ubingwa mpaka sasa halina mwenyewe kutokana
na ushindani ulivyo.
“Hatukuwa kwenye kipindi kizuri, lakini tumeanza kurejea taratibu kwa kupunguza pengo la pointi dhidi ya wapinzani wetu, kwetu ni jambo zuri kwa kuwa tumerejea katika malengo yetu japokuwa bado tunatakiwa kupambana zaidi kwa kuhakikisha timu inapata matokeo makubwa.
“Kuhusu suala la ubingwa ndiyo malengo yetu makubwa ingawa bado kwa sasa upo wazi kwa timu zote zinaweza kufanya maajabu kwani timu zina mechi nyingi, lakini kitu ambacho tunaendelea kukiangalia zaidi upande wetu ni kuhakikisha tunaendelea kupata matokeo makubwa ili kufika tunapotaka,” alisema Pablo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Morrison Agoma Kuandika Maelezo kwa Barbara.​

273129757_1293546667789867_7183809858415196594_n.jpg

HABARI kutoka kwa watu wa karibu wa nyota Benard Morrison wamesema kuwa winga huyo amegoma kuandika maelezo kwenda kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba kuhusu tuhuma za kinidhamu anazotuhumiwa na klabu hiyo.
Morrison raia wa Ghana anadai kuwa yeye hana kosa hawezi kuandika maelezo yoyote wakati huo wazee wa klabu ya Simba SC wameutaka uongozi wa klabu hiyo kuachana na Morrison haraka iwezekanavyo.
Aidha, Klabu ya Simba imethibitisha kutopokea barua ya maelezo kutoka kwa Morrison ambaye wamemsimamisha kwa makosa ya utovu wa nidhamu, Februari 4, 2022. ambapo klabu ya Simba ilitoa taarifa ya kumsimamisha mchezaji huyo.
Kwa mujibu wa Ofisa wa idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ahmed Ally amesema klabu bado haijapokea maelezo kutoka kwa mchezaji wao Bernard Morrison. Mchezaji huyo anapaswa kuandika barua ya maelezo kwenda kwa mtendaji mkuu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mkataba wa Morrison Yanga kufuru, Simba waitana.​

morrison pic

Mkataba wa Morrison ndani ya Simba umesaliwa muda usiozidi miezi mitatu na mabosi wa klabu hiyo wamemsimamisha kwa kudaiwa kutoroka kambini kwa kuruka ukuta, pamoja na kufanya vituko vingine kambini.
Lakini, habari za uhakika zinasema Mghana huyo aliyeondoka kwa kuwakera wanayanga anarejea tena kunako klabu hiyo iliyomleta nchini, baada ya matajiri wa klabu hiyo kumwekea mzigo wa maana ili kunasa saini yake.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya Yanga zinasema kuwa, vigogo wawili wakubwa wa klabu hiyo wameungana kuanzisha vita ya kumbeba Morrison kwa kumwekea mezani dau zito na tayari jamaa amewajibu;”sina tatizo kurejea Yanga.” Mwanaspoti linajua kwamba Simba wamenasa mchongo huo na wikiendi hii walikutana Jijini Dar es Salaam kujadili ishu hiyo pamoja na mwenendo wa klabu yao.
Morrison katika mkataba wake na Simba umebakiza siku 90 tu kumalizika huku hatua ya mazungumzo ya mkataba mpya yakikwama muda mrefu, na sasa hatua mbaya ni kwamba ana kesi ya utovu wa nidhamu na Wekundu hao.
Itakumbukwa akiwa na Yanga, Morrison aliondoka kwa utata mkubwa kisha kesi yake kufika mpaka Mahakama ya michezo (CAS) na mchezaji huyo kuwabwaga mabosi wa Yanga.
Matajiri hao wawili ambao Mwanaspoti ina majina yao wamekubaliana kwamba wapambane kumchukua wakitaka ufundi wake bila kujali vurugu zake.
Habari ambazo Mwanaspoti inazifahamu na kuwa na uhakika nazo kwa asilimia 100 ni kwamba Morrison ameahidiwa ofa nzito ya dola 100,000 (Sh230 Milioni) kama ada ya usajili tu ambapo matajiri hao kila mmoja akichanga dola 50,000 (Sh 115 milioni).
Ofa hiyo imeushtua upande wa mchezaji huyo ambapo tayari wameshajibu kwamba wamekubaliana na wanasubiri kuona kipi Simba wataamua katika mashtaka yao. Mbali na dau hilo mshahara wake ameahidiwa atachukua dola 8,000 (Sh18.4 Milioni) sawa na kiasi ambacho analipwa kiungo wa Simba Clatous Chama sasa aliporejea Msimbazi.
Hata hivyo, umetokea mgawanyiko kwa baadhi ya mabosi wa Yanga kuhofia kiungo huyo anaweza kuwavuruga tena wakipendekeza hata akirudishwa asipewe mkataba mwepesi ili umfunge na kumtuliza. Huku wengine wakitaka atolewe kwa mkopo arejee Yanga kama ikifika hatua ya makundi ya Afrika msimu ujao.
“Tunamtaka Morrison kweli na kuna watu tumeshawapa kazi hiyo na inakwenda vizuri,ukiachana na tabia zake hakuna klabu ambayo itakataa kuwa na mchezaji mwenye kipaji kama kile,” alisema tajiri huyo ambaye hakutaka jina lake liwe gazetini.
“Hebu fikiria msimu ujao unakuwa na Mayele (Fiston) pale juu kulia una Moloko (Jesus) huku kushoto una Morrison na chini ya Mayele una Feisal (Salum) utakuwa na timu ya aina gani?Kuna wenzetu wanataka apewe mkataba mgumu kidogo wengine wanaogopa lakini tutakubaliana tu.”