Yanga Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Manara Atamba: Msimu Huu ni Shangwe tu kwa Yanga.​

MANARA-1-1.jpg

WAKATI Simba SC wakihaha kurejea katika njia ya furaha na kusaka namna ya kutetea ubingwa wa Tanzania Bara kwa mara ya tano mfululizo, kwa majirani zao Young Africans wameapa msimu huu ‘PATACHIMBIKA’.
Simba SC imekua na matokeo mabaya katika michezo mitatu iliyopita, ikipoteza dhidi ya Mbeya City na Kagera Sugar kwa kufungwa 1-0, huku ikitoka sare ya 0-0 dhidi ya Mtibwa Sugar.
Akizungumza mapema leo Alhamisl (Januari 27), Msemaji wa Young Africans Haji Manara amesema msimu huu ni wa furaha kwa Wanachama na Mashabiki wa klabu hiyo.
Amesema Wachezaji wanatambua mchango wa Wanachama na Mashabiki wa Young Africans, hivyo jukumu lao ni kupambana na kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara kwa mara ya kwanza baada ya miaka mitano kupita.
“Wachezaji tumekua tukiwahimiza wapambane kwa ajili ya Mashabiki na Wanachama, hawa watu wamesubiri ubingwa kwa miaka minne, tumewaambia Wachezaji wasahau kuhusu Posho kwa sababu hili suala lipo kwenye mikataba yao, jambo la kwanza ni wao kupambana kwanza na mengine yatakuja yenyewe.”
Young Africans inaongoza msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kufikisha alama 35, baada ya kucheza michezo 13, ikiwaacha Simba SC kwa tofauti ya alama 10.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mastaa 10 Yanga Kuikosa Mbao FC.​

YANGA-9-1.jpg

KIKOSI cha Yanga SC kitashuka tena uwanjani Jumamosi ya Januari 29, 2022 kucheza na klabu ya Mbao FC ya jijini Mwanza katika mchezo wa kombe la shirikisho la Azam.
Awali, mchezo baina ya Yanga SC Vs Mbao FC ulipangwa kuchezwa katika uwanja wa michezo wa Benjamin W. Mkapa uliopo manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, mchezo baina ya Yanga SC na Mbao FC, sasa umepelekwa jijini Mwanza katika dimba la CCM Kirumba.
Sababu ya kuhamishwa kwa mchezo huo kutoka uwanja wa michezo wa Benjamin Mkapa ni kile kilichodaiwa uwanja huo kuwa kwenye matumizi mengine siku ya Jumamosi.

Kuwakosa wachezaji 10.

Kuelekea mchezo huo wa kombe la shirikisho la Azam, Yanga SC inatarajia kuwakosa wachezaji wake 10 kwa sababu mbalimbali.
Wachezaji wawili wa Kikongo Djuma Shabani na Yannick Bangala Litombo wenyewe watakosekana katika mchezo huo kwa kuwa wapo katika majukumu ya timu ya taifa huko Bahrain.
Mchezaji mwingine wa Kikongo katika kikosi cha Yanga SC, Herithier Ebenezer Makambo na yeye atakosekana katika mchezo huo baada ya kuomba ruhusa kwenda nchini kwao Kongo DR kushughulikia matatizo ya kifamilia.
Wachezaji Feisal Salum Abdallah, Yusuf Athuman, Yacouba Sogne, Kibwana Shomari, Abdallah Shaibu ‘ Ninja’ , na Denis Nkane wapo kwenye uwezekano mkubwa wa kuukosa mchezo dhidi ya Mbao FC kwa sababu ya kusumbuliwa na majeraha.
Mchezaji wa 10 ambaye ataukosa mchezo baina ya Yanga SC Vs Mbao FC ni Mganda Khalid Aucho ambaye anatumikia adhabu ya kadi tatu za njano.
Ikumbukwe kuwa, mlinda mlango namba moja wa Yanga SC, Djigui Diarra amekosekana katika kikosi cha Yanga SC kwa zaidi ya wiki 3 kwa kuwepo kwenye majukumu ya kuitumikia timu yake ya taifa ya Mali katika fainali za kombe la mataifa ya Afrika zinazoendelea huko nchini Cameroon.

Wafurahia Simba kupoteana.

Wadau na wachezaji wa Yanga SC pamoja na mashabiki wao wamefurahishwa na mwenendo mbovu wa klabu ya Simba SC. Simba SC imekusanya alama moja pekee katika michezo mitatu iliyocheza ya hivi karibuni.
Kwa matokeo hayo, Simba SC imeachwa pointi 10 na Yanga SC, kitendo ambacho kinawapa Wanayanga nafasi kubwa ya kuupata ubingwa wa ligi kuu ya soka Tanzania bara.

Wachezaji wa zamani wa Yanga SC na kismati cha kuifunga Simba SC.
Katika michezo miwili ya hivi karibuni ambayo Simba SC imepoteza, magoli ya wapinzani wa Simba SC yalifungwa na wachezaji wa zamani wa Yanga SC.
Katika mchezo dhidi ya Mbeya City, goli pekee la mchezo huo lilifungwa na mchezaji wa zamani wa Yanga SC, Paul Nonga. Na katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar Vs Simba SC, bao pekee la mchezo lilifungwa na mchezaji wa zamani wa Yanga SC, Mganda Hamis Kiiza Diego.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Nabi Ampa Saido Mchongo … Soma Hapa.​

yangasc_270073665_288327629934712_2729646942819960104_n2.jpg

SASA uhakika kiungo mshambuliaji wa Yanga Saidi Ntibazonkiza ‘Saido’ raia wa Burundi, ataendelea kuichezea timu
hiyo katika msimu ujao, hii ni baada ya Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi kutaka aongezewe mkataba.
Mrundi huyo ni kati ya wachezaji ambao mikataba yao inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Wengine baadhi ni Dickson Job, Kibwana Shomari, Bakari Mwamnyeto, Deus Kaseke na Farid Mussa.
Kwa siku za karibuni, kiungo huyo ameonekana kurejea kwa kasi akionesha kiwango bora na kumfanya aingie kikosi cha kwanza cha timu hiyo. Mmoja wa mabosi wa timu hiyo, ameliambia Spoti Xtra kuwa, Kocha Nabi ameridhishwa na kiwango kikubwa ambacho amekionesha Saido kwa siku za karibuni.
Bosi huyo alisema Nabi mara baada ya mchezo wa Polisi Tanzania, haraka aliwaambia viongozi wa timu hiyo, wamuongezee mkataba wa kuendelea kukipiga hapo.
Aliongeza kuwa, kocha huyo bado anaendelea kuwatazama baadhi ya wachezaji wengine ambao mikataba yao inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu kwa ajili ya kupendekeza usajili wao.
“Kocha Nabi ndiye anayependekeza usajili wote wa timu, hivyo kama yeye akipendekeza mchezaji fulani asajiliwe, basi hakutakuwa na pingamizi lolote kwa uongozi. “Hivyo Saido jina lake limependekezwa na Nabi ambaye amewaomba viongozi aongezewe mkataba wa kuendelea kuichezea Yanga.
“Ni suala la muda tu, hivyo muda wowote atapewa mkataba mpya mara baada ya kukaa meza moja na viongozi kwa ajili ya kufanya mazungumzo,” alisema bosi huyo.
Akizungumzia hilo, Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela, alisema: “Kila kitu kinachohusiana na usajili tumemuachia kocha, hivyo bado hatujakutana na kocha kujadiliana usajili.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Ubingwa Wanukia Jangwani, Takwimu Hizi Hapa.​

yanga-5.jpeg

Klabu ya Yanga imekuwa na nafasi kubwa sana msimu huu wa kuweza kutwaa ubingwa wa NBC Premier League hali hii imeonekana baada ya klabu hiyo kuanza vizuri sana toka mwanzoni mwa msimu huu hadi sasa licha ya kuanza vizuri laikini pia wakiwa na wachezaji bora sana katika kikosi chao.
Klabu ya Yanga Sc hadi sasa imecheza michezo 13 na kuvuna alama 35 na kupotenza alama 4 tu katika michezo yake ambapo wapinzani wao Simba Sc wakiwa wamecheza michezo 13 na kuvuna alama 25 huku wakiwa wamepoteza alama 14 kwa takwimu hizi Yanga wamekuwa na nafasi kubwa sana hadi sasa kuweza kutwaa ubingwa msimu huu wakiwa wanamuombea mpinzani wao aendelee kufanya vibaya katika mechi zake zijazo.
Klabu ya yanga Sc kwa sasa ndio timu pekee inayoonekana kufanya vizuri sana ukilinganisha na timu zingine katika NBC premier League ambapo imekuwa na wachezaji wazuri sana na wakuelewana katika kila idara sio beki sio viungo sio washambuliaji wote wwameonekana kupambana sana wakiwa uwanjani na kuweza kusaka alama tatu kwa pamoja ambapo hali hii inawafanya Yanga kuonekana kuwa bora sana katika msimu huu wa 2021- 2022.
Kunukia kwa ubingwa Yanga ni pamoja na wapinzani wao kuonekana kufanya vibaya sana katika michezo yao huku wakiendelea kuwa na matokeo mabaya ambapo wameweza kupoteza mchezo wao dhidi ya Kagera Sugar bao 1-0 huko mkoani Kagera katika uwanja wa Kaitaba.
Simba Sc wamepoteza mchezo huo lakini huku wakiwa wamepata nafasi nyingigi sana na kushindwa kuzitumia hasa kipindi cha kwanza ambapo hawakuweza kufungana, lakini pia Simba Sc bado ina nafasi ya kushindania taji ilo kwa sababu bado wana kikosi kizuri na wanaweza kufanya madiliko katika michezo yao ijayo.
Kwa sasa mashabiki wa Simba Sc wamekuwa ni watu ambo wamekuwa kwenye huzuni kubwa sana juu ya hali wanayoipitia kwa sasa wamekuwa ni watu wa kujiuliza maswali mengi sana juu ya timu yao huku wakiwa wanakosa majibu, mashabiki hao ambao hawajazoea hii hali kwa misimu minne mfululizo wakiwa ni watu wakufurahi mda wote huku wapinzao wao wakiwa na huzuni wakati je mwaka huu ni zamu yao Simba Sc au muda bado yote yanawezekana.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Yanga Waibomoa Simba SC, Mchongo Mzima Uko Hapa.​

YANGA-7-1.jpg

Simba Sc na Yanga ndio wababe na mabingwa wa nchi hii kwa miaka mingi sana kwenye michuano mbalimbali ikiwa ni pamoja na ligi kuu Tanzania bara, Mapinduzi Cup, Kagame Cup, ngao ya jamii pamoja na Azam Sports Federation Cup.
Moja ya vitu vya msingi vinavyopelekea Simba Sc na Yanga kushinda mataji haya ni pamoja na uwezo mkubwa wa fedha zinazotumika kuendesha timu zao, uwepo wa viongozi wazuri kwenye ngazi za juu za timu, uwepo wa watu bora kwenye benchi la ufundi la timu (makocha) pamoja na nguvu kubwa kutoka kwa mashabiki.
Ndani ya msimu miwili iliyopita klabu ya Yanga wameonekana kufanya jitihada kubwa ya kuhakikisha wanaweza mizizi ya ufalme wao kwenye ligi ili kuondoa ukubwa wa Simba Sc ambao wamekua wakitamba kwa kushinda mataji ligi kuu Tanzania bara kwa misimu minne mfululizo.
Yanga wametengeneza mazingira ya kuwavuta baadhi ya viongozi waliokua wanafanya kazi Simba Sc na kuwapa mikataba kwenye timu yao, mfano wa viongozi hao ni pamoja na Senzo Mbatha, Haji Sunday Manara pamoja na Milton Nienov.

GSM Na Jeuri Ya Fedha Ndani Ya Klabu ya Yanga
Klabu ya Yanga kwa sasa wameingia kwenye timu bora na kubwa nchini Tanzania kwa kua na uwezo wa kufanya mambo yao kwa wakati kwa kutegemea sana fedha ambazo zimewekwa na kampuni ya GSM ambao ndio wadhamini wakuu wa klabu ya Yanga.
Yanga wanafanya usajili wa wachezaji wakubwa, viongozi wakubwa na makocha wakubwa kutokana na hali nzuri ya kiuchumi iliyopo ndani ya klabu hiyo.
GSM mpaka sasa tunaweza kusema kwamba wamefanikiwa kubomoa kwa kiasi fulani ngome ya Simba Sc ambayo ilikua imara zaidi ndani ya misimu kadhaa iliyopita. GSM wamefanya mambo makubwa kwa kutoa mikataba minono kwa wachezaji wa klabu ya Yanga ambao wanaonyesha kiwango bora kwa sasa lakini pia wameongeza nguvu kubwa kwenye benchi la ufundi la klabu hiyo.

Nguvu Ya GSM Yahusishwa Kwenye Dili La Senzo Mbatha Kutoka Simba Sc na Kujiunga Na Yanga
Katika matukio makubwa ambayo yamewahi kutokea kwenye vilabu vya Simba Sc na Yanga miaka ya hivi karibuni ni pamoja na uhamisho wa mchezaji Bernard Morrison kutoka Yanga na kujiunga na Simba Sc, lakini pia uhamisho wa Senzo Mbatha kutoka Simba Sc na kuhamia Yanga ilikua ni habari ngumu sana.
Senzo ambaye kwa sasa anafanya kazi kama mtendaji mkuu wa klabu ya Yanga anatajwa kua mtu bora sana kwenye masuala ya maendeleo ya mpira. Senzo ameongeza kitu kikubwa sana ndani ya klabu ya Yanga kwa sasa na hakika GSM walifanya kitu bora sana kuhakikisha kwamba mtu huyu anashawishika na dili lao na kukubali kuachana na Simba Sc.
Klabu ya Simba Sc walifanya jitihada za kupata mtu sahihi wa kubadili nafasi ya Senzo na walifanikiwa kumpata Barbara Gonzalez ambaye pia anafanya kazi nzuri ndani ya kikosi cha Simba Sc. Barbara Gonzalez amefanikiwa kuziba vizuri pengo la Senzo licha ya kwamba kuna vitu anavikosa kutokana na mahitaji ya kazi yake katika klabu ya Simba Sc tofauti na wakati ule ambao klabu ilikua chini ya Senzo Mbatha.

Manara Awashangaza Simba Sc Baada Ya Kukubali Kujiunga na Yanga
Uhamisho wa Manara kutoka katika klabu ya Simba Sc kwenda kujiunga na Yanga lilikua ni jambo la kushangaza sana lakini uhalisia umeendelea kudumu na kuona kwamba Manara ni mfanyakazi wa klabu ya Yanga na kwa kinywa chake mwenyewe alithibitisha kwamba amedumu kwenye klabu ya Simba Sc kutoka na mazingira ya kazi lakini moyo wake wote ulikua unapenda kuwashabikia Yanga Sc.
Manara alipokua anajiunga na klabu ya Yanga alitoa taarifa kwamba moja kati ya sababu zilizofanya akubaliane na ofa ya Yanga ni pamoja na kiasi kikubwa cha pesa ambazo aliwekewa mezani na GSM ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya mkataba wake na matajiri hao. GSM amefanya ushawishi mkubwa sana kupata saini ya Manara na katika hili wanastahili pongezi nyingi sana.
Klabu ya Simba Sc pia wamefanya jitihada za kupata mtu sahihi ambaye anaweza kuongoza kitengo cha habari kwa umakini ambapo walifikia makubaliano ya kuingia mkataba na Ahmed Ally siku chache zilizopita. Ahmed ni mtu sahihi kwa Simba Sc lakini hawezi kufikia uwezo wa Manara katika suala la ushawishi kwa mashabiki wa klabu hiyo kama ilivyokua kwa Manara wakati alipokua anafanya kazi Simba Sc.

Milton Nienov Afuata Nyayo Za Manara Na Senzo Mbatha
Klabu ya Yanga bado wameendelea na utaratibu wa kuchukua watu muhimu kutoka Simba Sc ambapo siku chache zilizopita wamefanya utambulisho wa aliyekua kocha wa magolikipa wa klabu ya Simba Sc maarufu kwa majina ya Milton Nienov.
Milton Nienov anaenda kuongeza nguvu kwenye benchi la ufundi la klabu ya Yanga na hii inaonyesha wazi kwamba Yanga wamedhamiria kushinda taji la ligi msimu huu. Eng. Hersi ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya GSM anaendelea kutegeneza mazingira mazuri kwa Yanga kuweza kushinda taji la ligi msimu huu ili kuondoa ubabe wa Simba Sc ambao wameshinda taji la ligi kwa misimu minne mfululizo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Wafungaji Wanaoongoza kwa Mabao Ligi Kuu Mpaka Sasa.​

yangasc_271892792_662952828229685_5039591577653457978_n.jpg

Dalili za ubingwa zinanukia mitaa ya Jangwani ambapo mpaka sasa klabu hiyo imekua imara sana karibu maeneo yao yote ya yaani kuanzia eneo la ulinzi hadi eneo la ushambuliaji ambalo linaongozwa na mshambuliaji hatari Fiston Mayele raia ya Kongo.
Katika kuhakikisha kwamba tunalinda kumbukumbu na takwimu za wachezaji wa klabu hii bora msimu huu, chanzo cha kuaminika cha takwimu za wachezaji kimetoa orodha ya wachezaji wenye magoli mengi ndani ya kikosi cha Yanga baada ya timu hiyo kucheza jumla ya michezo 13 ya NBC Premier League.
Kwa mujibu wa chanzo hicho ni kwamba mshambuliaji tegemezi wa klabu ya Yanga kwa sasa Fiston Mayele anaongoza katika orodha baada ya kufunga magoli 6 kwenye michezo 6 ya NBC Premier League msimu huu.
Mayele licha kuongoza katika orodha ya wafungaji bora ndani ya kikosi cha Yanga lakini pia nyota huyu anashikilia nafasi pili kwenye orodha ya wafungaji bora ndani ya NBC Premier League ambapo kwa sasa mfungaji nambari moja ni R. Lusajo wa Namungo Fc.
Viungo washambuliaji wa klabu ya Yanga Feisal Salum na Saido Ntibazonkiza wanashikilia nafasi ya pili katika orodha ya wachezaji wenye magoli mengi ndani ya klabu ya Yanga baada ya kufunga magoli manne kwenye michezo 13 ambayo Yanga wamecheza mpaka sasa.
Saido na Feisal ndio wanaofanya kazi kumtengenezea Fiston Mayele nafasi za kufunga magoli lakini pia wanafanya jitihada za wao wenyewe kufunga magoli mengi kadri iwezekanavyo ili angalau kuwasogeza Yanga kwenye nafasi nzuri ya kutwaa taji la ligi msimu.
Yanga wamekua bora sana msimu huu na hii inaonyeshwa na namna ambavyo washambuliaji wa timi hii wanavyopambana kuhakikisha kwamba wanavuna alama tatu katika kila mchezo wanaocheza.
Takwimu hizi zinaonyesha wazi kwamba washambuliaji watatu wa klabu ya Yanga yaani Mayele, Feisal na Saido wamehusika kwenye magoli 14 ya kufunga wakiwa na kikosi cha Yanga msimu huu ambao ni M
magoli mengi kuliko safu za washambuliaji wa timi nyingine zinazoshiriki ligi kuu msimu huu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kocha wa Yanga Avunja Ukimya Kuhusu Diarra.​

diarra.jpg

KOCHA wa Makipa wa Klabu ya Yanga, Milton Nienov ameweka wazi kuwa michuano ya AFCON 2021 inayoendelea kutimua vumbi huko nchini Cameroon inaweza kuwa na athari kubwa kwa Djigui Diarra. Nyota ambaye amepata wakati mgumu kwenye kupata nafasi ya kucheza mpaka timu hiyo inaondolewa katika mashindano hayo hatua ya 16 bora.
Licha ya kuwa Mlinda mlango namba moja wa Yanga, Diarra ameonekana kukumbwa na wakati mgumu akiwa na timu take ya taifa. Ambapo muda mwingi amekuwa akiwekwa benchi pasipo kupata nafasi ya kucheza. Jambo ambalo limemuibua kocha mpya wa makipa wa klabu ya Yanga, Milton Nienov.
Ambapo Nienov amesema kuwa hali aliyokumbana nayo Diarra kwenye michuano ya AFCON 2021 ni hatarishi kwenye safari yake ya mpira wa miguu. Kwani anaamini kuwa kuwekwa benchi kwa nyota huyo kutampunguzia ufanisi kwenye utendaji kazi wake mpaka atakapokuja kurejea tena.
Kauli ya Milton Nienov imekuja mara baada ya kuzungumza na kunukuliwa katika tovuti ya Global Publishers Januari 25, 2021 akikiri kuwa Diarra ni mlinda mlango bora kwenye ligi kuu ya NBC. Huku akikiri kuwa analitambua hilo toka akiwa kama kocha wa Makipa wa Simba.
“Nilikuwa nikimtazama Diarra wakati nikiwa na Simba, naweza kusema huyu ni miongoni mwa makipa bora zaidi ndani ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa sasa na hili linathibitishwa na kuitwa kwake kwenye kikosi cha timu ya Taifa kubwa kama Mali,” alisema Nienov.
Milton aliongeza kuwa Diarra kukosa namba akiwa na timu yake ya taifa si jambo jema. Kwani jambo hilo linahatarisha ubora wa mchezaji huyo kwa kuwa anahitaji kucheza ndiyo aendelee kuwa kwenye ubora wake japokuwa hawawezi kuthibitisha moja kwa moja kuwa atarejea akiwa na kiwango cha chini. Hivyo basi wanasubiri arejee klabuni kwanza.
“Najua hajapata nafasi ya kucheza kutokana ushindani mkubwa wa namba anaokutana nao kwenye kikosi hicho na kwa upande wetu hilo sio jambo jema. Tunatamani kuona anacheza kwa sababu mara zote mchezaji anakuwa bora zaidi kadiri anavyopata nafasi ya kucheza. Kukaa benchi kunaweza hatarisha kiwango chake japokuwa hatuwezi kuthibitisha hilo kwa sasa mpaka atakaporejea,” alisema Nienov
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Nabi: Sitaki Kusikia Mchezaji wa Yanga Akizungumzia Simba.​

nabi-pic-data.jpg

KOCHA Mkuu wa Kikosi cha Yanga, Mohamed Nabi amesema amewapiga marufuku wachezaji na benchi la ufundi la timu hiyo kuzungumzia matokeo mabovu ya mahasimu wao Simba Sc ambayo wamekuwa wakiyapata katika mechi zao za hivi karibuni na badala yake wajikite katika michezo yao na kuhakikisha wanashinda.
“Nimewaambia wachezaji sitaki kusikia hata wanazungumza ishu za Simba kwani matokeo yao hayatuhusu na nimewataka wazingitie na kufikiria zaidi mechi zetu zinazotukabili.
“Nimewaambia kabisa nikimkuta mchezaji yeyote anafanya hivyo au mtu yeyote katika benchi langu la ufundi akiijadili Simba au timu nyingine juu ya matokeo yao nitawapa adhabu zilizopo kwenye miongozo yao ya kazi.
“Yanga tuna mechi zetu ambazo sasa zitazidi kuwa ngumu, nimewaambia kuanzia sasa kila mchezo utakaokuwa mbele yetu utakuwa ni sawa na fainali ngumu ambazo ni lazima tuzishinde,”- Mohamed Nabi, Kocha Mkuu wa Yanga Sc.
Simba katika michezo mitatu ya mwisho ya Ligi ameyeyusha dakika 270 bila kufunga bao wala kushinda huku akifungwa mechi mbili, ya Mbeya City na ile ya Kagera na kutoa sare mechi dhidi ya Mtibwa Sugar.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Yanga Yatumia Sh Mil 265 Kushinda Mechi Zao, Hersi Aanika.​

yanga.jpg

USHINDI wa 11 walioupata Yanga, umewapa wachezaji wa timu hiyo bonasi ya Tsh milioni 265 katika michezo ya Ligi Kuu Bara tangu kuanza kwa msimu huu.
Hiyo ikiwa ni siku chache tangu watoke kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Tanzania, mchezo uliopigwa wikiendi iliyopita kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.
Ushindi huo umewafanya waendelee kukaa kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 35 wakicheza michezo 13 ya ligi, huku watani wao Simba wakifuatia wakivuna pointi 25 kwa michezi yote 13.
Yanga tangu kuanza kwa msimu huu, wameshinda michezo 11 huku wakitoka suluhu miwili dhidi ya Simba iliyochezwa Uwanja wa Mkapa, Dar nyingine na Namungo FC nayo ilichezwa Uwanja wa Ilulu, Lindi.
Wadhamini wa Yanga ambao ni GSM mara baada ya kuanza kwa msimu waliwaahidi wachezaji kuwapa Sh 20Mil katika katika kila ushindi wa mchezo wa ligi.
Lakini katika michezo miwili ambayo ilikuwa migumu dhidi ya Coastal Union iliyochezwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga matajiri hao waliongezewa bonasi na kufikia sh 35Mil kama wakiwafunga, ikaja kuongeza na kufikia Sh 50Mil walipowavaa Polisi Tanzania ambayo yote walifanikiwa kushinda na kuchukua Sh 85Mil.
Mastaa hao wakishinda michezo hiyo 11 ya ligi walijikuta wakichukua Sh 265Mil zilizogawiwa kwa wachezaji na benchi la ufundi la timu hiyo, linaloongozwa na Kocha Mkuu Mtunisia, Nasreddine Nabi.
Hivyo wachezaji hao katika michezo 11 waliyocheza na kushinda, tisa walivuna Sh 180Mil kutokana na bonasi ya Sh 20Mil kabla ya kuongezewa dhidi ya Coastal na Polisi Tanzania ambazo zilifikia Sh 265Mil.
Wadhamini hao, huenda wakaendelea kutoa bonasi ya Sh 50Mil katika michezo miwili ya mwisho ya kumaliza mzunguko wa kwanza wa ligi watapocheza dhidi ya Mbeya City na Geita Gold.
Wachezaji hao wameahidiwa kupewa bonasi ya ushindi pekee, kama wakitoa sare hakutakuwa na bonasi, umewekwa utaratibu huo kwa ajili ya kuongeza hamasa ya wachezaji kupambana kupata ushindi pekee utakaowafanya watwae ubingwa mwishoni mwa msimu.
Mkurugenzi Uwekezaji wa GSM ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Injinia Hersi Said, hivi karibuni alizungumzia hilo la bonasi na kusema kuwa: “Bonasi ipo kwa wachezaji wetu ambayo maalum kwa ajili ya kuongeza hamasa wakiwa uwanjani.
“Bonasi hiyo imekuwa ikibadilika kwa kuongezeka kutokana na aina ya timu tunayokutana nayo. Na bonasi ni siri kati ya uongozi na wachezaji.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Yanga Hawazuiliki, Waonyesha Dalili 5 za Ubingwa.​

yanga-6.jpeg

YANGA huu msimu ni wao, kutwaa kombe la Ligi Kuu Bara wana asilimia kubwa sana, kwani wameonyesha dalili zote za kuchukua ubingwa huo waliokosa kwa misimu minne mfululizo.
Yanga hadi sasa wanaongoza kila kitu dhidi ya timu zote zinazoshiriki ligi kuu, hiyo ikiwa ni sababu ya kwanza. Wakiwa wamecheza mechi 13 sawa na dakika 1,170 bila kupoteza. Ni timu pekee ambayo haijapoteza mechi.
Sababu ya pili, Yanga wamekuwa wakipata alama kwenye kila uwanja, hasa vile viwanja vigumu ambavyo ni nadra kupata ushindi kwao.
Wakipata ushindi wa 2-0 dhidi ya Mbeya Kwanza, Uwanja wa Sokoine, wakiwachapa Coastal Union 2-0 pale Mkwakwani, wakiwaburuza Polisi Tanzania kwa mara ya kwanza wakiwa kwao kwa bao 1-0.
Wakiwachapa Tanzania Prisons kwa mabao 2-1, wakiwa kwao Uwanja wa Nelson Mandela. Uwanja pekee ambao bado umekuwa mgumu kwao ni ule wa Namungo wakitoka sare ya 1-1 kama ambavyo imekuwa kwa misimu yote.
Sababu ya tatu, Yanga wana wachezaji wenye uwezo mkubwa wa kufunga mabao msimu huu kama ambavyo ilikuwa kwa Simba msimu uliopita. Fiston Mayele ameshafunga mabao saba.
Feisal Salum amefunga manne sawa na Saidoo Ntibazonkiza, Jesus Moloko amefunga mabao matatu, Khalid Aucho kafunga mawili na Dickson Ambundo, Djuma Shaban na Mukoko Tonombe ambaye kasepa, wamefunga moja moja.
Sababu ya nne, Yanga tayari amevuna alama nne dhidi ya timu ambazo zinapewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa, waliwachapa Azam FC 2-0 na kutoka suluhu na Simba.
Simba wameachwa na Yanga kwa pointi 10 hadi sasa na Azam wamepitwa pointi 14, hali ambayo inazidi kuwapa nafasi kubwa ya kuweza kutwaa ubingwa wa msimu huu.
Sababu ya tano, ari na morali ya wachezaji msimu huu na hiyo imesemwa na msemaji wa timu hiyo, Haji Manara, ambaye amesema kila mchezaji wa timu hiyo ananukia ubingwa.
Manara alisema: “Ukipita kwenye kambi ya Yanga kila mchezaji anazungumzia ubingwa, hakuna mchezaji ambaye hataki kuwa bingwa au kuwapa ubingwa Yanga msimu huu.
“Ubingwa ni wa Yanga, kama Yanga hatakuwa bingwa mimi nitahama nchi hii. Tuna kila nafasi ya kuchukua ubingwa huu.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mshery Afungukia Ujio wa Diarra Yanga.​

Aboutwalib-Hamidu-Mshery-1.jpg

KIPA wa Yanga, Aboutwalib Mshery amesema kuwa atatumia uwezo wa kipa mwenzake, Djigui Diarra katika kujifunza mambo mbalimbali ndani ya timu hiyo akiamini atamsaidia kufikia uwezo wa kimataifa.
Mshery ameongeza kuwa kwake wala hahofii nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza mara baada ya kurejea kwa nyota huyo.
Diarra anarejea ndani ya Yanga baada ya kukosekana kwa muda kutokana na kwenda kulitumikia taifa lake la Mali kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) inayoendelea nchini Cameroon. Mali waliondolewa hatua ya 16 bora.
Mshery alisajiliwa maalum na Yanga kwa ajili ya kuziba nafasi ya Diarra akitokea Mtibwa Sugar ambapo kwa sasa kutakuwa na ushindani kati ya makipa hao.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Mshery alisema kuwa anaamini uwepo wa Diarra utakuwa chachu kwake katika kujifunza mambo mengi mbalimbali kutokana na uwezo wake huku akiwa hana hofu juu ya kucheza kwa sababu ya uwepo wa michezo mingi kikosini humo.
“Diarra ni kipa mkubwa, ana uzoefu katika soka la Afrika hivyo natarajia kujifunza mambo mengi kutoka kwake, hivyo kuwa naye tu katika timu moja inatosha mimi kupata baadhi ya vitu ambavyo vitakuwa na msaada mkubwa kwangu.
“Kuhusu kupata nafasi mbele yake, naamini kocha ndiyo anafahamu zaidi lakini kwa upande wangu naamini kuna michezo mingi sana ya ligi kuu na Kombe la Shirikisho, hivyo naamini nafasi ya kucheza nitapata,” alisema kipa huyo.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Nkane, Mshery Kutibua Usajili wa Nabi Yanga.​

1.jpeg


KOCHA Mkuu wa Yanga, raia wa Tunisia, Nasreddine Nabi, amenogewa na ubora wa wachezaji wazawa aliowasajili katika dirisha dogo huku akipanga kusimamisha usajili wa nyota wa kigeni katika msimu ujao.
Baadhi ya wachezaji wazawa waliosajiliwa katika dirisha dogo ni Aboutwalib Mshery, Denis Nkane, Chrispin Ngushi na Salum Aboubakari ‘Sure Boy’.
Wachezaji hao wote wamesajiliwa kwa mapendekezo ya Nabi baada ya kuwaona katika michezo ya Ligi Kuu Bara mara walipokutana kucheza na timu zao za zamani kabla ya kutua Yanga.
Mmoja wa mabosi wa timu hiyo, ameliambia Championi Jumamosi kuwa kocha huyo hafikirii kuongeza mchezaji mwingine wa kigeni katika usajili wa msimu ujao baada ya kuvutiwa na vipaji vya wachezaji wa hapa nchini.
Bosi huyo alisema kuwa kikubwa alichopanga ni kusajili wachezaji wazawa vijana wenye uwezo mkubwa kama waliokuwa nao Ngushi, Nkane na Mshery.
Aliongeza kuwa kikubwa anataka kuona timu hiyo ikiundwa na wachezaji wengi wazawa wenye umri mdogo watakaocheza kwa muda mrefu katika kikosi chake.
“Kama ikitokea kocha atasajili wachezaji wa kigeni, basi ni mmoja kwani mipango yake katika usajili wa msimu ujao ni kusajili wachezaji wazawa pekee katika timu.
“Kipaumbele hicho anakitoa kwa wazawa baada ya kuvutiwa na baadhi ya wachezaji ambao amewasajili katika dirisha dogo la msimu akiwemo Mshery, Nkane na Ngushi.
“Pia upo uwezekano wa kupunguza wachezaji wa kigeni, na kikubwa anataka kubaki na nane pekee ambao wanaanza katika kikosi cha kwanza kutokana na kanuni za TFF zilizopo za kutumia wachezaji nane katika kikosi cha kwanza,” alisema bosi huyo.
Alipotafutwa Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela kuzungumzia hilo alisema: “Muda wa usajili mkubwa bado haujafikia, kingine masuala ya usajili yote yapo kwa kocha wetu.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mshery Aingia Anga za Diarra.​

mshery.jpeg

ABOUTWALIB Mshery, kipa namba mbili wa Yanga, ameingia anga za Djigui Diarra kwa kugandamizia yale ambayo aliyafanya katika mechi tatu za mwanzo sawa na dakika 270.
Mshery ambaye ni ingizo jipya ndani ya Yanga akitokea Mtibwa Sugar, katika mechi tatu za mwanzo za Ligi Kuu Bara, hajaruhusu bao akiwa ameanza mwendo kama ambavyo Diarra alianza msimu huu.
Diarra raia wa Mali ambaye ni kipa namba moja wa Yanga, alijiunga na timu hiyo mwanzoni mwa msimu huu
ambapo alianza namna hii katika Ligi Kuu Bara; Kagera Sugar 0-1 Yanga, Yanga 1-0 Geita Gold na KMC 0-2 Yanga.
Kipa huyo wakati akiwa hajaruhusu bao kwenye mechi hizo ambazo ni sawa na dakika 270 mbili wakicheza ugenini na moja nyumbani, Yanga ilifunga mabao manne na kukusanya pointi tisa.
Kwa upande wa Mshery, kwenye mechi tatu za kwanza za ligi alizokaa langoni tangu atue Yanga kipindi cha usajili wa dirisha dogo msimu huu, timu yake imefunga mabao saba na kukusanya pointi tisa.
Mechi za Mshery hizi hapa zikiwa mbili ugenini na moja nyumbani kama Diarra; Yanga 4-0 Dodoma, Coastal Union 0-2 Yanga na Polisi Tanzania 0-1 Yanga.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Unaambiwa Nabi Hawazi Kingine Zaidi ya Ubingwa FA.​

nabi-pic-data.jpg

KOCHA Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi amesema ushindi wa bao 1-0 walioupata dhidi ya Mbao FC kwenye Uwanja wa CCM Kirumba ni hatua nzuri kuwania Kombe la Shirikisho la Azam ambalo msimu uliopita walipoteza katika mchezo wa fainali.
Yanga ilipata bao dakika ya 54 lililofungwa na Fiston Mayele akimalizia kwa kichwa mpira wa krosi iliyopigwa na Farid Musa.
Matokeo hayo yameifanya Yanga kufuzu hatua ya 16 ambapo sasa watakutana na Ruvu Shooting ambayo imetinga hatua hiyo baada ya kuiondoa KMC kwa mikwaju ya penalti 6-5 baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Akizungumza juzi baada ya mchezo huo, Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi alisema ulikuwa mchezo mgumu kwani Mbao ni timu nzuri na kuwashukuru wachezaji kwa kupambana na kuibuka na ushindi.
“Ni jambo zuri kupata ushindi inakupa nguvu kuingia kwenye mchezo unaofuata ukiwa na ari na akili yetu tunaihamishia katika mchezo unaofuata ambao naamini hautakuwa rahisi,” alisema Nabi.
Kocha wa Mbao FC, Ibrahim Mumba alisema ubora wa Yanga hasa safu ya ulinzi ulikuwa kikwazo kushindwa kutumia nafasi walizopata na kuwafanya kuibuka na ushindi kwenye mchezo huo.
“Huu ulikuwa mchezo wetu muhimu kushinda katika mashindano ya Kombe la Shirikisho la Azam lakini tumeondolewa na sasa tunajipanga na michezo ya First League,” alisema Mumba.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kibwana Anahesabu Siku Yanga.​

kibwana_shomari_273112201_272030598349199_7772982237318078876_n.webp1_.jpg

BEKI kiraka wa Yanga, Kibwana Shomari na mwenzake Abdallah Shaibu ‘Ninja’, wanahesabu siku tu
za kurudi uwanjani mara baada ya kupona majeraha yao.
Kibwana anayemudu kucheza beki wa kulia na kushoto, wiki mbili zilizopita alikwenda Tunisia sambamba
na Ninja kwa ajili ya kufanyiwa operesheni ya majeraha yanayowasumbua.
Kurejea kwa mabeki hao kutampa upana wa kikosi Kocha Mkuu wa Yanga, Mtunisia, Nasreddine Nabi katika michezo ijayo ya Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho la Azam Sports.
kibwana_shomari_271384970_452502713192771_5412131257490739282_n.jpg

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Spoti Xtra na kuthibitishwa na daktari wa timu hiyo, Youssef Ammar, mabeki hao watarejea uwanjani mara baada ya mchezo wa ligi dhidi ya Mbeya City utakaopigwa Februari 5, mwaka huu.
Ammar alisema mabeki hao wataanza kufanya mazoezi mepesi ya uwanjani baada ya kumaliza program ya gym wanayoendelea nayo hivi sasa.
“Kibwana na Ninja walifanyiwa operesheni ndogo ya goti ambayo itawarejesha haraka uwanjani tofauti na
Yacouba (Songne) ambaye operesheni yake ilikuwa kubwa na kumfanya kukaa nje karibia miezi minne.
“Hivyo Kibwana na Ninja upo uwezekano wa kujiunga na mazoezi ya uwanjani pamoja na wachezaji wenzake hivi
karibuni,” alisema Ammar.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Tukio Hili kwa Mwamnyeto Lawaibua Simba.​

mwamnyetoz.jpg

MKUU wa Idara ya Habari na Mawasilino wa Klabu ya Simba SC, Ahmed Ally amehoji tukio la Kiongozi wa Young Africans kuingia Uwanjani dakika chache kabla ya kuanza kwa mchezo wa Kombe la Shirikisho Tanzania Bara ‘ASFC’ uliochezwa Jumamosi (Januari 29), Uwanja wa CCM Kirumba.
Young Africans
walikua wenyeji wa mchezo huo uliohamishwa kutoka Dar es Salaam na kupelekwa Mwanza, ambapo kabla ya kuanza, nahodha wa kikosi cha ‘Wananchi’ Bakari Nondo Mwamnyeto alimkabidhi jezi Hersi Said kama ishara ya kumpongeza kwa kupata mtoto wa kiume.
Ahmed Ally amehoji tukio hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika: “Kwa mujibu wa kanuni ya 17 ya Ligi hairuhusiwi mtu asiyehusika na mchezo kuingia Uwanjani wakati mchezo unaendelea. Huyu Kiongozi anaingiaje kwenye pitch wakati mchezo umeanza tena kwa tukio lisilokua la kimichezo?
“Anapataje ruhusa ya kuingia Uwanjani kupongezwa juu ya uzao wa Mtoto tena Kick Off inasimamishwa Ili wao wapongezane. Mmewahi kuona wapi hili likitokea?
“Tukio halijaja bahati mbaya, kawaida lazima utoe taarifa kwa Kamishna wa mchezo juu ya kufanyika kwa tukio kama hilo? Kamishna alikubali kwa vigezo vipi tukio lisilokua la kimichezo lifanyike kwenye mechi rasmi ya kimashindano?
“Na kama hawakuomba ruhusa huyu anatoa wapi mandate ya kufanya hivyo?? Huku ni kuunajisi mpira, ipo siku mtu atataka kumvisha Pete mchumba ake halafu atafanya hivyo kwenye mechi.
TFF tafadhalini simamiemi misingi ya mpira. Udhamini wa Bilioni 1 kwa Mwaka usiwatie upofu. Nasema haya sio kwa sababu ya upinzani ni bali tunataka taratibu za mpira zifuatwe ili tuwe na mashindano bora zaidi.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Yacouba amerudi, aitaka namba yake.​

yakuba pic

HABARI ya mjini sasa kwa upande wa soka ni straika wa Yanga, Fiston Mayele ambaye amekuwa mwiba kwa mabeki na makipa wa timu pinzani, kumbe moto huo umemshtua hadi Yacouba Songne ambaye ameukubali mziki huo, ila amepiga mkwara.
Mayele ameibuka shujaa juzi baada ya kuifungia Yanga bao pekee dhidi ya Mbao na kuivusha timu hadi 16 Bora ya michuano ya Shirikisho (ASFC) katika mechi kali iliyopigwa kwenye Uwanja wa CCM KIrumba, jijini Mwanza.
Kumbe Yacouba amekuwa akimfuatilia mwenzake mwenye mabao sita katika Ligi Kuu Bara akishika nafasi ya pili nyuma ya Reliants Lusajo wa Namungo na kusema anafurahishwa na juhudi za Mayele na kukiri hofu aliyonayo kwa namba yake.
Yacouba yupo nje ya uwanja kwa muda kutokana kusumbuliwa na jeraha la goti amefunguka, kwa sasa anaendelea vizuri na ameanza mazoezi ya nguvu, akiweka wazi kuwa muda wowote anaweza kurudi uwanjani kuipigania namba yake.
“Tumesajiliwa Yanga kujenga nyumba moja mazuri yanayofanywa na Mayele ni ya wanayanga wote, nafurahia juhudi zake na nakiri kuwa ni mchezaji bora kwa sasa pamoja na mastaa wengine wanaocheza nao kikosini, kwani peke yake hawezi,” alisema Yacouba na kuongeza;
“Nimemisi vingi tangu niwe nje ya uwanja, hakuna pengo linaloonekana baada ya kukosekana kwangu, kwani timu inafanya vizuri inapata matokeo kwa hakika nina kazi kubwa kuhakikisha narudi kikosini kwani kwa sasa kila mmoja ni bora.”
Akiizungumzia Yanga kwa ujumla, mshambuliaji huyo aliyekuwa kinara wa mabao wa timu hiyo kwa msimu uliopita akifunga nane, alisema anaiona ikiwa na mafanikio makubwa zaidi msimu huu tofauti na misimu minne nyuma waliyokosa mataji.
“Kwa sasa kila mchezaji ana uchu na kiu ya mafanikio kwa timu ndio maana imekuwa ikifanya vizuri, nami kwa vile nimeanza kujifua naamini nitarudi kuongeza nguvu.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Yanga bado kidogo tu.​

yanga pic

WANACHAMA na mashabiki wa Yanga wanaendelea kuchekelea mafanikio ya timu yao ndani ya msimu huu, lakini sasa wameongezewa mzuka baada ya mabosi wa klabu hiyo kuwapa taarifa kwamba Yanga ya kisasa bado kidogo tu.
Yanga ipo kwenye mchakato wa klabu yao kuendeshwa kisasa kwa mfumo wa hisa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Yanga, Senzo Mazingisa amewahakikisha wanayanga kuwa, bado siku chache kabla ya klabu hiyo haijaongozwa na Rais badala ya Mwenyekiti.
Katika mahojiano maalumu na Mwanaspoti, Senzo alisema kwa sasa wapo kwenye sehemu nzuri ya mabadiliko baada ya kupewa ruksa huku kamati zote za katiba mpya zinaendelea kuhakikisha mchakato huo unakamilika.
“Yanga haipo chini ya BMT tu. ipo pia kwa TFF na baada ya Katiba yetu kukamilika tuliipeleka kwao na wao wametupa miezi sita, wametuambia kila kitu kilichopo kwenye Katiba yetu kikamilike ndani ya miezi hiyo,” alisema.
Senzo alisema kwa sasa wanashughulikia kuwabadili mashabiki kuwa wanachama na hawana muda wa kupoteza kwani tayari mchakato huo unaendelea vizuri.
“Tumeanza kusajili wanachama wetu na namba zinaenda vizuri, mpaka sasa tunaona mabadiliko yanaenda vizuri na kutakuwa na mabadiliko ya kimuundo kwenye uongozi wa Yanga na lengo likiwa ni kupata muundo wa timu.”
Senzo alisema baada ya kukamilika kwa usajili wa wanachama wanageukia upande wa thamani halisi ya klabu yao ili wawekezaji wapate picha kamili ya Yanga kabla ya kuweka pesa zao akisisitiza hakutakuwa na cheo ya mwenyekiti na badala yake klabu hiyo itaongozwa na Rais wa Klabu.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5
Zoezi la Usajili Mkoani 𝗞𝗔𝗚𝗘𝗥𝗔 linaendelea kwa kasi kwenye Ukumbi wa 𝗟𝗜𝗡𝗔𝗦 Bukoba mjini. Njoo Ujisajili Kidigitali na kupata Elimu juu ya faida za kuwa Mwanachama wa Young Africans Sc. Aidha Usajili wa Wanachama unaendelea katika Mikoa yote Tanzania tembelea Tawi la Young Africans Sc Karibu yako Ujisajili.
Image
Image
Image
Image
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mwenye Y anga yake karudi, Fei Toto nje mwezi.
Diarra PIC

SIKIA hii. Mshindani mkubwa wa Aishi Manula wa Simba ni Djigui Diarra wa Yanga anayerejea leo Jijini Dar es Salaam akitokea kwenye Afcon ambako timu yake ya Mali ilitolewa hatua ya 16 Bora. Tangu Diarra aende Afcon, Aishi amecheza mechi nne na kuambulia pointi nne kwenye Ligi Kuu Bara. Mashabiki wa Yanga wanamsubiri kwa hamu Diarra kujiunga na kambi yao inayoanza leo kujiandaa na mechi ya Ligi dhidi ya Mbeya City itakayopigwa Jumamosi pale kwa Mkapa.
Lakini Diarra anarejea katika kipindi ambacho langoni anamkuta kipa mpya, Aboutwalib Mshery, aliyesajiliwa katika dirisha dogo la uhamisho akitokea Mtibwa Sugar, akiwa gari limewaka ile mbaya.
Diarra anatarajiwa kuchukua namba yake kikosini hata kama haitakuwa dhidi ya Mbeya City, ambao waliizamisha Simba 1-0 kwenye Uwanja wa Sokoine Januari 17, lakini bado uamuzi mzito unabaki mikononi mwa kocha Nasreddine Nabi na benchi lake la ufundi kuhusu nani aanze katika mechi hiyo ya Jumamosi.
Diarra hakupata nafasi ya kudaka katika Afcon ya nchini Cameroon iliyofikia hatua ya nusu fainali
hivi sasa, lakini uzoefu wake unatarajiwa kumbakisha kuwa namba moja katika kikosi cha Nabi huku Mshery akitarajiwa kumpa ushindani wa uhakika.
Mbali na mechi tatu za Kombe la Mapinduzi Zanzibar ambako Yanga walitolewa kwa penalti katika nusu fainali dhidi ya Azam FC, Mshery amesimama langoni katika mechi nyingine tatu za Ligi Kuu Bara ambazo hajaruhusu bao hata moja dhidi ya Dodoma Jiji (4-0), Coastal Union (2-0) na Polisi Tanzania (1-0) na amedaka pia mechi nyingine moja ya Kombe la Shirikisho (ASFC) waliyoshinda 1-0 dhidi ya Mbao FC.
Kocha Nabi atakuwa na mtihani wa kuamua nani asimame langoni wakati wa mechi na Mbeya City kabla ya kuwavaa Biashara United katika mechi ya hatua ya 16-Bora ya Kombe la Shirikisho kati ya Februari 12 hadi 17, mwaka huu.Yanga imeanza mazoezi yake jana na leo wachezaji wanaingia rasmi kambini kujiandaa na mechi hizo lakini itawakosa baadhi ya nyota wao ambao ni majeruhi akiwemo Feisal Salum ‘Fei Toto’ anayesumbuliwa na nyama za paja na atakuwa nje mwezi mmoja, Abdallah Shaibu ‘Ninja’,
Yacouba Sogne na Kibwana Shomary ingawa hawa watatu wameanza mazoezi mepesi.
Katika mazoezi ya jana pia iliwakosa nyota Said Ntibazonkiza, Kocha Msaidizi Cedric Kaze ambao wapo kwao Burundi kwa ruhusa maalumu kama ilivyo kwa Heritier Makambo, huku Djuma Shabani na Yanick Bangala nao wakiwa kwenye timu yao ya taifa ya DR Congo iliyokuwa ikicheza mechi ya kirafiki.
Nabi alisema hivi sasa ratiba ya mazoezi inayofuata ni kurudisha miili ya wachezaji katika utimamu na hali ya kiushindani na ndani yake watafanya mazoezi ya mbinu kulingana na kile walichokionyesha katika mechi iliyopita na Mbao.
“Kuna maeneo tulifanya makosa hapo tutapambana kurekebisha ili kuondoa makosa hayo katika mechi zijazo na tulipokuwa imara kuboresha ili kufanya vizuri zaidi, akili yetu na nguvu sasa ni mechi ya Mbeya City tufanye vizuri kwa kupata ushindi na kujiweka katika mazingira mazuri kwenye msimamo wa ligi,” alisema na kuongeza:
“Baada ya kumalizana na Mbeya City na kufahamu tulichokipata akili na nguvu zitahamia michezo inayofuata ikiwamo ya Biashara na ya Ligi Kuu dhidi ya Mtibwa Sugar tutakayokuwa ugenini.”